Elections 2010 Live From TV's: Upigaji wa kura, matokeo na yatokanayo

Mpaka naondoka kituoni hali ilikuwa kama hivi:

attachment.php



attachment.php
 

Attachments

  • DSC00008.jpg
    DSC00008.jpg
    48.9 KB · Views: 231
  • DSC00009.jpg
    DSC00009.jpg
    40.5 KB · Views: 227
Damn so wht were they doing for all these dayz???????????? With all the technology that the promised kwa nini isiwe kwamba unaandika sms with your reg no and then inakupa kituo cha kupiga kura! Kma mambo ndiyo hivi kupiga kura nje ya nchi mpaka 2050!
 
Wakati naondoka kituoni saa 1:45 asubuhi hali ilikuwa hivi:

attachment.php
 

Attachments

  • DSC00010.jpg
    DSC00010.jpg
    37.5 KB · Views: 203
Nilipiga Kura yangu saa 1.30 asubuhi nikiwa mtu wa 5.

Uhakiki wa wapiga kura unachua muda:

Ofisa wa Kwanza wa NEC anapokea kadi ya mpiga kura na kuangalia kama jina lako lipo.

Ofisa wa pili anaangalia kama uko katika daftari ya wapiga kura. Akiona jina anaoanisha na picha na kisha mawakala wa vyama nao wanashuhudia. Baada ya hapo anasoma namba yako na niliona mawakala wa CUF, CCM na CHADEMA wananakili namba ya mpiga kura.

Baada ya hapo unaenda kwa msimamizi wa kituo, anakagua kadi yako na kisha anaisoma kwa sauti na mawakala wanahakiki. Kisha anakupa karatasi tatu. Ya blue nyuma - Urais, Nyeusi nyuma - Ubunge na nyeupe nyuma - Madiwani. Anazikunja na kisha kugonga mihuri miwili kwa nyuma katika kila karatasi. Kisha anakupatia.

Kisha unaenda katika sehemu iliyoandaliwa kupiga kura kuna pen hapo, unakunjua karatasi zako na kuweka vema kwa mgombea unayemtaka na kisha unazikunja.

Ukimaliza: Blue-Urais unatumbukukiza katika sanduku la kura za Rais, Black-sanduku la Ubunge na Nyeupe sanduku la mwadiwani.

Ukimaliza hapo kuna mdau wa NEC anakupaka wino katika kidole kidogo kisha unaondoka.

mimi katika kituo nilichoenda huku Tegeta bahari beach utaratibu ulikuwa hivi:

  1. ukifika kituoni unapanga mstari mita kama 20 toka maafisa wanaoendesha upigishaji kura walipo.. wanaume mstari wao, wanawake mstari wao
  2. Afisa wa Polisi anaigiza wanawake 7 na wanaume 7..
  3. kwa kuwa kituo changu kilikuwa na sehemu 7 za kupigia, ukiingia either unaenda direct kwenye sehemu yako (kama ulifika kabla ya leo na kunakiri namba ya sehemu ya wewe kupigia --- naamanisha namba 1 mpaka 7) kama hujui unatakiwa uende sehemu majina yalipobandikwa na kutafuta jina lako na namba ya kituo.. KUMBUKA MAJINA YAMEPANGWA ALPHABETICALLY
  4. ukishajua NAMBA YA sehemu unayotakiwa kupigia kura, karani mwongozoji atakuelelekeza wapi pa kwenda
  5. ukifika sehemu ya kupiga mstari.. utapanga mstari.. kama utakuta kuna wengine mbele yako
  6. zamu yako ikifika unaenda kwa karani wa kwanza ambaye unampa kadi yako, anahakiki jina lako kwenye rejister, na kisha anataja kwa sauti ambapo mawakala wa vyama nimeona wanaandika kumbukumbu kwenye writing pad zao (ila mmoja nimeona kama anasinzia)..
  7. ukitoka hapo unaenda kwenye karani mwingine ambaye anaandika namba yako kwenye karatasi ya rejester (kipande kinachobaki kitabuni) na kisha kukuchania katarasi za kupigia kura
  8. then, unaenda kwenye kibanda cha kupigia kura
  9. ukishamaliza kupiga unatumbukiza kwenye box kwa kuzingatia rangi-- bluu ya raisi, nyeusi mbunge na nyeupe diwani
  10. ukishatumbukiza, karani mwingine anakuwekea wino mweusi
  11. baada ya hapo unaondoka kituoni
huo ndo utaratibu nilipitia... ila kasheshe moja nimeona kwa wasio jua kusoma.. nimeona kuna uwezekano mkubwa kudanganywa... kwa sababu wanaambiwa chagua mtu yeyote (minogoni mwa wapiga kura kama utakuwa hujaenda na mtu wa kukusaidia)

habari ndio hiyo!!
 
Ule uvumi kwamba ukiweka Tick kwa Slaa na baadaye ukikunja karatasi ile Tick inaamia kwa JK hakika si za kweli.

Mpangilio wa majina katika karatasi na hata karatasi yenyewe baada ya kuitafiti kwa muda haikuwa na na mwelekeo wa ukweli wowote.

