LHRC yaitisha Maandamano nchi nzima kupinga malipo ya DOWANS

Hawa waache ujinga. Mahakama imeamru ilipwe na hapo wanapinga maamuzi ya mahakama. Maamuzi ya mahakama yanapingwa mahakamani.
Watu waache kutufanya mataahira, kinachotakiwa waangalie ni vipi tumeingia katika hali tuliyoingia? Uongo ulikuwa wapi? Nani kamdanganya nani?
Huu ndio ukweli ambao haujasemwa ambao utaendelea kuwaumiza wananchi na watu wengi. Waishinikize bunge waunde kamati mpya waangalie ni kwanini badala ya kuikoa nchi kutokana na giza na kulipa mapesa mingi sasa tunalipa mapesa bure. mitambo iliyokuwa mibovu ndiyo sasa inatupa umeme kupitia symbion. wale wabunge waliosema tusinunue wako wapi leo?

Kuna unafiki mkubwa na hawa LHRC inatakiwa waandamane siyo kwa kupinga malipo ya dowans bali kudai tume huru ya kuchunguza tatizo kwa ujumla wake kuanzia kwa wabunge waliochunguza mara ya kwanza nao wachunguzwe kuwa je walikuwa na manufaa binafsi ya kisiasa na kiuchumi au vipi. Kuna mambo mengi ya kuangalia kwa ujumla wake na siyo hizi dalili za juujuu tu.
Hakijaharibika kitu,Kupitia wanachi serikali itaamka na kwenda mahakamani kupinga.Lakn bila PUBLIC PRESSURE mabadiliko hayatakuwepo....upo?dont blame juhudi za wapigania Haki.kwani wewe umefanya nini ?
 
huwa hakuna rufaa kwenye abitration,once abitral award ikitolewa inakuwa final and conclusive and it binds both parties!hata kama kutakuwa na ukiukwaji wa sheria katika utolewaji wake stil inabind both parties!so anayeongelea kukata rufaa mahakaman hakuta2saidia chochote!i guess wananch wenyewe kupinga mayb inaweza kusaidia!
 
Tujitokezeni ndugu zangu kwa wingi tusiogope kufa ndio ushujaa ndugu zangu.

Tuwaage wake zetu tunaweza tusirudi tunakwenda vitani
 
Kama kweli tuna uzalendo wa kweli na nchi yetu, kama tunathamini kodi zetu na tuanhitaji serikali iwajibike kwetu na muda wote iwe sikivu na kufanya kazi kwa maslahi ya umma, basi hatuna budi kujitolea kuingia barabarani kadri itakavyokuwa imeelekezwa na waandalizi wa maandamano hayo.

Tusiishie kuandika maneno mengi kwenye mitandao tukiwa tumejificha nyuma ya computer lakini tunapohitajika kuonyesha yale tunayoyasema kwenye mitandao kwa vitendo, tunapoteana.

Bila shaka kipimo cha uzalendo wetu ndio hiki, tuonyeshe uzalendo wetu, tupinge wizi wa mchana na zaidi tushinikize wale wote waliotuingiza kwenye huu mkenge washughulikiwe kikamilifu.
 
Inatia moyo kuona sehemu kubwa kiasi hiki cha Wa-Tanzania KUNAONEKANA MWAMKO NA UELEWA MPANA zaidi kiasi cha kuweza kuiambia serikali kwamba ufisadi hapana.

Haya maandamano yalioitishwa ni ya HAKI TENA WAJIBU wa kila mmoja wetu kukataa ufisadi wa Dowans ili ugumu wa maisha usijeongezeka zaidi.
 
Me nasema wawalipe kwa 7bu hayo ndo Matokeo ya kuwa na Serikali Mbovu, Wala hakuna haja ya Mwananchi kuandamana, Mangapi tulipinga lkn serikali yetu ikayafanya kwa nguvu? Cha msingi tukubaliane na kila hali, NGUVU kubwa tuilekeze kwe Uchaguzi wa 2015, tuwafyatue hawa Magamba. "NCHI IMECHAKAA INAHITAJI UKARABATI WA HALI YA JUU IRUDISHE HESHIMA YAKE"

Ukilipa umelipa mafisadi wa ccm.halipwi falah yoyote
 
Jamani acheni kupiga kelele Tanzania tunafuata utawala wa sheria hivyo tusitegemee kupindasha sheria wakati SISI ndio tulikiuka makubaliano ya mkataba halili
 
Tujitokezeni ndugu zangu kwa wingi tusiogope kufa ndio ushujaa ndugu zangu.

