Waziri Mkuu wa zamani aliyejiuzulu mwaka 2008 kwa kashfa kubwa ya ufisadi ya Richmond, Edward Lowassa, ametuma ujumbe wa watu wawili waende Nijeria kukutana na Pastor TemitopeBalogun Joshua a.k.a. Prophet T.B. Joshua ambaye 'alimtabiria' Mbunge Beatrice Shellukindo kuwa Lowassa atakuwa Rais wa Tanzania baada ya uchaguzi wa mwaka 2015.
Wajumbe hao wa Lowassa ni mtoto wake Frederick Lowassa na mshauri wake mkuu wa masuala ya vyombo vya habari, Absalom Kibanda, ambaye ni mhariri wa gazeti la Tanzania Daima linalomilikiwa na Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe.
Frederick na Kibanda wako safarini Nijeria kwenda kuchukua 'upako' ili wamletee Lowassa asafishe nyota na kuepuka na dhoruba kubwa ya kisiasa katika kipindi hiki kigumu ambacho wajumbe wa NEC ya CCM wamedhamiria kuwafukuza mafisadi kwenye chama, akiwemo Lowassa, Andrew Chenge na Rostam Aziz.
Wajumbe hawa wa Lowassa wanatarajiwa kukutana na TB Joshua siku ya Jumapili Juni 12, 2011, ambayo mchungaji huyo atakuwa anasherehekea birthday yake na atawapa "dawa" wamletee Lowassa Tanzania ili asafishe nyota yake.
Ikumbukwe kuwa 'nabii' huyu wa Nijeria aliwahi kumwambia Mbunge wa CCM, Beatrice Shellukindo, kuwa anatabiri Lowassa atakuwa Rais ajaye wa Tanzania.
Beatrice, ambaye mume wake William Shellukindo, aling'olewa ubunge kwenye jimbo la Bumbuli na kina Lowassa-Rostam-Chenge na kisha wakamuweka January Makamba, sasa amehamia kwenye kambi ya kumpigia debe Lowassa awe Rais pamoja tuhuma kubwa za ufisadi dhidi yake, ikiwemo kujilimbikizia sana mali, ufisadi wa Richmond, kununua hekaru la sh bilioni 1 London na mengine mengi.
Siri ya Edward Lowassa nje | Gazeti la MwanaHalisi
Eti huyu fisadi kweli anadhani atakuwa Rais wa Tanzania?
Wajumbe hao wa Lowassa ni mtoto wake Frederick Lowassa na mshauri wake mkuu wa masuala ya vyombo vya habari, Absalom Kibanda, ambaye ni mhariri wa gazeti la Tanzania Daima linalomilikiwa na Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe.
Frederick na Kibanda wako safarini Nijeria kwenda kuchukua 'upako' ili wamletee Lowassa asafishe nyota na kuepuka na dhoruba kubwa ya kisiasa katika kipindi hiki kigumu ambacho wajumbe wa NEC ya CCM wamedhamiria kuwafukuza mafisadi kwenye chama, akiwemo Lowassa, Andrew Chenge na Rostam Aziz.
Wajumbe hawa wa Lowassa wanatarajiwa kukutana na TB Joshua siku ya Jumapili Juni 12, 2011, ambayo mchungaji huyo atakuwa anasherehekea birthday yake na atawapa "dawa" wamletee Lowassa Tanzania ili asafishe nyota yake.
Ikumbukwe kuwa 'nabii' huyu wa Nijeria aliwahi kumwambia Mbunge wa CCM, Beatrice Shellukindo, kuwa anatabiri Lowassa atakuwa Rais ajaye wa Tanzania.
Beatrice, ambaye mume wake William Shellukindo, aling'olewa ubunge kwenye jimbo la Bumbuli na kina Lowassa-Rostam-Chenge na kisha wakamuweka January Makamba, sasa amehamia kwenye kambi ya kumpigia debe Lowassa awe Rais pamoja tuhuma kubwa za ufisadi dhidi yake, ikiwemo kujilimbikizia sana mali, ufisadi wa Richmond, kununua hekaru la sh bilioni 1 London na mengine mengi.
Siri ya Edward Lowassa nje | Gazeti la MwanaHalisi
Eti huyu fisadi kweli anadhani atakuwa Rais wa Tanzania?