Licha ya kukimbia kero nyumbani, anaapa kamwe hatamuacha mkewe

Mbunge wa CCM

JF-Expert Member
Nov 13, 2009
475
22
Waungwana,
Kuna mwanaume mmoja aliyefanikiwa kimaisha kwa kiasi cha kuridhisha, alinisimulia kisa chake kikanisikitisha sana.

Alipokuwa anatafuta mchumba wa kuoa, bila kutarajia alipata maradhi mabaya ya mfumo wa uzazi yaliyopelekea kufanyiwa upasuaji katika taasisi ya mifupa muhimbili (MOI). Kwa mujibu wa madaktari, kulikuwa na uwezekano mdogo sana wa kupata watoto maishani mwke.
Hii haikuwa habari nzuri kwake, akachanganyikiwa, akaazimia kuwa lazima apate motto/mimba haraka iwezekanavyo hata kabla hajapona upasuaji aliofanyiwa!

Ndio, alikurupuka akaongea na binti mmoja waliyekutana nae kwa jirani yake suku za nyuma na ambaye hakupata kuwa mpenzi wake kabla, amsaidie kumzalia motto angalau wa kumbukumbu ya maisha yake, na yeye yuko tayari kwa lolote. Binti alimpa sharti la kumuoa, akakubali kama kufumba na kufumbua na kumtaka siku hiyohiyo apeleke taarifa kwao na ikawa hivyo.

siku hiyohiyo wakakutana kitandani Yule bwana akiwa bado kafungwa bandeji sehemu nyeti alikofanyiwa upasuaji na kwa kukiuka ushauri wa madaktari wake waliomzua kufanya ngono hadi watakaridhika kuwa afya yake imetengemaa, wakafanya shughuli kwa uangalifu mkubwa kuzuia asitoneshwe na waliendelea hivyo hadi walipopata walichokuwa wakikitafuta yaani mimba. ndoa ikafungwa, mtoto akazaliwa, mume akashusha pumzi kwa shukrani

Kabla ya mwaka mmoja wa ndoa maisha yakabadilika. Kila wanapopishana jambo, mwanamke anatishia kuwa atatoa siri yake na kujiua yeye pamoja na mtoto kwani anasema hawezi kufa peke yake akamuacha mwanae alelewe na mwanmke mwingine. ugomvi ukavuka mipaka ya nyumba yao, ukafika kazini, polisi, ustawi wa jamii, mahakamani, yaani kila mahali. Wakawa vituko mbele za watu
Huku akimpenda mwanae kupita kiasi, visa navyo viliongezeka. Akaamua kupanga chumba maeneo ya magomeni. Kila akichoka kero za mkewe, anaaga kuwa kasafiri kikazi na kujipunzisha hadi wiki moja kwenye chumba chake cha kupanga kisha anarudi kumwona mwanae.

Anaongeza kuwa hatamuacha mwanamke huyo kamwe licha ya visa vyote anavyomtendea kwa kuheshimu jinsi alivyompa faraja pale alipokubali kuzaa nae wakati ambapo alianza kupoteza matumani ya kuwa baba wa mtu maishani wake.

niliposikia habari zake kwanza nilimhurumia nikamtafuta nizungumze nae kuangalia kama kama naweza kumsaidia. Tunaendelea na mashauriano na wote wawili wanatoa ushirikiano wa kutosha,
mnawashauri nini hawa?
 
Waungwana,
Kabla ya mwaka mmoja wa ndoa maisha yakabadilika. Kila wanapopishana jambo, mwanamke anatishia kuwa atatoa siri yake na kujiua yeye pamoja na mtoto kwani anasema hawezi kufa peke yake akamuacha mwanae alelewe na mwanmke mwingine. ugomvi ukavuka mipaka ya nyumba yao, ukafika kazini, polisi, ustawi wa jamii, mahakamani, yaani kila mahali. Wakawa vituko mbele za watu>
</p>
Mbona ghafla mambo yameenda mbali namna hii....Kwanini kuongelea habari za kujiua? .. Kuna kisa kikubwa sana hapa ambacho UMEKIRUKA..hujasimulia...PIA NINACHOSHINDWA KUELEWA, KWANINI HUYO MWANAMKE ASEME ATATOA SIRI,,kuna siri gani?..maana kama ni ile ishu ya ku'do huku akiwa na mabandeji kwenye naniliu, mi sioni kama ni siri ya tishio kihivo!.....Iko kitu hapa...N/W/Searching~~~~~~~~~~~~~~~~~</p>
 
