Lipumba: Kazi ya Makamba ni kuisambaratisha CCM

Luteni

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
2,274
301
MWENYEKITI wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba amewapuuza wanasiasa wanaobeza hatua yake ya kutangaza nia ya kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu ujao, akiwemo Katibu Mkuu wa CCM, Bw. Yusufu Makamba.

Akizungumzia kauli iliyotolewa na Bw. Yusufu Makamba dhidi yake kuwa kusimama kwake kugombea kazi itakuwa ni rahisi kwa CCM, Prof. Lipumba alisema kuwa tangu Bw. Makamba achaguliwe kuwa Katibu Mkuu amekuwa akiwasaidia (wapinzani) kukisambaratisha chama tawala.


"Katika kazi ambayo anatusaidia Bw. Makamba ni kukisambaratisha chama chake, karibu viongozi wote wa CCM ukiwauliza Makamba ana kazi gani kwenye chama wanakwambia kabisa kwamba hana lolote, wanashindwa tu kuwa wawazi na kusema ukweli, lakini Makamba hatakiwi CCM.


"Tangu alipochaguliwa kuwa Katibu Mkuu chama kimekuwa katika hali ya mapandemapande, amechangia kwa kiasi kikubwa kukisambaratisha," alisema.


Alisema kuwa Rais Kikwete asipokuwa makini na Bw. Makamba na kuendeleza usanii wake utasambaratisha nchi nzima.


Mwishoni mwa wiki hii, Prof. Lipumba alitangaza nia yake ya kuwania tena urais, lakini baadhi ya watu wakiemo viongozi na wanasiasa walimkejeli kwa uamuzi huo.


Chanzo: Majira
 
Sielewi baadhi ya watu wanaolalamikia kitendo cha watu kugombea urais mara nyingi...Kumbukeni rais was sasa wa Senegal, Wade - aligombea urais kupitia upinzani tangu miaka ya 1979 na kufanikiwa kushinda in late 1990's. Na kuna mifano mingi duniani na watu wameishia kushinda.
 
kama Makamba anaisambaratisha CCM basi LIPUMBA anatakiwa kumsifu na si kumkejeli
 
Makamba alipopewa ukatibu mkuu wa CCM na swahiba wake alikuwa na mtazamo w kizamani wa kutumia "MKONO WA CHUMA" kuendesha chama kama alivyofanya akiwa mkuu wa mkoa, yaani kuuliza watu maswali mbele ya raia na kuwatoa nishai na hata kuwafuta kazi, kitu ambacho kimemshinda CCM na kujikuta akiwa katikati ya njia panda mguu huu upo kwa mafisadi na huu upo kwa wazalendo matokeo yake kawa mdooooooogoooo na porojo zake za kukopi biblia na misahafu zimekwenda na maji.
 
simwungi lipumba mkono lakini aliyosema kuhusu makamba ni kweli

lakini kwa upande wa lipumba kusema madhaifu ya makamba . je anataka ccm wachague katibu mwingine
mzuri atayekiimarisha chama na kufanya upinzani upungue kasi? tulipenda siku moja tuone uwiano wa wawakilishi
katika bunge, unajua kila anayelitakia mema taifa hili anatakiwa kuomba siku moja kuwe na uwiano wa wawakilishi
katika bunge, kwani kutawezesha kuwa na sheria bora urais si muhimu kusema achukue nani kwani kama kutakuwa
na wawakilishi bora basi na rais atakuwa makini pia
 
Sielewi baadhi ya watu wanaolalamikia kitendo cha watu kugombea urais mara nyingi...Kumbukeni rais was sasa wa Senegal, Wade - aligombea urais kupitia upinzani tangu miaka ya 1979 na kufanikiwa kushinda in late 1990's. Na kuna mifano mingi duniani na watu wameishia kushinda.

Mwacheni Lipumba agombee URAIS hata mara mia kwani ATAFUTAE HACHOKI UKIONA AMECHOKA UJUE AMEPATA!!
 
