Leo naomba nimtetee mheshimiwa raisi wangu ndugu J M Kikwete

Binafsi naamini kuwa kwa sasa lile Azimio la Arusha haliwezi kufanya kazi kwa sasa kwa sababu ujamaa kwa Tanzania ya sasa ni kitu kigumu sana, mi nadhani kama wataalamu wetu wakikaa na kutoka na kitu kinachofanana na Azimio la Arusha lakini liwe Azimio linaloendana na maisha yetu ya sasa.

Maisha yetu ya sasa ndio yapi hayo?
 
unanchoongea na dhani labda ni kutokana na uelewa mdogo au vipi,kwanza

  • kanda ya ziwa kuwa nchi au pwani sio kigezo cha kuwa tajiri maana hiyo ni mikoa tu au kanda,na wakuu wake huteuliwa na rais wa nchi maana ndio kapewa power hiyo kwa hiyo hata kama kanda ya ziwa ingekuwa nchi na rais wake akawa kikwete ingekuwa masikini hivyo hivyo maana iko chini yake sasa,
  • kwa kawaida wananchi hawachagui rais ili rais yule aende tra akakusanye kodi za bidhaa,au akaendeshe katapila ajenge barabara au abebe chaki aingie darasani afundishe watoto ,hapana hatuchagui rais ili ayafanye yeye,anachaguliwa ili ateue timu imara itakayoweza kutekeleza yote kwa vitendo,kwa hiyo ubora wa rais yeyote utauona kwenye timu yake inavyotekeleza yale anayoiagiza timu yake ifanye,ndio maana tumempa mamlaka ya kuteua mawaziri,wakuu wa mikoa na wengine wengi ili hao watekeleze yale rais amepanga kufanyia wananchi,wanaposhindwa wale sio wao ni rais maana aliomba ridhaa ya kuliongoza taifa kumbe hajui timu aipange vipi kwa hiyo RAIS ndio msaliti namba moja kwa yote unayoona mikoa ilivomasikini

Unadhani ni kwa nini hao wasaidizi wake wameshindwa kumsaidia vya kutosha mh. raisi?
 
Kwanza kabisa naomba niseme kama wewe unadhani utachangia hizi hoja zangu kwa matusi ni bora ukasoma tu na kupotezea, natamani kuona wale wote watakao changia hapa wachangie kwa lengo la kujenga na sio kujionesha bora zaidi ya wengine. Nikiwa kama mtanzania wa kawaida nisiyeamini katika chama chochote kile cha siasa katika hii dunia lakin mfuatiliaji mzuri wa masuala ya siasa za dunia (nadhan ni kwa vile nasoma POLITICAL SCIENCE AND PUBLIC ADMINISTRATION (BA PSPA)) nimeguswa kidogo leo walau kumtetea raisi Kikwete japo mi sio msaidizi wake wala sio mfuasi wake ila kama mtanzania nliye chini ya utawala wake naamini nina haki 100% kumtetea raisi wangu kwa nguvu zangu zote.
Katika mitandao mbalimbali na hata hapa JF raisi Kikwete amekuwa akipewa lawama kibao mfano juu ya ufisadi, umaskini wa mtanzania, kushuka kwa uchumi, kuwa mzito wa kutoa maamuzi n.k naamini hizi lawama zote JK anazifahamu ila aidha kwa kuzipuuzia, au kwa kuwaacha watu waongee tu watakavyo coz kuna uhuru wa kuongea am eamua kukaa kimya. Binafsi naomba nitoe ufafanuzi kidogo wa baadhi ya lawama kwa mh. raisi.