</p>
Mbona ghafla mambo yameenda mbali namna hii....Kwanini kuongelea habari za kujiua? .. Kuna kisa kikubwa sana hapa ambacho UMEKIRUKA..hujasimulia...PIA NINACHOSHINDWA KUELEWA, KWANINI HUYO MWANAMKE ASEME ATATOA SIRI,,kuna siri gani?..maana kama ni ile ishu ya ku'do huku akiwa na mabandeji kwenye naniliu, mi sioni kama ni siri ya tishio kihivo!.....Iko kitu hapa...N/W/Searching~~~~~~~~~~~~~~~~~</p>

mi nilivyoongea nao ,sikuona kosa kubwa la mtu kutishia kujiua. nilichokiona ni kuwa mama alitaka kumfunga mzee mdomo, hivyo ilikuwa kama kutishia nyau! nasema hivyo kwa sababu kabla mama hajakubali kukutana na mimi niliwahi kumshauri mzee kupuuza tishio hilo na asimamie suala lolote analoamini kuwa sawa, baada ya mama kuona mzee hatishiki tena na tishio lake, ndio akaanza kusemasema ovyo nje kuhusu kila wanchogombania huku akimkomoa kwa kufika kazini mara kwa mara na mwanae kwa kisingizio cha kufuata matumizi hata pale ambapo ameishaachiwa matumizi nyumbani!

siri anayotishia kutoa ni kuhusu maumbile ya mzee, kwani yalibadilika baada ya upasuaji. naona ni upungufu tu wa hekima kumnyanyapaa mwenzi wake kwa matatizo ua ugonjwa!
 
Anaongeza kuwa hatamuacha mwanamke huyo kamwe licha ya visa vyote anavyomtendea kwa kuheshimu jinsi alivyompa faraja pale alipokubali kuzaa nae wakati ambapo alianza kupoteza matumani ya kuwa baba wa mtu maishani wake.

ilikuwa ni mtoto mapatano yao,mtoto ndo kashapatikana,baba hana mapenzi na mama,na mama hana mapenzi na baba.na hiyo njemba inampenda mwanae tu na si mkewe.mi nadhani ushauri mzuri ambao utakuwa na faida kwao ni kuwashauri hawa watu wajifunze kupendana kazi ambayo ni ngumu sana tena sana.kwa sababu kaz hiyo ni ngumu ni vyema wafanye kitu rahisi ambacho ni kuachana.kuna namna nyingi ya kulipa hisani si lazima kumng'ang'ania mtu ambae humpendi na yeye hakupendi.mwache aende zake.inaelekea vituko vinakuja kwa kuwa huyo mwanamama kashaona mapenzi hakuna baada ya njemba kupata alichotaka.
 
ilikuwa ni mtoto mapatano yao,mtoto ndo kashapatikana,baba hana mapenzi na mama,na mama hana mapenzi na baba.na hiyo njemba inampenda mwanae tu na si mkewe.mi nadhani ushauri mzuri ambao utakuwa na faida kwao ni kuwashauri hawa watu wajifunze kupendana kazi ambayo ni ngumu sana tena sana.kwa sababu kaz hiyo ni ngumu ni vyema wafanye kitu rahisi ambacho ni kuachana.kuna namna nyingi ya kulipa hisani si lazima kumng'ang'ania mtu ambae humpendi na yeye hakupendi.mwache aende zake.inaelekea vituko vinakuja kwa kuwa huyo mwanamama kashaona mapenzi hakuna baada ya njemba kupata alichotaka.

mimi naona tofauti kidogo mkuu

kwa kuwa tatizo ni tabia, linaweza kurekebishwa na ushauri nasaha, tabia hubadilika na naamini hata huyu mama atabadilika. pia naona kuwa mapenzi yapo, na commitment pia zipo za kutosha.

