Ligi ya Madam na Mchaga..

Travibela

Member
Mar 10, 2016
76
58
Maselebriti watu wazima, Madam wa Biesiesi na huyu Jacky Mchaga wanafanana sana tabia.. Hawa ni ndege? Nachozungumzia ni tabia ya kuruka na vi-underage.. Imo damuni mwao!

Nisameheni mie sijui kuandika vizuri, ila nitajitahidi kueleweka..

Siku nyingi sana niliwahi kusikia kuhusu Mchagga kutoka na Kibanio, kipindi anamiliki Saluni yake pale Ilala.. Kibanio aliwahi kufunguka alipoulizwa kuhusu kutoka na overage na kujitetea 'mchaga mwenyewe sio mkubwa kiihivyo'.. Hayo yakapita.

Mchagga baada ya kupata kiki town akarukia kwa Plate Number na kumrithisha Kibanio kwa Madam Biesiesi (sijui ni hiari au kwa kuchepukwa).

Kwa pleti namba akauza nyago pia kwa muda mfupi, nae akampasishia kwa Mama Ubaya.. Hapo akapumua kidogo kwanza ili kutunisha kamfuko kake. Ndipo akaanza kuripotiwa kutoka na wakina Mashilingi na Wabolingo..

Ligi kwa upande wa Biesiesi ikaendelea kwa kasi lakini baada ya kuona kibanio kimechakaa na kimeanza kuota vidotidoti, akaamua kukitupa na kuhamishia uwekezaji kwa mmoja wa matunda yake ya Biesiesi (jina kwenye kikapu kwasasa).

Sasa Mchaga amerudi kwenye fomu. Amejidumbukiza kwenye zao la Pleti Namba ili kulichepua.. Swali la kujiuliza ni; Je, zao hili safari hii litapelekwa soko lipi baada ya mavuno?

Kodi hujibiwa kwa kodi!

(IMEONGEZEWA)

Wapendwa, nina minuso mingi ya kuwaalika. Mnaweza kunifuatilia hapa hapa JF kila uchwao.. Huenda mkapata nyeti nyingi zaidi, japo mwendo wangu utakuwa ni huu huu (CODE)..

Sasa mnuso ujao ni tata zaidi. Lakini kwa sasa naongeza nyama kidogo kwenye ligi hii ya Madam na Mchaga... Kumbe bhana hii ishu sio ya Madam na Mchaga tu... Wamo wengi mno na kila siku wanaongezeka. Hata hivyo Madam na Mchaga watabaki kuwa ni alama ya utambulisho.. Kuna siri gani?

Tipu nyingine ni hii.. Si wote humu mnamfahamu Dada Pesa, ambae alikuwa na Mwana wa Sultani kwenye Mjengo wa Kaka Mkubwa pale Kusini kwa Makaburu? Ambao kwa sasa wako nje ya mjengo na wanashirikiana kikazi kwenye kituo cha Chaguo Fm, basi naye amejiunga kwenye mkondo huu wa ''Tete a tete''.

Pesa naye anahitaji mng'aro wa Silva kwa dogo Vanilla... Huyu Vanilla yuko kwenye falme ya Wachafu Beibe.. Zamani alikuwa TPTP kabla hajasainiwa na lebo ya Mwanamageuzi Plate Number.. Tuko pamoja?? Enhee, sasa Dada Pesa yuko resi haswaaa.. Na soon or later tutaanza kuona mapicha picha.

Hata kama hayatuhusu, lakini ni nini siri ya haya yote? Kwanini Ugumegume?!

Tukutane kwenye Mnuso mwingine, Kodi nyingine.
 
Maselebriti watu wazima, Madam wa Biesiesi na huyu Jacky Mchaga wanafanana sana tabia.. Hawa ni ndege? Nachozungumzia ni tabia ya kuruka na vi-underage.. Imo damuni mwao!

Nisameheni mie sijui kuandika vizuri, ila nitajitahidi kueleweka..

Siku nyingi sana niliwahi kusikia kuhusu Mchagga kutoka na Kibanio, kipindi anamiliki Saluni yake pale Ilala.. Kibanio aliwahi kufunguka alipoulizwa kuhusu kutoka na overage na kujitetea 'mchaga mwenyewe sio mkubwa kiihivyo'.. Hayo yakapita.

Mchagga baada ya kupata kiki town akarukia kwa Plate Number na kumrithisha Kibanio kwa Madam Biesiesi (sijui ni hiari au kwa kuchepukwa).

Kwa pleti namba akauza nyago pia kwa muda mfupi, nae akampasishia kwa Mama Ubaya.. Hapo akapumua kidogo kwanza ili kutunisha kamfuko kake. Ndipo akaanza kuripotiwa kutoka na wakina Mashilingi na Wabolingo..

Ligi kwa upande wa Biesiesi ikaendelea kwa kasi lakini baada ya kuona kibanio kimechakaa na kimeanza kuota vidotidoti, akaamua kukitupa na kuhamishia uwekezaji kwa mmoja wa matunda yake ya Biesiesi (jina kwenye kikapu kwasasa).

Sasa Mchaga amerudi kwenye fomu. Amejidumbukiza kwenye zao la Pleti Namba ili kulichepua.. Swali la kujiuliza ni; Je, zao hili safari hii litapelekwa soko lipi baada ya mavuno?

Kodi hujibiwa kwa kodi!
Acha umbeya wewe. Underage ipi? Huyu Jak hata 35 bado. Huko huru kutoa Love yake kwa ampendaye. Kwa info yako underage hamuwezi demu. Wababa wanaishi na under age girls hamsemi
 
hapo kwa harmonise anapoteza muda tu ili asikike, akimpata bonge la bwana mwenye pesa zake dogo anaachwa aidha tutajua au hatutojua, ingekuwa plate number hana ka kid ingekuwa rahisi kurudi
 
Bongo movie wadada wameamua cku hzi,ukiacha jack na madam,shishi,riyama nawengi tu wanaofanya kwa siri!!ila hpo wte wana 28 kasoro riyama nadhan atakuwa kwny 30 na kitu!!!!acha movie iendelee!!!
 
Huu ubuyu umefichwa kama sukari..... Nimetoka kapa hapa zaidi ya kibanio na biesiesi sijaelewa kitu

Tumia MAGAZIJUTO tu,nakupa msaada tutani plate number ni sukari ya warembo toka Madale na zao lake ni kijana wa kimakonde anaemfuga,Jack Mchaga ni kipozeo cha Mkongo kilichoingizwa mjini,kidotidoti ni kipozeo cha kibanio changanya na hao wawili uliopatia nenda kwenye thread kafungue mabano kwa kutumia hizo codes utakua umeelewa.
 
Tumia MAGAZIJUTO tu,nakupa msaada tutani plate number ni sukari ya warembo toka Madale na zao lake ni kijana wa kimakonde anaemfuga,Jack Mchaga ni kipozeo cha Mkongo kilichoingizwa mjini,kidotidoti ni kipozeo cha kibanio changanya na hao wawili uliopatia nenda kwenye thread kafungue mabano kwa kutumia hizo codes utakua umeelewa.
Ewaaaah ahsante, huyu mleta ubuyu nadhani ana BACHELOR OF GOSSIP AND UDAKU lol sio kwa code hizo
 
imenibidi nisome sredi hii kwa mtindo wa kisengelenyuma ili nisimiss point....uu ubuyu ni classic
 
Back
Top Bottom