Lipumba Na Mbowe yupi kiongozi bora na makini?

Emc2

JF-Expert Member
Sep 26, 2011
16,808
16,836
Hapa naomba tujadiliane kati ya hawa wawili bila kutumia hasira. Na ninaomba mtu akikomenti atoe sababu.
1. Kiongonzi shupavu mwenye mtazamo chanya si kigeugeu.
2. Aweza akawa Rais na kuiongoza nchi vyema.
3. Sio dictator.
Haya jamani tujadiliane.
 
kwa mujibu wa vigezo vyako, yeyote kati yao anaweza kuwa.ila kwa kuongezea tu, tunahitaji mtu mwenye mtazama sahihi wake binafsi na chama chake (maana ndicho kitakachoongoza nchi), awe mpambanaji kwelikweli, asiyehadaika na magamba, mwenye 'political will' ya kweli. mchapakazi. asiyeonea haya mafisadi. katika vigezo hivyo, mbowe anaibuka kidedea.
kumb. urais sio 'level ya elimu' nk. ni dhamira ya dhati ya kuliletea taifa mabadiliko stahiki. kati ya hawa wa2, wanatanguliwa na Dr. slaa. huyu ni kiboko.
 
kwa mujibu wa vigezo vyako, yeyote kati yao anaweza kuwa.ila kwa kuongezea tu, tunahitaji mtu mwenye mtazama sahihi wake binafsi na chama chake (maana ndicho kitakachoongoza nchi), awe mpambanaji kwelikweli, asiyehadaika na magamba, mwenye 'political will' ya kweli. mchapakazi. asiyeonea haya mafisadi. katika vigezo hivyo, mbowe anaibuka kidedea.
kumb. urais sio 'level ya elimu' nk. ni dhamira ya dhati ya kuliletea taifa mabadiliko stahiki. kati ya hawa wa2, wanatanguliwa na Dr. slaa. huyu ni kiboko.

Mimi sijamtaja Slaa kwani Slaa ndio nani huyo?
 
Unamfananisha Mbowe kamanda na Lipumba wapi na wapi? Mbowe ni jembe la ukweli.
Halafu mbona umeanza kwa kujihami coz unajua majibu ni yepi. Yan unadhani mtu ukiwa na elimu kubwa ndo unauwezo wa kuongoza? Tazama chama lake ccm b linamfia huku akiona.
 
Kiongozi bora ni yule mwenye elimu, kwa upande wa elimu Mbowe ni form 4 na Prof Lipumba PhD...na wote walishawahi kugombea urais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania na Prof Lipumba alishika nafasi ya pili na Mbowe alishika nafasi ya tatu.
 
dogo! Si bure kuna kitu,maana leo posti zako zote ulizotuma ni za kipuuzi....afu upo bize kupost bila kupumua,inaonekana posho yako leo umevuta ndefu sana
 
Lipumba kitaaluma ni mzuri hasa katika mambo ya kiuchumi tatizo lake kubwa ni MTU WA JAZBA sana hasa anapotibuliwa kidogo na CCM wamekua wakiufahamu udhaifu wake ndio maana wanamchezea kama mtoto mdogo kwa upande wa mbowe si mtu wa jazba japo kielimu hajamfikia lipumba.. hii inamfanya awe na advantage over lipumba..

Lakini all in all katika masuala ya uongozi maproffesa si wazuri sana kutokana na elimu zao .. nchi za wenzetu watu kama hawa huwa hawapewi uongozi wa siasa huwa wanaachwa watumikie taifa kwa elimu zao