naona baba anafanya vyema kuheshmu wema wa mama na ni hii hii heshima ndiyo itakayomleta mama miguuni kwa baba kuomba msamaha siku moja, ni suala la muda tu ndugu yangu. na watu hawa bado wako kwenye mchakato wa kujenga mapenzi na kuheshimiana. kumbuka walifunga ndoa chini ya shinikizo la kimaumbile, kwa hiyo hawajawahi kupendana kwa dhati hadi nyoyo zao zikaridhika na sasa ndio wanajenga mapenzi wakiwa tayari na mtoto. naamini huyu mtoto atayakoleza zaidi mapenzi yao pindi yatakapoanza.
 
Huenda huyo mwanamke anadhani anaweza kum-blackmail jamaa. Kwani kuna maumbile mazuri ya kike au kiume? Kama huyo bwana aliweza kumega mpaka kumpa ujauzito hapo hata akitoa hiyo siri namwambia we toa tu sioni kama kuna tatizo..
 
Waungwana,
Kuna mwanaume mmoja aliyefanikiwa kimaisha kwa kiasi cha kuridhisha, alinisimulia kisa chake kikanisikitisha sana.

Alipokuwa anatafuta mchumba wa kuoa, bila kutarajia alipata maradhi mabaya ya mfumo wa uzazi yaliyopelekea kufanyiwa upasuaji katika taasisi ya mifupa muhimbili (MOI). Kwa mujibu wa madaktari, kulikuwa na uwezekano mdogo sana wa kupata watoto maishani mwke.
Hii haikuwa habari nzuri kwake, akachanganyikiwa, akaazimia kuwa lazima apate motto/mimba haraka iwezekanavyo hata kabla hajapona upasuaji aliofanyiwa!

Ndio, alikurupuka akaongea na binti mmoja waliyekutana nae kwa jirani yake suku za nyuma na ambaye hakupata kuwa mpenzi wake kabla, amsaidie kumzalia motto angalau wa kumbukumbu ya maisha yake, na yeye yuko tayari kwa lolote. Binti alimpa sharti la kumuoa, akakubali kama kufumba na kufumbua na kumtaka siku hiyohiyo apeleke taarifa kwao na ikawa hivyo.

siku hiyohiyo wakakutana kitandani Yule bwana akiwa bado kafungwa bandeji sehemu nyeti alikofanyiwa upasuaji na kwa kukiuka ushauri wa madaktari wake waliomzua kufanya ngono hadi watakaridhika kuwa afya yake imetengemaa, wakafanya shughuli kwa uangalifu mkubwa kuzuia asitoneshwe na waliendelea hivyo hadi walipopata walichokuwa wakikitafuta yaani mimba. ndoa ikafungwa, mtoto akazaliwa, mume akashusha pumzi kwa shukrani

Kabla ya mwaka mmoja wa ndoa maisha yakabadilika. Kila wanapopishana jambo, mwanamke anatishia kuwa atatoa siri yake na kujiua yeye pamoja na mtoto kwani anasema hawezi kufa peke yake akamuacha mwanae alelewe na mwanmke mwingine. ugomvi ukavuka mipaka ya nyumba yao, ukafika kazini, polisi, ustawi wa jamii, mahakamani, yaani kila mahali. Wakawa vituko mbele za watu
Huku akimpenda mwanae kupita kiasi, visa navyo viliongezeka. Akaamua kupanga chumba maeneo ya magomeni. Kila akichoka kero za mkewe, anaaga kuwa kasafiri kikazi na kujipunzisha hadi wiki moja kwenye chumba chake cha kupanga kisha anarudi kumwona mwanae.

Anaongeza kuwa hatamuacha mwanamke huyo kamwe licha ya visa vyote anavyomtendea kwa kuheshimu jinsi alivyompa faraja pale alipokubali kuzaa nae wakati ambapo alianza kupoteza matumani ya kuwa baba wa mtu maishani wake.

niliposikia habari zake kwanza nilimhurumia nikamtafuta nizungumze nae kuangalia kama kama naweza kumsaidia. Tunaendelea na mashauriano na wote wawili wanatoa ushirikiano wa kutosha,
mnawashauri nini hawa?
hii khabbar ni kweli? jamaa kapindua serikali na mabendeji afta kupasuliwa?
huyu jamaa anaitwaje? huyu ni shujaa na inabidi japo barabara moja hapa bongo tuipe jina la shujaa huyu.
 
hii khabbar ni kweli? jamaa kapindua serikali na mabendeji afta kupasuliwa?
huyu jamaa anaitwaje? huyu ni shujaa na inabidi japo barabara moja hapa bongo tuipe jina la shujaa huyu.

hahahahaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!!!!!!!!!!!!!!!

nalifikiria wazo lako mkuu.

lakini siku zote nakumbusha kuwa usifanye mchezo na vita ya kisaikolojia, unaweza kufanya jambo ukamwacha kila mtu kinywa wazi!!!!!!!!!!!!!

huyu jamaa alikuwa atika vita kali na saikolojia yake
 
Huenda huyo mwanamke anadhani anaweza kum-blackmail jamaa. Kwani kuna maumbile mazuri ya kike au kiume? Kama huyo bwana aliweza kumega mpaka kumpa ujauzito hapo hata akitoa hiyo siri namwambia we toa tu sioni kama kuna tatizo..

kimsingi, mimi binafsi sioni siri hapo! kwani nani asiyejua ugonjwa, au nani asiyejua maumbile yoyote hata mguu ukifanyiwa upasuaji mkubwa waweza kubadilika maumbile, sembuse nanihii????

ndio maana moja ya ushauri wangu kwake ni kupuuza hofu hiyo ya siri na tishio la mama kwa mtoto
 
Waungwana,
Kuna mwanaume mmoja aliyefanikiwa kimaisha kwa kiasi cha kuridhisha, alinisimulia kisa chake kikanisikitisha sana.

Alipokuwa anatafuta mchumba wa kuoa, bila kutarajia alipata maradhi mabaya ya mfumo wa uzazi yaliyopelekea kufanyiwa upasuaji katika taasisi ya mifupa muhimbili (MOI). Kwa mujibu wa madaktari, kulikuwa na uwezekano mdogo sana wa kupata watoto maishani mwke.
Hii haikuwa habari nzuri kwake, akachanganyikiwa, akaazimia kuwa lazima apate motto/mimba haraka iwezekanavyo hata kabla hajapona upasuaji aliofanyiwa!

Ndio, alikurupuka akaongea na binti mmoja waliyekutana nae kwa jirani yake suku za nyuma na ambaye hakupata kuwa mpenzi wake kabla, amsaidie kumzalia motto angalau wa kumbukumbu ya maisha yake, na yeye yuko tayari kwa lolote. Binti alimpa sharti la kumuoa, akakubali kama kufumba na kufumbua na kumtaka siku hiyohiyo apeleke taarifa kwao na ikawa hivyo.

siku hiyohiyo wakakutana kitandani Yule bwana akiwa bado kafungwa bandeji sehemu nyeti alikofanyiwa upasuaji na kwa kukiuka ushauri wa madaktari wake waliomzua kufanya ngono hadi watakaridhika kuwa afya yake imetengemaa, wakafanya shughuli kwa uangalifu mkubwa kuzuia asitoneshwe na waliendelea hivyo hadi walipopata walichokuwa wakikitafuta yaani mimba. ndoa ikafungwa, mtoto akazaliwa, mume akashusha pumzi kwa shukrani

Kabla ya mwaka mmoja wa ndoa maisha yakabadilika. Kila wanapopishana jambo, mwanamke anatishia kuwa atatoa siri yake na kujiua yeye pamoja na mtoto kwani anasema hawezi kufa peke yake akamuacha mwanae alelewe na mwanmke mwingine. ugomvi ukavuka mipaka ya nyumba yao, ukafika kazini, polisi, ustawi wa jamii, mahakamani, yaani kila mahali. Wakawa vituko mbele za watu
Huku akimpenda mwanae kupita kiasi, visa navyo viliongezeka. Akaamua kupanga chumba maeneo ya magomeni. Kila akichoka kero za mkewe, anaaga kuwa kasafiri kikazi na kujipunzisha hadi wiki moja kwenye chumba chake cha kupanga kisha anarudi kumwona mwanae.

