Lipumba Slams IMF's Stance On EPA Scam

Ochu

JF-Expert Member
May 13, 2008
975
47
Lipumba aishangaa IMF




MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, amelishangaa Shirika la Fedha Duniani (IMF), kummwagia sifa, Rais Jakaya Kikwete, kwa jinsi anavyoshughulikia suala la wizi wa fedha katika Akaunti ya Malipo ya Nje (EPA).

Lipumba ameonyesha hali hiyo, ikiwa ni siku moja tu imepita, baada ya Mkurugenzi wa IFM, Dominique Strauss-Khan, kutoka Washington, Marekani, kummiminia sifa Rais Kikwete kwa jinsi uongozi wake ulivyosimamia urejeshwaji wa fedha za EPA, zilizoibwa kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu jana, mwenyekiti huyo, alisema kitendo cha Rais Kikwete kutotumia ipasavyo madaraka yake kukabiliana na wezi na wahujumu uchumi wa nchi, hakipaswi kupongezwa kwani ni ukiukwaji wa utawala wa sheria.

Profesa Lipumba ambaye ni mtaalamu wa mambo ya uchumi, alisema kashfa ya EPA, haijawahi kutokea katika benki yoyote duniani.

“Tukio kama hilo halijawahi kutokea katika benki yoyote ile duniani, lakini IFM wanapongeza hatua za rais za kutowachukulia hatua wezi hao, hili kwa kweli linanishangaza,” alisema Lipumba.

Akikaririwa na vyombo vya habari juzi, Mkurugenzi wa IMF, alisema tukio kama la wizi uliofanyika BoT, linaweza kutokea popote duniani, jambo ambalo Profesa Lipumba alipingana nalo.

Mapema mwezi uliopita, CUF iliandaa mkutano na waandishi wa habari ambapo Lipumba aliwalaumu wahisani wakubwa wa Tanzania kama Benki ya Dunia (WB) na IMF, kwamba wamekuwa nyuma kuisaidia serikali katika vita dhidi ya ufisadi na badala yake wamekuwa wakiisifia kwa kila jambo, hali inayochochea kuongezeka kwa vitendo vya ufisadi.

Akilihutubia Bunge mjini Dodoma Agosti 21 mwaka huu, Rais Kikwete alisema serikali imekamata mali za wamiliki wa kampuni 13 kati ya 22, waliothibitika kuhusika na uchotaji wa sh bilioni 133 kwenye Akaunti ya EPA, ambapo kiasi cha sh bilioni 53.7 zimekusanywa, huku hati zao za kusafiria zikishikiliwa.

Rais Kikwete alisema watuhumiwa hao wameongezewa siku 72 kuanzia Agosti 21 ili wawe wamerejesha sh bilioni 74, baada ya muda huo kupita watachukuliwa hatua za kisheria.

Kutokana na hatua hiyo, viongozi wa kambi ya upinzani na makundi kadhaa ya wanaharakati, walipinga, na kuitafsiri kuwa ni sawa na kutangaza msamaha kwa wezi hao.


source: Tanzania Daima
 
Date::10/6/2008
Profesa Lipumba adai IMF inachochea ufisadi
Na Kizitto Noya
Mwananchi

MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF) Profesa Ibrahim Lipumba amelituhumu Shirika la Fedha Duniani (IMF) kwamba linachochea na kuendekeza rushwa na ufisadi nchini.

Profesa Lipumba alitoa shutuma hizo nzito upitia barua yake aliyomwandikia Mkurugenzi Mtendaji wa IMF, Dominique Strauss-Khan.

Katika barua hiyo ambayo jana aliamua kuigawa kwa vyombo vya habari, Profesa Lipumba alidai amebaini kwmba IMF ambayo imekuwa ikiheshimika kwa miaka mingi, ina mkono katika matukio ya ufisadi yanayoendelea hapa nchini.

Alisema amebaini hilo kutokana na shirika hilo kufumbia macho matukio kadhaa ya ufisadi nchini na kitendo chake cha kumpongeza Rais Jakaya Kikwete kwa hatua ya kuwapa muda wa kurejesha fedha mafisadi wa EPA badala ya kumponda.

