Elections 2010 Let's not lose hope

Newvision

JF-Expert Member
Nov 9, 2010
446
29
Nipo ughabuini Brazil ambapo nako siku hiyo hiyo walikuwa na uchaguzi. Majibu ya Rais yalitoka hadharani masaa 6 badaa ya kufunga kupiga kura huko kwetu kuna mdudu gani kama si wizi mtupu??? Nawashukuru sana wana JF kwa habari kem kem juu yaliyojiri kuhusu uchaguzi ingawa pia JF inao watu wasio na progressive minds pia.
Nasikitika kuwa katika ndoto yangu haikutimia kwani hatimaye hatuna serkali ya watu bali ya watetezi wa mafisadi kwa miaka mingine mitano!! INANIUMA. Hapa Brazil elimu ni bure mpaka University ila kazi ni kwa kijana kufanya kazi darasani apte grades nzuri na wala si kucheza bongo fleva.Huko kwetu eti pesa zimewekwa benki ughaibuni na mafisadi na elimu bure eti HAIWEZEKANI. Hawa jamaa hawana madini wala mbuga za wanyama wala bandari inayotegemewa na nchi 6 kama ya Dar! Wana JF kuna mengi lakini hayo ni machache tu. Lakini kwa sasa ni kuwa uchaguzi umeisha na baba wa mafisadi ameapishwa la kufanya ni kujenga mkakati mpya kwa ajili ya 2015. Ninaamni watanzania waliiondoa CCM kupitia ballot box hakuna asiye jua hilo. Msomi Peter Slaa (PhD) anajua hilo pia. Tufanye nini sasa??
a) Mbinu zote zilizotumika ziwekwe hadharani ili dunia yote ijue kwa hiyo kila mwenye hard evidence juu ya udanganyifi uliofanyika awape wapenda mapinduzi tuufahamu na tuzifanyie kazi ikiwezekana the law of the land has to take its course.
b) Tumepata wabunge si wengi lakini wapo, tuhimize uwajibikaji wao ili iwepo difference kati ya hao jamaa wapenda status quo na wanapenda maendeleo ya kweli kwa nchi yetu Tanzania. Wasidhanie wamefika sasa kazi imeisha they have to prove that they have something to offer for our blessed nation. J.F.Kennedy alisema “ask yourself what you can do for your nation and not what the nation can do for you”wajiulize watafanya nini kuisaidia TZ yetu ijikomboe na ufisadi huko bungeni
c) Vijana regardless of political ideologies zetu tusiogope tuitee Tanzania yetu kwa kukataa kuwa wanafiki kama wengi katika tulionao. Tuingie katika mapambano tusiogope lakini sina maana tuanze vita. Wapinzani wasibebe wanafiki mpaka 2015 kwenye vyama waondoeni haraka sana tuinject new and trustworthy blood.
d) Tuendelee kumwunga mkono Peter rais wetu in the waiting na wapenda maendeleo wengine he has a chance and God Knows.

Naomba kuwasilisha
 
Amina na tuzidi kuelimisha raia mmoja baada ya mwingine kuhusu haki na elimu nzima ya kupiga kura,naamini kwa miaka hii mitano elimu hii itakuwa imewafikia wengi.
 
hujui unachokisema ndo maana mtumwa huko...... ungekuwa unajua unachokisema ungekuwa tandahimba, kajamba nani kweni
 
Back
Top Bottom