LIVE : Channel Ten - Mauaji ya Daud Mwangosi

Kumuua mtu kwa kiwango kile haiwezi kuwa bahati mbaya...

Mwangosi amekufa kifo cha kimkakati... Bahati mbaya ni Ile mikakati ya kijinga kabisa kiasi kwamba hata mtoto anajua hili ni la kupanga.

Familia ya Mwangosi isimame kidete ikisaidiwa na wataalamu wa sheria na haki za binadamu kudai haki.
 
Mkuu naamini kabisa unachokisema,very sad indeed!RPC aliona kwa macho yake akipigwa na polisi,na kama unavyojuwa,tayari walikuwa wamemkamata mwandishi mmoja,nadhani kwasababu walijuwa yeye ndo mwenyekiti wao,basi walijuwa lazima aende kujaribu kufahamu kulikoni akamatwe.Na polisi walipokuwa wakimpa kichapo,RPC anayemfahamu,akajidai hata hamfahamu,akayafumbia macho,sawa na pilato aliponawa mikono,wahunu wanaojiita polisi,wakammalizia pale pale.Mbele ya mchacho ya RPC na OCD,wakijuwa kuwa wanawafurahisha mabosi wao.Na kuna taarifa za waandishi waliokuwa wamejibanza kwenye kona,ambao walisikia polisi wakijigamba kuwa lazima wauwe siku hiyo,kumbe walijuwa kabisa ni nani wanakwenda kumwua?Then ccm bado wana balls za kusingizia amani tena?labda amani ina maana ya tofauti kwao.

yule askari aliyemwekea bunduki tumboni alishapewa kazi ya kummaliza Mwangosi,haiwezekani askari afanye vile wakati boss wake RPC akijaribu kumwokoa,nimefurahi kwa sababu hawakujua wapiga picha wanachukua kila tukio,taarifa tulizo nazo zinasema baadhi ya askari hawatoki pale na wameandaliwa kutoka background mbovu kabisa walikotoka,kumbuka kuna ile picha ya mwisho askari amesimama akimshangaa Mwangosi wakati ameshakufa??yule kwa roho yake asingeweza kufanya vile,aliwekwa kwenye lile kundi bila kujua mipango nini kinaendelea,yule aliyempiga bomu ndiye alitumwa kwa kazi ile maalam,amini usiamini sio askari wote wanafurahia mambo yanayofanywa na jeshi hili dhalimu,Mwisho wa huyu MwemA utakuwa kama wa Bilal,yote haya tunayajua kwa kuwa tunaona mbali kuliko waanavyofikiri
 
Subirin Postmoterm report kwanza nauhakika huyo mwandishi aliuliwa na dude fulan la ajabu sana lililorushwa na wafanya fujo toka mbeya!
Dude la ajabu ndo nini, jini au?. Polisi waache upumbavu wao, Mwangosi kauliwa na bomu la machozi alilolipuliwa nao na polisisiemu. Kuna mwananchi anayemiliki bomu la machozi?
 
Mwema hatoguswa na mtu yeyote yule,nadhani msilolijua ni kwamba muheshimiwa mwema ni shemeji yake mkuu wa kaya.subirini utawala dhalimu wa ccm uatakapoondoshwa ndiyo watashtakiwa hawa wauaji,polisi ni wauaji wakubwa wako watu wengi sana wanauwawa kila mara bila hao (polisi)wauaji kuchukuliwa hatua yoyote.
 
Kwa taarifa fupi kutoka Ebony Fm ya Iringa ni kwamba mwili wa marehemu utaagwa usiku huu nyumbani kwa marehemu maeneo ya Kihesa na kesho mwili utasafirishwa kuelekea Mbeya kwaajili ya mipango ya mazishi.
 
TAARIFA YA JUKWAA LA WAHARIRI (TEF)
KWA VYOBO VYA HABARI
KUHUSU KUUAWA KWA MWANDISHI DAUDI MWANGOSI

3. Kwa matukio ya aina hii, tunadhani wakati mwafaka kwa uongozi wa Jeshi la Polisi nchini kuwajibika, kuazia kwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa na uongozi wa Makao Mkuu, akiwamo Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Saidi Mwema.


8. Kwa maana hiyo, mbali na uchunguzi ambao utafanywa na polisi, tunatoa wito kwa Serikali kuunda chombo huru, ambacho kitabaini ukweli, na matokeo yake yatangazwe kwa umma, huku wahusika wa aibu hiyo wakichukuliwa hatua za kisheria. Tunasema hivyo, tukifahamu kwamba tayari kuna jitihada za kuficha ukweli na kueneza propaganda za uongo kuhusu tukio zima.


IMETOLEWA NA:


NEVILLE MEENA,
KATIBU MKUU – JUKWAA LA WAHARIRI TANZANIA (TEF)
SEPTEMBA 3, 2012

Hapana, hapana, hapana, kuwajibika pekee hakutoshi, wahusika wanapaswa kushitakiwa na kupewa adhabu stahiki kwa makosa waliyofanya.