"[B said:
Katika kazi ambayo anatusaidia Bw. Makamba ni kukisambaratisha chama chake, karibu viongozi wote wa CCM ukiwauliza Makamba ana kazi gani kwenye chama wanakwambia kabisa kwamba hana lolote, wanashindwa tu kuwa wawazi na kusema ukweli, lakini Makamba hatakiwi CCM.[/B]

"Tangu alipochaguliwa kuwa Katibu Mkuu chama kimekuwa katika hali ya mapandemapande, amechangia kwa kiasi kikubwa kukisambaratisha," alisema.

Alisema kuwa Rais Kikwete asipokuwa makini na Bw. Makamba na kuendeleza usanii wake utasambaratisha nchi nzima.
Majira.


Bwana Lipumba, Usimuamshe alielala......
 
Makamba alipopewa ukatibu mkuu wa CCM na swahiba wake alikuwa na mtazamo w kizamani wa kutumia "MKONO WA CHUMA" kuendesha chama kama alivyofanya akiwa mkuu wa mkoa, yaani kuuliza watu maswali mbele ya raia na kuwatoa nishai na hata kuwafuta kazi, kitu ambacho kimemshinda CCM na kujikuta akiwa katikati ya njia panda mguu huu upo kwa mafisadi na huu upo kwa wazalendo matokeo yake kawa mdooooooogoooo na porojo zake za kukopi biblia na misahafu zimekwenda na maji.
Umesema kweli alipokuwa mkuu wa mkoa Dar alikuwa akiwaendesha watu hata viongozi wenzake kijeshi utakuta anamdhalilisha hadharani mkuu wa wilaya kwa kumwomyesha kidole bila aibu.
 
What would you expect Lipumba to say about Mzee Makamba? That he is doing a good job? He should be more concerned and asking himself hivi CUF hakuna vichwa vingine vya kugombea urais? This guy has been on a ballot with Mkapa (twice) and now with JK twice. I'm thinking there are more ground for self awareness and democracy in CCM than in CUF.

Maybe he is a career presidential candidate, not necessarily he want to become a President. He just enjoys the perks and marupurupu that comes with the campaign. This says a lot about a party (CUF) that wants us to trust them to lead the country, but they can't even get rid of their career presidential candidates, that is Maalim Seif included.
 
kama Makamba anaisambaratisha CCM basi LIPUMBA anatakiwa kumsifu na si kumkejeli
Wanasiasa wetu bwana! Sasa profesa wa uchumi uliyebobea katika fani na mwanasiasa mahiri unatakiwa uombe makamba aendelee hivyo hivyo ili arahisishe wewe kuingia ikulu AU ndiyo hadithi ya sungura na zabibu?????????????
 
Makamba alipopewa ukatibu mkuu wa CCM na swahiba wake alikuwa na mtazamo w kizamani wa kutumia "MKONO WA CHUMA" kuendesha chama kama alivyofanya akiwa mkuu wa mkoa, yaani kuuliza watu maswali mbele ya raia na kuwatoa nishai na hata kuwafuta kazi, kitu ambacho kimemshinda CCM na kujikuta akiwa katikati ya njia panda mguu huu upo kwa mafisadi na huu upo kwa wazalendo matokeo yake kawa mdooooooogoooo na porojo zake za kukopi biblia na misahafu zimekwenda na maji.

Jamani wacheni wivu kwani huyu mzee alikubaliwa na mkutano mkuu wa chama chake [ambacho wengi tunakiponda]. Kwa wale waliomteua wanaona anafaa kwa kazi hiyo kwa vigezo ambavyo mimi na wewe hatuvijui na kama tukitaka kumpima uwezo wake kwa kutumia chaguzi ndogo zilizofanyika katika kipindi chake majibu yako wazi na kama mnasema uzee wake ni liabilitiy kwa ccm basi inatakiwa wale wapinzani wa chama tawala wafurahi maana kwa vile siasa zake zimepitwa na wakati basi kushindwa kwa ccm itakuwa rahisi.
 
Makamba hana jipya kama walivyo hao wanaomtuhumu.....hivi ni kweli CUF haikusambaratika Tz Bara.Big up Lwakatare!
 
