Mbunge wa CCM
JF-Expert Member
- Nov 13, 2009
- 475
- 22
Waungwana,
Kuna mwanaume mmoja aliyefanikiwa kimaisha kwa kiasi cha kuridhisha, alinisimulia kisa chake kikanisikitisha sana.
Alipokuwa anatafuta mchumba wa kuoa, bila kutarajia alipata maradhi mabaya ya mfumo wa uzazi yaliyopelekea kufanyiwa upasuaji katika taasisi ya mifupa muhimbili (MOI). Kwa mujibu wa madaktari, kulikuwa na uwezekano mdogo sana wa kupata watoto maishani mwke.
Hii haikuwa habari nzuri kwake, akachanganyikiwa, akaazimia kuwa lazima apate motto/mimba haraka iwezekanavyo hata kabla hajapona upasuaji aliofanyiwa!
Ndio, alikurupuka akaongea na binti mmoja waliyekutana nae kwa jirani yake suku za nyuma na ambaye hakupata kuwa mpenzi wake kabla, amsaidie kumzalia motto angalau wa kumbukumbu ya maisha yake, na yeye yuko tayari kwa lolote. Binti alimpa sharti la kumuoa, akakubali kama kufumba na kufumbua na kumtaka siku hiyohiyo apeleke taarifa kwao na ikawa hivyo.
siku hiyohiyo wakakutana kitandani Yule bwana akiwa bado kafungwa bandeji sehemu nyeti alikofanyiwa upasuaji na kwa kukiuka ushauri wa madaktari wake waliomzua kufanya ngono hadi watakaridhika kuwa afya yake imetengemaa, wakafanya shughuli kwa uangalifu mkubwa kuzuia asitoneshwe na waliendelea hivyo hadi walipopata walichokuwa wakikitafuta yaani mimba. ndoa ikafungwa, mtoto akazaliwa, mume akashusha pumzi kwa shukrani
Kabla ya mwaka mmoja wa ndoa maisha yakabadilika. Kila wanapopishana jambo, mwanamke anatishia kuwa atatoa siri yake na kujiua yeye pamoja na mtoto kwani anasema hawezi kufa peke yake akamuacha mwanae alelewe na mwanmke mwingine. ugomvi ukavuka mipaka ya nyumba yao, ukafika kazini, polisi, ustawi wa jamii, mahakamani, yaani kila mahali. Wakawa vituko mbele za watu
Huku akimpenda mwanae kupita kiasi, visa navyo viliongezeka. Akaamua kupanga chumba maeneo ya magomeni. Kila akichoka kero za mkewe, anaaga kuwa kasafiri kikazi na kujipunzisha hadi wiki moja kwenye chumba chake cha kupanga kisha anarudi kumwona mwanae.
Anaongeza kuwa hatamuacha mwanamke huyo kamwe licha ya visa vyote anavyomtendea kwa kuheshimu jinsi alivyompa faraja pale alipokubali kuzaa nae wakati ambapo alianza kupoteza matumani ya kuwa baba wa mtu maishani wake.
niliposikia habari zake kwanza nilimhurumia nikamtafuta nizungumze nae kuangalia kama kama naweza kumsaidia. Tunaendelea na mashauriano na wote wawili wanatoa ushirikiano wa kutosha,
mnawashauri nini hawa?
Kuna mwanaume mmoja aliyefanikiwa kimaisha kwa kiasi cha kuridhisha, alinisimulia kisa chake kikanisikitisha sana.
Alipokuwa anatafuta mchumba wa kuoa, bila kutarajia alipata maradhi mabaya ya mfumo wa uzazi yaliyopelekea kufanyiwa upasuaji katika taasisi ya mifupa muhimbili (MOI). Kwa mujibu wa madaktari, kulikuwa na uwezekano mdogo sana wa kupata watoto maishani mwke.
Hii haikuwa habari nzuri kwake, akachanganyikiwa, akaazimia kuwa lazima apate motto/mimba haraka iwezekanavyo hata kabla hajapona upasuaji aliofanyiwa!
Ndio, alikurupuka akaongea na binti mmoja waliyekutana nae kwa jirani yake suku za nyuma na ambaye hakupata kuwa mpenzi wake kabla, amsaidie kumzalia motto angalau wa kumbukumbu ya maisha yake, na yeye yuko tayari kwa lolote. Binti alimpa sharti la kumuoa, akakubali kama kufumba na kufumbua na kumtaka siku hiyohiyo apeleke taarifa kwao na ikawa hivyo.
siku hiyohiyo wakakutana kitandani Yule bwana akiwa bado kafungwa bandeji sehemu nyeti alikofanyiwa upasuaji na kwa kukiuka ushauri wa madaktari wake waliomzua kufanya ngono hadi watakaridhika kuwa afya yake imetengemaa, wakafanya shughuli kwa uangalifu mkubwa kuzuia asitoneshwe na waliendelea hivyo hadi walipopata walichokuwa wakikitafuta yaani mimba. ndoa ikafungwa, mtoto akazaliwa, mume akashusha pumzi kwa shukrani
Kabla ya mwaka mmoja wa ndoa maisha yakabadilika. Kila wanapopishana jambo, mwanamke anatishia kuwa atatoa siri yake na kujiua yeye pamoja na mtoto kwani anasema hawezi kufa peke yake akamuacha mwanae alelewe na mwanmke mwingine. ugomvi ukavuka mipaka ya nyumba yao, ukafika kazini, polisi, ustawi wa jamii, mahakamani, yaani kila mahali. Wakawa vituko mbele za watu
Huku akimpenda mwanae kupita kiasi, visa navyo viliongezeka. Akaamua kupanga chumba maeneo ya magomeni. Kila akichoka kero za mkewe, anaaga kuwa kasafiri kikazi na kujipunzisha hadi wiki moja kwenye chumba chake cha kupanga kisha anarudi kumwona mwanae.
Anaongeza kuwa hatamuacha mwanamke huyo kamwe licha ya visa vyote anavyomtendea kwa kuheshimu jinsi alivyompa faraja pale alipokubali kuzaa nae wakati ambapo alianza kupoteza matumani ya kuwa baba wa mtu maishani wake.
niliposikia habari zake kwanza nilimhurumia nikamtafuta nizungumze nae kuangalia kama kama naweza kumsaidia. Tunaendelea na mashauriano na wote wawili wanatoa ushirikiano wa kutosha,
mnawashauri nini hawa?