Live kutoka Diamond Jubilee: Utoaji tuzo kwa waandishi bora 2011 - JK Mgeni rasmi

michezo hawamo hata kina bwigane, swedi mwinyi, maulid kitenge, etc? nasikia majina mapya!!
 
shughuli nzima inaendeshwa ovyo ovyo kabisa'mtu ameshika mic huku anapewa laptop huku anapewa tuzo
 
mbona hata nathan anachora kama masoud au kisa hana jina..



Mimi namfahamu Nathan kwa siku nyingi kidogo, na kwa mtamzamo wangu nilitaraji kuona wote wawili wakichuana hapo (Masoud na Nathan) lakini tumesikia majina mageni kabisaaaaa!!
 
Idea ya wa kuwa na hizi awards ni nzuri sana lakini naomba nitoe mapungufu;
1. Uendeshaji wa shughuli uko hovyo (sina maneno mazuri ya kutumia) ni hovyo kabisa. 3 or 2 nominees wanatajwa, wote wanatakiwa waende mbele then ndio mshindi anatangazwa? Kwa nini wasisome hao nominees then mshindi tu ndio anaenda mbele/jukwaani kupokea zawadi?

2. Clips za hao nominees hazioneshwi hivyo watazamaji hawawezi kuelewa ni habari gani hasa ilishinda.

3. Stage arrangement iko miguu chini sijui nianze wapi! Utaratibu mbovu sana. Hivi nyingi wanahabari hamuoni sehemu nyingine wanafanyaje kwenye awards ceremenies kama hizi?

4. Mshindi hapewi muda wa kutoa shukrani! hili nalo ni kituko. yuko mwanamama anaongea kama kafungiwa kengele. Mhehereshaji mwenziwe kabaki bubu!

5. Kwa kuangalia inaonekana kama hii ni 'formal event' Sielewi ni madharau au kutojua, lakini kuna watu wamevaa kama alikuwa anaenda kununua mboga mboga, hasa wanaume. Wanawake wamejitahidi lakini wanaume kwa kweli kazi ipo.
 
nitawapatia live update kutoka hapa Diamond Jubilee ambako muda mfupi ujao waandishi kadhaa nchini watatuzwa kwa kutambua mchango wao katika kuhabarisha jamii kwa mwaka 2011.

pia atakuwepo mwandishi bora wa jumla ,huyu atalamba takribani sh milioni 7


wageni wanaingia kwa wingi

nadokezwa kuwa TBC1 watakuwa live


Updates
Najulishwa hapa kuwa pia Rais atatumia muda huo kutoa hotuba.
Mwandishi bora wa jumla ni kati ya hawa-David Azaria (Habari Leo, Mwanza); Neville Meena (Mwananchi ,Dar ) Joseph Bura(TBC Taifa ,Dar) na Polycarp Machira(The Citizen ,Dar).

1.mpiga picha bora
ni Khamis Said kutoka uhuru

2.mchoraji bora wa kibonzo
ni Nathan Mpangala
alichora katuni iliyoonesha wabunge wakijongeza posho huku wanananchi wakisota

3.Utawala bora gazeti
Nevile meena-Mwananchi

4.utawala bora tv
emmanuel buohera-itv

5.utawala bora radio
Noel Thomson

6.Habari za Malaria-Gazeti
Audax Mutiganzi-Rai

7.Habari Malaria-Radio
Gelvas Hubile-TBC

8.Mwandishi bora Michezo-gazeti
Iman man
9.Habari za michezo -radio
Abdala Majura
10.Habari michezo Tv
Anuary Mkama

11.Habari za Watu wenye ulemavu-gazeti
David Azaria

12.Watu wenye ulemavu -tv
Lekoko-Channel ten

13.Mwandishi wenye ulemavu-radio
Tuma Dandi

14.Jinsia -Gazeti
Nasra Abdalah-Tanzania daima

15.Habari za Ukimwi-Gazeti
Elias Msuya

16.Habari za UKIMWI-Radio
Beatrice Nangawe

17.Habari za Afya
Sharifa Karokola
Hizi tuzo batili haiwezekani gazeti la uhuru na mzalendo hayamo!
 
