Yona F. Maro
R I P
- Nov 2, 2006
- 4,202
- 218
Mwanakijiji lawama hazijengi bali zinabomoa tu
ADELADIUS MAKWEGA
Iringa
WATU wa pwani wana msemo kuwa kila kifo kina sababu yake, huo ni msemo miongoni mwa misemo mingi katika jamii yetu ya waswahili ambapo kila jambo linalotokea basi msemo, nahau na methali zinaweza kuibuka katika kusudio la kuelezea jambo hilo.
Februari 11 mwaka huu nilisoma gazeti la Tanzania daima katika kurasa yake ile ya 10 upande wa kulia wa gazeti hilo ambayo ilipambwa na na makala ya siasa ambayo ni hoja ya Mwanakijiji yenye kubeba kichwa chake kisemacho
Tuseme Ukweli, Bunge letu lina matatizo.
Kama kawaida niliisoma hoja ya mzalendo huyo mwenye jina laM.M Mwanakijiji na kuangalia je makala yake ina kitu gani juu ya Bunge letu lililoharishwa hivi karibuni na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kutoa hotuba ilyohitimisha kwa kikao hicho Mkaoni Dodoma.
Ndani ya hoja za Mwanakijiji zilikuwa zimebebwa na mikasa sita ambayo iliwafika wabunge wa Bunge letu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa vipindi mbalimbali tangu kuanza kwa Bunge letu chini ya Spika Samwel Sitta mwaka 2006.
Lakini kwa hakika hoja za M.M.Mwanakijiji zilibebwa na hisia zisizo na ukweli wowote ule ambapo kwa ujumla zilikuwa na mtazamo wa kumtafuta mchawi katika misiba na matukio ambayo kwa hakika ni sehemu ya maisha ya binadam ambayo lazima atayapitia tu.
Kwa hakika suala la kutafuta mchawi kwa kila tukio hasa ya misiba inayowakuta ndugu zetu waliofariki dunia ni tabia mbaya ambayo kwa hakika inatokana na watu ambao kwa hakika si Watanzania wa leo bali ninaamini ni tabia mbaya ambayo wengi wetu inatutia simanzi na uchungu mwingi kwenye lindi la ukungu mkubwa wa kukumbuka mambo yalikwisha pita na misiba ya kupoteza ndugu zetu ambao wengine tulikuwa tukiwapenda, tukifanya nao kazi au kuwajua kwa mema yao mengi.
Hivi kweli anapokufa kabwela mbona hatuwezi kusema mkono wa fulani?. Lakini kwanini kila anapofariki kiongozi na mtu maarufu basi litasema hili na lile.
Kwani ninaamini hii ni dhana potofu ambayo sisi wana wa Tanzania ni vema kutokupenda kukuza na kuendeleza tabia hizi ambazo kwa hakika ni propaganda ambazo ndani yake kuna uongo mkubwa ambao si kitu chema kuukuza.
Watanzania mpaka sasa tumeshuhudia matukio mangapi yakishugulikiwa vema na jeshi letu la Polisi kwa kina na kuweka hadharani na hatua kadhaa zimekuwa zikichukuliwa bila ya kujali vyeo vya wahusika hao?
Adolf Hitler aliyewahi kuwa kiongozi wa Ujerumani mwaka aliwahi kusema kama unataka propaganda iweze kuenea na kuonekana kuwa ni kweli katika vichwa vya wananchi ni vema kuisema kila mara . Basi watu waliowengi wataamini kuwa ni kweli.
Kwa hiyo hoja ya kudai hili na lile na lawama tele kwa Bunge letu ni propaganda tu ambazo si vema kuziendeleza tuwaache wabunge wetu wachape kazi kwani maneno matupo hayafunni mfupa Mwanakijiji.
Nikianzia na hoja ya M.M Mwanakijiji ya sita ambayo kwa hakika mimi binafsi ninaamini ndiyo iliyomsukuma kuandika makala yake ya tukio la Dokta Wilbroad Slaa na Daktari mwenzake Taarabu Ally juu ya kukutwa kwa vinasa sauti ndani ya vyumba vyao.
Mimi binafsi ninaamini ni matukio ambayo ni miongoni mwa matukio kazaa ambayo yanatokea na si suala la kuanza kulaumu polisi au serikali kwani kwa hakika adui hauwezi kujau anakuja lini kukufanyia tukio hilo baya.
Ni vigumu kusema kuwa Bunge kuwawekea utaratibu wa walinzi wabunge wote katika vyumba vyao wanavyoishi kwani kila mbunge anajua ni wapi atakapoishi wakati wa kikao vya bunge vinapoanza. Inakuwa ni vigumu kwa Jeshi la Polisi kuweza kufanya kazi ya kulinda wabunge hao katika kila makazi wanayoishi labda basi Jeshi hilo kuacha kabisa kazi zingine na kujiingiza kwenye majukumu ya kumlinda kila mbunge.