“Sikusoma popote zaidi kujiridhisha kwamba ulisema, niliamini kwamba taarifa iliyotolewa na gazeti la serikali hapa nchini, The Daily News kuhusu mazungumzo yako na Rais Kikwete ni sahihi. Kauli yako inachochea rushwa na kuendekeza ufisadi Tanzania,” alisema Profesa Lipumba katika barua hiyo ya Septemba 26, mwaka huu yenye kumbukumbu namba CUF/AK/ DSM/MKT/001/IMF/2008.

Septemba mosi mwaka huu, gazeti la Daily News lilimkariri Mkurugenzi Mtendaji wa IMF akimsifia rais Jakaya Kikwete kwa hatua alizochukua dhidi ya watuhumiwa wa ufisadi wa EPA.

Kwa mujibu wa gazeti hilo, katika mkutano wao uliofanyika kwenye hoteli ya Omni Shoreham, nchini Marekani, Mkurugenzi huyo wa IMF alisema “Tumeridhirika sana na kukupongeza jinsi ulivyoshughulikia suala la EPA. Suala hilo linaweza kutokea popote duniani lakini cha msingi ni jinsi ulivyolishughulikia. Na umelishughulikia vizuri kwa umahiri na utalaam wa hali ya juu. IMF sasa imefunga suala la EPA,”

Profesa Lipumba alisema kauli hiyo ya IMF, inachochea rushwa kwani ni ukweli usiofichika kwamba serikali imeshindwa kushughulikia suala hilo kwa umahiri wala utaalam wa hali ya juu kama mkurugenzi huyo anavyodai.

Akifafanua alisema: “Serikali haikuwa wazi kuueleza umma jinsi fedha hizo zilivyochotwa, watuhumiwa bado hawajulikani kwa majina na makampuni hayajafikishwa mahakamani,”

Kwa mujibu wa Profesa Lipumba kitendo cha Rais Kikwete kutaka watuhumiwa wa ufisadi wa EPA warejeshe fedha, kinaleta shaka kuwa hatawafikisha mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili, kitendo ambacho ni kinyume na utawala bora na sheria.

Alisema rais Kikwete amewasamehe watuhumiwa wa EPA na kauli yake haionyeshi nia thabiti ya serikali kuwafikisha mahakamani hivyo kumsifu kwamba amelishughulikia suala hilo kwa umahiri sio sahihi.

Aliitaka IMF kuongeza umakini katika kupitia hali ya uchumi wa Tanzania katika vikao vyake vijavyo na kuishikiza serikali kusimamia mapendekezo ya ripoti ya awali iliyokagua akaunti ya EPA mwaka 2006 iliyotaka nchi iache kuendelea kulipa madeni hayo kwa kuwa yamepitwa na wakati.

Katika hatua nyingine Profesa Lipumba jana ameeleza kuwa msimamo wa chama chake kuandamana kwa lengo la kuishinikiza serikali itaje majina ya watuhumiwa wa EPA na kuwafikisha mahakamani, uko palepale.

Aliwaambia waandishi wa habari kuwa maandamano hayo yamepangwa kufanyika Oktoba 6 mwaka huu kuanzia Buguruni kupitia barabara ya Uhuru hadi viwanja vya Mnazi Mmoja ambako viongozi wakuu wa CUF watahutubia.

Profesa Lipumba alibainisha kuwa ingawa polisi wameshajulishwa kuhusu maandamano hayo, baadhi ya watendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala wameanza kuyawekea mizengwe kwa kuzuia viwanja hivyo.

Alisema baada ya CUF kumwandikia barua mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala kumjulisha juu ya maandamano hayo kuishi katika viwanja vya Mnazi Mmoja, aliwajibu kwa barua kwamba viwanja hivyo haviruhusiwi kwa shughuli za kisiasa.
 
Date::10/6/2008
Profesa Lipumba adai IMF inachochea ufisadi
Na Kizitto Noya
Mwananchi

MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF) Profesa Ibrahim Lipumba amelituhumu Shirika la Fedha Duniani (IMF) kwamba linachochea na kuendekeza rushwa na ufisadi nchini.

Profesa Lipumba alitoa shutuma hizo nzito upitia barua yake aliyomwandikia Mkurugenzi Mtendaji wa IMF, Dominique Strauss-Khan.

