Loliondo pananuka mauti

Popote duniani hakuna dawa ya kuzuia au kutibu kifo
Wagonjwa wanakufa hata kwenye hospitali kubwa kabisa zenye wataalam wa hali ya juu kabisa
Dawa ya babu ni dawa na imani (neno la Mungu)
Hata wakati wa Yesu watu walikuwa wanakufa; Lazaro anatajwa kwa vile alifufuliwa.
Yesu alianza peke yake lakini alipotaka watu wengi wahubiriwe, aliwatuma wanafunzi wake; Babu ameanza peke yake, kadri watu wanavyoongezeka, tuombe Mungu amfunulie ili awatumie hao wanaomsaidia kugawa dawa (nao wawe na uwezo wa kutoa dawa kama babu)
Malaria ina dawa tena ambayo kisayansi inaaminika kutibu, lakini wapo watu wanaokunywa dawa hiyo na wanakufa hadi inafikia mahali pa kutafuta kinga (net).
Kwa kuwa watu wengi bado wanapona kwa kunywa kikombe cha babu, serikali inatakiwa kuimarisha huduma za dharura ili wale walio mahututi waendelee na dawa zao za kawaida kabla ya kufika kwa babu. Wakati niko kwenye msitari wa kufika kwa babu niliona gari la ambulance la Halmashauri likizunguka kwenye foleni likiwa na mganga tayari kuhudumia wale walio mahututi - wa pumu, kifafa nk. Hii ni step nzuri. Ile kodi ya Tshs 2000 kwa kila gari, halmashauri iitumie kuimarisha hali ya usafi pale. Chimba vyoo vya muda along the road up to say 10 km. Chimba mashimo ya kutupa takataka along the road, na watu waelekezwe kutupa takataka humo. Siku hizi watu ni wastaarabu, ukiwaelekeza usafi wanafuata. Kwa kuwa kikombe cha babu kinakubalika na wengi, tumuwezesha kuchemsha dawa kwa wingi zaidi na kuimarisha namna ya kusafisha vikombe. Kwa mfano akiwezeshwa kuchemsha kwa kutumia gesi, hii inaweza kuchemsha dawa nyingi na hata maji ya kuoshea vikombe yakawa ya moto pia; Hii pia itazuia uharibifu wa mazingira utakaosababishwa na ukataji kiti kwa ajili ya kuni nk.
Pamoja na tahadhari na wasiwasi juu ya kikombe cha babu, as long as wengi wanakikubali, ebu tuboreshe mazingira yake; tukubali kwamba kwa hivi sasa ni vigumu kuwazuia watu wasiende!

Si rahisi sana kama sio mtu wa rohoni kuyatambua mambo kama haya! Babu haui, dawa yake haiui, serikali haiui, wagonjwa hawajiui ila Hii ni mbinu kubwa ya shetani kuua watu!
 
Nadhani problem tree yako ingeonyehsa mzunguko kamili, kwani ilioita matokeo, mengine ndio yamesababisha tiba ya babu kuwa kama ilivyo,
Tiba hii ni kati ya matokeo ya matatizo makubwa tulionayo. umasikini, ujinga na maradhi!!!

hahahahahahahahaha wewe umekula kweli mchana huu?
 
BBC News:Tanzanian 'miracle' pastor Mwasapile calls for a break


A Tanzanian pastor has asked people to stop going to his remote home for a "miracle cure" after thousands flocked there, causing chaos in the surrounding area.
Rev Ambilikile "Babu" Mwasapile, 76, says he does not want any new arrivals until after Friday 1 April, to let the crowds die down.
Local media report that about 52 people have died while waiting to see him.
A BBC reporter says the queues to see him stretch for 26km (16 miles).
Belief in magic and the powers of traditional healers are widespread in Tanzania.
Some witchdoctors say that the body parts of people with albinism are effective when making magic charms, leading to the killing of dozens of albinos in recent years.
Mr Mwasapile's concoction is made from herbs and water, which he sells for 500 Tanzanian shillings (five cents; 3p).
Medical experts in Tanzania are investigating both whether it is safe and if it has any medicinal properties.
When she visited Mr Mwasapile's home near the northern Loliondo town recently, the BBC's Caroline Karobia found 6,000 people waiting to see the retired Evangelical Lutheran Church of Tanzania (ELCT) pastor.
_51865366_img_6092.jpg
The queues stretched for 26km (16 miles) down the road
They are waiting for days by the roadside and outside his home in Samunge village without shelter, clean water or toilets.
As word has spread in the past month of the pastor's supposed ability to cure any ailments, some people have even been taken out of hospital by their relatives who believe they are more likely to be cured by Mr Mwasapile.
Some of these have died before seeing him, while others are reported to have died after taking his concoction.
Extra police have been deployed to the area to control the huge crowds, some of whom have travelled from neighbouring countries such as Kenya and even further afield.
Mr Mwasapile asked for the break following a meeting with local officials.

