Nicholas
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 25,260
- 7,195
Mambo ambayo mleta mada(ambaye ni kiongozi) ameyaorodhesha kama ndiyo kikwazo,lakini kwa namna ambayo ni kama hana uhakika kwasababu ameyaorodhesha kama maswali.Nilitegemea hoja yake hii ingekuwa walau na mapendekezo mawili matatu given the fact that he's a leader.
Kama alivyofanya kwenye kutolea mfano wa ufisadi wa mbolea,ameuliza maswali,tena kuna hilo ambalo rafiki yake JK kalisema kuwa "watu hawapendi kuona maendeleo",nadhani akimaanisha wapinzani.Hilo la Zitto sijui kama alizungumzia individually ama as a society(kwamba hatupendi kuona maendeleo).Kwa namna nyingine,ni kama haamini moja kwa moja kuwa ufisadi ndo tatizo kuu.
Pamoja na kwamba ni kweli ufisadi unaweza kuwa pia ni tatizo la kimfumo,lakini hajatoa mapendekezo ama solutions.Makala hiyo ni nzuri tu lakini siyo yenye kuprovide solutions.Mleta hoja ametolea mifano ya mambo yanaoonyesha usawa ama mfanano kati ya mkoa/mikoa yetu wa/ya Lindi/mtwara vs Taifa la Sir Lanka,bila kuona kuwa mipango yetu kwa Lindi ni ya kimkoa na ile ya Sir Lanka ni ya kitaifa.Inawezekana kabisa kwamba Lindi ingekuwa Taifa basi lingekuwa mbali sana.
Sisi tatizo letu kubwa ni uongozi hilo siyo siri hata kidogo.Ni hatuwa walizozichukuwa viongozi wa mataifa hayo ndizo zilizowafikisha hapo walipo.Viongozi kulalamikia wananchi ndo tatizo lenyewe.Tunategemea solutions kutoka kwa viongozi na si malalamishi.Kiongozi akilalamika wananchi nao wafanyaje?Kiongozi asipokuwa na solution ya nini cha kuwafanyia wananchi,wananchi wanatakiwa wafanyeje?
We lack leadership,thats the fact,ngoja tusubiri kama kiongozi wetu atatoa na ushauri wa nini kifanyike,yeye si mmojawapo wa watunga sheria?Mbona China wananyonga mafisadi na ni ushahidi tosha kabisa kwamba hilo limesaidia taifa hilo kusonga mbele?
Kwanini asiseme yeye kama kiongozi,tufanye so and so kuutokomeza ufisadi kama ni kweli anaamini kuwa ni kikwazo cha maendeleo yetu?
kwa jinsi nilivyoona kiongozi kakataa utamaduni katumia mfumo.Ila huo mfumo ni wa siku nyingi sana na ni wa kitaifa ,kwa kihalisia ni utamaduni.Utamaduni si lazima uwe km DNA.kama anakubali ufisadi na wizi upo kila kijiji,na kila office na ni tabia iliyooota mizizi mikubwa there is no way mheshimiwa akataka usiitwe utamaduni.mwovu hafukuzwi na kushitakiwa bali huamishwa kituo.