Katika barua hiyo ambayo jana aliamua kuigawa kwa vyombo vya habari, Profesa Lipumba alidai amebaini kwmba IMF ambayo imekuwa ikiheshimika kwa miaka mingi, ina mkono katika matukio ya ufisadi yanayoendelea hapa nchini.

Alisema amebaini hilo kutokana na shirika hilo kufumbia macho matukio kadhaa ya ufisadi nchini na kitendo chake cha kumpongeza Rais Jakaya Kikwete kwa hatua ya kuwapa muda wa kurejesha fedha mafisadi wa EPA badala ya kumponda.

“Sikusoma popote zaidi kujiridhisha kwamba ulisema, niliamini kwamba taarifa iliyotolewa na gazeti la serikali hapa nchini, The Daily News kuhusu mazungumzo yako na Rais Kikwete ni sahihi. Kauli yako inachochea rushwa na kuendekeza ufisadi Tanzania,” alisema Profesa Lipumba katika barua hiyo ya Septemba 26, mwaka huu yenye kumbukumbu namba CUF/AK/ DSM/MKT/001/IMF/2008.

Septemba mosi mwaka huu, gazeti la Daily News lilimkariri Mkurugenzi Mtendaji wa IMF akimsifia rais Jakaya Kikwete kwa hatua alizochukua dhidi ya watuhumiwa wa ufisadi wa EPA.

Kwa mujibu wa gazeti hilo, katika mkutano wao uliofanyika kwenye hoteli ya Omni Shoreham, nchini Marekani, Mkurugenzi huyo wa IMF alisema “Tumeridhirika sana na kukupongeza jinsi ulivyoshughulikia suala la EPA. Suala hilo linaweza kutokea popote duniani lakini cha msingi ni jinsi ulivyolishughulikia. Na umelishughulikia vizuri kwa umahiri na utalaam wa hali ya juu. IMF sasa imefunga suala la EPA,”

Profesa Lipumba alisema kauli hiyo ya IMF, inachochea rushwa kwani ni ukweli usiofichika kwamba serikali imeshindwa kushughulikia suala hilo kwa umahiri wala utaalam wa hali ya juu kama mkurugenzi huyo anavyodai.

Akifafanua alisema: “Serikali haikuwa wazi kuueleza umma jinsi fedha hizo zilivyochotwa, watuhumiwa bado hawajulikani kwa majina na makampuni hayajafikishwa mahakamani,”

Kwa mujibu wa Profesa Lipumba kitendo cha Rais Kikwete kutaka watuhumiwa wa ufisadi wa EPA warejeshe fedha, kinaleta shaka kuwa hatawafikisha mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili, kitendo ambacho ni kinyume na utawala bora na sheria.

Alisema rais Kikwete amewasamehe watuhumiwa wa EPA na kauli yake haionyeshi nia thabiti ya serikali kuwafikisha mahakamani hivyo kumsifu kwamba amelishughulikia suala hilo kwa umahiri sio sahihi.

Aliitaka IMF kuongeza umakini katika kupitia hali ya uchumi wa Tanzania katika vikao vyake vijavyo na kuishikiza serikali kusimamia mapendekezo ya ripoti ya awali iliyokagua akaunti ya EPA mwaka 2006 iliyotaka nchi iache kuendelea kulipa madeni hayo kwa kuwa yamepitwa na wakati.

Katika hatua nyingine Profesa Lipumba jana ameeleza kuwa msimamo wa chama chake kuandamana kwa lengo la kuishinikiza serikali itaje majina ya watuhumiwa wa EPA na kuwafikisha mahakamani, uko palepale.

Aliwaambia waandishi wa habari kuwa maandamano hayo yamepangwa kufanyika Oktoba 6 mwaka huu kuanzia Buguruni kupitia barabara ya Uhuru hadi viwanja vya Mnazi Mmoja ambako viongozi wakuu wa CUF watahutubia.

Profesa Lipumba alibainisha kuwa ingawa polisi wameshajulishwa kuhusu maandamano hayo, baadhi ya watendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala wameanza kuyawekea mizengwe kwa kuzuia viwanja hivyo.

