Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 233
Wana-JF hii ni stori kuuu ya ukurasa wa mbele wa gazeti la Mtanzania Daima leo. Hivi imekaa vipi stori hii, hasa kwa Profesa kuyasema haya wakati huu, na hasa kwa kupitia gazeti hili?
(Operesheni Sangara katika ibara ya pili ni makosa ya mhariri ambalo bila shaka halitamfurahisha Mbowe hata kidogo.
**********************
Lipumba amhusisha JK na Richmond
* Asema ndiye aliyetoa kibali kwa kampuni hiyo
* Adai kujiuzulu kwa Lowassa ni kutolewa kafara
* Asema serikali yajitafutia umaarufu kesi za EPA
* Aishangaa CCM kukwepa mahakama ya Kadhi
Tanzania Daima, Julai 13, 2009
Jinamizi la ufisadi wa Kampuni ya kufua umeme ya Richmond, limefufuliwa upya, baada ya Mwenyekiti wa Chama cha wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, kumtaja hadharani rais jakaya Kikwete, akimhusisha na ufisadi wa kampuni hiyo.
Lipumba alitoa madai hayo mazito aliyoyaita siri kubwa iliyofichwa juzi jioni mbele ya maelfu ya wananchi waliohudhuria mkutano wa hadhara wa CUF wa uzinduzi wa Operesheni Sangara katika viwanja vya shule ya Mirongo, Kata ya Mirongo, Wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza.
Akifafanua alisema, taarifa alizonazo zinaeleza kuwa Kikwete ndiye aliyekuwa mtu wa mwisho kutoa kibali ambacho hatimaye kiliiruhusu Richmond ambayo baadaye ilibainika kuwa ni kampuni ya kitapeli, kuleta mitambo ya kuzalisha umeme wa dharura.
Alisema kutokana na ukweli huo basi, mtu ambaye kimsingi alikuwa akipaswa kujiuzulu kutokana na sakata hilo la Richmond lililosababisha kuanguka kwa aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa na mawaziri wengine ni rais Kikwete mwenyewe.
Akiendelea, Lipumba alisema ili kujinusuru na kuanguka au kuwajibika kutokana na kashfa hiyo ya kifisadi ya Richmond, Rais Kikwete aliona ni vyema akamtoa kafara rafiki yake.
Wananchi, leo nawatobolea siri juu ya Kampuni ya Richmond mhusika mkuu wa ufisadi wa Richmond ni Rais Jakaya Kikwete. Ukiangalia vizuri ripoti iliyotolewa na Kamati Teule ya Bunge iliyoongozwa na Dk Harrison Mwakyembe, utaona inamhusisha Rais Kikwete na ufisadi huo.
Kwa ukweli huo, Lowassa yeye katolewa kafara tu na rafiki yake Kikwete, lakini rais huyu ndiye aliyepaswa na mpaka sasa ndiye anayepaswa kuwajibika kwa taifa. Hatuwezi kufika kwa mtindo huu, alisema Profesa Lipumba huku akishangiliwa na umati wa watu waliohudhuria mkutano huo wa hadhara
(Operesheni Sangara katika ibara ya pili ni makosa ya mhariri ambalo bila shaka halitamfurahisha Mbowe hata kidogo.
**********************
Lipumba amhusisha JK na Richmond
* Asema ndiye aliyetoa kibali kwa kampuni hiyo
* Adai kujiuzulu kwa Lowassa ni kutolewa kafara
* Asema serikali yajitafutia umaarufu kesi za EPA
* Aishangaa CCM kukwepa mahakama ya Kadhi
Tanzania Daima, Julai 13, 2009
Jinamizi la ufisadi wa Kampuni ya kufua umeme ya Richmond, limefufuliwa upya, baada ya Mwenyekiti wa Chama cha wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, kumtaja hadharani rais jakaya Kikwete, akimhusisha na ufisadi wa kampuni hiyo.
Lipumba alitoa madai hayo mazito aliyoyaita siri kubwa iliyofichwa juzi jioni mbele ya maelfu ya wananchi waliohudhuria mkutano wa hadhara wa CUF wa uzinduzi wa Operesheni Sangara katika viwanja vya shule ya Mirongo, Kata ya Mirongo, Wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza.
Akifafanua alisema, taarifa alizonazo zinaeleza kuwa Kikwete ndiye aliyekuwa mtu wa mwisho kutoa kibali ambacho hatimaye kiliiruhusu Richmond ambayo baadaye ilibainika kuwa ni kampuni ya kitapeli, kuleta mitambo ya kuzalisha umeme wa dharura.
Alisema kutokana na ukweli huo basi, mtu ambaye kimsingi alikuwa akipaswa kujiuzulu kutokana na sakata hilo la Richmond lililosababisha kuanguka kwa aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa na mawaziri wengine ni rais Kikwete mwenyewe.
Akiendelea, Lipumba alisema ili kujinusuru na kuanguka au kuwajibika kutokana na kashfa hiyo ya kifisadi ya Richmond, Rais Kikwete aliona ni vyema akamtoa kafara rafiki yake.
Wananchi, leo nawatobolea siri juu ya Kampuni ya Richmond mhusika mkuu wa ufisadi wa Richmond ni Rais Jakaya Kikwete. Ukiangalia vizuri ripoti iliyotolewa na Kamati Teule ya Bunge iliyoongozwa na Dk Harrison Mwakyembe, utaona inamhusisha Rais Kikwete na ufisadi huo.
Kwa ukweli huo, Lowassa yeye katolewa kafara tu na rafiki yake Kikwete, lakini rais huyu ndiye aliyepaswa na mpaka sasa ndiye anayepaswa kuwajibika kwa taifa. Hatuwezi kufika kwa mtindo huu, alisema Profesa Lipumba huku akishangiliwa na umati wa watu waliohudhuria mkutano huo wa hadhara