Kitu kimoja ambacho nime-observe ni kuwa wasimamizi wote ni vijana wadogo sana na baada ya kuwahoji wawili watatu nimejiridhisha kuwa wengi Elimu yao inaweza kuwa haifiki ile ya Chuo.
 
mimi katika kituo nilichoenda huku Tegeta bahari beach utaratibu ulikuwa hivi:


  1. ukifika kituoni unapanga mstari mita kama 20 toka maafisa wanaoendesha upigishaji kura walipo.. wanaume mstari wao, wanawake mstari wao
  2. Afisa wa Polisi anaigiza wanawake 7 na wanaume 7..
  3. kwa kuwa kituo changu kilikuwa na sehemu 7 za kupigia, ukiingia either unaenda direct kwenye sehemu yako (kama ulifika kabla ya leo na kunakiri namba ya sehemu ya wewe kupigia --- naamanisha namba 1 mpaka 7) kama hujui unatakiwa uende sehemu majina yalipobandikwa na kutafuta jina lako na namba ya kituo.. KUMBUKA MAJINA YAMEPANGWA ALPHABETICALLY
  4. ukishajua NAMBA YA sehemu unayotakiwa kupigia kura, karani mwongozoji atakuelelekeza wapi pa kwenda
  5. ukifika sehemu ya kupiga mstari.. utapanga mstari.. kama utakuta kuna wengine mbele yako
  6. zamu yako ikifika unaenda kwa karani wa kwanza ambaye unampa kadi yako, anahakiki jina lako kwenye rejister, na kisha anataja kwa sauti ambapo mawakala wa vyama nimeona wanaandika kumbukumbu kwenye writing pad zao (ila mmoja nimeona kama anasinzia)..
  7. ukitoka hapo unaenda kwenye karani mwingine ambaye anaandika namba yako kwenye karatasi ya rejester (kipande kinachobaki kitabuni) na kisha kukuchania katarasi za kupigia kura
  8. then, unaenda kwenye kibanda cha kupigia kura
  9. ukishamaliza kupiga unatumbukiza kwenye box kwa kuzingatia rangi-- bluu ya raisi, nyeusi mbunge na nyeupe diwani
  10. ukishatumbukiza, karani mwingine anakuwekea wino mweusi
  11. baada ya hapo unaondoka kituoni

huo ndo utaratibu nilipitia... ila kasheshe moja nimeona kwa wasio jua kusoma.. nimeona kuna uwezekano mkubwa kudanganywa... kwa sababu wanaambiwa chagua mtu yeyote (minogoni mwa wapiga kura kama utakuwa hujaenda na mtu wa kukusaidia)

habari ndio hiyo!!

nilisahau hili..

ukienda kupiga kura hakikisha karatasi yako ya kupigia kura inapigwa muhuri sehemu ya nyuma.. muhuri unapigwa mbele yako,, isiyopigwa kura inaharibika
 
Baada ya briefing ya hapo juu, sasa naamia katika TV's kuwapa updates: ITV wako Live wanaohoji waandishi sehemu mbalimbali, , TBC pia wanarusha matangazo; , Channel 10 nao wako hewani na Star TV pia.

. . . . . . .
 
Baada ya briefing ya hapo juu, sasa naamia katika TV's kuwapa updates: ITV wako Live wanaohoji waandishi sehemu mbalimbali, , TBC pia wanarusha matangazo; , Channel 10 nao wako hewani na Star TV pia.

. . . . . . .


slaa.jpg
 
hivi TBC wanaumwa????? what a scrap? yaani wakati ITV wapo mitaani wanafuatilia mambo yanavyoendelea ... eti TBC wapo studio wanajadili jinsi vyombo vya habari vilivyokuwa vinaripoti na jinsi wagombea walivyokuwa wanatoa ahadi..... jamani leo ni upigaji kura kwa nini vyie TBC msiende mtaani.. si mnatumia kodi zetu jamani.. wewe MHANDO unafanya nini hapo... mbona uzoefu wa kufanya kazi BBC hausaidii hapa...

hongera ITV hongera STARTV...
 
According to ITV, vituo vingi vya Kigamboni mambo ni shwari. Kuna amani na utulivu.
 
Baada ya briefing ya hapo juu, sasa naamia katika TV's kuwapa updates: ITV wako Live wanaohoji waandishi sehemu mbalimbali, , TBC pia wanarusha matangazo; , Channel 10 nao wako hewani na Star TV pia.

Thanks Superman

Acid kasema TBC1 wapo biased.....ni kweli? wapo biased Kivipi?
 
Singida mambo shwari ila kuna kituo kimoja ambacho kuna wapiga kura hawajaona majina yao. Na kuna mzee anaojiwa anasema asaidiwe apate haki yake ya kupiga kura.
 
Baadaye leo tutashirikiana na BongoRadio kurusha matangazo ya ITV online!!!! sijui saa ngapi.. naenda kulala maana kuna kukesha kesho au maandalizi ya safari!!!
 
Back
Top Bottom