Alisema baada ya CUF kumwandikia barua mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala kumjulisha juu ya maandamano hayo kuishi katika viwanja vya Mnazi Mmoja, aliwajibu kwa barua kwamba viwanja hivyo haviruhusiwi kwa shughuli za kisiasa.


Hao ndio watanzani. Wanaona matatizo na wana-react kutokana na wakati uliopo. Sio wengine wakiona matatizo wanataka kurudi kwenye Ujima.
 
Huyu naye keshaishiwa
angeanza na bilateral agreements kama tulizo nazo na waingereza kupitia DFID ambao wana chochea ufisadi zaidi Tanzania kuliko hao IMF

mchumi mzima anaboa
 
Huyu naye keshaishiwa
angeanza na bilateral agreements kama tulizo nazo na waingereza kupitia DFID ambao wana chochea ufisadi zaidi Tanzania kuliko hao IMF

mchumi mzima anaboa

GT.
Nadhani ingekuwa bora zaidi kama ungetufahamisha kuhusu hizo bilateral agreements tulizonazo hasa ya DFID tuweze kujua jinsi gani ufisadi umejikita.
 
Civic United Front national chairman Ibrahim Lipumba yesterday criticised the International Momentary Fund (IMF) over its approval of Tanzania's war on corruption.

Prof Lipumba said the opposition party had been 'shocked' by reports that the IMF recently praised the Government's handling of the Sh133 billion EPA scandal.

The CUF chairman has written to IMF managing director Dominique Strauss-Kahn to protest the manner in which the institution viewed good governance in Tanzania.

The letter was copied to President Jakaya Kikwete and other development partners. In the letter, Prof Lipumba, who is an economist, said they were not satisfied with measures taken by the Government in dealing with the EPA scandal suspects.

Speaking in Dar es Salaam yesterday, Prof Lipumba said IMF must not support President Kikwete's government because measures taken so far 'are not enough'.

On September 1, the IMF was quoted in the local media as saying that it was satisfied with the way the Government was handling the EPA scandal in which the Bank of Tanzania made dubious payments totalling Sh133 million to 22 shadowy firms.

Mr Strauss-Kahn repeated IMF's position when he recently met President Kikwete in the US.

The IMF director was reported as saying: "We are satisfied and congratulate you for the way you handled the issue. This thing can happen anywhere in the world. What is important is the way it is being handled. And you have handled it very well, with competence and professionalism of highest order. The EPA case is now closed as far as IMF is concerned."

But Prof Lipumba said the Government has not been transparent in informing the public about the looting of public funds through the EPA account.

"It is high time the IMF showed that it is supporting Tanzania to fight grand corruption and not supporting minor steps it must make sure all the money is returned," he said.

President Kikwete told Parliament in August that suspects in the EPA scandals were required to return cash paid to them irregularly by October 31 of face prosecution.

Prof Lipumba said the President's decision to give more time to those implicated to return the money was a sign of failure.

"Giving them more time is treating them like ordinary people who have borrowed money from saccos (savings and credit cooperative societies) these are thieves twho must be prosecuted," he said.

Prof Lipumba warned that moving the EPA account from BoT to a commercial bank would prevent auditors from certifying whether the funds had been recovered or not.

"It's highly suspicious that funds recovered from EPA suspects should be deposited outside BoT, which is supposed to be the custodian of State funds."

Prof Lipumba added that CUF was planning to hold a peaceful demonstration on Thursday to press for the revelation of the names of EPA suspects and their prosecution.

"The aim is to let the President know that his handling of EPA suspects is contrary to the people's wishes these people must be made to face the full force of the law."
By Beatus Kagashe
hearder1.jpg
 
Huyu poor profesa amechoka kufikiri..

Kikwete ameamua kutokuwachukulia hatua za kisheria watu waliohusika na EPA, skandali ambalo yeye alionyesha bungeni kwamba lilikuwa ni ufisadi. Kwa maneno mengine amewasamehe.

IMF imesema Kikwete ame handle vizuri scandle la EPA.

Profesa Lipumba akasema IMF wanachochea ufisadi kwa kumpongeza Kikwete kwa sababu hizo hatua za Kikwete hazitoshi.