Wewe ndo mwenyewe mwayaaa!
 
ndio !! Babu anaua!sio kitu cha kusema taratibu.anawahadaa watu kuwa anatibu magonjwa sugu,amesababisha mass hysteria watu wametoroka mahospitali kuufuata unabii hewa!kwa nini tusiseme babu ni muuaji?
Naomba mungu afe kiongozi mmoja ili watu watambue kuwa babu hafai.
Aisee umenifurahisha sana yaaniView attachment 25819
 
.... babu hana shida SHIDA NI KWAMBA INATAKIWA BABU AWEKE WAZI TU KWAMBA YEYE NI MGANGA WAJADI (naogopa kusema) pia watu wanatakiwa watambue kuwa huo unaweza kuwa mtego mbaya wa shetani ili awaue watu!

Usiogope Mkuu....kwa mujibu wa sheria za Tanzania (The Traditional and Alternative Medicines Act, 2002) Babu ni Traditional Health Practitioner, bahati mbaya sheria imeandikwa kizungu. Lakini kwa tafsiri nyepesi yes, kisheria anaangukia kwenye kundi la 'waganga wa jadi' (Traditional Health Practitioners).
 
Nashukru umeanza kujenga hoja nzuri zisizo na jaziba! Ukweli umeuleta kama ulivyo! Ila nikuulize kwa jinsi dawa ilivyotolewa na masherti yake:-
Mtu anaruhusiwa kunywa na kwenda kuendelea na dawa za kurefusha maisha?

Kama msururu ni mrefu kiasi hicho wasiwasi wangu ni kwamba, Tiba ya Babu inaonyesha wazi kuwa ni kama tiba zingine za kawaida za waganga wa jadi kwa sababu haizai matunda ya nguvu za Kimungu zaidi! tuliona wakati wa Yesu kuna sehemu alibadili mbinu na kutumia za kiustadi zaidi ili ziponye wengine kwa haraka! Sasa unataka kuniambia Mungu amezidiwa nguvu kuwahudumia watu mpaka wanafika kilomita 50?? Na kama Babu anasema watu hawa bado ni tone wengine zaidi watakuja unategema nini kama kashindwa kuwatosheleza hawa tone kwa muda mfupi? Bado nasita ila Loliondo itaua watu wengi sana!

mkuu kwa mujibu wa maelezo ya babu ni kua kaagizwa kutengeneza tiba ya magonjwa sugu na sio kuhubiri injili.na ndio maana haijalishi imani yako kidini as long as utaamini kua uponyaji upo utapona.wanaokufa inawezekana kabisa hawakua na imani maana sharti moja wapo ni imani juu ya ile huduma na sio Imani juu ya udini wako bali imani kua ukinywa dawa yake utapona.so usilaumu kua huduma ya babu hasaidii kuzalisha matunda ya nguvu ya kiMungu coz hayo sio makusudio yake.makusudio ni kutoa tiba kwa magonjwa sugu kwa binadamu yeyote atakae amini.mtu yeyote atapona mradi tu awe na imani ndio maana huitaji kua mlokole ili dawa ya babu ikuponye, ni imani tu!!
 
Nawewe unajiendea tu lakini unaonekana tu usivyoweza kugundua vitu! Hahahaaaa sasa unafikiri wewe kwanini Yesu alienda kumponya tena? Hii ni wazi kwamba Yesu aliona kuwa kuchelewa kwake ndiko kulikosababisha kifo cha Lazaro ndio maana aliumia akatoa na machozi kwani aliona kweli kuchelewa kwake kumesababisha hayo! Sasa akaona afute makosa kwa kumponya na ikawa hivyo! Sasa waliochelewa kupata dawa Loliondo wakafa wameponywa au wamezikwa?? Angalia impact baada ya tukio ndio ujaji!

