Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
Lipumba azungumzia katiba mpya
Salim Said
CHAMA cha Wananchi (CUF), kimemtaka Rais Jakaya Kikwete kuhakikisha kuwa anasimamia rasimu ya katiba mpya yenye misingi ya kidemokrasia.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara wa kutambulisha safu mpya ya uongozi wa chama hicho kwenye Uwanja cha Kidongo Chekundu jijini hapa, Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba alisema katiba mpya yenye misingi ya kidemokrasia ndio itakayomjengea heshima Rais Kikwete.
Alifafanua kuwa rasimu ya katiba hiyo iko kwa wadau kushughulikiwa na akamtaka rais kusimamia kupitishwa kwa rasimu hiyo baada ya kutoka kwa wadau ili iwe sheria kamili.
Akizungumza wakati wa kumkaribisha mwenyekiti, katibu mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad alisema CCM lazima iondoke madarakani kwenye uchaguzi wa mwaka 2010.
"Ndugu zangu udhalilishaji na manyanyaso yaliyopo kwa Watanzania ni kwa sababu ya Serikali ya CCM... imechoka na lazima iondoke 2010," alisema nana huku wananchi wakimshangilia kwa kusema yes we can.
Maalim Seif aliongezea "CCM Ikubali kutunga katiba mpya au isikubali, lazima itaondoka; ikubali kuunda tume huru ya uchaguzi au isikubali lazima itangoka tu. Kipimo tutakiona katika uchaguzi mdogo wa jimbo la uwakilishi la Magogoni Zanzibar. Ni jimbo letu ila tuliporwa kwa vifaru na magari ya kumwaga maji ya kuwasha."
___________________
Hiki kipande cha mwisho ni siasa au ni mtego kwa CCM kwa anaejua siasa katika hali ya leo,hapo ni dhahiri kuna mtego kwa CCM ,nawashauri CCM bora hilo jimbo wawaachie CCM kuliko kutaka kufanya ubabe.Kwani CCM wakifanya hila hapo basi wajue ndio wamekwisha kabisa.
Salim Said
CHAMA cha Wananchi (CUF), kimemtaka Rais Jakaya Kikwete kuhakikisha kuwa anasimamia rasimu ya katiba mpya yenye misingi ya kidemokrasia.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara wa kutambulisha safu mpya ya uongozi wa chama hicho kwenye Uwanja cha Kidongo Chekundu jijini hapa, Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba alisema katiba mpya yenye misingi ya kidemokrasia ndio itakayomjengea heshima Rais Kikwete.
Alifafanua kuwa rasimu ya katiba hiyo iko kwa wadau kushughulikiwa na akamtaka rais kusimamia kupitishwa kwa rasimu hiyo baada ya kutoka kwa wadau ili iwe sheria kamili.
Akizungumza wakati wa kumkaribisha mwenyekiti, katibu mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad alisema CCM lazima iondoke madarakani kwenye uchaguzi wa mwaka 2010.
"Ndugu zangu udhalilishaji na manyanyaso yaliyopo kwa Watanzania ni kwa sababu ya Serikali ya CCM... imechoka na lazima iondoke 2010," alisema nana huku wananchi wakimshangilia kwa kusema yes we can.
Maalim Seif aliongezea "CCM Ikubali kutunga katiba mpya au isikubali, lazima itaondoka; ikubali kuunda tume huru ya uchaguzi au isikubali lazima itangoka tu. Kipimo tutakiona katika uchaguzi mdogo wa jimbo la uwakilishi la Magogoni Zanzibar. Ni jimbo letu ila tuliporwa kwa vifaru na magari ya kumwaga maji ya kuwasha."
___________________
Hiki kipande cha mwisho ni siasa au ni mtego kwa CCM kwa anaejua siasa katika hali ya leo,hapo ni dhahiri kuna mtego kwa CCM ,nawashauri CCM bora hilo jimbo wawaachie CCM kuliko kutaka kufanya ubabe.Kwani CCM wakifanya hila hapo basi wajue ndio wamekwisha kabisa.