Tuwaage wake zetu tunaweza tusirudi tunakwenda vitani

Najua unajituma kutisha watu ili nape akipita usiku aone kazi nzuri uliyofanya kutwa nzima ya leo.

Lakini utambue ya kwamba pamoja na vitisho vyako watu tutajitokeza kwa wingi sana kuandamana.

Na haki yetu watanzania na ukombozi wa nchi yetu utakapopatikana tutakukaribisha kujumuika nasi kwani tunajua ni njaa tu inakusumbua, huna mapenzi yoyote na ccm.

Kama ccm wangekuwa wamekuandaa vizuri kielimu na kiajira, usingekuwa unatumika vibaya kiasi hiki, pole lakini tutafika tu.
 
Yah ni jambo la kuunga mkono! but hawa watu mara zoto mambo yao wamekuwa wakifanya kwa shinikizo, na hela kutoka kwa wahisani. hapo tu ndo wanaponimaliza nguvu, na kuwaona kuwa ni wasanii..
 
Hakijaharibika kitu,Kupitia wanachi serikali itaamka na kwenda mahakamani kupinga.Lakn bila PUBLIC PRESSURE mabadiliko hayatakuwepo....upo?dont blame juhudi za wapigania Haki.kwani wewe umefanya nini ?

Habari yake mama, umeadimika sana mpendwa.

Kwa taarifa yako serikali imeshatoa notice ya kusudio la kukata rufaa kupinga hukumu hiyo mahakama ya rufaa.

Lakini wajuvi wa sheria wanasema hiyo rufaa ni kanyaboya. Wanasema kwa mujibu wa mkataba kati ya TANESCO na Dowans, na kwa mujibu wa ruling ya ICC hakuna rufaa hapo. Ruling yao ndio mwisho. Hapa serikali inataka kutupiga mchanga wa macho.
 
This is a good move.

Kudos my fellow Tanzanians back home!!!

Suala la kutaja tarehe litasababisha wale wazee wa intelijensia wakiongozwa

na kaka yao S. Mwema wajipange.

I think the date should be communicated in less than 12 hours

to maintain that surprise element and catch them off guard.

Pia ni vizuri kubeba ndoo za maji na vitaamba vimlivoloa na pia wakipiga mabomu

hayo ya machozi dawa ni kuyakamata na kuyatupia katika ndoo hizo zenye maji

na hayatakua na athari tena. If we manage to hold them up for half an hour they

will run out of their tear gas and their water canon vehicle cant hold more than

10,000lts and spits 300lts in a minute.

If all this is taken into account this peaceful demonstration would be the very

successful event ever organised and carried by Tanzanians together.
 
Serikali legelege ya CCM,Serikali isiyo kuwa na kichwa wala miguu,serikali ya malimbukeni inayoongozwa na rais mvivu kufikiri.
 
Wanaharakati ni sehemu ya cdm?

Kwanini wasiandamane kwa kuwa sasa tanesco inalipa gharama kubwa sana kwenye mkataba na symbion kuliko wakati wa doawans

Au kwakuwa symbion ni wakristo?
 
Mm tayari nguo nyeusi ninayo, hapa nachosubilia ni siku na muda. tukimaliza hizo siku 10 za lhrc tunaunganisha tena siku 10 za cdm.
 
member wa jf kwa kuunga mkono hoja hawajambo ila kwenye kucomment baada ya tukio utajuta kila mtu mtaalam..

ngoja nione impact yake mi kazi yangu itakuwa ku upload image tu..
 
Wanaharakati ni sehemu ya cdm?

Kwanini wasiandamane kwa kuwa sasa tanesco inalipa gharama kubwa sana kwenye mkataba na symbion kuliko wakati wa doawans

Au kwakuwa symbion ni wakristo?

wewe ndio wasema
 
Kwa mujibu wa chanzo makini maandamano hayo yameandaliwa na LHRC ili kutoa fursa kwa wananchi wengi kuhudhuria bila kujali itikadi. Ni kweli kama yangekuwa ya kichama zaidi kuna baadhi ya wananchi si wanachama au wafuasi wa chama hicho lakini wanachukia malipo ya Dowans hivyo watakosa fursa au watakuwa marginalized katika mchakato huu. Licha ya hivyo, chama cha CDM kitatoa wito wa wafuasi na mashabiki wake kuyaunga mkono maandamo hayo kwa nguvu zote.

Kwani haya ndo aliyoyatangaza Mh Mnyika au?!
 
Aisee nikiangalia wardrobe yangu Nguo nyeusi ni za kutokea usiku tu; ngoja kesho nikatafute Nguo black za kutosha hizo siku kumi.

I am in total support of maandamano!
 
Back
Top Bottom