my goodness! yani sasa umefikia kiwango cha kusema Yesu alifanya makosa? Tafadhali sana...kubali kuwa huelewi hii ishu. Hapa utaishia kukufuru bure! Sema tu mimi sio mjuzi, na haya ni mawazo yangu. Kwisha. Usijaribu kabisa kueleza vitu usivyojua. Utakosa uzima wa milele bure. Kama huamini Loliondo na unaona kuna vitu basic kwenye biblia vimevunjwa...sawa weka wazi. lakini kama unaanza kwa kuweka story nusu nusu za biblia, utaishia kukufuru kabisa.
Yesu alijua toka mwanzo kuwa atamfufua Lazaro. Huu ulikuwa ni mmoja wa miujiza yake mikubwa. Na 'kuchelewa' kwake (siku tatu) kulikuwa ni njia ya kutimiza huo muujiza.
But my point remains, kuwa watu wanaweza kufa wakiwa wanasubiri msaada Mungu. Huwezi sema kuwa kufa ukiwa njiani ina maana kuwa Mungu hayupo involved. It may suggest that but its not a strong suggestion. Wewe fanya sala muombe Mungu akufunulie ukweli juu ya hii ishu.
 
my goodness! yani sasa umefikia kiwango cha kusema Yesu alifanya makosa? Tafadhali sana...kubali kuwa huelewi hii ishu. Hapa utaishia kukufuru bure! Sema tu mimi sio mjuzi, na haya ni mawazo yangu. Kwisha. Usijaribu kabisa kueleza vitu usivyojua. Utakosa uzima wa milele bure. Kama huamini Loliondo na unaona kuna vitu basic kwenye biblia vimevunjwa...sawa weka wazi. lakini kama unaanza kwa kuweka story nusu nusu za biblia, utaishia kukufuru kabisa.
Yesu alijua toka mwanzo kuwa atamfufua Lazaro. Huu ulikuwa ni mmoja wa miujiza yake mikubwa. Na 'kuchelewa' kwake (siku tatu) kulikuwa ni njia ya kutimiza huo muujiza.
But my point remains, kuwa watu wanaweza kufa wakiwa wanasubiri msaada Mungu. Huwezi sema kuwa kufa ukiwa njiani ina maana kuwa Mungu hayupo involved. It may suggest that but its not a strong suggestion. Wewe fanya sala muombe Mungu akufunulie ukweli juu ya hii ishu.
Wacha kukosoa na amplify hoja inayolenga! Kama Yesu aliambiwa mapema kwenda kumombea Mgonjwa na akachelewa unadhani ilikuwa haki? Na lazima uelewe si kila mtu akisema kukosea amamaanisha unavyodhamiria wewe! Unaonekana hata hujui maana ya kufuru! Vipi? mbona hujengi hoja iliyokuwa inaendelea?? Yesu alienda kumponya Lazaro hata kama alikufa babu amemponya nani aliyekufa?? BABU MUUAJI TU! WIZI WA NAMNA HIYO HAUVUMILIKI!
 
Haya ndiyo alikuambia Babu au wewe mwenyewe umejitungia?

Mbona anawaambia watu watumie dawa nyingine? Mnajitungia na kuanza kuamini....

Babu hawezi kukataza mtu kutumia hiyo dawa ya kurutubisha mwili uliochakaa.....

Kwani umeambiwa Babu anatoa KINGA? Babu anaponya tu, basi.

Unataka kusema babu kasema pia ukinywa dawa basi USILE maana UMEPONA? Ila dawa ni kama Chakula.

Hakuna aliyechakachua ila wenyewe MNAJIDANGANYA na mwisho mnaamini MATAPISHI YENU.

Kasitisha matibabu kwa WIKI moja sasa mtapumua maana HOSPITAL zilikuwa zimekauka, hahahaaaa........
Acheni kupamba hoja zilizowazi! Hairuhusiwi kunywa ARV ukinywa dawa ya Babu haya ndiyo masharti ya awali labda kama mmeyachakachua sawa!
 
Acheni kupamba hoja zilizowazi! Hairuhusiwi kunywa ARV ukinywa dawa ya Babu haya ndiyo masharti ya awali labda kama mmeyachakachua sawa!

Usipende kutumia chanzo kimoja cha habari ili kufikia conclusion,

Kwa bongo hii ambayo vyombo vya habari vinaandika habari kutokana na matakwa binafsi ama kutia chumvi habari kwa maslahi binafsi, unatakiwa kufuatilia vyombo vingi vya habari kabla hujatoa hukumu.

Hii habari ya kwamba babu kazuia waathirika wa VVU kutotumia ARVs unaikuza tu ili kujenga hoja dhidi ya babu, ama umepotoshwa na chanzo chako cha habari.

Nitakupa mfano mmoja tu, jana kwenye kipindi cha njia panda kinachorushwa na clouds fm kila jumapili kuanzia saa nane kamili mchana, kuna binti anaitwa jack ametoa ushuuda wake, alikwenda loliondo kupata kikombe na yeye ni muathirika.

