Lonely Me...... Nimefiwa na baba yangu

Mkuu pole sana! Mungu akujalie uende na urudi salama. Bwana ametoa na Bwana ametwaa, jina la Bwana lihimidiwe, Amina.
 
Pole sana Buji, safari njema kuwahi mazishi na Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi~AMEN
 
Sisi ni wa mwenyezi Mungu na kwake,ndipo marejeo ya viumbe wote.
 
Pole sana Ndugu yetu Mungu amempenda zaidi Ametoa na Ametwaa Jina la Bwana Libarikiwe sote hiyo ni njia yetu.
 
Wenzangu wana JF, nasikitika kuwajulisha kuwa nimefiwa na baba yangu mdogo, ambaye tulikuwa tumeshibana naye sana, na alikuwa ndiye baba yangu pekee aliyenijali na kunitunza tangu alipofariki baba yangu mzazi.
Nimeachwa mpweke sana, na kesho natarajia kwenda Usukumani kwa ajili ya maziko.
Mungu ailaze mahali pema roho ya marehemu.

RIP Baba mdogo! Bujibuji Mungu akupe moyo wa subira, nakutakia safari njema ya kwenda na kurudi msibani na nakutakieni shughuli njema za maziko.
 
mungu ametoa na pia ametwaa,jilake bwana lizidi kuabudiwa

kukatika kwa nyavu sio mwisho wa uvuvi,ingawaje ni vigumu sana kuipata nyavu ile uizoeayo,kwa hiyo mkuu jipe moyo kuwa na nguvu ya kuyakabili yote yatakayo kusibu baada ya kuondoka kwa mzee

RIP baba mdogo wetu
 
Pole sana buji....najua upo katika wakati mgumu pia nasi tupo nyuma yako hauko peke yako katika wakati huu mgumu sana ila kwa kuwa mungu alipend hivyo tunashukulu mana alisha ahidi kuwa kila nafsi itaonja mauti mapenz yake yatimizwe.mungu akutangulie na akupe falaja hasa kipindi hiki kigumu
 
pole sana kazi yake mola haina makosa.Mola ailaze roho yake mahala pema peponi.Amina
 
condolence-bujibuji.jpg

Pole sana mkuu wangu, pokea na ua hilo kama ishara yangu ya kuungana na nyie ktk kipindi hiki kigumu.
 
Back
Top Bottom