Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 15,499
- 19,340
Wanaforum,
Sheria moja ya kazi huwa inaweka conditions za mtu kulipwa mafao baada ya kuacha kazi; sheria hii huwa inaelekeza kuwa mtu atalipwa mafao yake ya mwisho endapo tu mtu huyo ataacha kazi yake ile honorably: yaani ame amestaafu au kustaafishwa, siyo kufukuzwa na mwajiri wake au kwa kujiuzulu mwenyewe. Katika kuzuia waajiri wasiwe wanawafukuza waajiriwa wao makusudi ili kukwepa kuwalipa mafao, kuna vyombo mbalimbali vya kuwathibiti ikiwa ni pamoja na mahakama ya kazi.
Sababu za mtu kuacha kazi honorably ni pamoja na umri au afya yake, muda aliokwisha fanya kazi kwa mwajiri yule, na kuisha kwa uhai wa kazi ile bila matakwa yake mwenyewe (kustaafishwa.) Sote tunajua wazi kabisa kuwa kuna tofauti kubwa sana kati ya kustaafishwa na kufukuzwa kazi.
Sasa sababu ya kuandika hayo ni pale ninapoona kuwa Lowasa anakuwa addressed kama Waziri Mkuu Mstaafu ( ikiwa na maana kuwa ana haki ya kulipwa mafao yake ya kazi) huku inajulikana kuwa hakuachia madaraka yale honorably. Nionavyo mimi ni kuwa Lowasa ni Waziri Mkuu wa Zamani, yeye ni tofauti na wenzie kama Sumaye, Msuya, Malecela, Warioba, Salim, Sokoine, na Kawawa ambao ndio mawaziri wakuu waliostaafu. Lowasa anaweza kuwa grupu moja na Nyerere kwa vile Nyerere naye alijiuzulu Uwaziri Mkuu ingawa sababu zao za kujiuzulu ni diametrically opposite. Hatujawahi kumwita Nyerere kama waziri mkuu mstaafu kwa vile hakustaafu madaraka yale; ila katika kumbukumbu huwa tunasema kuwa alikuwa Waziri Mkuu wa Kwanza.
Lowasa angeweza kuonekana kuwa ameachia madaraka hayo honorably, endapo angetengeneza mazingira yayanyoonyesha kuwa uhai wa madaraka yale umekwisha bila yeye mwenyewe kutaka, kwa mfano kama rais angevunja baraza lote la mawaziri na kuliunda upya huku nafasi ya waziri mkuu ikiwekwa mikononi mwa mtu mwingine bila kumhukumu Lowasa. Kwa vile Lowasa alijiuzulu kwa hiari yake mwenyewe na hivyo kuvuruga uhai wa madaraka yake yeye mwenyewe, basi mtu huyu si mstaafu na wala hastahili kulipwa mafao ya mwisho wa kazi. Tukiruhusu Lowasa apewe hadhi ya Waziri Mkuu mstaafu basi tutakuwa tunaweza mazingira mabaya sana ya kimaadili. Tutakuwa tumeruhusu watu watakaopewa madaraka haya kuyatumia vibaya halafu wakakimbilia kujiuzulu ili waendelee kupata marupurupu ya Uwaziri Mkuu. Hebu fikiria kuwa kama katika kipindi cha miaka mitano kila waziri mkuu atakuwa anajiuzulu baada ya miezi miwili na kuhesbabiwa kuwa ni waziri mkuu mstaafu; je, taifa litaishia kulea mawaziri wakuu wastaafu wangapi?
Moderator
Inawezekana topiki ya aina hii iliwahi kujadiliwa huko nyuma; samahani kwa kuirudia ila naomba uipe thread hii muda kidogo kabla hujaiunganisha na zinazofanana.
Sheria moja ya kazi huwa inaweka conditions za mtu kulipwa mafao baada ya kuacha kazi; sheria hii huwa inaelekeza kuwa mtu atalipwa mafao yake ya mwisho endapo tu mtu huyo ataacha kazi yake ile honorably: yaani ame amestaafu au kustaafishwa, siyo kufukuzwa na mwajiri wake au kwa kujiuzulu mwenyewe. Katika kuzuia waajiri wasiwe wanawafukuza waajiriwa wao makusudi ili kukwepa kuwalipa mafao, kuna vyombo mbalimbali vya kuwathibiti ikiwa ni pamoja na mahakama ya kazi.
Sababu za mtu kuacha kazi honorably ni pamoja na umri au afya yake, muda aliokwisha fanya kazi kwa mwajiri yule, na kuisha kwa uhai wa kazi ile bila matakwa yake mwenyewe (kustaafishwa.) Sote tunajua wazi kabisa kuwa kuna tofauti kubwa sana kati ya kustaafishwa na kufukuzwa kazi.
Sasa sababu ya kuandika hayo ni pale ninapoona kuwa Lowasa anakuwa addressed kama Waziri Mkuu Mstaafu ( ikiwa na maana kuwa ana haki ya kulipwa mafao yake ya kazi) huku inajulikana kuwa hakuachia madaraka yale honorably. Nionavyo mimi ni kuwa Lowasa ni Waziri Mkuu wa Zamani, yeye ni tofauti na wenzie kama Sumaye, Msuya, Malecela, Warioba, Salim, Sokoine, na Kawawa ambao ndio mawaziri wakuu waliostaafu. Lowasa anaweza kuwa grupu moja na Nyerere kwa vile Nyerere naye alijiuzulu Uwaziri Mkuu ingawa sababu zao za kujiuzulu ni diametrically opposite. Hatujawahi kumwita Nyerere kama waziri mkuu mstaafu kwa vile hakustaafu madaraka yale; ila katika kumbukumbu huwa tunasema kuwa alikuwa Waziri Mkuu wa Kwanza.
Lowasa angeweza kuonekana kuwa ameachia madaraka hayo honorably, endapo angetengeneza mazingira yayanyoonyesha kuwa uhai wa madaraka yale umekwisha bila yeye mwenyewe kutaka, kwa mfano kama rais angevunja baraza lote la mawaziri na kuliunda upya huku nafasi ya waziri mkuu ikiwekwa mikononi mwa mtu mwingine bila kumhukumu Lowasa. Kwa vile Lowasa alijiuzulu kwa hiari yake mwenyewe na hivyo kuvuruga uhai wa madaraka yake yeye mwenyewe, basi mtu huyu si mstaafu na wala hastahili kulipwa mafao ya mwisho wa kazi. Tukiruhusu Lowasa apewe hadhi ya Waziri Mkuu mstaafu basi tutakuwa tunaweza mazingira mabaya sana ya kimaadili. Tutakuwa tumeruhusu watu watakaopewa madaraka haya kuyatumia vibaya halafu wakakimbilia kujiuzulu ili waendelee kupata marupurupu ya Uwaziri Mkuu. Hebu fikiria kuwa kama katika kipindi cha miaka mitano kila waziri mkuu atakuwa anajiuzulu baada ya miezi miwili na kuhesbabiwa kuwa ni waziri mkuu mstaafu; je, taifa litaishia kulea mawaziri wakuu wastaafu wangapi?
Moderator
Inawezekana topiki ya aina hii iliwahi kujadiliwa huko nyuma; samahani kwa kuirudia ila naomba uipe thread hii muda kidogo kabla hujaiunganisha na zinazofanana.