Alikanusha kabisa hii propaganda kwamba babu amewazuia wagonjwa wa ukimwi kuendelea kutumia ARVs, babu ameendelea kuwasisitizia wale wote walioathirika waendelee na tiba zao hadi hapo watakapopima na kuthibitika kupona.Na si waathirika wa ukimwi tu, bali pia na wanaougua maginjwa mengine hawajazuiliwa kuendelea na tiba zao.
 
Wacha kukosoa na amplify hoja inayolenga! Kama Yesu aliambiwa mapema kwenda kumombea Mgonjwa na akachelewa unadhani ilikuwa haki? Na lazima uelewe si kila mtu akisema kukosea amamaanisha unavyodhamiria wewe! Unaonekana hata hujui maana ya kufuru! Vipi? mbona hujengi hoja iliyokuwa inaendelea?? Yesu alienda kumponya Lazaro hata kama alikufa babu amemponya nani aliyekufa?? BABU MUUAJI TU! WIZI WA NAMNA HIYO HAUVUMILIKI!

hahaha...umeanza na kubadilisha maneno. Kubali hujui tu na huna jipya.
babu amesema anaponya au kikombe na imani ndio vinaponya? Yeye kapewa maagizo specific. Hayo mengine ni juu yenu. Kama unataka ku-disprove, onyesha kuwa kikombe na imani haviponyeshi. Sio unakuja hapa na story nyingi.
 
Ya kaisari mpe Kaisari na ya MUNGU mpe MUNGU! Huwezi kumjaribu BWANA MUNGU wako! MUNGU alimtoa YESU auawawe kwa ajili yetu, MUNGU pia alileta gharika na kuteketeza kizazi chote na kumuacha NUHU na wanyama aliowateua, Mungu pia anasema kila roho itaonja mauti ili ifike kwake. Haina maana kuwa ukinywa kikombe cha Babu hautakufa na kuwa utaishi milele! Babu haombei bali anakupa dawa unywe hivyo tusimbeze umati wote huu unaoenda kwake unaonesha wazi yote ni ya kweli kama ni uongo ungejulikana mapema na watu wangesitisha! Kumbuka huwezi kumjaribu BWANA MUNGU wako!!!!
 
mkuu kwa mujibu wa maelezo ya babu ni kua kaagizwa kutengeneza tiba ya magonjwa sugu na sio kuhubiri injili.na ndio maana haijalishi imani yako kidini as long as utaamini kua uponyaji upo utapona.wanaokufa inawezekana kabisa hawakua na imani maana sharti moja wapo ni imani juu ya ile huduma na sio Imani juu ya udini wako bali imani kua ukinywa dawa yake utapona.so usilaumu kua huduma ya babu hasaidii kuzalisha matunda ya nguvu ya kiMungu coz hayo sio makusudio yake.makusudio ni kutoa tiba kwa magonjwa sugu kwa binadamu yeyote atakae amini.mtu yeyote atapona mradi tu awe na imani ndio maana huitaji kua mlokole ili dawa ya babu ikuponye, ni imani tu!!

Naomba kuuliza, Hivi mpaka mtu afunge safari na kwenda huko kwa Babu, bado anakuwa hana Imani tu?
Mpaka anakunywa hiyo dawa bado anakuwa hana Imani tu?
Dah, Huyu Mungu wa babu mi nina mashaka naye!!!!
 
Ya kaisari mpe Kaisari na ya MUNGU mpe MUNGU! Huwezi kumjaribu BWANA MUNGU wako! MUNGU alimtoa YESU auawawe kwa ajili yetu, MUNGU pia alileta gharika na kuteketeza kizazi chote na kumuacha NUHU na wanyama aliowateua, Mungu pia anasema kila roho itaonja mauti ili ifike kwake. Haina maana kuwa ukinywa kikombe cha Babu hautakufa na kuwa utaishi milele! Babu haombei bali anakupa dawa unywe hivyo tusimbeze umati wote huu unaoenda kwake unaonesha wazi yote ni ya kweli kama ni uongo ungejulikana mapema na watu wangesitisha! Kumbuka huwezi kumjaribu BWANA MUNGU wako!!!!

Hmethod kaka kumbe Babu haombei tena?
Siku mbili zilizopita ilikuwa inasemekana humu anaombea kwa jina la Yesu!!!
Na tukisafari na hoja ya wengi wape, sijui kama itafaa kwa kila kitu aisee.
Ujue ni mateso na matatizo tu, ndio yanayowafanya watu wahangaike hivi.
 