MWENYEKITI wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba amewapuuza wanasiasa wanaobeza hatua yake ya kutangaza nia ya kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu ujao, akiwemo Katibu Mkuu wa CCM, Bw. Yusufu Makamba.

Akizungumzia kauli iliyotolewa na Bw. Yusufu Makamba dhidi yake kuwa kusimama kwake kugombea kazi itakuwa ni rahisi kwa CCM, Prof. Lipumba alisema kuwa tangu Bw. Makamba achaguliwe kuwa Katibu Mkuu amekuwa akiwasaidia (wapinzani) kukisambaratisha chama tawala.

"Katika kazi ambayo anatusaidia Bw. Makamba ni kukisambaratisha chama chake, karibu viongozi wote wa CCM ukiwauliza Makamba ana kazi gani kwenye chama wanakwambia kabisa kwamba hana lolote, wanashindwa tu kuwa wawazi na kusema ukweli, lakini Makamba hatakiwi CCM.

"Tangu alipochaguliwa kuwa Katibu Mkuu chama kimekuwa katika hali ya mapandemapande, amechangia kwa kiasi kikubwa kukisambaratisha," alisema.

Alisema kuwa Rais Kikwete asipokuwa makini na Bw. Makamba na kuendeleza usanii wake utasambaratisha nchi nzima.

Mwishoni mwa wiki hii, Prof. Lipumba alitangaza nia yake ya kuwania tena urais, lakini baadhi ya watu wakiemo viongozi na wanasiasa walimkejeli kwa uamuzi huo.

Chanzo: Majira
Lipumba anamtuhumu Makamba kwa kuwasaidia wapinzani na hapohapo yeye anafanyakazi ya kuwasidia ccm kwa kumwonyesha Kikwete, Makamba hafai.
 
MWENYEKITI wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba amewapuuza wanasiasa wanaobeza hatua yake ya kutangaza nia ya kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu ujao, akiwemo Katibu Mkuu wa CCM, Bw. Yusufu Makamba.

Akizungumzia kauli iliyotolewa na Bw. Yusufu Makamba dhidi yake kuwa kusimama kwake kugombea kazi itakuwa ni rahisi kwa CCM, Prof. Lipumba alisema kuwa tangu Bw. Makamba achaguliwe kuwa Katibu Mkuu amekuwa akiwasaidia (wapinzani) kukisambaratisha chama tawala.



"Katika kazi ambayo anatusaidia Bw. Makamba ni kukisambaratisha chama chake, karibu viongozi wote wa CCM ukiwauliza Makamba ana kazi gani kwenye chama wanakwambia kabisa kwamba hana lolote, wanashindwa tu kuwa wawazi na kusema ukweli, lakini Makamba hatakiwi CCM.


"Tangu alipochaguliwa kuwa Katibu Mkuu chama kimekuwa katika hali ya mapandemapande, amechangia kwa kiasi kikubwa kukisambaratisha," alisema.


Alisema kuwa Rais Kikwete asipokuwa makini na Bw. Makamba na kuendeleza usanii wake utasambaratisha nchi nzima.


Mwishoni mwa wiki hii, Prof. Lipumba alitangaza nia yake ya kuwania tena urais, lakini baadhi ya watu wakiemo viongozi na wanasiasa walimkejeli kwa uamuzi huo.


Chanzo: Majira
Siri hii alipaswa kubaki nayo LIPUMBA lakini kwa kuwa yeye yupo upinzani kuisaidia CCM basi ameamua kuiweka wazi.
Hii inaonesha between lines how most upinzanis are in line na chama tawala na wapo huko kuhakikisha wanatoa upinzani bandia. Ndo maana haachi kugombea huyu hataki kumpisha mwingine kuchukua kijiti.

Tuna wapinzani wa kweli wachache mno nakwambia
 
Kaenda Iringa kwa kazi hiyo hiyo kuwachanganya vijana lakini wamemuonya asijaribu kuegemea upande wowote
 
Back
Top Bottom