Kitendo hicho ni kigumu kufanyika kwani nchi yetu ni kubwa na ninaamini ni ubinafsi ambao si kitu chema kwa taifa letu. Suala la kulaumu Jeshi la Polisi kuwa ni wanaboronga si la kiungwana kwani mangapi mema vijana wa jeshi hili wanawafanyia Watanzania hadi kudai kuwa Jeshi ili linaboronga.Kwa Hakika Mwanakijiji hapo utakuwa umekwenda kombo mno kwa kutoa hoja ambayo kwa hakika haikufanyiwa uchunguzi wa kutosha juu jambo hili na hakika hapo sichelei kusema umekwenda kombo mno.
Ni jambo baya na la kushangaza kutoa lawama pale ambapo unachokifikilia kuwa sahihi pale unapokiona hakiwi kama unavyotaka kwani hiyo ni tabia
mbaya ambayo si ya kizalendo kwa mtu yeyote anayetakia mema taifa letu la Tanzania.Hivi tulitaka hao polisi wawe kama watwana wetu kwa kitu
Labda mazuri yote ynayofanywa na Bunge, serikali na vyombo vingine ya umma si kitu kwetu au tungekuwa sisi ni miongoni mwa watekelezaji tungefanya zaidi ya hayo?
Binafsi ninaamini kuwa Jeshi la Polisi la Mkoani Dodoma chini ya Kamanda Omari Mganga wanafanya vema kazi zao ili kuhakikisha raia wa taifa hili bila kujali itikadi wanaishi kwa amani na utulivi bila uonevu.
Labda wenzetu mmekuwa hamkumbuki enzi zile za kamata kamata ya polisi mitaani na kuwapa watu kesi ya kubambikia, hivi sasa imekuwa ni hadithi ya kale kwani polisi wanajitahidi kufanya kazi kwa kujali utu na utaratibu wa haki ni vema tukawapongeza sana.
Uchapakazi huo ndio maana unahakikisha wabunge wetu kwa sehemu kubwa wamekuwa wakihudhuria vikao vya bunge bila shaka yoyote na kurudi kwenye majimbo yao kwa amani kubwa na utulivu.
Mwakijiji kama hilo halitoshi pia ameshutumu sana suala la Serikali ya Chama cha Mapinduzi katika kuitisha uchaguzi pale linapotukia tukio lolote kulingana na katiba jimbo linapokuwa wazi . Hiki si kitu chema kwani si maamuzi ya serikali bali ni katiba ya nchi hii ndivyo inavyoelekeza.
Hivi kwani ata ingeingia madarakani serikali ya kikundi gani uchaguzi usifanyike labda serikali hiyo iwekuwa ya dikteta. Kwa hakika si mbunge tu bali kila raia wa nchi hii wanalindwa ndani ya nchi na katika mipaka ya taifa letu bila shaka lolote chini ya usimamizi wa Jeshi la Wananchi la Tanzania na na Jeshi la Polisi .
Kwa kifo cha Mhe Chacha Wangwe ni jambo la ajali kama ambavyo jeshi letu la polisi lilivyotoa taarifa na uchunguzi wa Daktari ulivyodokeza hivi Mwanajijiji embu tujiulize kama kungekuwa na lakini hivi ndugu wa marehemu wangeweza kukaa kimya juu ya kifo cha ndugu yao?
Si kwa Wangwe tu bali ata kwa Bi Salome Mbatia na Juma akukweti ni ajali tu ,ambazo kwa hakika ni sehemu ya maisha ya binadamu yeyote yule ambayo inaweza kumkuta katika maisha yake. Hivi tunaweza kujiuliza ni ajali ngapi zinazoweza kutokea katika taifa ili zote zina mkono wa mtu? Binafsi ninaamini imani haba ambazo kwa hakika ni vema kuwekwa kando katika maisha yetu.
Kwa hakika embu tujiulize ni Watanzania wangapi ambao wanafariki kwa magonjwa mbalimbali, Je akifariki mbunge au waziri ni lazima iwe mkono wa mtu katika taifa letu? Hilo ni swali ambalo kila mtu ni vema kujiuliza na kupata jibu kuwa wabunge, mawaziri au kiongozi yeyote wa taifa hili ni binadamu ambao wamezaliwa ,wamekua na ni wajibu wao kama binadamu yeyote yule kuonja huo umauti ambao mimi, wewe lazima utatufika tu.
