jouneGwalu
JF-Expert Member
- Apr 11, 2011
- 2,687
- 1,780
Kutoka kwenye experience yangu binafsi.
Nilikuwa na mrembo, mambo yalikuwa mazuri sana kati yetu... Tukapitia mengi sana kwa takribani miaka 3.
Mipango ilikuwa mingi sana baina yetu.... baadae kidogo mambo taratibu yakawa yanabadilika, chating za mara kwa mara zikaanza kupungua, maongezi kwenye simu yakawa ni mafupi sana tofauti na enzi zile za "kata wewe" na ikawa hata tukionana na tukiwa pamoja stori hamna kabisa uchangamfu wake kwangu ukapungua sana hata kama hatujaonana kwa muda mrefu mkionana sikuhyo hata hug utapewa kwa kulazimisha tu, mbaya zaidi hata radha ya mechi ikawa kwenye hatihati akawa kama mtu asiye na hisia kabisa so anajilazimisha ili asiniboe sababu mi bado nilikuwa hot kwa mapenzi yake.
Nikanotice hayo mabadiliko, tukajadili. Aksema hata yeye anajiona kama hayupo sawa ila hajui hasa tatizo ni nini ila akaniahidi kubadilika na kila kitu kitakuwa poa, nikamuelewa, tukaendelea! Kwakweli wala hakuna kilichobadilika, ikatokea siku nikamuandalia zawadi ambayo binafsi niliithamini sana..... Sitakuja kuisahau hiyo siku, aliipokea kwa kawaida sana afu wala hakusema ameipata hadi baada ya siku kama 3 hivi, ikabidi nimpigie kumuuliza kama ameipata, akasema atanipigia. Baada ya mda akapiga ndiyo kunishukuru, hata hvyo na moyo ushavunjika so nikamuitikia tu.
Huwezi kujua nini kipo kwenye moyo wa mwanamke ila kwa siku zile (nadhani mpaka sasa) nilikuwa namwamini sana yule mtoto, so nikawa najua ni moods zake tu sifikirii kama kuna mtu mwingine (japo inawezekana yupo).
Kama january hivi akaniambia hana hisia za kimapenzi tena kwangu. Sababu nilishaziona dalili toka mwanzo so haikunishtua sana japo "its hard to let go" nikamwambia sawa kama mapenzi yameisha basi nakuacha, uniache, tuachane! Badala yake akaniomba tuwe marafiki tu, nikamwambia haiwezekani. Mi toka siku ile nikaachana nae sikuhangaika kumpigia simu wala kumtext...
Tunakutana FaceBook kwenye (status) comment za marafiki zetu, sometime anaandika post kwenye wall yangu, so huwa inabidi nimjibu. Majuzi kama mwezi umepita akanitext kujua naendeleaje nikamjibu nipo poa nafanya vizuri.
Niwe muungwana kwa kukiri kuwa yule mtoto bado nampenda bado ila sina mpango wa kumlilia kwa penzi lake since ametamka kuwa "PENZI LAKE LIMEKWISHA", kinachoniweka kwenye mapenzi na mtu ni yeye anipende na mimi nimpende. Hiyo statement ndiyo inazunguka kichwani mwangu kilasiku na imenifanya nililete suala hili mbele ya WANAJAMII wenzangu mnisaidie kidogo, inakuwaje? eti mapenzi huwa yanakufa?
Kwa hii hali ndiyo maana nikasema "love; knocked me out"
Naomba kuwasilisha jamvini wana-JF.
Kama haupo interested potezea usizingue!
Nilikuwa na mrembo, mambo yalikuwa mazuri sana kati yetu... Tukapitia mengi sana kwa takribani miaka 3.
Mipango ilikuwa mingi sana baina yetu.... baadae kidogo mambo taratibu yakawa yanabadilika, chating za mara kwa mara zikaanza kupungua, maongezi kwenye simu yakawa ni mafupi sana tofauti na enzi zile za "kata wewe" na ikawa hata tukionana na tukiwa pamoja stori hamna kabisa uchangamfu wake kwangu ukapungua sana hata kama hatujaonana kwa muda mrefu mkionana sikuhyo hata hug utapewa kwa kulazimisha tu, mbaya zaidi hata radha ya mechi ikawa kwenye hatihati akawa kama mtu asiye na hisia kabisa so anajilazimisha ili asiniboe sababu mi bado nilikuwa hot kwa mapenzi yake.
Nikanotice hayo mabadiliko, tukajadili. Aksema hata yeye anajiona kama hayupo sawa ila hajui hasa tatizo ni nini ila akaniahidi kubadilika na kila kitu kitakuwa poa, nikamuelewa, tukaendelea! Kwakweli wala hakuna kilichobadilika, ikatokea siku nikamuandalia zawadi ambayo binafsi niliithamini sana..... Sitakuja kuisahau hiyo siku, aliipokea kwa kawaida sana afu wala hakusema ameipata hadi baada ya siku kama 3 hivi, ikabidi nimpigie kumuuliza kama ameipata, akasema atanipigia. Baada ya mda akapiga ndiyo kunishukuru, hata hvyo na moyo ushavunjika so nikamuitikia tu.
Huwezi kujua nini kipo kwenye moyo wa mwanamke ila kwa siku zile (nadhani mpaka sasa) nilikuwa namwamini sana yule mtoto, so nikawa najua ni moods zake tu sifikirii kama kuna mtu mwingine (japo inawezekana yupo).
Kama january hivi akaniambia hana hisia za kimapenzi tena kwangu. Sababu nilishaziona dalili toka mwanzo so haikunishtua sana japo "its hard to let go" nikamwambia sawa kama mapenzi yameisha basi nakuacha, uniache, tuachane! Badala yake akaniomba tuwe marafiki tu, nikamwambia haiwezekani. Mi toka siku ile nikaachana nae sikuhangaika kumpigia simu wala kumtext...
Tunakutana FaceBook kwenye (status) comment za marafiki zetu, sometime anaandika post kwenye wall yangu, so huwa inabidi nimjibu. Majuzi kama mwezi umepita akanitext kujua naendeleaje nikamjibu nipo poa nafanya vizuri.
Niwe muungwana kwa kukiri kuwa yule mtoto bado nampenda bado ila sina mpango wa kumlilia kwa penzi lake since ametamka kuwa "PENZI LAKE LIMEKWISHA", kinachoniweka kwenye mapenzi na mtu ni yeye anipende na mimi nimpende. Hiyo statement ndiyo inazunguka kichwani mwangu kilasiku na imenifanya nililete suala hili mbele ya WANAJAMII wenzangu mnisaidie kidogo, inakuwaje? eti mapenzi huwa yanakufa?
Kwa hii hali ndiyo maana nikasema "love; knocked me out"
Naomba kuwasilisha jamvini wana-JF.
Kama haupo interested potezea usizingue!