Elections 2010 Lawrence masha, basil mramba, makongoro mahanga wapeta!!!!!!

Status
Not open for further replies.
Home
arrow.png
Habari za Kitaifa
arrow.png
Personal Tech
arrow.png
KIKWETE HAKAMATIKI
KIKWETE HAKAMATIKI

Monday, 01 November 2010 00:24 administrator



* Dk. Willibrod Slaa aongeza kasi
* Profesa Lipumba anajikongoja

Na Waandishi Wetu

MATOKEO ya awali ya uchaguzi mkuu uliofanyika nchini jana, yanaonyesha mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Rais Jakaya Kikwete, anaongoza kwa kura nyingi. Kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa katika baadhi ya vituo, yanaonyesha Rais Kikwete amewaacha kwa mbali wapinzani wake wanaowania kushika dola. Awali, akipiga kura katika kituo cha Msoga Shuleni, kata ya Msoga, wilayani Bagamoyo, mkoani Pwani, Rais Kikwete alisema ana uhakika atashinda kwa kishindo. Akiwa ameongozana na mkewe, Mama Salma, Rais Kikwete alipiga kura kituoni hapo saa 5.39 asubuhi, kwa kutumia kitambulisho chake namba 487314557, ambapo aliongozwa na karani Gerald Muya.

Baada ya kukamilisha taratibu za kupiga kura, alizungumza na waandishi wa habari na waangalizi wa uchaguzi kutoka Jumuia ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC). Aliwataka wananchi kuheshimu maamuzi yaliyofanywa na Watanzania, kwani kuna maisha baada ya uchaguzi.

Rais Kikwete akizungumza na waangalizi wa uchaguzi wa SADC, alisema ana matumaini kuwa serikali yake imefanya kazi kubwa katika utawala na kwamba, anaomba amani. Alisema amefurahishwa na hali ya amani na utulivu iliyoonyeshwa katika vituo vya kupigia kura katika maeneo mbalimbali nchini.

Wagombea wa nafasi ya urais ni Kikwete wa CCM, Dk. Willibrod Slaa (CHADEMA), Profesa Ibrahim Lipumba (CUF), Hashim Rungwe (NCCR-Mageuzi), Peter Mziray (APPT MAENDELEO), Mugahywa Muttamwega (TLP) na Fahmi Dovutwa (UPDP), ambaye alitangaza kujitoa.

Matokeo ya awali yanaonyesha ifuatavyo:

Kata ya Makumbusho, jimbo la Kinondoni
 
Tena acha kabisa utani wako kabisaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa, naona umeishiwa cha kusema
 
Huu sasa ni utani CCM mnachotaka Kufanya ' Yani inaonyesha mnataka kuweka history Tanzania' huyo brazamen arudi state akale bata.atuachie wapiganaji wetu waingie bungeni lol
 
jf kwa uzushi tuko fiti

Nahisi sasa tuko mambar'wani. Maana kila dakika unsikia story tofauti na zote zinaonyesha zinatokea sehemu moja. Nini hii?
au ndio mpango wenyewe wa kuchakachua, kwamba wanaanza na kusambaza taarifa nyingi kiasi kwamba zitakosa reliability na hivyo watu wengi kukosa imani nazo na hatimaye kukaa mkao wa kusubiri na kukubali matokeo yale yalochakachuliwa na tume!!! Hilo nalo neno!!! Ni maoni yangu tuu
 
mpaka sasa mabomu yanapigwa rakini wananchi wameapa hawaondoki halmashauri ya jiji la mwanza mpaka kieleweke mabomu yanapigwa watu wanalala chini
Masha hajashinda hata kituo kimoja iweje atangazwe mshindi kama hawataki mauaji kama yaliyotokea kenya?
 
Jamani tupeni data zenye uhakika mtatupa presha wengine kwa data zisizo kweli pllllllllllllllllllllllllllllllease
 
Hivi naomba mnieleweshe kwa nini kuna kuwa na tetesi au hawa wakati tuna mawakala katika
vituo vya kupigia kura ambao wameshatupa matokeo yanaonyesha tayari nani kashinda.Au hawa
wanafanyaje sasa ili kubadilisha matokeo?
 
Katika hali ya kutatanisha, kuna tetesi kutoka makao makuu ya NEC yanayohashiria kwamba, Hawa jamaa wamepita, lakini bado hawajatangaza rasmi, hebu wenye taarifa kamili watumwagie. Hii itakuwa ni tatizo kubwa
Lau masha kaukalia....na kesharudi dar kuchukua chake wizarani kwetu
 
ILemela chadema imechukua,Nyamagana Chadema imechukua kupitia Kijana Ezekiah Wenje aliye pata kura 38,171 dhidi ya kura 27,883 alizopata waziri wa mambo ya Ndani ndg.Lawrence Kego Masha.
 
Nyamagana,ilemela zaenda chadema. Uliyeleta thread hii tutakuhoji kwa kudanganya umma. Hawakupeta, wako chalii!
 
Nec makao makuu hawamtangazi Mbunge , wanachakachua matokeo ya urahisi , Msimamizi wa uchaguzi wa jimbo ndo mwenye mamlaka kisheria kumtangaza mshindi wa ubunge

Chinga nenda ukosome kwanza , usikimbilia biashara ya mkononi tu

Huyu chinga ametumwa kuja kutuharibia janvi letu lionekane la watu wazushi; sio mtu wa kumtia maanani!!
 
wandugu ingekuwa vyema tupost ishu za uhakika ili tasmini yetu iwe nzuri. tusiwe kama CCM kuwaleta watu kwenye mkutano kuwavalisha t shert na kofia kwa malipo mwisho wakasema wanakubaLIKA. Tutafute data za kweli ili itusaidie kujiridhisha na tujue nini cha kufanya au sio wakuu
 
Katika hali ya kutatanisha, kuna tetesi kutoka makao makuu ya NEC yanayohashiria kwamba, Hawa jamaa wamepita, lakini bado hawajatangaza rasmi, hebu wenye taarifa kamili watumwagie. Hii itakuwa ni tatizo kubwa

Please make correction on ur heading ASAP!
 
JAMII FORUMS naipenda mno. lakini sasa nimeanza kupatwa na wasiwasi mkubwa kuhusu namna watu wanavyoichezea. Wanapost vitu vya uongo visivyofanyiwa utafiti. Hii ni mbaya sana. Kwa wengi wetu Jamii forums ilipaswa itumike vema kwani hii ni social media ambapo watu wasiopata nafasi kwenye media za kawaida hapa ndipo wanapotoa maoni yao. Ni ajabu kwamba sasa Jamii forums inageuzwa kuwa kichaka cha porojo na uongo huku baadhi wakitumia vibaya uhuru wa wa kutoa maoni na mawazo. Kwa hakika inasikitisha mno.
Hao mamluki wametumwa na ccm kuchakachua matokeo hadi huku JF wala wasikuumize kichwa.
 
Nimepata habari kwa simu kutoka Rombo kama dakika 40 zilizopita kuwa Mramba amekataa kusaini matokeo baada ya Selasini wa Chadema kumshinda kwa kura elfu moja na ushee, kuna mwenye taarifa yoyote juu ya hilo?
 
Mimi ni-mind sana hawa watu wanaoingia kwenye majadiliano bila kuwa makini. Nahisi kuna watu wanataka tu kuvuruga mtiririko wa mawazo na michango ya watu makini. Komeni kuchezea JF!!!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom