Listening Audio Booth:John Malecela: Alichoongea

Learned Jasha
umesema ukweli mtupu.
Serikali haina nia ya dhati kupambana na mafisadi ndo maana vyombo vya habari vinavyopiga vita dhidi ya mafisadi vinaundiwa zengwe ili vibanwe....
 
Andrew Chenge yupo ktk Kamati ya Maadili ya CCM,

Sasa Chenge atakuwa na Moral Authority gani kukemea uovu na wizi kwa viongozi wa CCM?
 
Mzee (Jumanne) John Malecela, aliwahi kuwaambia watanzania waliokuwa wakilalamikia huduma mbovu za Shirika la Reli wakati yeye akiwa Waziri wa Mawasilano na Uchukuzi kwamba waende kuzimu "they go to hell". Sasa wakati umefika wa kumwambia "Mzee hovyo Malecela, go to hell" Sasa hivi hana la maana la kusema. Angekuwa mtu mwenye busara ilimpasa kuacha mambo ya siasa na akapumzika Mtera akibaki mshauri tu.
 
Huyu akapimwe akili kwanza tusije poteza muda wetu kumbe mwenzetu wadudu wameshaingia kichwani
 
God help Tanzania - Babu anaongelea CCM wakati Watanzania wanatangaziwa NCHI KUWA GIZA, MARA MAJI HAMNA, MARA AJALI BARABARANI ZINAZIDI, MARA FOLENI ZINAZIDI, MARA SEHEMU NYINGINE YA NCHI KUNA NJAA, MARA MAJI HAYATOKI NA HATA KWENYE MADIMBWI HAMNA,WATOTO WANATOKA SHULE HAWANA USAFIRI, WENGINE VIJIJINI WANATEMBEA MILES, WENGINE WANAKAA CHINI WAKITAFUTA ELIMU, WALIMU HAWANA NYUMBA ZA KUISHI, VIJIJINI WAALIMU WANAKUWA OVERWORKED NA MISHAHARA HAWAIPATI ON TIME (just to mention a few keros in Tanzanian's life) Yeye kwa vile anatibiwa anapotaka, chakula anacho tele na cha kumwaga, usafiri kwake poa, anaweza kuita press conference nyumbani kwake - kuwasumbua tu Waandishi kwa faida ya politics zake ......... yaani ajiulize WATANZANIA TUNA ADHA NGAPI?? JAMANI SIE HATUNA INTEREST YA SIASA ZAO TUMECHOKAAAAAAAAAAAA - TUNAHITAJI MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA - OH GOD COME AND RESCUE US FROM MAFISADI OF THIS COUNTRY -
 
...duh!huyu mzee kweli hana mpya.bora ajitoe tu kwenye siasa.hana lolote jipya.....!
sielewi hasa nini cha maana alitaka kuongelea,yaani mkutano mzima wa habari badala ya kuongelea habari za maana sijui hata anaongelea nini!!?
 
Wakuu, Malecela anazungumza kama makamu mwenyekiti wa CCM, ni muhimu sisi tuifahamu lugha yake kwanza...Huyu sii kiongozi wa serikali na hana nguvu huko..
Pili, alichosema ni ukweli mtupu.. kwani kama kweli hawa jamaa wanaotaka kumeguka CCM watoke! hizi habari za kutuzuga hata sisai wananchi hatufahamu wanachosimamia ni kutuzidishia hasira tu.. Waondoke CCM, wananchi tujue moja kama ni hao Mafisadi wanatishia kuondoka waondoke.. na kama kuna wale wanaojiona wasafi na CCM sio mahala pao - waondoke...
Jamani ndilo sisi wananchi tunachotaka kuona na tunatarajia mtu yeyote mwenye kujali maslahi ya Taifa atakuwa amechukua maamuzi ya maana isipokuwa wale wanaotaka kutubeza..sio kuitisha vikao kila siku kujitangaza wajkati bado wamo ndani ya chungu wakipikwa..

Makamu wa CCM ni Msekwa.

Yeye anazungumza kama kichaa fulani tu. Baada ya kupigwa chini na wana CCM wenzake huyu babu bado tu anajipendekeza kwa vijana kama akina JK??? Nafikiri akili yake imezeeka, ndiyo maana retirement age imewekwa 60 - 65 years. Sasa ukipitiliza sana ujue uwezakano wa kuchanganya mahesabu ni mkubwa ndiyo sababu kuna watu wanafikiria may be kakichaa kamempata au ni mambo ya whisky na Konyagi. Hata kwenye Bible wanasema umri wa mtu ni miiaka sabini. He is leaving on borrowed time now. Akili yake haiko katika ulimwengu huu. Mfano wake ni watu kama akina Mugabe jinsi walivyopungukiwa uwezo wa kufikiri kwa kufikiria kwamba wao ni bora kuliko wengine.

Anyway, simulaumu yeye ila wale waliomueka pale awawakilishe. CCM Wameamua kumtuma babu yao apige hadithi kwa wajukuu............!!!!!!

Ananikumbusha kipindi cha mama na mwana.
 
Sasa Mzee Malecela Unajichanganya,

Umesema hutaki malumbano kwenye vyombo vya Habari, wakati na wewe umeenda kulumbana huko huko, kama hutaki kulumbana ungeongelea huko huko CCM,

To hell, mapambano mbele nyuma mwiko,

Magazeti andikeni mpaka kieleweke.
 
Kuhani, kwa hili Mzee Malecela yuko sahihi. Mwalimu aling'atuka mara mbili, katika nafasi mbili tofauti. Mwaka 1985 aling'atuka na kuachia u-rais wa nchi, lakini aliendelea kubaki na kofia ya Mwenyekiti wa Chama. Mwaka 1992 aling'atuka Uenyekiti wa Chama (CCM). Hayo maneno aliyasema wakati anang'atuka Uenyekiti.

Ambacho nashindwa kumuelewa yeye na viongozi wenye hulka kama yake, ni kwa nini wanadhani kuwa CCM hii ya sasa ni "madhubuti"? Kwa kuwa tu wanashinda chaguzi haina maana kuwa ni madhubuti! CCM baada ya kuwa kwenye siasa/utawala kwa miaka takribani 55 (1954 - 2009), bado kina wanachama milioni 4 tu na kinasumbuliwa na vyama vilivyo na uhai usiozidi miaka 15! Huu ni mpambano wa mtu mwenye malaria vs mwenye kipindupindu, hakuna madhubuti hapo.

Mkuu Kiungani,

Mambo kama haya ndivyo yanavyotakiwa. Unaona mwenzako amekosea, unamweka sawa kwa facts ulizonazo. Na sisi wengine tusiojua tunaelimika.

Amandla............
 
Mkuu Kiungani,

Mambo kama haya ndivyo yanavyotakiwa. Unaona mwenzako amekosea, unamweka sawa kwa facts ulizonazo. Na sisi wengine tusiojua tunaelimika.

Amandla............

Nakuunga mkono FM. Lakini sahihisho dogo kutokana na kumbukumbu zangu Nyerere aling'atuka CCM mwaka 1990. Wakati wanapitisha vyama vingi mwaka 1992 Mwalimu Nyerere alialikwa tu. Tena katika ushauri wake kwa CCM ilikuwa lazima wakubali mfumo wa vyama vingi. Ni Malecela huyo huyo aliyesema kwamba wale watakaohama CCM 'they be left out in cold'
 
Duh, mzee wa watu kazungumza kwa nia njema tu, naona wabongo hamchangamkii hoja zake. Hamkipendi Chama?
 
Kuhani, kwa hili Mzee Malecela yuko sahihi. Mwalimu aling'atuka mara mbili, katika nafasi mbili tofauti. Mwaka 1985 aling'atuka na kuachia u-rais wa nchi, lakini aliendelea kubaki na kofia ya Mwenyekiti wa Chama. Mwaka 1992 aling'atuka Uenyekiti wa Chama (CCM). Hayo maneno aliyasema wakati anang'atuka Uenyekiti.

Ahsante Kiungani.

Mambo ya kuwekana sawa katika usahihi wa facts ndio yenyewe.

Ni hivi. Vyanzo na kumbukumbu zangu vinasema by 1990 Nyerere alikuwa ameshang'atuka vyeo vyote viwili.

NEW WORLD ENCYCLEOPIDIA: After the Presidency, Nyerere remained the Chairman of CCM until 1990, when Ali Hassan Mwinyi took over. In one of his famous speeches during the CCM general assembly, Nyerere said in Swahili "Ninang'atuka..."