Jukwaa la wahariri lilipaswa hata kukataa tume iliyoundwa na jeshi la polisi, kwani haiwezekani kutenda haki na kutokana na ushahidi eye witnesses Polisi ndiyo wahusika wakati RPC anatoa taarifa tofauti. Kuweka statement kuwa pamoja na tume ya polisi, ni dalili ya kuwa tayari kupokea matokeo ya tume hiyo. Sidhani kama ni sawasawa.
 
Dude la ajabu ndo nini, jini au?. Polisi waache upumbavu wao, Mwangosi kauliwa na bomu la machozi alilolipuliwa nao na polisisiemu. Kuna mwananchi anayemiliki bomu la machozi?

alishababu wanayo kibao kaka.....subiri report ya police utaona
 
Kajubi anasema baraza linataka kuanza kutoa mafunzo ya kuchukua taarifa kta mazingira hatarishi kwa kuwa mikutano ya siasa imekuwa sehem hatari, pia ameshauri wahariri kuanza kurinda wandishi wao

waende jeshini au? Reporters considered to be learned guys in their job. This is black and white murder; dont turn mwangosi a lab mouse. Angefanyaje ktk kundi la ffu kama hilo! Mkajanga and the whole lot seek'the truth and only truth. Labda hizo picha ni za kugushi..
 
alishababu wanayo kibao kaka.....subiri report ya police utaona
Sima uhakika kama ni kweli Al-shabaab wanaweza kutumia mabomu ya machozi ktk shughuli zao za kigaidi, ili iweje? Unategemea polisi hao hao waliomuua mwandishi wa habari watoe report ambayo ni fair?. Nashukuru hakuna ndugu yangu wa karibu anaefanya kazi hii ya polisi, ni afadhali ya panzi hutumia akili yake kujifikirisha kuliko polisi anayeamrishwa kila kitu hata kikiwa kibaya.
 
Kama na huu utakuwa ni upepo tu...na ukapita, basi watanzania itabidi tubadili mbinu za kudai haki zetu za msingi.
 
Du! tulitegemea jeshi letu baada ya kuingia Said Mwema, IGP, msomi,na aliyefanya shughuli za kimataifa,lingekuwa la kisasa lakini mambo yalinayofanyika na jeshi la polisi na yanayoendelea yameonyesha mapungufu makubwa kwa Mwema.Tunaendelea kusikiliza Channel 10!

Hivi Said Mwema ameishia darasa la ngapi?
 
The most important thing to discuss should be the secrets behind the series of killings on opposition rallies. Someone (perhaps high ranking gov officials) who is/are quite should be questioned now. Police receives orders, who gives orders?

That is simple! Its some body who has got authority on these armed forces! If not, why IGP and The minister of home affair are getting away with this without resigning as part of accountability?
 
yule askari aliyemwekea bunduki tumboni alishapewa kazi ya kummaliza Mwangosi,haiwezekani askari afanye vile wakati boss wake RPC akijaribu kumwokoa,nimefurahi kwa sababu hawakujua wapiga picha wanachukua kila tukio,taarifa tulizo nazo zinasema baadhi ya askari hawatoki pale na wameandaliwa kutoka background mbovu kabisa walikotoka,kumbuka kuna ile picha ya mwisho askari amesimama akimshangaa Mwangosi wakati ameshakufa??yule kwa roho yake asingeweza kufanya vile,aliwekwa kwenye lile kundi bila kujua mipango nini kinaendelea,yule aliyempiga bomu ndiye alitumwa kwa kazi ile maalam,amini usiamini sio askari wote wanafurahia mambo yanayofanywa na jeshi hili dhalimu,Mwisho wa huyu MwemA utakuwa kama wa Bilal,yote haya tunayajua kwa kuwa tunaona mbali kuliko waanavyofikiri

Aliyekwambia RPC alijaribu kumwokoa Mwangosi nani?

maana taarifa za habari ambazo waandishi wenzie wa habari ndo mashuhuda wa mauaji hayo, mmoja wao akihojiwa amesema wakati Mwangosi anapigwa kwa virungu na mateke, yeye alikimbilia gari la RPC kumsihi azuie vijana wake wasitishe kumshambulia jamaa, lakini anasema RPC alishusha kioo kumsikiliza kisha akapandisha na kuondoa gari kwa honi na ving'ora.

Shuhuda mwingine anasema ilifikia hatua alimwona askari mwenye nyota 3, akiingilia kile kipigo kumwokoa Mwangosi, na kwenye picha Nafikiri ndo Yule ambaye Mwangosi amemkumbatia, lakini peke yake haikuwezekana, anaonekana askari mwingine akinyooshea mtutu tumboni mwa Mwangosi, na mashuhuda wanaeleza kishindo kikasikika na nyama kutawanyika, huku yule askari aliyekuwa anajaribu kumwokoa jamaa nae akijeruhiwa vibaya miguuni.

Walikuwa, wanamtafuta... Sasa wamempata, tena bila kujali kuna watoto wanaomtegemea, mke, n.k.

Huu ushemeji wao kwa bro inaonekana utatukosti vibaya sana. Maana sasa hivi wanatamba tu...
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom