Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,315
- 33,111
Venance George, Morogoro
TANZANIA katika kipindi cha huu wa fedha, imezalisha kiasi cha tani 60,741 za tumbaku badala ya lengo la kuzalisha tani 75,000.
Hayo yalisemwa juzi na Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Tumbaku Tanzania, Frank Urio alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mjini Morogoro.
Urio alisema katika kipindi cha mwaka jana, uzalishaji wa zao hili ulikuwa tani 50, 784 na kwamba hali hiyo inaleta matumaini ya kufikia malengo la kuzalisha tani 100,000 kwa mwaka.
Mkurugenzi huyo alisema kutofikia kwa lengo la kuzalisha tani 75,000 katika kipindi cha mwaka huu, kutokana na matatizo mbalimbali yaliyojitokeza katika uzalishaji wa zao hilo la biashara.
Alitaja matatizo hayo kuwa ni pamoja na uhaba wa wataalam, zana duni za kilimo, elimu ndogo kwa wakulima na miundobinu duni.
Urio alisema matatizo hayo na mengine, yameilazimisha Bodi ya Tumbaku Tanzania, kuitisha mkutano wa wadau wa zai hilo mkoani Tabora, ili kujadili namna ya kuyapatia ufumbuzi.
Kwa mujibu wa mkurugenzi huyo,mkutano huo utawajumuisha pia wakuu wa mikoa na wilaya 23 zinazozalisha tumbaku.
Hali kadhalika wenyeviti wa halmashauri za wilaya hizo, wawakilishi wa idara na wizara za serikali, wawakilishi wa mashirika ya umama na binafsi na wanunuzi wa tumbaku.
.
Alisema mkutano huo utafanyika katika ya Machi 17 na 18 mwaka huu katika ukumbi wa Chuo cha Ufundi Stadi (Veta), mjini Tabora.
http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=18486
TANZANIA katika kipindi cha huu wa fedha, imezalisha kiasi cha tani 60,741 za tumbaku badala ya lengo la kuzalisha tani 75,000.
Hayo yalisemwa juzi na Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Tumbaku Tanzania, Frank Urio alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mjini Morogoro.
Urio alisema katika kipindi cha mwaka jana, uzalishaji wa zao hili ulikuwa tani 50, 784 na kwamba hali hiyo inaleta matumaini ya kufikia malengo la kuzalisha tani 100,000 kwa mwaka.
Mkurugenzi huyo alisema kutofikia kwa lengo la kuzalisha tani 75,000 katika kipindi cha mwaka huu, kutokana na matatizo mbalimbali yaliyojitokeza katika uzalishaji wa zao hilo la biashara.
Alitaja matatizo hayo kuwa ni pamoja na uhaba wa wataalam, zana duni za kilimo, elimu ndogo kwa wakulima na miundobinu duni.
Urio alisema matatizo hayo na mengine, yameilazimisha Bodi ya Tumbaku Tanzania, kuitisha mkutano wa wadau wa zai hilo mkoani Tabora, ili kujadili namna ya kuyapatia ufumbuzi.
Kwa mujibu wa mkurugenzi huyo,mkutano huo utawajumuisha pia wakuu wa mikoa na wilaya 23 zinazozalisha tumbaku.
Hali kadhalika wenyeviti wa halmashauri za wilaya hizo, wawakilishi wa idara na wizara za serikali, wawakilishi wa mashirika ya umama na binafsi na wanunuzi wa tumbaku.
.
Alisema mkutano huo utafanyika katika ya Machi 17 na 18 mwaka huu katika ukumbi wa Chuo cha Ufundi Stadi (Veta), mjini Tabora.
http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=18486