1) Tanzania tupo nyuma kimaendeleo tukijilinganisha na jirani zetu. Hii ni kweli sisi tupo nyuma kimaendeleo ukitulinganisha na nchi kama Kenya na Rwanda, lakin hii sio kwa sababu ya JK, kihistoria Kenya ilikuwa kolononi la kilowezi yaani ni kwamba wazungu walikaa/kuishi Kenya na kujenga miundombinu na huduma za kijamii mfano hospitali, shule n.k, pia walianzisha mashamba makubwa pia kwa kuwa Muingereza ndiye aliyekuwa mtawala wa nchi nyingi za Afrika mashariki, aliifanya Kenya kama makao makuu yake, kwa sababu hii Muingereza aliweza kuijenga Kenya zaidi kuliko koloni lolote lile ndani ya Afrika Mashariki ndo maana leo Kenya ipo juu zaidi ya nchi zote za Afrika Mashariki.
Kwa upande wa Rwanda, naamini wote mnatambua kuwa Rwanda kijografia ni nchi ndogo sana kwa kuilinganisha na Tanzania kitu ambacho kinawasaidia wanyarwanda kusimamia shughuli za kimaendeleo na mali asili zao kikamilifu zaidi.

2) Kuwateua rafiki zake kuwa wasaidizi wake wakuu katika uongozi wake. wengi wanaamini kuwa kosa kubwa alilofanya JK ni kuwateua rafiki zake kuwa wasaidizi wake kitu ambacho kinamsababisha kushindwa kuwachukulia hatua za kinidhamu pindi wanapofanya makosa, Binafsi naamini kuwa JK hakufanya kosa kuwateua rafiki zake kwa sababu kiongozi yeyote yule huteua wasaidizi ambao kwa 100% anaamini kuwa watamsaidia katika uongozi wake, hakuna raisi anayeteua watu asioamini kama watamsaidia kutimiza lengo lake, naamin hata siku mimi nikiwa raisi siwezi kukuteua wewe nisiyekufaamu wala kuamini kama kweli utanisaidia katika uongozi wangu. Kuhusu kutokuwachukulia hatua hawa wasaidizi wake naielezea hapa kwa chini.

3) Kuchelewa kufanya maamuzi au kushindwa kabisa kufanya maamuzi. Inasemekana kuwa na huu ni udhaifu wa JK, kwanza naomba niseme kuwa mtu kuwa raisi ni tofauti na mtu kuwa baba au mwenyekiti wa taasisi fulani, sifa kubwa ya mfanya maamuzi ni kupima faida na hasara za maauzi atakayofanya katika jamii husika na kama maauzi hayo yana faida kubwa kwa jamii yambidi ayafanye na kama hayana faida kubwa kwa jamii sio lazima/haitakiwi kuyafanya hayo maamuzi. Hapa naomba niwakumbushe tu kuwa JK ni raisi na mwenyekiti wa CCM ivyo basi katika maamuzi yake ni lazima yawe na faida kote kote kwa CCM na kwa serikali, maamuzi yeyote kwa serikali yasiyo na faida kwa chama hayatakiwi, hii sio kwa CCM tu bali hata wewe chama chako kikiingia madarakani kitafanya hivi, na kwa sababu hii ndio maana anashindwa kuwachukulia hatuna wasaidizi wake wa karibu haswa haswa mawaziri kwa lengo la kukilinda chama kisisambaratike.

4) Kusafiri nchi za nje na kuomba misaada. Naamini hata kama Obama ndo angekuwa raisi wetu naye angekuwa anasafiri kama JK anavyosafiri, watanzania wenzangu, japokuwa tuna rasilimali nyingi sana hapa kwetu tatizo ni kwamba hatuwezi kuzitumia hizo rasilimali sisi wenyewe, mbali na kuzitumia hata namna ya kuzivuna hatujui kwa sababu teknolojia yetu ni ya chini saaaana, hivyo ili walau tufaidi kidogo hizi rasilimali zetu tutahitaji kuwaomba wenye ujuzi na teknolojia yao waje watunyonye kidogo, hali hii haisababishwi na JK bali ni kwa sababu ya mfumo tulioachiwa na wakoloni (ukoloni mamboleo)

kwa udogo na uchache ndo hayo tu kwa leo.