Mimi namfahamu Nathan kwa siku nyingi kidogo, na kwa mtamzamo wangu nilitaraji kuona wote wawili wakichuana hapo (Masoud na Nathan) lakini tumesikia majina mageni kabisaaaaa!!
Wamemkomoa Masoud Kipanya!! Wameniudhi kweli! Masoud huwa anagusa pasipo gusika alafu wanamtema kirahisi hivi wanadhani tutakaa kimya!! Kwanini wanahabari wanaolilia uhuru wa habari wanakosa weledi? Kweli wamenichefua! Hata kwa washindani?
 
Idea ya wa kuwa na hizi awards ni nzuri sana lakini naomba nitoe mapungufu;
1. Uendeshaji wa shughuli uko hovyo (sina maneno mazuri ya kutumia) ni hovyo kabisa. 3 or 2 nominees wanatajwa, wote wanatakiwa waende mbele then ndio mshindi anatangazwa? Kwa nini wasisome hao nominees then mshindi tu ndio anaenda mbele/jukwaani kupokea zawadi?

2. Clips za hao nominees hazioneshwi hivyo watazamaji hawawezi kuelewa ni habari gani hasa ilishinda.

3. Stage arrangement iko miguu chini sijui nianze wapi! Utaratibu mbovu sana. Hivi nyingi wanahabari hamuoni sehemu nyingine wanafanyaje kwenye awards ceremenies kama hizi?

4. Mshindi hapewi muda wa kutoa shukrani! hili nalo ni kituko. yuko mwanamama anaongea kama kafungiwa kengele. Mhehereshaji mwenziwe kabaki bubu!

5. Kwa kuangalia inaonekana kama hii ni 'formal event' Sielewi ni madharau au kutojua, lakini kuna watu wamevaa kama alikuwa anaenda kununua mboga mboga, hasa wanaume. Wanawake wamejitahidi lakini wanaume kwa kweli kazi ipo.[/QUOT

Frankly nakubaliana na wewe, ndio maana hapo juu nimesema wako dis-organised sana!!
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Nilitarajia kwa habari za biashara tena kwa TBC no body could beat Stanley Ganzel.... lakini amekuja mtu hata sikumbuki kama nimewahi kumuona..... sijui nikalale tu!!
 
Ni kama vile hayumo mle ukumbini,kwani lazima ahudhurie yeye..kakaa na baadhi ya makanjanja..nchimbi yumo..nae ataenda ku2nuku baadae,yupo anatabasam tu na kupiga miayo ya usingizi...KWELI TASISI YA URAIS INADHALILIKA.makamu wa rais angemwakilisha pale.
 
Hivi wameishiwa hata pesa ya kukaalika kakijana kamoja angalau kawaimbie kidogo!! Maana toka wameanza kutoa zawadi hakuna mapumziko! na wanaongea tuuuuuuuuuu.......... Frankly nahisi waliopo hapo labda wanaenjoy kampani na kukaa pamoja lakini sio event yenyewe!!
 
sasa kafunikwa nini?
Nayeye alikuwa anashindania.

Hebu tulia uandike ulichotaka kuandika kwa ufasaha ili tupate point za kuchangia.
Umekurupuka mno.
 
Nilitarajia kwa habari za biashara tena kwa TBC no body could beat Stanley Ganzel.... lakini amekuja mtu hata sikumbuki kama nimewahi kumuona..... sijui nikalale tu!!

Nadhani mwandishi anatakiwa yeye mwenyewe a-submit kazi yake kwenye mashindano thena majaji wanachagua mshindi. Hivyo inawezekana Stanley na Kipanya hawakupeleka kazi zao.

Hata hivyo mimi naona huu mfumo unaweza kuboroshwa kwa MCT wenyewe kuanza kufuatilia habari na kujua ni ipi nzuri. Maana ukiangalia hizi awards huwelewi ni kitu gani washindi wamefanya. Totally out of tune! Labda Neville Meena lakini wengi wao sijui wameandika nini cha maana?
 
Event kwenye tv tu inaboa! Ningekuwa pale ningeagiza kreti la bia kwa hela yangu nile monde weeee then huyo home!
 
sasa kafunikwa nini?
Nayeye alikuwa anashindania.

Hebu tulia uandike ulichotaka kuandika kwa ufasaha ili tupate point za kuchangia.
Umekurupa mno.

umekuwa gongo leo wewe pale matejoo.hangover mbaya kaa u2lie.NAMAANISHA KUWA KAMA VILE rais hayupo ukumbini
 
Km ni movie basi hii ni ya kihindi maana imeanzia mwisho, watu wameanza kula kabla ya sherehe, wageni wamechoka wanatamani kuondoka kwa vile washashiba
 
Back
Top Bottom