Lazima tuwekane sawa kuhusu UKIMWI

Yona F. Maro

R I P
Nov 2, 2006
4,202
218
Siku moja nilikuwa katika ofisi fulani nataka kufanya kazi, kabla sijaanza ile kazi, dada moja wa office ile akaniambia kwamba anayetumia office hiyo ni muadhirika wa UKIMWI, angalia vizuri sana hapo mezani unavyofanya kazi na kushugulika, ni kweli nilishangaa yule jamaa ni kigogo lakini ana viwembe mezani kwake, kuna pini ameziweka tu bila mpango na mambo mengine ambayo ukigusa unaweza kuchomwa na kuweza kuambikizwa labda

Kuona vile sikuendelea kufanya ile shuguli, nilimwomba huyu mama abebe mzigo wake aulete kazini kwangu kwa pale ni ngumu kuendelea nayo kwa sababu ni mtu ambaye ninatembea na kuzunguka naweza kujisahau na kushika vitu vyake alinikubalia

Kwa hiyo hii ndio jamii ya watu tuliokuwa nao katika jamii yetu wameadhirika na ugonjwa Fulani lakini, anaweka mitego au chambo kwa wenzake waingie katika mambo yake ambayo kwa kweli hayavutii mbele ya jamii iliyostarabika hata kidogo hata kama anacheo gani

Huo ni ukumbusho tu -- KUMBUKA KWAMBA

Tarehe 1 Desemba kila mwaka ni siku ya UKIMWI duniani, siku hiyo watu mbalimbali hukumbushana na kuelimishana kuhusu Ugonjwa wa UKIMWI na kushirikiana katika mambo mengi ambayo nia yake au malengo yake ni kupunguza maambukizo ya UKIMWI sio kuzuia, kuzuia ni ngumu kwa sababu watu wengi wameshaadhirika na wengi wao wamejificha majumbani, maofisini, mashuleni, vyuoni na sehemu zingine nyingi sana ndio maana tunaongelea kupunguza na sio kuzuia.

Kuzuia maambukizi ya UKIMWI au ugonjwa wowote wa zinaa ugumu wake unakuja kuwa ngumu kwa sababu ni jukumu la mtu binafsi ( personal ) yeye mwenyewe ajizuie sio wewe umwambie aache , na mbaya zaidi watu wengi wanaoambukiza au kuambukizwa ukimwi ni watu wenye akili timamu na wengi wao wanajijua wameadhirika na kuendelea kuambukiza wengine na wengine kadri ya siku zinavyozidi kwenda

Kwa upande wa wale watu wenye kipato kidogo wao hawana wasiwasi , si ARV ziko ? kwahiyo atafanya anachojua yeye akiadhirika anapesa kidogo, za kuweza kuzitumia anunue hizo dawa za kuongeza nguvu na mambo kama hayo pamoja na madawa mengine mengi ambayo masikini wa kawaida sio rahisi apata, I wish kungekuwa hakuna ARV watu wengi wangeona hali halisi ya mtu anayeadhirika yukoje inakuwaje .

Wengi wameadhirika tunatembea nao njiani , wamependeza , wanavutia , wana furaha na mambo mengine mazuri lakini siri wanazijua wao wenyewe kwa hapa Tanzania hakuna mtandao maalumu wa kuwaweka wazi watu wanaosumbuliwa au walioadhirika na ukimwi , mfano USA kuna website maalumu yenye majina ya wagonjwa wote wa ukimwi kwahiyo unaweza katika tovuti ya serikali na kuangalia majina halisi na mahala wanapoishi waadhirika.

Hali hiyo na ujuzi huo umesaidia kupunguza maambukizi na kuzuia kabisa maambikizi kwa baadhi ya watu na jamii zingine , kila mtu sasa najua nani ameadhirika na anakuwa makini katika mahusiano yake na maisha yake ya kawaida bila hofu bila hiyana yoyote .

Wakati hapa naendelea kuandika , kuna mambo nafikiria kuhusu aina za jamii ambazo ziko hapa duniani kuhusu huu ugonjwa wa ukimwi , MWINGINE ATASEMA AHH NAJUA KUNA UKIMWI KWAHIYO ?? , HUYU NAE ATAKUJA NA LAKE , NAJUA UPO NA NINATUMIA KONDOM , MPENZI WAKE NAYE ANASEMA AHH BWANA MIMI NAMWAMINI MPENZI WANGU , MZAZI WAKE ANASEMA MIMI NIMEKUWA NA MKE WANGU KWA MUDA MREFU KWAHIYO SIWEZI KUADHIRIKA , NA MTOTO WAKE NAYE ATASEMA SIKU HIZI KUNA ARV NIKIPATA UKIMWI NTATUMIA ARV NIISHI MUDA MREFU .

Vituko kibao na majigambo kibao ambayo hayana msingi wala maana ukifikiria kwa umakini zaidi , lakini yote tisa , la kumi na mwisho ni mtu kujua kwamba ukimwi upo , utaendelea kuwepo na kusambaa zaidi kama hujaadhirika basi rafiki yako ameadhirika , ndugu yako , mpenzi wangu au jirani yako , mfanyakazi mwenzako na watu wengine ambao huwa unakutana nao mitaani au sehemu za mihangaiko yako .

Inahitajika jitihada za dhati na za uhakika kuweza kupunguza na kufanya ugonjwa wa ukimwi historia na usiendelee kuuwa na kuambukiza ndugu zetu na jamaa zetu wengine wa karibu , hawa tunawapenda , wengine ndio wametusomesha mpaka kufikia hapa tulipo , wengine wanatufundisha mashuleni , wengine tunashirikiana nao katika mambo kadhaa , tunaenda kuendelea kushirikiana nao kwa vitu vingi zaidi ili kujenga jamii na taifa lililo kuu na lisilo na wagonjwa wa UKIMWI .

UKIMWI UPO , UTAENDELEA KUWEPO , KUANGAMIZA WATU NA KULETA MADHARA KATIKA JAMII NYINGI , DUNIANI , NA WEWE NI TARGET YA UKIMWI , LAKINI UNAWEZA KUUKWEPA USILENGWE NJIA ZINAJULIKANA NA ZIKO WAZI KABISA .
 
Nimeona hii article kwenye ippmedia, ikiongelea Ukimwi na Zanzibari, lakini si vibaya tukaijadili kwa level ya Tanzania kwa ujumla. Ni topiki ya siku nyingi, imeongelewa sana, mengi yamefanyika, lakini haichuji, kwani tatizo halijaisha bado:)

- Kwanini katika sub-sahara Africa, Ukimwi ni tatizo kubwa kiasi hiki?


http://www.ippmedia.com/ipp/guardian/2006/07/21/70793.html

Talking on HIV/Aids in Z’bar yes, but no condoms please!

2006-07-21 09:17:43
By Issa Yussuf, Zanzibar

Speaking about condoms in Zanzibar is still largely a taboo though HIV/Aids awareness raising campaigns have been registering great successes according to the Population Services International (PSI).

’’Although it is still a taboo to talk about the use of condoms in public, people are ready to be informed about HIV/Aids,’’ PSI Information Director Mary, Machuche Mwanjelwa told The Guardian early this week.

Despite continued resistance in speaking about condoms as a major means in combating the spread of HIV/Aids, hundreds of Zanzibaris including the youths have been turning up in the awareness gatherings on the endemic organised by the PSI-Tanzania during the on going ten-days Zanzibar International Film Festivals (ZIFF).

’’One cannot easily find a condom in most of the shops in Zanzibar, people prefer talking about AB � abstinence and being faithful,’’Mwanjelwa said on Sunday shortly after returning from an awareness campaign at Mchangani in the north of Zanzibar stone town where PSI is using Mobile Video Units (MVUs).

According to Mwanjelwa, MVUs and road show teams utilises entertaining and educational videos, skits and contests to educate target audiences on HIV/Aids and other sexually-transmitted infections.

’’We are promoting protective behaviour using ABC (Abstinence, Be faithful and use Condoms) message strategy as part of the 9th ZIFF event,’’ she said.
Amina Hussein, a mother of three children who attended the show said:

’’I think it is not good to talk about Salama condoms because if you abstain from illicit sex there is no way you will get HIV/Aids.’’

Despite lack of enthusiasm for condoms, Mwanjelwa said her organisation was going to ensure Salama condoms were available in over 90 per cent high-risk outlets in the isles (bars, guesthouses, brothels).

PSI is a US based NGO founded in 1970 to improve health using commercial marketing strategies.
 
SERIKALI imepiga marufuku wahubiri wa dini na waganga wa jadi wanaojitangaza kuwa wana uwezo wa kutibu ugonjwa wa UKIMWI, kwani kufanya hivyo ni kuendelea kuchochea maambukizi ya ugonjwa huo ambao hadi sasa hauna tiba wala chanjo.

Akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalumu, Lucy Mayenga (CCM) kuhusu watu wanaojitangaza kutibu UKIMWI wakati hauna tiba, Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Aisha Kigoda alisema watu hao ni wapotoshaji kuhusu hali halisi ya ugonjwa huo.

Alisema wananchi wawe makini na watu hao na wazingatie maagizo yanayotolewa na serikali kupitia wahudumu wake wa afya kuwa, UKIMWI hauna tiba yoyote zaidi ya dawa za kuongeza kinga ya mwili.

Akijibu swali la Msingi la Mbunge wa Viti Maalumu, Margareth Mkanga (CCM), aliyetaka kujua lini serikali itasitisha matumizi ya Kadi za Bluu zinazotumiwa na waathirika wa UKIMWI wakati wa kutibiwa kwani zinawanyanyapaa, Naibu Waziri huyo alisema kwa sasa serikali haina mpango wa kusitisha matumizi yake.

Alisema kuwa kadi hizo zinawasaidia wagonjwa wa UKIMWI kupatiwa tiba hata katika vituo ambavyo hawakuwa wakivitumia awali, kwani kwa kuonyesha vitambulisho hivyo, hutambuliwa na kupatiwa tiba.

Naibu waziri huyo alisema vitambulisho si sababu ya kuwepo kwa unyanyapaa, unatokana na uelewa wa jamii husika kuhusu ugonjwa huo kwani wapo wagonjwa wa kifua kikuu ambao nao pia hutibiwa kwa kutumia kadi za kijani.

Kwa upande wa wahudumu wa afya ambao wanaonyesha unyanyapaa kwa wagonjwa wa UKIMWI baada ya kuwaona wakitibiwa kwa kadi hizo za bluu, Naibu Waziri alisema serikali haitakuwa tayari kuwavumilia na kuahidi kuwachukulia hatua ikiwa ni pamoja na kuwafukuza kazi.
 
yah nime-googled na nimepata ya CCN http://www.cnn.com/2007/WORLD/africa/03/15/koinange.africa/index.html lkn CCN walinyimwa interview na President na LKn Jamaa wa Aljazeera wamepewa. ila Pia aliwaambia Aljazeera kuwa hayupo tayari kutoa FORMULA ya vit gani anachanganya ili kutibu, na akatoa mfano wa Cocacola na fomula zao. Kifupi Serikali yetu ya TZ kwa kuwa inakubalika na Gambia basi wachukulie wagonjwa wachache watibie tuone. Aina Haja ya kama wazungu kutaka sample ili ionekane wao ndio wamevumbua....Kama atakuwa amafanikiwa tunampa Hongera...
 
AIDS spread, truancy headache for Kikwete

2007-06-07 09:56:40
By Guardian Reporter
President Jakaya Kikwete has said there is need to curb the number of people infected with HIV/AIDS. At the moment, about two million people in Tanzania have fallen victim to the scourge.

He also decried growing truancy in the country`s schools.
``For about 24 years now since 1983, Tanzanians have been fighting a difficult battle against this disease,`` he said.
``A lot of efforts have been directed towards fighting against the disease. We have registered encouraging achievements because the infection rate has fallen from 13 percent of the population in the 90s to the current 7 percent.

There are indications that the rate might even drop lower to 6.5 percent,? the President said.

He announced that the countrywide HIV voluntary testing campaign that was slated to take off on June 8 had been pushed forward to July 14, 2007. The President said the Ministry of Health and Social Welfare was going to announce full details of the programme.

``Through the countrywide HIV voluntary tests, the nation shall establish the exact number of those already infected, `` he said.

On school pregnancies, the President said the sum of primary school girls who were forced to cut short their studies because of pregnancy had shot up from 2,590 in 2005 to 3,479 in 2006.

He said a total of 772 secondary school girls had to cut short their studies in 2005 while the number had hit 993 students by March 2006.
``This is unacceptable.

SOURCE: GUARDIAN

Wana JF,

Katika mambo mambo yanayotishia mustakabali wa Taifa letu na kizazi chetu ni gonjwa hili hatari la UKIMWI. Taarifa zote muhimu juu na namna ya kujikinga na gonjwa hili zipo na kwa kiasi kikubwa zinafahimika.

Kwa bahati nzuri au mbaya, idadi ya wanaharakati walio vitani dhidi ya gonjwa hili inaongezeka sana; wengine wao ni waathirika wa VVU na wengine ni waathirika kupitia ndugu au jamaa zao.

Matumizi ya kondomu yanapigiwa kampeni kali sana na Wanaharakati hawa ingawa Wachungaji na Masheikh wanapiga vita sana kondomu kwa madai kuwa Wanaharakati wanasisitiza sana juu ya matumizi ya kondomu kwa sababu ya maslahi yao binafsi.

Kinachonishangaza mimi ni kuwa pamoja na harakati hizi dhidi ya UKIMWI bado idadi ya Waathirika inazidi kupaa/kuongezeka kitu ambacho Rais wetu JK kimemgusa sana na kwa mujibu wa Rais (akinukuliwa na The Guardian) inagwa Rais anasema kuwa maambukizi yamepungua (nadhani anamaanisha kasi ya maambukizi).

Hata hivyo Mhe. Rais anasema idadi ya watoto wa kike wanaoacha shule kwa sababu ya mimba inaongezeka! Hii kwangu ni ishara kuwa hadi sasa Kondomu haijasaidia maana hizi mimba za watoto wa shule zisingeongezeka na kuwafanya watoto wakatishe masomo SHIDA NI NINI HASA?

Naomba kutoa hoja.


Naomba maoni yenu Wadau,
 
Ibrah,

Kondomu zinasaidia sana kujenga usugu wa nyoyo zetu na kufifisha kabisa dhamiri zetu. Kwa maneno mengine kampeni ya kondomu inazidi kuchochea ngono haramu. Na wanazipotumia mara ya kwanza labda wanagundua kuna kitu wanakikosa; kwa hiyo wanakubaliana kuivua. Mimba.

Pili hakuna uthibitisho wa kimaabara,narudia, hakuna uthibitisho wa kimaabara kwamba kondomu inazuia ukimwi. Haiwezekani mtengeneza kondomu ndiyo huyo huyo awe mthibitisha ubora wake. Kwani yeye hataki kufanya biashara?

Tatu sijamuona hata mmoja katika wale wanaoeneza kampeni ya kondomu aliyesimama hadharani na kuelezea jinsi ambavyo yeye ameitumia na ikauepusha na maambukizi. Utahubirije kitu ambacho wewe mwenyewe hukitumii? Kama ni sumu je? Na ndivyo ilivyo. Na ajabu ni kwamba hata mimba bado zinatungwa licha ya matumizi ya kondomu. Kwa hiyo kondomu haizuii mimba pia.

Kama unavyoona siasa zinavuta "watanzania walio wengi" kwa vile zimegeuka ajira za uhakika, ndivyo na ugonjwa huu wa ukimwi umegeuka kuwa ajira kubwa sana na yenye mafao ya haraka. Tunafanya biashara ya mauaji kabisa.

Walioathirika tayari, hawana cha kupoteza kwa maana tayari ni waathirika. Tunachotakiwa ni kuwatunza, kuendelea kuwathamini na kutowanyanyapaa. Lakini wanaposhiriki katika kampeni hizi na kuhamasisha jamii isahau maadili yake na kushabikia "kondomu" wanajidharaulisha. Ni kama wana ajenda ya "Tufe Sote". Ingawa kufa ni kwa kila mwanadamu, lakini madhara na mateso ya huu ugonjwa ni makubwa muno kuliko kifo chenyewe.

Nadhani elimu ya kuwahudumia waliothirika na kujikinga (kwa kutofanya) itiliwe mkazo ili kuondoa uwezekano wa maambukizi yasiyokuwa ya lazima na hasa kwa wale uliowataja kwamba wanaathirika kwa kuwahudumia jamaa na ndugu zao.

Ikionekana kwamba watu tumejizuia ngono haramu na bado maambukizi yakaendelea, basi hakuna jinsi isipokuwa kufanya kama kipindupindu na hivi majuzi RVF ili kuzuia watu wasiambukizwe katika mazingira ya kuwahudumia waathirika.

Vinginevyo: ACHA TUTEKETEE. Sikio la kufa ....
 
Tatizo kondomu huwa zinatumika pale tu wanauhusiano wanapokuwa wageni ila wakizoeana tu kondomu huwekwa pembeni na kila mtu anamwamini mwenzie hapo sasa ndio shughuli inapokuwa. Hivyo kondomu haipunguzi ukimwi.
 
Asante sana Ilongo kwa mawazo yako.

Tusubiri maoni ya Wanaharakati waliomo humu.
 
Tatizo kondomu huwa zinatumika pale tu wanauhusiano wanapokuwa wageni ila wakizoeana tu kondomu huwekwa pembeni na kila mtu anamwamini mwenzie hapo sasa ndio shughuli inapokuwa. Hivyo kondomu haipunguzi ukimwi

Domokaya,

Hilo si tatizo bali ni ukweli usioweza kupingika kuwa kondomu hutumiwa washiriki wanapofanya mara ya kwanza, wakijitahidi wataitumia tena mara ya pili. Baada ya hapo hawatitumia tena maana mioyo imeshaungana; hata kama ni mimi au wewe!
 
Domokaya,

Hilo si tatizo bali ni ukweli usioweza kupingika kuwa kondomu hutumiwa washiriki wanapofanya mara ya kwanza, wakijitahidi wataitumia tena mara ya pili. Baada ya hapo hawatitumia tena maana mioyo imeshaungana; hata kama ni mimi au wewe!

Kuna sauti ndani mwetu ambayo kwa kawaida utuonya pale tudhamiriapo kutenda jambo ovu. Hutuonya siyo mara moja au mara mbili bali hata mara tatu. Sasa kwa ugumu wa nyoyo zetu, sisi tunaipuuza. Tunaendelea hadi tunatenda hilo ovu. Kinachofuata ni ovu hilo kuzaa ovu jingine na jingine na jingine.

Na kwa taarifa ni kwamba hata hiyo mnapokutana mara ya kwanza inategemea mmejamiiana kwa muda gani (nadhani naeleweka hapa). Vinginevyo katikati ya kitendo hicho si ajabu mmoja akamshawishi mwenzake na wakaamua kubanjuana vivyo hivyo. Si nyite tayari mmeshaamua kuzipuuza sauti za maonyo zilizomo ndani mwenu!!
 
Sikubaliani kabisa na matumizi ya kondom, kwani kwa kiasi kikubwa kondom zinachangia kuenea kwa ukimwi, hii inatokana na hoja zifiatazo,

1. Uafirishaji, kondom zinatengezewa ulaya na asia, zinafungwa ndani ya matena na kusafirishwa kwa meli kwa wastani wa siku ishirini, zikiwa njiani zinakabiliwa na madiliko ya hali ya hewa yani joto na baridi na hii inapelekea zipunguze ubora wake, zinapofika bandai ya Dar zinachukua wastani wa siku 7 zikipigwa na jua. kumbuka kondom ni mpira.

2.Uifadhi, mara baada ya kundom kutolewa bandaini husambazwa kwa wauzaji, ambao nao pia uhifadhi wao hutofautiana, kunawenye maduka yenye viyoyozi na wengine wanahifadhi kwenye maduka yasiyo na viyoyozi ambapo ubora unazidi kuporomoka.

3.Elimu kwa mtumiaji, watumiaji wa kondom hawana elimu ya matumizi ya kondom, ni watu wengi hawajua jinsi kuvaa kondom, kwani wengi hugeuza, au kuongeza mafuta juu ya kondom ili kuongeza ulaini, vijijini ndio hatari zaidi kwani kuna watu wanafanya biashara ya kukodisha, yaani kondom inatumiwa na zidi ya mtu mmoja, kuna watu wengi wanahifadhi kondom kwenye wallet humo kukaa siku kadhaa kabla ya kutumia, hii yote inapoteza ubora wa kondom.

Kutokana na hoja hizo hapo juu, sikubaliani kabisa na matumizi ya kondom, kwani si salama kama tunavyoshawishiwa tuamini..... bali tunalazimiswa tuikubali kondom kwa maslahi ya watu fulani.....
 
Nimesoma michango ya Ilongo na Mgumu. Wana mawazo mazito. Hata hivyo nakubaliana na hoja moja ya Mgumu, kuwa kuna tatizo na elimu ya utumiaji wa condom. Nakubaliana na jambo hili kwa sababu tafiti zote za kisayansi zinaonesha hivyo. Pale ambapo condom ilitumiwa ipasavyo, mafanikio yake yalithibitika katika kuzuia mimba na hata virusi vya Ukimwi.

Kwamba condom inaleta usugu wa mioyo ni imani potofu na haina hata hata chembe ya ukweli kisayansi. Unless ndugu Ilongo utuwekee hapa ushahidi wa kitafiti ambao umeonesha hivyo.

Baada ya hoja hizi za condom, nichangie katika upana zaidi kuhusu jambo hili. Katika mustakabali wa ngono, binadamu anakabiliwa na matatizo mawili makubwa ambayo ni: mimba zisizotarajiwa/zisizotakiwa na maambukizi ya virusi vya ukimwi. Matatizo haya huwa dhahiri zaidi kwa vijana (miaka 15-24) kwa kuwa wao huwa ni wepesi zaidi wa kujiingiza katika tabia hatarishi ikiwemo ngono zembe. Kwa hiyo katika mchango wangu kwa mada hii najikita zaidi katika kundi hili kwa maana ya samaki mkunje angali mbichi. Ili kuepuka matatizo haya, kuna njia mbili ambazo zimethibitika kisayansi kwamba ndio mwafaka kuwaepusha vijana na matatizo haya:

i) Kuchelewa kuanza kufanya mapenzi na wale waliokwisha anza..
ii) kufanya mapenzi salama

Tulichokosea sisi katika harakati zetu ni kutafuta majibu rahisi kwa maswali magumu. Tukaanza kugawa condom bila elimu ya kutosha. Ili kutatua matatizo ya mimba za utoto na maambukizi ya virusi vya ukimwi, tunapaswa kuchukua hatua za muda mfupi na muda mrefu. Hatua za muda mfupi ndio kama hizo anazofanya Rais za kuhamasisha na kutoa elimu mlipuko kuhusu majambo haya. Lakini jambo la maana zaidi ni kuchukua hatua za muda mrefu. Kwa maoni yangu hatua za muda mrefu ni kwa kutoa elimu ya uzazi na mahusiano mashuleni kwa lengo la kuwapatia vijana uelewa, hamasa na mbinu za kufikia (a) matokeo chanya katika mahusiano ya kimapenzi ikiwemo namna ya kuepuka ngono shurutishi na umuhimu wa tendo la ndoa katika kuonesha, kukuza na kuimarisha mapenzi kwa wapendanao., na (b) kuepuka matatizo ya kiafya yatokanayo na tendo la ngono yakiwemo mimba za utotoni na maambukizi.

Ili elimu hii iweze kuwa na mafanikio inabidi ianze kutolewa mapema katika shule za msingi. Tafiti zote zinaonesha kuwa nchi zote zilizofanikiwa kudhibiti mimba za utotoni na hata maambukizi miongoni mwa vijana zinatowa elimu ya uzazi na mahusiano mashuleni, na nchi inayoongoza katika hili ni Uholanzi ambayo mimba za utotoni/ujanani ni chini ya 1%.

Tatizo la wanasiasa wetu wa CCM wanataka majibu rahisi kwa maswali magumu, na wanapenda kuchukua zile tu hatua ambazo zinawaongezea umaarufu. Hatua ambayo Rais anapaswa kuisimamia kwa nguvu zake zote ni kuibuka na sera itakayosababisha marekibisho ya mitaala ili kuingiza elimu hii mashuleni. Hili alilofanya juzi ni zuri, lakini naamini linaweza kufanywa vizuri zaidi na watoa ushauri nasaha na wataalamu wa afya kuliko yeye.

Mwisho, niseme tu kuwa tatizo sio condom, tatizo ni sisi watumiaji. Kama wewe hupendi condom, acha kufanya mapenzi kama hujaoa na kama umeoa, baki na mumeo au mkeo na mhakikishe wote hamjaambukizwa. Ni ujinga mkubwa kukataa kutumia condom kama wewe unafanya mapenzi nje ya ndoa.

Katika majadiliano yanayohusu mambo muhimu na mazito kama haya tuongozwe na ushahidi wa kisayansi badala ya hisia na mazoea; hasa tuachane na imani potofu ambazo hazina chembe ya ukweli. Imani potofu ni moja ya sababu za kuongezeka kwa matatizo haya.
 
Umetoa mawazo mazito bwana Kitila, mii nakuunga mkono kabisa.
Siamini kwamba kusisitiza na kuwepo kwa kondomu kunachangia kuongeza ari ya ngono. Kwa hiyo watu wasisitizwe kuacha ngono na walioshindwa kuacha [ni vigumu - ngono ni hitaji muhimu kama chakula, mavazi na malazi] na watumie kondomu zitawasaidia wengi.
Na ni kweli kabisa ikitumika ipaswavyo inasaidia sana kupunguza maambukizi. Tatizo effect ya kuzuia ugonjwa hauwezi kui-feel moja kwa moja, inahitaji 'intuition'!
Kuhusu usafirishaji na utunzaji, hali ni ile ile kwa bidhaa zingine iwe vyakula ama madawa lakini tunazitumia kila siku na hazina matata [mara nyingi]
Ila naomba ku-appreciate kwamba UKIMWI ni mtihani mkubwa!
 
Ndugu zangu, naomba niwaulize swali (hili ni kwa watu wazima ambao mmeshawahi kutumia kondomu).

Swali hili ni muhimu sana na katika kulijibu hili tuache unafiki na tuzzungumze ukweli.

Swali: Je, kuna tofauti gani ya vionjo (ladha) wakati unafanya tendo la kujamiiana kwa kutumia kondomu Vs Unapofanya bila kutumia kondomu? Ipi inakuwa tamu, bila ya kondomu (kavukavu) au unapokuwa umevaa kondomu?

Naomba majibu yasiyo unafiki.
 
weee nawe hivi kulamba pipi kwenye jani lake na kulamba pipi bila ya jani(ganda) lake ipi ta mu?

mie nimekwazika jamani hii mada ni ya siasa au .................?

kama kila anachoongea rais kiwekwe kwenye siasa sawa tusonge mbele
 
There is NO SIGNIFICANT DIFFERENCE katika ladha.
Ila mambo ya ngono yako zaidi katika psyche ya mtu. Ukiingia kwa mawazo ya kuwa condom yapunguza ladha, uta-feel what you expect!
Lakini pia kama unatoka nje ya ndoa unakuwa na ka-amani kidogo ukitumia condom la sivyo utapata post-coital depression ya kama wiki 2 hivi. Teh teh teh.
 
mie nimekwazika jamani hii mada ni ya siasa au .................?

kama kila anachoongea rais kiwekwe kwenye siasa sawa tusonge mbele

Mtumwitu,

uiskwazike jamaa yangu hii issue ni nzito sana ndiyo maana hata Rais ameizungumzia. Natumai siku hiyo ya 14th July utajitokeza kwenye hiyo voluntary testing!

Pia ujue Rais ni mtu mkubwa sana ndiyo maana kila kauli yake lazima ipewe vipau mbele; kujadili kauli zake pia itamsaidia yeye rais na Washauri wake kuwa makini wanpotoa kauli yoyte ile, hata kama ni jokes!

There is NO SIGNIFICANT DIFFERENCE katika ladha

Saikosisi,

Lakini umekubali ipo tofauti; now which is that signifacant difference, kwamba inanoga zaidi ukiwa na kondomu au ikiwa bila kondomu?

Sikuelewi, hivi unaweza kujidanganya kuwa hujavaa kondomu wakati umeivaa mwenyewe!
 
Back
Top Bottom