Kwa uchambuzi huu inaonesha wazi alama ya juu uliyowahi kupata katika somo lolote la PS ni karai (alama C).
 
Mtoa mada utanisamehe na naomba ukubali nikisema kwamba, ingawa ulikuwa na nia njema (sina hakika sana na hilo), lakini ujafaulu kumtetea Kikwete na kwa kweli umemuumbua zaidi. Nitathibitisha kwamba umemuaibisha Raisi wetu. Kwa kusema kuwa Kenya imepaa kiuchumi kwasababu ya urithi wa wakoloni, unataka kusema kwamba kuwafukuza wakoloni Kenya na mahali pengine ilikuwa kosa? Mimi sioni hoja hiyo inavyomtetea kikwete. Je, nia yako ni kusema tumwache aende ende ulaya labda wakoloni watarudi tena watuendeleze kama Kenya? Halafu kuhalalisha uteuzi wa marafiki kuwa madarakani kwa kigezo cha kujuana, unaonesha kuwa Kikwete hakustahili kuwa Rais wa nchi kubwa kama Tanzania ambayo hata ujaliwe vipi uwezi kuwajua watu wote isipokuwa kwa kutumia mifumo ya kiutawala. Kwa maneno mengine, unataka kusema angefaa zaidi kuwa mwenyekiti wa kijiji ambaye anawafahamu wanakaya wenzake wote. Huku ni kumdhalilisha Rais wetu. Hoja ya kwamba anachelewa kufanya maamuzi kwa kuchelea kuvuruga mustakabali wa CCM pia haimuokoi. Rais anaapa kuwa kiongozi wa nchi, si wa chama chake tu. Na ni vizuri ukafahamu kuwa wapo waliomchagua ambao hawana vyama na wengine hawakumchagua lakini wanaishi katika nchi ambayo yeye ameapa kuitumikia. Ndiyo kusema katika urais nchi ndio ya kwanza na chama kinafuata. Kwa takwimu za karibuni, CCM ina wanachama kama milioni tano na kidogo hivi. Je, ni haki kuwatoa kafara raia zaidi ya milioni 35 kwa manufaa ya hao milioni 5? Hapa pia umemuabisha kwa kuonyesha kuwa alikula kiapo cha urais bila kuelewa kinamdai nini. Mwisho nikukumbushe kanuni ya maadili inayosema kuwa na nia njema pekee haitoshi, lazima pia uwe na uwezo wa kutenda na utende jambo jema kwa wakati wake.
 
Wewe nawe unasoma BA PSPA hujadisko au uko mwaka wa kwanza? au ubadilishe kozi haraka hakuna unachojaribu kuongea kama msomi wa hiyo kozi.
 
[h=2]Wewe utakuwa ni Shabiki la Liverpool Umechanganyikiwa ma Mwenenda wa Timu Yako
Man U Tunatesa tu Mwanzo Mwisho

2011/12 Barclays Premier League Table / Standings[/h]

  • Season:



April 10, 20122011-2012 Barclays Premier League Table
OverallHomeAway
POSTEAMPWDLFAWDLFAWDLFAGDPts
1
right_arrow.gif
Manchester United322543782713124215123136125179
2
right_arrow.gif
Manchester City32225575261510471074528164971
3
right_arrow.gif
Arsenal32194963411222351272728292261
4
right_arrow.gif
Tottenham Hotspur33178857381133351765522211959
5
up_arrow.gif
Newcastle United3317885042105226157362427859
6
down_arrow.gif
Chelsea33169856381033332066523181857
7
right_arrow.gif
Everton3313812383483621145561720447
8
right_arrow.gif
Liverpool32111011373459220136191721343
9
up_arrow.gif
Fulham33111012434385432243581119043
10
up_arrow.gif
Norwich City33111012465266425215482131-643
11
down_arrow.gif
Sunderland3311913424175424144491827142
12
down_arrow.gif
Stoke City3311913324575421164491129-1342
13
right_arrow.gif
West Bromwich Albion3211615394352918196462124-439
14
right_arrow.gif
Swansea City3210913354166419144391627-639
15
right_arrow.gif
Aston Villa3271411354445718223941722-935
16
right_arrow.gif
Bolton Wanderers32922136654210193250111733-2929
17
right_arrow.gif
Queens Park Rangers3277183556457192532111631-2128
18
right_arrow.gif
Blackburn Rovers3277184367511022292682138-2428
19
right_arrow.gif
Wigan Athletic3261016305727714254391632-2728
20
right_arrow.gif
Wolverhampton Wanderers3257203470321119382591532-3622


Champions League: 1st , 2nd , 3rd
Champions League qualifying: 4th
Europa League: 5th
Relegation: 18th , 19th , 20th
 
Mbona hakuna utetezi wowote? unazidi kuainisha kasoro tu. fanya utafiti kwanza uje na utetezi wa kisayansi.
 
Hiki kidenti lazima kilisoma HGK au HKL au HGL afu litakuwa kilipata division Three lazima kitakuwa kale kachuo pale KIGAMBONI tu... very poor thinking and un logical conclusions!
 
asije kuwa ni riz 1 au miraji ndo kaandika kumsafisha baba? Kama siyo wahi dodoma kuna hospitali iitwayo mirembe wacheki medula oblangata nahisi ina pancha

Atakua MwanAsha, what do you expect from her
 
If I were in his shoes I would do the exact opposite of what he is doing. People would be appointed to leadership positions not on the basis of religion or friendship but on the basis of their professionalism and ability to deliver. I would spend more time in the country making timely decisions on pressing issues instead of globetrotting. I would promptly fire any civil servant a' la Jairo who had been proven to put his hands in the nation's till.
those are your thought even a child would have the dream of becoming the great businessman but when he actual grow up he will realise that was a day dream...childish
 
Mtoa mada naomba niungane na wewe asilimia 100,watanzania baadhi yao wana akili fupi wenyewe all time they are think negative ,kwa mtindo huu mnajifanya mnafahamu kumbe bogas.hakuna kiongonzi anayesifiwa tanzania akiwa bado kiongozi(madarakani) ata kikwete atakuja kuwa mzuri pale atakapoondokoa madarakani lakini awali ya yote yapo mazuri na mengi zaidi yaliyofanywa na kikwete,acheni ubinafsi tusikalie kusema mabaya na mazuri pia tuyaweke wazi,kikwete ni rais anayekubalika kwa zaidi ya asilia 70 hapa tz na vile vile ata kimataifa. Lakini watanzania tulio wengi ni WAVIVU hatutaki kufanya kazi ili tuijenge nchi yetu na mwisho tumebakia kuiraumu selikari iliopo madarakani,ndugu watanzania tushikamane kuijenga tz tuachane na ubinafsi pamoja na unafki usio na tija katika maendeleo ya nchi yetu na wala tusipandikizwe uchafu wa viburi kuvuruga amani ya nchi yetu iliyoachwa na baba wa taifa.
 
wewe siye au wewe ni yule mbukoba wake nini? unatafuta urafiki akupe cheo na wewe? huu sio uwanja wako, dah!!! imenichosha
 
binafsi nimechoka kuandika poorand weak argument

Naona ubongo wako umechoka zaidi. Hivi ukiyarejea haya matakataka uliyoandika hata wewe mwenyewe husikii kichefuchefu? Mawazo yako yananipa shida kuamini kuwa ulifika form 2. Acha nitumie kajimuda kidogo kufanya kazi ambayo iliwashinda walimu wa shule ya kata uliyosoma:
1. RWANDA NA KENYA: Ni akili potofu kuendelea kuulaumu ukoloni kwa yanayotokea miaka 50 baadaye. Unao ushahidi kama hii reli ya kati walioijenga wao wakoloni imekufa kwa sababu ya wakoloni?
Tumia akili yako vizuri wewe, kama Rwanda ni nchi ndogo basi na rasilimali zake nazo pia ni ndogo. Hapa unachojaribu kusema ni kuwa viongozi wa Tanzania wangeiongoza Rwanda ingeendelea zaidi. FOOLISH! Migodi, mito, mwaziwa na Bahari Rwanda hawana, sisi tunavyo na hilo hulioni. Sijui unasoma nini. Labda nikukumbushe kuwa, kuendelea kiuchumi kwa China na USA kunachangiwa na ukubwa wa hizo nchi na rasilimali.

2. UTEUZI: Bwana mjinga, uteuzi wa nyadhifa haufanywi kwa kuangalia nani unamfahamu bali nani anaweza. Kama aliwateua rafiki zake kwa vigezo unavyovijua wewe na sasa wameshindwa, unataka tumlaumu nani? Baba yako? Kama unadhani uongozi wa nchi ni sawa na kupanga orodha ya watu wa kuhudhuria harusi ya binti yako, basi ni bure kutumia fedha kukusomesha mtu kama wewe

3. MAAMUZI: Nikikuita mjinga utasema nimekutusi lakini nashindwa kupata jina lingine kwa ajili yako. Hapa ulivyoanzisha mada ulisema unamtetea Kikwete kama Rais wa Tanzania na si kama Mwenyekiti wa chama. Kwa akili yako mbovu unafikia kuamini kwamba unaweza kuilinda CCM kwa kutowawajibisha waovu walio ndani ya chama. Hivi (hebu tumia hiyo akili yako ndogo tu kufikiri) kwa kutomwajibisha aliyesababisha TWIGA wetu wabebwe na ndege ya jeshi la Qatar ni kukinusuru chama au kukiangamiza? Kutotoa tamko la mwisho juu ya nini ikulu inasema kuhusu posho za wabunge ni kukiinua chama au kukiangusha?

4.
Kusafiri nchi za nje na kuomba misaada. Naamini hata kama Obama ndo angekuwa raisi wetu naye angekuwa anasafiri kama JK anavyosafiri, watanzania wenzangu, japokuwa tuna rasilimali nyingi sana hapa kwetu tatizo ni kwamba hatuwezi kuzitumia hizo rasilimali sisi wenyewe, mbali na kuzitumia hata namna ya kuzivuna hatujui kwa sababu teknolojia yetu ni ya chini saaaana, hivyo ili walau tufaidi kidogo hizi rasilimali zetu tutahitaji kuwaomba wenye ujuzi na teknolojia yao waje watunyonye kidogo, hali hii haisababishwi na JK bali ni kwa sababu ya mfumo tulioachiwa na wakoloni (ukoloni mamboleo)
Hapa sasa naona si ujinga tu, na utoto ndani yake. Hatuwezi sababu ya uwepo wa watu wenye akili kama zako. Kwa hiyo wewe umeona ni bora kuomba badala ya kujifunza; ndicho unachosoma huko shuleni kwako hicho?!!!!!

Mimi naona unaidhalilisha elimu. Kama una zaidi ya miaka 25 basi ni disaster na kama still under 25 basi anza kukaa mbali na dada zako.

"Be wise with speed; a fool at forty, is a fool indeed"
 
Sidhani kama ni kweli mimi nafanya hicho unachodhani nakifanya, hebu tujaribu kufanya kitu kimoja hivi, jiweke kwenye nafasi ya JK then tell us what your going to do to save our country?

haki ya mungu mimi na wasiwasi na uzalendo wako, kama wewe si muhindi, mw arabu koko, utakua mchina, hata historia ya nchi hujui, kwani huyo unae mwita rais wako umesahau ndo alikuja na ari mpaya kasi mpaya nguvu mpaya, maisha bora kwa kila mtanzania, ajira kwa vijana. Kajipange upya.
 
Back
Top Bottom