Lema kuwatoa wafungwa gerezani

Hapo kwenye red; you're right. Lakini unadhani ni sahihi? Well, utasema sheria zetu na Katiba vinamruhusu lakini bado ni sahihi kwa mtu mmoja kurundikiwa mamlaka na uwezo kama huo?

Mh. J. M. Kikwete ni rais lakini rais si Kikwete! Siku akiibuka mwendawazimu Ikulu hizo sheria tunazoshabikia leo kwa kuwa tu tuko madarakani au chama chetu ndicho chenye dola kuna siku zitatugeuka. Tume ya Jaji Mkuu Mtaafu Mh. Nyalali ilipendekeza sheria za aina hiyo zifutwe lakini kutokana viburi vya watawala wetu hadi leo hakuna kilichofanyika.

Taifa litadumu lakini sisi na vyama vyetu ni wa kupita - Tujenge mazingira bora kwa ajili ya Taifa letu na siyo kwa ajili ya makundi yetu.

Tulikuwa nae mmoja zamani akiitwa Nyerere alizitumia sana hizo sheria kwa ukamilifu wake. Tunashkuru toka alipoondoka yeye hakuna Rais aliyezitumia kama ilivyokuwa kwake.
 
Sijaelewa kitu kimoja..........hao unaosema atawalipia faini zao walizoshindwa kulipa wameshahukumiwa au ni mahabusu?
Kama ni mahabusu, amejuaje hukumu itakuwa faini?
Kama hukumu ilishatolewa.......1)Faini 100k 2) au kwenda gerezani 3months..............kama walishindwa kulipa, maana yake option ya pili inakuwa excuted kama adhabu sahihi...........na huwezi kufikia half way ukasema sasa nalipa faini nusu ili nitoke gerezani. Haipo hiyo.

haipo kwa sababu ni Lema au haipo kwa sababu sheria hairuhusu? kama ingekuwa ni rositamu anataka kuwalipia isingekuwepo pia au ingebadilka iwepo?? rositamu katuibia bilioni arobani, kaambiwa arejeshe yaishe na kweli ikawa hivyo, je ndivyo sheria za Tz zinavyoelekeza majambazi watendewe??
 
Siyo siri kwamba una haki ama hauna, bongo anayeamuwa hilo ni polisi na wanasiasa walioko madarakani.Haki yako haitokani na katiba na sheria za nchi,haki ya mtanzania inategemeana na utashi wa watawala!

Hili suala la kubambikiziwa kesi mbona tulishazoea kabisa?

Kuna watu wenye pesa ambao walishawahi kuhukumiwa miaka mingi kutokana na makosa yao,lakini amini usiamini.polisi huwa wanaenda mtaani kukamata mtu,anapewa hiyo kesi na anatumukia miaka ya huyo aliyehonga amabye anaachiwa.

Amabalo silijui ni hapo kwenye majina na document kutoka mahakamani kuwa kama ni kweli aliyeshitakiwa ndiye anatumukia kifungo hicho.

Pia kama kuna ujambazi ambao askari wameshiriki ama mkuu wao kahongwa,basi hiyo kesi ili iweze kufungwa,lazima apatikane mtu wa kubambikiziwa hiyo kesi na kuhukumiwa ili tu wafunge faili.

Nina uhakika kabisa kuwa wengi wasiokuwa na makosa wako ndani jela na wale wenye makosa wako nje.Wenye pesa hawakai ndani,na wenye connection na polisi ama wanasiasa pia hawakai ndani.

Na hata kama wakipata kesi,polisi wanaenda tu mtaani kuokoteza raia,na kuwapa hizo kesi ili kufunga mafaili na kuwafumba macho wananchi.

Na mara nyingi kwasababu polisi huwa wanaonekana wamefanya kazi nzuri mara baada ya kusolve kesi na kufunga jalada,basi huwa wanafanya hivyo kwa kwenda kuokoteza watuhumiwa na kuwapa kesi zilizoko kwenye makabrasha huko polisi na wanawapelekea watu mahakamani kwa kesi ambazo siyo zao.

Hili ni la kawaida kabisa bongo,nashangazwa kama kuna ambao hawajui!

Haya yote yanayotokea ni mambo amabyo ni ya kawaida sana bongo,na wengine yalishatuchosha kabisa na ni rahisi sana kujutia kuzaliwa Tanzania!

Sioni ni kwa njia gani tunaweza kumove forward bila mapinduzi,mfumo mzima ni hovyo bongo,na kupigia kelele Arusha peke yake siyo solution bali ni mwanzo tu,ni wananchi wachache sana wanojuwa haki zao na hata wale wenye kuzijua,ni wachache sana wanaamini kuwa zitakaa zipatikane bila rushwa nk....ni maoni tu.

kaka ambaye haamini haya maneno yako aamke kesho asubuhi aende mahakama yoyote ya mwanzo na/au ya wilaya....ahesabu wenye uwezo pale wanaohudhuria kesi ni wangapi? halafu awahesabu na wakulima(yani peasants, sababu Tz almost hakuna mkulima, wengi wetu ni ma peasants) na labourers(casual) ni wangapi? wenye pesa TZ huwa hawavunji sheria kama watu hawajui..wakiiba huwa ni kuwa wamechukua tu na watarudisha
 
Safi sana kamanda ni jambo zuri hilo kuwasaidia wanyonge,machozi yanayotiririka katika mioyo ya wanyonge wengi bila kuonekana katika nyuso zao ,ni fimbo tosha kwa hawa fedhuli wa fadhila.
Na Mungu hatatuacha wenye haki katika safari ya ukombozi
 
Azungukie magereza ya Tanzania nzima, asiishie Arusha.
 
Hongera kamanda Lema onyesha njia na wwengine wapite,pigania kwa vitendo haki ya watanznaia na wapiga kura wako,kiuhisia lazima tuungane kuikomboa nchi kutoka kwa walafi na mafisadi wa nchi hii wakiongozwa na CCM
 
kaka ambaye haamini haya maneno yako aamke kesho asubuhi aende mahakama yoyote ya mwanzo na/au ya wilaya....ahesabu wenye uwezo pale wanaohudhuria kesi ni wangapi? halafu awahesabu na wakulima(yani peasants, sababu Tz almost hakuna mkulima, wengi wetu ni ma peasants) na labourers(casual) ni wangapi? wenye pesa TZ huwa hawavunji sheria kama watu hawajui..wakiiba huwa ni kuwa wamechukua tu na watarudisha

impunity freedom or exemption from punishment hii ni tatizo kubwa tulilo nalo hapa..
 
Lema saaaaafi sana,hata sie huku udom tuko pamoja nawe kama mlezi wa tawi la cdm udom,magamba lazima wakubali mziki.
 
Endelea kuvumbua mengi mkuu ila ukweli utajulikana juu ya hii serikali dhalimu ya Magamba
 
MKUU LEMA wewe kama mlezi wetu wa cdm tawi la udom,tuko nawe hadi kieleweke.PEOPLEEEEEEEEEEEEEES,POWEEEEEEEEEEEEEEER
 
tulikwisha sema kuwa haki ya mtu huwa haipotei,ni suala la wakati tu.unapofika muda wa makajanja kukaa madarakani ulevi wao madaraka huwasababisha kuona kila kitu kiko sawa tu lakini hawajui impact yake inakuwa na negative side.big up sana mh.Lema hata manabii nao waliteseka lakini mwisho wa siku walifanikiwa katika harakati za kupigania haki na usawa.Siku zote haki inakwenda sambamba na wajibu,hata kutembea huwezi kwenda kushoto tu,lazima uende kushoto kulia.Tupo hapa Shinyanga unajua kauli mbiu yetu ni kuhakikisha tunachangishana mpaka wa magamba wanatoka,na sisi tunasupport movement ya kuwatoa wanyonge wasio na hatia.
 
Haki yako haitokani na katiba na sheria za nchi,haki ya mtanzania inategemeana na utashi wa watawala!
JUSTICE IS AN INTEREST OF THE MIGHTY......mambo ya zamaniiiiii....THE LAW OF THE JUNGLE.. kitakachotutoa hapa ni action plan kama ya Tunisia!
 
Sasa ninaamini kuwa, ukombozi wa mtanzania mnyonge anayeteswa ktk nchi yake aliyopewa na Mungu UMEKARIBIA! Kwani hili lipo wazi kabisa,kwa mifano ambayo nchi nyingi za Africa zilipitia hayo,exmpls countries is S.Africa and Namibia ukombozi ulipatikana kupitia wachache waliokuwa tayari kufungwa kwa ajili ya kutafuta haki ktk nchi yao!
 
Natokea kisongo saa hii kumuona Lema, nimemkuta akinyoa nywele na still ana furaha utadhani yupo uraiani. Miongoni mwa mambo aliyoyakuta ni idadi kubwa ya wafungwa waliopo ndani eti kwa sababu walishindwa kulipa faini kesi zao, faini hizi sio kubwa na pia zimepungua kwa sababu tayari wameshatumikia miaka kadhaa ndani.

Lema ameandija barua tayari na imeshapokelewa na mkuu wa gereza, mahesabu yanapigwa na kesho hesabu itafika ili walipiwe hizo faini na watoke.

Hizi ni faini Kama za laki 1, 2, elfu 50, laki tano, etc. Lakini wana Kama miaka Tisa, 5, 6, 11 etc.

Kuna mzee Ana miaka 85 kapewa kesi ya kubaka kafungwa miaka 30 na anasema hakuwahi kubaka, na kamwambia Lema Hana hata uwezo wa nguvu za kiume, Ila alisingizuwa kesi kwa sababu ya mgogoro wa ardhi.

Kuna kesi nyingi zenye utata lakini watu wamo gerezani. This week watatoka over 40 kwa msaada wa Lema.


na iwe kweli sababu nshachoka na politics za tz
 
Back
Top Bottom