Anaongeza kuwa hatamuacha mwanamke huyo kamwe licha ya visa vyote anavyomtendea kwa kuheshimu jinsi alivyompa faraja pale alipokubali kuzaa nae wakati ambapo alianza kupoteza matumani ya kuwa baba wa mtu maishani wake.

niliposikia habari zake kwanza nilimhurumia nikamtafuta nizungumze nae kuangalia kama kama naweza kumsaidia. Tunaendelea na mashauriano na wote wawili wanatoa ushirikiano wa kutosha,
mnawashauri nini hawa?

hivi wewe ulisoma IJMC?
 
Huyo mama hana cha kumtisha huyo bwana, hofu kubwa ni hapo tu anasema kujiua na kuua mtoto. Hakuna siri dunia hii yeyote anaweza pata maradhi, mbona kuna watu wengi sana wako ndani ya ndoa hawana watoto na wake au waumeza zao hawana vitisho.

Tatizo la huyo bwana hakuangalia nani apate ane mtoto kwa wakati ule. Wanawake wengine ni Primitive especially unapowambia ukweli kuhusu yanayokusibu. Hatuna subira wala nini tunavehave differently. Huyo bwana akaze uzi tu, akitishiwa aende zake magomeni akirudi mambo shwari. Aombe Mungu amuonyeshe njia, kama anatishia kuua mtoto ni police case, apimwe akili anayang'anywe mtoto au aache vitisho.
 
sasa huyu mama ajiue sababu ya nini? mbona mie sioni cri hapo....ndoa zina majaribu jamani, na huyu baba kinachomuhamisha kwake ni nini?....mgombea ubunge samahani ni visa gani huyu mama anavifanya kwa huyu baba mpaka ahame kwake wiki nzima?
 
sasa huyu mama ajiue sababu ya nini? mbona mie sioni cri hapo....ndoa zina majaribu jamani, na huyu baba kinachomuhamisha kwake ni nini?....mgombea ubunge samahani ni visa gani huyu mama anavifanya kwa huyu baba mpaka ahame kwake wiki nzima?

kuna visa vingi sana na thread nimeifupisha tu, vipo vinavyohusu simu, housegirl wao, jirani yake mmoja, ndugu za mkewe wanaokaa pale, mashoga zake wa barabarani nk. mfano kuna siku amepiga mlango kwa mawe usiku mzima kumshinikiza akiri kuwa anatembea na jirani yao mmoja na haikuwa kweli, siku nymingine kamkuta ananunua bidhaa dukani akamshambulia kwa mawe hadi akamjeruhi mkono kwa sababu amepitia dukani kabla hajafika nyumbani nk. ni visa vingo sana
 
Huyo mama hana cha kumtisha huyo bwana, hofu kubwa ni hapo tu anasema kujiua na kuua mtoto. Hakuna siri dunia hii yeyote anaweza pata maradhi, mbona kuna watu wengi sana wako ndani ya ndoa hawana watoto na wake au waumeza zao hawana vitisho.

Tatizo la huyo bwana hakuangalia nani apate ane mtoto kwa wakati ule. Wanawake wengine ni Primitive especially unapowambia ukweli kuhusu yanayokusibu. Hatuna subira wala nini tunavehave differently. Huyo bwana akaze uzi tu, akitishiwa aende zake magomeni akirudi mambo shwari. Aombe Mungu amuonyeshe njia, kama anatishia kuua mtoto ni police case, apimwe akili anayang'anywe mtoto au aache vitisho.

ni kweli mambo haya yameishawafikisha polisi, ustaw wa jamii mahakamani nk. mimi niliwashauri waondoe shauri lao huko kwenye vyombo vya sheria tuliangalie kijamii zaidi, walikubali na tunaendelea na mazungumzo vizuri
 
Back
Top Bottom