Sasa huyu "poor profesa" amechoka vipi kufikiri hapo ?
 
Huyu poor profesa amechoka kufikiri..

unajua kuna mtu aliwahi kuniuliza idadi ya marais duniani wanaoitwa ma professa nikashindwa kuwataja hata mmoja labda OBAMA akiwa rais maana university of Chicago wamesema alikuwa ni professor
PH2008033100939.jpg

Huyu Lipumba kusema ukweli ni disgrace na alizidi kuwa disgrace pale alipokuwa akikampeni nchi za Scandinavia zitukatie misaada in the 90's

saya alot about where his priorities are

ngja tukishamaliza na Mbowe itabidi tuhamie kwa hili kubwa jinga
 
Kikwete ameamua kutokuwachukulia hatua za kisheria watu waliohusika na EPA, skandali ambalo yeye alionyesha bungeni kwamba lilikuwa ni ufisadi. Kwa maneno mengine amewasamehe.

IMF imesema Kikwete ame handle vizuri scandle la EPA.

Profesa Lipumba akasema IMF wanachochea ufisadi kwa kumpongeza Kikwete kwa sababu hizo hatua za Kikwete hazitoshi.

Sasa huyu "poor profesa" amechoka vipi kufikiri hapo ?


You are missing the point
kagombea urais 1995 kashindwa

kagombea tena 2005 kashindwa

sasa bado anataka kugomea urais

sasa kama kweli angekuwa na akili na alitaka awe taken serious then ilitakiwa akae pembeni awapishe wenzie.

Nimesema angetuletea info jinsi DFID TANZANIA wanavyochochoea ubadhirifu na ufisadi ningemwona wa maana lakini Lupumba comes across as another useless professors tulionao ambaye at most he is good for nothing really
 
unajua kuna mtu aliwahi kuniuliza idadi ya marais duniani wanaoitwa ma professa nikashindwa kuwataja hata mmoja labda OBAMA akiwa rais maana university of Chicago wamesema alikuwa ni professor
PH2008033100939.jpg

Huyu Lipumba kusema ukweli ni disgrace na alizidi kuwa disgrace pale alipokuwa akikampeni nchi za Scandinavia zitukatie misaada in the 90's

saya alot about where his priorities are

ngja tukishamaliza na Mbowe itabidi tuhamie kwa hili kubwa jinga

Kumbe hili lijamaa ni mashoto...
 
You are missing the point
kagombea urais 1995 kashindwa

kagombea tena 2005 kashindwa

sasa bado anataka kugomea urais

sasa kama kweli angekuwa na akili na alitaka awe taken serious then ilitakiwa akae pembeni awapishe wenzie.

Nimesema angetuletea info jinsi DFID TANZANIA wanavyochochoea ubadhirifu na ufisadi ningemwona wa maana lakini Lupumba comes across as another useless professors tulionao ambaye at most he is good for nothing really

Anhaa, kumbe mlikuwa mnaongelea criticisms za jumla jumla mlizonazo dhidi ya Lipumba. Oh yeah, hata mimi nina misgivings zangu dhidi yake, haswa hilo la kuwa mgombea wa kudumu wa CUF. Nilifikiri mnaongelea hili lililoletwa kwenye mada hapa, ambalo naona Lipumba yuko picture perfectly correct:

Kikwete kasamehe wahusika wa alicholionyesha Bunge kuwa ni ufisadi. IMF ikampongeza Kikwete kwa jinsi alivyo handle skandali la EPA. Profesa Lipumba akasema IMF wanachochea ufisadi kwa kupigia debe hatua ambazo hazitoshi. Exquisite point.

Nyinyi mnasema Profesa kachoka kufikiri. Kumbe mnaongelea yenu mengine. Yes, to the extent that you were just venting unrelated frustrations then I missed the point, you are right.
 
Last edited:
Anhaa, kumbe mlikuwa mnaongelea criticisms za jumla jumla mlizonazo dhidi ya Lipumba. Oh yeah, hata mimi nina misgivings zangu dhidi yake, haswa hilo la kuwa mgombea wa kudumu wa CHADEMA. Nilifikiri mnaongelea hili lililoletwa kwenye mada hapa, ambalo naona Lipumba yuko picture perfectly correct:

Kikwete kasamehe wahusika wa alicholionyesha Bunge kuwa ni ufisadi. IMF ikampongeza Kikwete kwa jinsi alivyo handle skandali la EPA. Profesa Lipumba akasema IMF wanachochea ufisadi kwa kupigia debe hatua ambazo hazitoshi. Exquisite point.

