Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,988
Mwandishi Maalumu, New York
Daily News; Tuesday,September 30, 2008 @00:02
Habari nyingine
Tanzania itatokomeza kabisa ugonjwa wa malaria katika miaka saba ijayo, yaani ifikapo mwaka 2015, kwa kutumia njia tatu zilizothibitishwa kimataifa kuwa zinamaliza ugonjwa huo, Rais Jakaya Kikwete alisema hayo juzi mjini hapa.
Vile vile, amesema kuwa ziara yake kwenye Umoja wa Mataifa (UN) mjini New York imekuwa ya manufaa makubwa kwa sababu Afrika imefanikiwa kuwasilisha sauti yake katika masuala muhimu yanayohusu Bara hili. Rais Kikwete aliondoka hapa jana kurejea nyumbani.
Akizungumza na waandishi wa habari wa Tanzania walioandamana naye katika ziara hiyo kuhusu mafanikio ya ziara hiyo, Rais Kikwete alisema moja ya mafanikio ya ziara yake ni kwamba Tanzania imepata uhakikisho kuwa itatokomeza malaria ifikapo mwaka 2015.
Alisema ahadi mpya za kupambana na matatizo ya Afrika, ukiwamo mwelekeo mpya wa kupambana na magonjwa na hasa malaria, inayoua watu wengi zaidi Afrika, ni moja ya mafanikio ya ziara yake UN.
Katika Tanzania, tunapambana na malaria kwa njia tatu zinazokubalika duniani, kuhakikisha kuwa wananchi wetu wanatumia vyandarua vyenye dawa, tunanyunyizia dawa za kuua mbu katika madimbwi ya maji, na pia kuhakikisha kuwa wagonjwa wanapata dawa, alisema Raia Kikwete katika mahojiano hayo kwenye Hoteli ya Intercontinental jijini New York.
Alisema njia zote tatu tayari zimeleta mafanikio makubwa Zanzibar ambako vifo kutokana na malaria vimeteremka mno, kutoka vifo 120,000 hadi 60,000 tu kwa mwaka. Na mafanikio hayo yanatokana na matumizi ya asilimia 40 tu ya vyandarua Tanzania Visiwani, lakini Zanzibar haiwezi kutokomeza malaria bila kuhakikisha kuwa Bara nayo inakuwa salama.
Hii ni mara ya tatu, tunafikia hatua ya kutokomeza malaria Tanzania Visiwani na bado ugonjwa huo umerejea kwa sababu Bara haitiliwa maanani, alisema Rais Kikwete. Alisema Tanzania inahitaji kiasi cha vyandarua milioni 15 vyenye dawa, kwa kila Mtanzania kulala bila bughudha ya mbu, na kuwa vyanzo mbalimbali vya misaada vimekwishahakikisha kuwa vyandarua hivyo vitapatikana baada ya awamu ya kwanza ya vyandarua milioni 5.2 kuwa vimepatikana.
Kama mlivyosikia, Waziri Mkuu wa Uingereza, Gordon Brown, pekee yake ameahidi kutoa kiasi cha vyandarua milioni 100 katika miaka michache ijayo. Tanzania itanufaika na sehemu na vyandarua hivyo. Pili, tunao msaada wa sekta binafsi ambayo pia itatoa vyandarua.
Mpango ni kutokomeza malaria ifikapo mwaka 2015 ni dhahiri utafanikiwa, alisisitiza Rais. Rais Kikwete aliyewasili New York, Septemba 21, mwaka huu, ameliwakilisha Bara la Afrika kwa maana ya kushiriki katika mikutano kadhaa muhimu, ikiwa ni sehemu ya mikutano ya mwaka huu ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.
Daily News; Tuesday,September 30, 2008 @00:02
Habari nyingine
Tanzania itatokomeza kabisa ugonjwa wa malaria katika miaka saba ijayo, yaani ifikapo mwaka 2015, kwa kutumia njia tatu zilizothibitishwa kimataifa kuwa zinamaliza ugonjwa huo, Rais Jakaya Kikwete alisema hayo juzi mjini hapa.
Vile vile, amesema kuwa ziara yake kwenye Umoja wa Mataifa (UN) mjini New York imekuwa ya manufaa makubwa kwa sababu Afrika imefanikiwa kuwasilisha sauti yake katika masuala muhimu yanayohusu Bara hili. Rais Kikwete aliondoka hapa jana kurejea nyumbani.
Akizungumza na waandishi wa habari wa Tanzania walioandamana naye katika ziara hiyo kuhusu mafanikio ya ziara hiyo, Rais Kikwete alisema moja ya mafanikio ya ziara yake ni kwamba Tanzania imepata uhakikisho kuwa itatokomeza malaria ifikapo mwaka 2015.
Alisema ahadi mpya za kupambana na matatizo ya Afrika, ukiwamo mwelekeo mpya wa kupambana na magonjwa na hasa malaria, inayoua watu wengi zaidi Afrika, ni moja ya mafanikio ya ziara yake UN.
Katika Tanzania, tunapambana na malaria kwa njia tatu zinazokubalika duniani, kuhakikisha kuwa wananchi wetu wanatumia vyandarua vyenye dawa, tunanyunyizia dawa za kuua mbu katika madimbwi ya maji, na pia kuhakikisha kuwa wagonjwa wanapata dawa, alisema Raia Kikwete katika mahojiano hayo kwenye Hoteli ya Intercontinental jijini New York.
Alisema njia zote tatu tayari zimeleta mafanikio makubwa Zanzibar ambako vifo kutokana na malaria vimeteremka mno, kutoka vifo 120,000 hadi 60,000 tu kwa mwaka. Na mafanikio hayo yanatokana na matumizi ya asilimia 40 tu ya vyandarua Tanzania Visiwani, lakini Zanzibar haiwezi kutokomeza malaria bila kuhakikisha kuwa Bara nayo inakuwa salama.
Hii ni mara ya tatu, tunafikia hatua ya kutokomeza malaria Tanzania Visiwani na bado ugonjwa huo umerejea kwa sababu Bara haitiliwa maanani, alisema Rais Kikwete. Alisema Tanzania inahitaji kiasi cha vyandarua milioni 15 vyenye dawa, kwa kila Mtanzania kulala bila bughudha ya mbu, na kuwa vyanzo mbalimbali vya misaada vimekwishahakikisha kuwa vyandarua hivyo vitapatikana baada ya awamu ya kwanza ya vyandarua milioni 5.2 kuwa vimepatikana.
Kama mlivyosikia, Waziri Mkuu wa Uingereza, Gordon Brown, pekee yake ameahidi kutoa kiasi cha vyandarua milioni 100 katika miaka michache ijayo. Tanzania itanufaika na sehemu na vyandarua hivyo. Pili, tunao msaada wa sekta binafsi ambayo pia itatoa vyandarua.
Mpango ni kutokomeza malaria ifikapo mwaka 2015 ni dhahiri utafanikiwa, alisisitiza Rais. Rais Kikwete aliyewasili New York, Septemba 21, mwaka huu, ameliwakilisha Bara la Afrika kwa maana ya kushiriki katika mikutano kadhaa muhimu, ikiwa ni sehemu ya mikutano ya mwaka huu ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.