SO GENERALLY MBOWE NI KIONGOZI MZURI KULIKO LIPUMBA
 
CCM HAWAACHI KUOTA MCHANA KWEUPE,KATIKA KAMPENI ZAO ZA KUWAPUUZA WATANZANIA WAMEANDAA ULAGHAI MWINGINE ILI WAPATE KURA ZA WAPUMBAVU.
1.KUANZISHWA BENKI YA WAKULIMA
2.KUANZISHA BENKI YA VIJANA
KATIKA UANZISHWAJI BENKI HIZO SERIKALI INA MPANGO WA KUWAHADAA WATZ KWA KUWAAMBIA WATAWAKOPESHA MIKOPO YENYE RIBA NAFUU,KUANZIA MILLION 1MPAKA 15.LAKINI KATIKA UOMBAJI HUO UNAHUSISHA WAJUMBE WA NYUMBA KUMI KAMA MAWAKALA WAO ILI UPATE MKOPO,CHA KUCHEKESHA ZAIDI INAAMINIKA CCM IMEJIPANGA KUTUMIA KITAMBULISHO CHA URAIA NA HASA CHA KUPIGIA KURA KAMA MTAJI WA KUWAPATA HAO WALENGWA.NA KUHAKIKISHA WANAOCHUKUA MIKOPO WOTE WATAIPIGIA CCM UCHAGUZI KUANZIA UDIWANI WA 2014 NA UCHAGUZI MKUU 2015.LAKINI WAJUMBE WENGI WANA WASIWASI KUWA VIJANA WALIO WENGI WAMEELEVUKA SANA NA WATAKULA PESA ZAO NA KUWAPIGIA WAPINZANI.CCM ILITUMIA MKUTANO WA JANGWANI KAMA KIPIMA JOTO SASA WAMEANZA KUINGIWA NA WASIWASI MAANA MKUSANYIKO ULE HAUKUKAMILIKA BILA YA PESA SASA WANAJIULIZA BILA VIKINDI VYA SANAA KWELI WATAKUBALIKA,MJUMBE ALIYE KARIBU NA NAPE KASEMA CHADEMA INAWANYIMA USINGIZI KULIKO HATA MAGONJWA YA WAZAZI WAO AU WANANDOA WAO.
BINTI MREMBO LUMUMBA CCM
:confused2:
 
dogo! Si bure kuna kitu,maana leo posti zako zote ulizotuma ni za kipuuzi....afu upo bize kupost bila kupumua,inaonekana posho yako leo umevuta ndefu sana

Kubwa. Hebu nipe maelezo post ipi ya kipuuzi na nikwann ni ya kipuuzi. Usiibane akili yako iache ifikirie. ndio maendeleo hayo. Halafu nani kanipa posho unadhani mimi nategemea posho mimi ni kijana nimepewa nguvu na Mungu nakula kwa nguvu zangu.

Mimi nataka maendeleo sio maneno maneno sawa?
 
CCM HAWAACHI KUOTA MCHANA KWEUPE,KATIKA KAMPENI ZAO ZA KUWAPUUZA WATANZANIA WAMEANDAA ULAGHAI MWINGINE ILI WAPATE KURA ZA WAPUMBAVU.
1.KUANZISHWA BENKI YA WAKULIMA
2.KUANZISHA BENKI YA VIJANA
KATIKA UANZISHWAJI BENKI HIZO SERIKALI INA MPANGO WA KUWAHADAA WATZ KWA KUWAAMBIA WATAWAKOPESHA MIKOPO YENYE RIBA NAFUU,KUANZIA MILLION 1MPAKA 15.LAKINI KATIKA UOMBAJI HUO UNAHUSISHA WAJUMBE WA NYUMBA KUMI KAMA MAWAKALA WAO ILI UPATE MKOPO,CHA KUCHEKESHA ZAIDI INAAMINIKA CCM IMEJIPANGA KUTUMIA KITAMBULISHO CHA URAIA NA HASA CHA KUPIGIA KURA KAMA MTAJI WA KUWAPATA HAO WALENGWA.NA KUHAKIKISHA WANAOCHUKUA MIKOPO WOTE WATAIPIGIA CCM UCHAGUZI KUANZIA UDIWANI WA 2014 NA UCHAGUZI MKUU 2015.LAKINI WAJUMBE WENGI WANA WASIWASI KUWA VIJANA WALIO WENGI WAMEELEVUKA SANA NA WATAKULA PESA ZAO NA KUWAPIGIA WAPINZANI.CCM ILITUMIA MKUTANO WA JANGWANI KAMA KIPIMA JOTO SASA WAMEANZA KUINGIWA NA WASIWASI MAANA MKUSANYIKO ULE HAUKUKAMILIKA BILA YA PESA SASA WANAJIULIZA BILA VIKINDI VYA SANAA KWELI WATAKUBALIKA,MJUMBE ALIYE KARIBU NA NAPE KASEMA CHADEMA INAWANYIMA USINGIZI KULIKO HATA MAGONJWA YA WAZAZI WAO AU WANANDOA WAO.
BINTI MREMBO LUMUMBA CCM
:confused2:

Dio nini sasa? halafu font nyekundu sio nzuri inaumiza macho.
 
Kama uongozi ni elimu basi mwenye elimu yake anajulikana,Ila kama ni kipaji basi mwenye kipaji chake anajulikana
 
Kiongozi bora ni mbowe hapo kwani ameweza kuongoza cdm mpaka kuwa chama makini kikuu cha upinzani na kinachoaminiwa na wa-tz kwa sasa,pia ameweza kuwajenga wanachama na viongozi ktk maadili ya uongozi bora kwahyo mbowe anamzidi lipumba kwa asilimia nyingi tu mbowe yupo segera njia panda arusha-tanga wakati lipumba yupo mbezi louis.
 
Back
Top Bottom