Nyinyi mnasema Profesa kachoka kufikiri. Kumbe mnaongelea yenu mengine. Yes, to the extent that you were just venting unrelated frustrations then I missed the point, you are right.


U have no clue on what ur talking abt.. yes! its shows clearly ur unrelated frustrations!
 
Ukiona mzungu anakusifia usifikiri wewe ni mahiri sana bali ndondocha lake, usishangae imf kumsifia kikwete kuchukua hatua dhidi ya epa, huu ndo undondocha wenyewe,ingekuwa ulaya au marekani watuhumiwa wa epa wangepewa muda kurudisha pesa walizoiba?
 
Benki ya Dunia yataka mafisadi wabanwe
Na Ramadhan Semtawa

BENKI ya Dunia (WB), imesema inatarajia kuona serikali inachukua hatua zaidi za kupambana na ufisadi, ili kujijengea imani zaidi kwa wahisani.

Kauli hiyo ya WB imekuja wakati wananchi wakitaka hatua zaidi zichukuliwe dhidi ya watuhumiwa wa ufisadi, wakiwamo watuhumiwa wa ufisadi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu (BoT).

Akizungumza jijini Dar es Salaam juzi wakati wa maswali kwa waandishi, Mchumi Mkuu wa benki hiyo nchini, Paulo Zacchia, alisema Tanzania imekuwa ikifanya vizuri katika mapambano dhidi ya ufisadi.

Zacchia alisema BoT na serikali zimekuwa zikichukua hatua za makusudi katika kupambana na ufisadi, lakini mategemeo ni kuona hatua hizo zinaendelea.

"Tunaridhishwa na hatua kubwa zinazochukuliwa na Benki Kuu na serikali katika kupambana na rushwa, jambo la msingi ni kuendeleza zaidi hatua hizo," alisema Zacchia.

Akifafanua kuwa hakuna nchi duniani ambayo haina rushwa au ina rushwa kwa kiwango cha asilimia sifuri ndiyo maana benki yao na hata Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) imekuwa zikijikita katika kusaidia mapambano hayo.

"Hakuna nchi unaweza kusema ina kiwango cha rushwa asilimia sifuri, kila nchi rushwa ipo, kitu kikubwa ni kuzidi kuongeza rasilimali kupambana nayo," alisisitiza.

Alisema hata Marekani na nchi nyingine duniani bado rushwa ipo, ila jambo la msingi ni kuongeza nguvu katika kupambana na tatizo hilo.

Alisema kwa kufahamu hilo, ndiyo maana benki ya dunia na washirika wengine wamekuwa wakisisitiza umuhimu wa kuimarisha utawala bora.

Mkuu huyo wa Uchumi wa WB, alisema katika kusimamia hilo nchi 14 wafadhili zinazochangia katika Mfuko Mkuu wa Bajeti (GBS), zilikuwa zimesitisha kwa muda misaada yao kwa Tanzania lakini baadaye zikatoa.

Alisema hatua hiyo inatokana na kuridhishwa na hatua kubwa zinazochukuliwa na serikali katika kupambana na rushwa.

"Mtaona kwamba wahisani 14 wanaochangia katika GBS walikuwa wamesitisha kwa muda michango yao katika bajeti, lakini waliamua kutoa baada ya kuridhishwa na hatua aza serikali katika kupambana na rushwa," alisisitiza.

Katika siku za karibuni, Tanzania ilijikuta katika wakati mgumu kuweza kupata misaada ya bajeti kutoka wahisani 14 wanaochangia katika GBS, kutokana na kutakiwa ichukue hatua zaidi dhidi ya mafisadi.

Hata hivyo, kutokana na hatua mbalimbali zinazochukuliwa na serikali chini ya Rais Jakaya Kikwete, wahisani hao wameanza kumimina misaada yao baada ya kuridhishwa.
 
Back
Top Bottom