Wacha kukosoa na amplify hoja inayolenga! Kama Yesu aliambiwa mapema kwenda kumombea Mgonjwa na akachelewa unadhani ilikuwa haki? Na lazima uelewe si kila mtu akisema kukosea amamaanisha unavyodhamiria wewe! Unaonekana hata hujui maana ya kufuru! Vipi? mbona hujengi hoja iliyokuwa inaendelea?? Yesu alienda kumponya Lazaro hata kama alikufa babu amemponya nani aliyekufa?? BABU MUUAJI TU! WIZI WA NAMNA HIYO HAUVUMILIKI!

Mwenye uwezo na mamlaka ya kufufua wafu ni Mungu pekee.

Kama mnataka kumlinganisha babu na Mungu hapo ndipo mnaposhindwa hata kuyaelewa maandiko matakatifu, badala yake mnajaribu kujificha kwenye maandiko matakatifu kumshambulia babu kwa sababu ya chuki zenu binafsi.

Ndugu yangu usiwe unasoma Biblia kama unavyosoma gazeti la udaku, unahitaji uwezo wa KiMungu kuisoma na kuielewa Biblia.
 
Si rahisi sana kama sio mtu wa rohoni kuyatambua mambo kama haya! Babu haui, dawa yake haiui, serikali haiui, wagonjwa hawajiui ila Hii ni mbinu kubwa ya shetani kuua watu!

Labda nikuulize swali la msingi hapa, mtu wa rohoni ni nani? na utamtambuaje?
 
Hivi kuna KUPONYA mtu ALIYEKUFA?

Mie nilikuwa najua kuwa Mtu aliyekufa akipata UHAI basi ni kuwa KAFUFUKA.

Na kwa maana hiyo, huko siyo kuponya bali KUFUFUA.

Kweli mie Mnyamwezi sifahamu KISWAHILI.
 
Nionavyo mimi ni kwamba huduma anayoifanya babu sii ya kawaida kama wanavyofikiri wengi. Kuna watu wanamjadili babu kwa muono wa kuhubumia watu mia kadhaa. Kwa babu kuna mkusanyiko usio kawaida kwa maana ya wingi bila support ya miundombinu stahiki. Hata hivyo serikali imekubali kumonitor zoezi la kuhakiki idadi itakayokuwa haimuelemii babu kwa siku. Na kutengeneza mazingira ikiwa ni pamoja na vyoo na mashimo ya taka na mahema ya kujikinga mvua. Kama barabara zingepitika na watu kumfikia babu kwa siku moja tu nafikiri kusingekuwa wingi wa vifo.
Sitaki nifikiri kwamba wale waliokufa wamepungukiwa na imani, kwani kutoroka hospital na kwenda kuunga foleni ni imani tosha. Tatizo ni mazingira tu. Kwa watu wa imani na hasa ya ukristo tunapaswa kufahamu kuwa hata wana wa Israel walipotoka Misri Musa aliwaambia kwamba wanaelekea nchi ya ahadi. Jangwani mchana walifunikwa na wingu jua lisiwapige na usiku wingu la moto liliwaangazia nuru lakini hata hivyo pamoja na uwepo mkuu wa Mungu walikufa mbele zake na kuzikwa jangwani. Tena tunaambiwa kati ya wote waliondoka misri wakiwa na akili za kupambanua ni wawili tu walioingia Kaanani.
Binafsi mimi namwona babu kama mtu anaeupendeza moyo wa Mungu na wanadamu pia kwa kuwa pamoja na muujiza aliopewa hana kiburi cha kujisikia. Anasikilizana na viongozi wa kitaifa na kuafikiana nao katika masuala mihimu, bila kuyaasi maono aliyodai kupewa na Mungu.
Tujiulize pia kwamba hospitali zote za tanzania ndugu wamewatorosha wagonjwa wao tena wale sugu kuelekea kwa babu, kwa hali ya kawaida tu tukiondoa ushabiki na chuki, hatutarajii vifo? Maana waliopaswa kuwekwa mortuary zote nchini kwa wakati huo wapo njia moja kuelekea kwa Babu.
.
 
Hii mada ya Loriondo siipendi kwa sababu haina mambo endelevu zaidi ya kuleta utata wa matusi, na kejeli kwenye maanadiko ya Mungu. Ebu, acha wafu wawazike wafu wenzao. Kama wewe una akili timamu unamchukua mgonjwa mahututu umpeleke kwa babu, obvious kuna mawili kufa unasubiri dawa au hujafika.

ACHA WAFU WAWAZIKE WAFU WENZAO.
 
Back
Top Bottom