Baadhi ya matatizo yanayotukabili watanzania tulio wengi ni haya:
1. Wengi wetu ni waoga. Tunaiogopa system na watawala wake. Kifupi tuna nidhamu za woga! hatutaki kuonekana "wakorofi mbele ya wakubwa"
2. Wengi wetu tumeshakata tamaa na maisha kwa sababu ya ugumu wa hali ya maisha. kuna wale wanaoamini kwamba Tanzania hapa ilipo haiwezi tena kurudi kwenye hali ya kawaida..kwa hiyo yeyote anayejaribu kupambana na system "anapoteza mda" na (hawa wako wengi-wasomi kwa wakulima-hata humu JF wamo)
3. Wengine wanaamini kwamba jukumu la kuikomboa na kuijenga Tanzania iliyo bora na yenye manufaa kwa kila raia litafanywa na "wengine".."Mimi simo". Hawa ni wabinafsi..as long as Iam fine..I dont care the rest.
4. Wengine tunasikia neno Ufisadi lakini kwa sababu tumebahatika kuwa katika maisha mazuri "hatu-ifeel" impact ya huu ufisadi. MATOKEO YAKE..TUMESHALIZOEA HILI NENO NA TUNALIONA KAMA NENO LA KAWAIDA TUU... Kifupi we dont know what is happening.
5. Waliobaki wako kwenye comfort zone..wameridhika na hawataki status quo ibadilike. Hawa ndo wako karibu na watawala (akina Salva et al). Wako against any change.
6. Na mwisho kuna wale wachache wanaoamini kwamba iwe leo au kesho TZ yenye neema inawezekana kama kila mtu akitimiza wajibu wake. Hawa wanaamini kwamba maadui wa Tanzania yetu ni wale wanaopewa dhamana ya kuwaongoza wenzao na wanawageuka along the way.
Sasa sijui wewe uko wapi...
Umesahau kuna wakina SHY ambao wako migingoni kwa mafisadi wakiwatetea kutokana na kuendekeza NJAA ZAO bila kujali maslahi ya nchi.