BEYOND CAPITALISM v. SOCIALISM IN KENYA AND TANZANIA
Joel D. Barkan, 1994, page 31:
After stepping down as president in 1985, Nyerere continued as chairman of CCM until August 1990

WIKIPEDIA: Ali Hassan Mwinyi (born May 8, 1925, Kivure, Coast Region, Tanzania) was the president of the United Republic of Tanzania from 1985 to 1995. He also was chairman of the ruling party, the Chama Cha Mapinduzi (CCM) from 1990 to 1996.

ENCYCLOPEDIA BRITANICCA Nyerere continued as chairman of the CCM until 1990.

WIKIPEDIA Julius K. Nyerere: Re-elected president in 1970, 1975, and 1980, he retired in 1985 but continued as chairman of the Chama cha Mapinduzi (Revolutionary Party), created by the merger of TANU and Zanzibar's ruling party, until 1990.

Mzee Malecela na wewe Kiungani mnasema Nyerere aliondoka na kusema anang'atuka wakati vyama vingi vinaanza, akiwa waziri mkuu, mwaka 1992. Sasa Kiungani, kabla hatujakurupuka kusahihishana labda tuendelee kutafuta jibu la uhakika, Nyerere aling'atuka lini na vyama vingi vilianza lini? Malecela should know better.

i296_Malecela.jpg"
 
Nakuunga mkono FM. Lakini sahihisho dogo kutokana na kumbukumbu zangu Nyerere aling'atuka CCM mwaka 1990. Wakati wanapitisha vyama vingi mwaka 1992 Mwalimu Nyerere alialikwa tu. Tena katika ushauri wake kwa CCM ilikuwa lazima wakubali mfumo wa vyama vingi. Ni Malecela huyo huyo aliyesema kwamba wale watakaohama CCM 'they be left out in cold'

Sasa nani yuko sahihi? Kuhani au Kiungani?
 
Sijaona mahali ambapo Kuhani anasema maneno ya "mimi nang'atuka" yalitolewa lini?!

Yalitolewa mwaka 1985 ama 86,nakumbuka gazeti la UHURU nikiwa mtoto mdogo tu,na ile picha imenikaa maana ni dingi yangu alisimama kununua hilo gazeti na maneno ya mtaani yakawa ni kwamba hakutaka kuachia madaraka bali kulikuwa na kama shinikizo flani.
 
Wakati mwingine huwaga nashindwa kuelewa kwa nini watu tunabishana wakati records zipo wazi. Invisible, unaweza kututafutia audio ya spichi ya Mwalimu aliposema "anang'atuka"?

Kutoka Wikipedia.....

Positions held
1954 A Founder Member of TANU
1958-1960 Member of the Legislative Assembly in the first elections in which Africans were allowed to vote.
1958 Leader of the Opposition in Parliament.
1960 Chief Minister of the first Internal Self-Government Administration.
1961 Prime Minister of the first Government of Independent Tanganyika
1962 Elected President of Tanganyika when it became a Republic.
1963-1970 Chancellor of the University of East Africa.
1964-1985 President of the United Republic of Tanzania.
1970-1985 Chancellor of University of Dar-es-Salaam.
1977-1990 Chairman of Chama Cha Mapinduzi which was formed by a merger between TANU and the Afro-Shiraz Party of Zanzibar. CCM was born in Zanzibar on February 5, 1977.
1984-1985 Chancellor of Sokoine University of Agriculture.
1985: Retired from Presidency.
1999: Died of leukemia in London and was buried in Musoma - Tanzania.
 
- What a Great thinkers, kwa muda mfupi niliokuwemo hapa nimegundua kuwa viongozi watano wa Tanzania wanapendwa sana hapa JF, nao ni Rais Kikwete, DK. Malecela, Mheshimiwa Lowassa, Mh. Rostam, na Mama kilango.

- Saafi sana wakuu tunakula elimu ya bure kwa pembeni wekeni elimu nzito hii kwa faida ya taifa.


William.
 
Hivi Jonh aliwahi kwenda shule akapewa PhD? Au alitunukiwa?

Mwal. aliwahi naye kunukiwa PhD ila hakuwahi kupenda kuitwa Dr. Nyerere!
 
Back
Top Bottom