jessetz
Member
- Nov 30, 2010
- 55
- 9
Mimi ni kijana mwanamume, nina rafiki yangu wa kike tumejuana kwa njia ya mtandao. Tumetokea kupendana sana hatuwezi kabisa kupita muda kidogo bila kuongea. Sikua na mpango wa kumtafuta mtu kwa sasa ila kwa kuwa tumependana niliamua kuipa nafasi, ninaishi nchi za nje na ilipidi nisafiri tuende tukaonane.
Baada ya kuonana tulilala wote na tulikua na muda mzuri pamoja japo ulikua sio muda mwingi kwa sababu nilitakiwa kurudi mapema.
Kuna vitu nilimkosea kwa kumdanganya na ilimuumiza sana, nilimuomba msamaha sana na niliwatumia pia watu wazima waliojua uhusiano wetu. Alinisamehe ila baada ya hapo yeye hakua tena na upendo ule tuliokua nao awali, nilimuuliza tatizo haswa ni nini na mbona hivyo!? Hakuweza kujibu na nilimuuliza kama labda kapata mtu au vipi ila amesema yupo single na hajapata mtu ila hajisikii tu kunipenda kama zamani, anakazana lakini haiwezekani. Imefikia muda ikabidi nimpressurize ili nijue ukweli maana nilikua naumia sana, sikujua la kufanya, nilifikia sehemu nipo kwenye stress kubwa....baada ya kufanya hivyo/kum-pressurize alinijibu kuwa kwa sasa anaona awe peke yake na awe na muda wake binafsi, apange maisha yake hivyo mimi na yeye tuachane. Haya yote ni mimi niliyasababisha!
Nilichanganyikiwa kusikia hivyo maana ninampenda mno, sikujua tena la kufanya. Nilitamani nife ili nisahau yote. Niliugua pressure/stress nikalazwa ka siku moja hospitalini. Ndugu zangu walijua kitu kilichotokea na yeye aliambiwa na marafiki zangu. Amenipigia na kuniambia anavyojisikia na anaomba nipone tujue la kufanya ila zaidi nifikirie maisha. Ameniambia kiasi yeye imemuumiza pia ila bado ameshikilia msimamo wake. Bado sijajua kuwa ni nini hasa cha kufanya. Ninampenda na hii ndio nafasi nilionayo, nifanye nini, nisaidieni kwa mawazo endelevu......mapenzi yameniteka, sijui la kufanya, kwa sasa nipo kitandani naugulia!!:decision:
Baada ya kuonana tulilala wote na tulikua na muda mzuri pamoja japo ulikua sio muda mwingi kwa sababu nilitakiwa kurudi mapema.
Kuna vitu nilimkosea kwa kumdanganya na ilimuumiza sana, nilimuomba msamaha sana na niliwatumia pia watu wazima waliojua uhusiano wetu. Alinisamehe ila baada ya hapo yeye hakua tena na upendo ule tuliokua nao awali, nilimuuliza tatizo haswa ni nini na mbona hivyo!? Hakuweza kujibu na nilimuuliza kama labda kapata mtu au vipi ila amesema yupo single na hajapata mtu ila hajisikii tu kunipenda kama zamani, anakazana lakini haiwezekani. Imefikia muda ikabidi nimpressurize ili nijue ukweli maana nilikua naumia sana, sikujua la kufanya, nilifikia sehemu nipo kwenye stress kubwa....baada ya kufanya hivyo/kum-pressurize alinijibu kuwa kwa sasa anaona awe peke yake na awe na muda wake binafsi, apange maisha yake hivyo mimi na yeye tuachane. Haya yote ni mimi niliyasababisha!
Nilichanganyikiwa kusikia hivyo maana ninampenda mno, sikujua tena la kufanya. Nilitamani nife ili nisahau yote. Niliugua pressure/stress nikalazwa ka siku moja hospitalini. Ndugu zangu walijua kitu kilichotokea na yeye aliambiwa na marafiki zangu. Amenipigia na kuniambia anavyojisikia na anaomba nipone tujue la kufanya ila zaidi nifikirie maisha. Ameniambia kiasi yeye imemuumiza pia ila bado ameshikilia msimamo wake. Bado sijajua kuwa ni nini hasa cha kufanya. Ninampenda na hii ndio nafasi nilionayo, nifanye nini, nisaidieni kwa mawazo endelevu......mapenzi yameniteka, sijui la kufanya, kwa sasa nipo kitandani naugulia!!:decision: