Gosbertgoodluck
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 2,855
- 401
Kwa heshima na taadhima nachukua nafasi hii kukusifa Dokta wa Heshima (UDOM), Kanali, Mheshimiwa Sana Jakaya Mrisho Kikwete kwa mengi uliyoifanyia nchi hii tangu ushike hatamu ya uongozi wa juu kabisa.
Yapo mengi tena sana uliyoifanyia nchi hii kama vile kuwapa nafasi za uongozi kwenye chama unachoongoza na serikali wahujumu uchumi (mafisadi) ambao wamekivuruga na kukivua nguo chama na serikali yako. Kupitia hilo, watanzania tumejifunza kwa vitendo kwamba uongozi na biashara haviendi pamoja. Lakini kubwa kuliko yote ni FUNDISHO UTAKALOTUACHIA KUHUSU UMUHIMU WA KUPIGA KURA NA UMUHIMU WA KUTAFAKARI KWA KINA KABLA YA KUPIGA KURA.
Kupitia kwako watanzania tumejifunza kuwa kumbe umaarufu wa mgombea unaweza ukatengenezwa kirahisi tu kwa fedha za wahujumu uchumi kupitia vyombo vya habari na ukawasukuma wengi kumpigia kura. Wakati wa uchaguzi uliokuweka wewe madarakani watu waliacha kutafakari historia yako kiutendaji na kitabia na uzalendo wako kwa nchi wakaiishia kushabikia ulimbwende na ujana wako wa bandia. Sasa cha moto wanakiona.
Ama kweli wazee wetu hawakukosea walipotuasa ''baniani mbaya lakini kiatu chake dawa''
Mungu akubariki sana.
Yapo mengi tena sana uliyoifanyia nchi hii kama vile kuwapa nafasi za uongozi kwenye chama unachoongoza na serikali wahujumu uchumi (mafisadi) ambao wamekivuruga na kukivua nguo chama na serikali yako. Kupitia hilo, watanzania tumejifunza kwa vitendo kwamba uongozi na biashara haviendi pamoja. Lakini kubwa kuliko yote ni FUNDISHO UTAKALOTUACHIA KUHUSU UMUHIMU WA KUPIGA KURA NA UMUHIMU WA KUTAFAKARI KWA KINA KABLA YA KUPIGA KURA.
Kupitia kwako watanzania tumejifunza kuwa kumbe umaarufu wa mgombea unaweza ukatengenezwa kirahisi tu kwa fedha za wahujumu uchumi kupitia vyombo vya habari na ukawasukuma wengi kumpigia kura. Wakati wa uchaguzi uliokuweka wewe madarakani watu waliacha kutafakari historia yako kiutendaji na kitabia na uzalendo wako kwa nchi wakaiishia kushabikia ulimbwende na ujana wako wa bandia. Sasa cha moto wanakiona.
Ama kweli wazee wetu hawakukosea walipotuasa ''baniani mbaya lakini kiatu chake dawa''
Mungu akubariki sana.