Kweli watanzania mpaka leo hii bado tunaamini kuwa kila kifo cha mtu maarufu ni mkono wa mtu. Hii ni imani haba ambayo kwa hakika inanikumbusha mchezo wa kuigiza wa Edwini Semzaba ambao ulikuwa ukionyesha watu waliokuwa matatizo miaka ile 1970 ambayo imani haba ziliwafanya kutokwenda kupata ata huduma muhimu za afya, kushiriki sensa na mambo kadha muhimu kwa taifa lao.
Kwa hakika Mwanakijiji kama Mtanzania mzalendo ni vema kwa kila kiachoandikiwa ni vema kuwa na mtazamo chanya wa kuiletea maendekleo taifa letu. Ata kama ungepewa nafasi ya kufanyia majukumu ya mbalmbali ya Tanzania nawe naamini usingeweza kukamilisha kila kitu.
Kuendesha taifa si lele mama bali kila jambo linafanywa kwa wakati ni vigumu kuweza kufanikisha kila jambo kwa wakati mmoja kama Mungu alivyowalisha mana wana wa Israeli kule jangwani wakati wa kuwapeleka wana hao kwenye nchi ya ahadi.
Hivi kweli Watanzania tuna mambo mangapi yakuyashughulikia mpaka kufikia hatua ya kulaumiana kila kukicha na kuyaacha mambo ya msingi. Kwa hakika jukumu letu ni kufanyakazi hili kuleta maendeleo na si vinginevyo.
Huu uandishi wa kila kukicha wa kulaumu, kwa hakika unakuwa haujengi bali ni kitu kibaya kwa hakika unabomoa taifa letu na hata taaalumu hii ya uandishi wa habari ni vema kukawa na mtazamo wa kina kwa kila kinachoweza kuandikwa kwenye magazeti au vyombo vyetu vya habari.
MWISHO
ADELADIUS MAKWEGA
Iringa
WATU wa pwani wana msemo kuwa kila kifo kina sababu yake, huo ni msemo miongoni mwa misemo mingi katika jamii yetu ya waswahili ambapo kila jambo linalotokea basi msemo, nahau na methali zinaweza kuibuka katika kusudio la kuelezea jambo hilo.
Februari 11 mwaka huu nilisoma gazeti la Tanzania daima katika kurasa yake ile ya 10 upande wa kulia wa gazeti hilo ambayo ilipambwa na na makala ya siasa ambayo ni hoja ya Mwanakijiji yenye kubeba kichwa chake kisemacho
Tuseme Ukweli, Bunge letu lina matatizo.
Kama kawaida niliisoma hoja ya mzalendo huyo mwenye jina laM.M Mwanakijiji na kuangalia je makala yake ina kitu gani juu ya Bunge letu lililoharishwa hivi karibuni na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kutoa hotuba ilyohitimisha kwa kikao hicho Mkaoni Dodoma.
Ndani ya hoja za Mwanakijiji zilikuwa zimebebwa na mikasa sita ambayo iliwafika wabunge wa Bunge letu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa vipindi mbalimbali tangu kuanza kwa Bunge letu chini ya Spika Samwel Sitta mwaka 2006.
Lakini kwa hakika hoja za M.M.Mwanakijiji zilibebwa na hisia zisizo na ukweli wowote ule ambapo kwa ujumla zilikuwa na mtazamo wa kumtafuta mchawi katika misiba na matukio ambayo kwa hakika ni sehemu ya maisha ya binadam ambayo lazima atayapitia tu.
Kwa hakika suala la kutafuta mchawi kwa kila tukio hasa ya misiba inayowakuta ndugu zetu waliofariki dunia ni tabia mbaya ambayo kwa hakika inatokana na watu ambao kwa hakika si Watanzania wa leo bali ninaamini ni tabia mbaya ambayo wengi wetu inatutia simanzi na uchungu mwingi kwenye lindi la ukungu mkubwa wa kukumbuka mambo yalikwisha pita na misiba ya kupoteza ndugu zetu ambao wengine tulikuwa tukiwapenda, tukifanya nao kazi au kuwajua kwa mema yao mengi.
Hivi kweli anapokufa kabwela mbona hatuwezi kusema mkono wa fulani?. Lakini kwanini kila anapofariki kiongozi na mtu maarufu basi litasema hili na lile.
Kwani ninaamini hii ni dhana potofu ambayo sisi wana wa Tanzania ni vema kutokupenda kukuza na kuendeleza tabia hizi ambazo kwa hakika ni propaganda ambazo ndani yake kuna uongo mkubwa ambao si kitu chema kuukuza.
Watanzania mpaka sasa tumeshuhudia matukio mangapi yakishugulikiwa vema na jeshi letu la Polisi kwa kina na kuweka hadharani na hatua kadhaa zimekuwa zikichukuliwa bila ya kujali vyeo vya wahusika hao?
Adolf Hitler aliyewahi kuwa kiongozi wa Ujerumani mwaka aliwahi kusema kama unataka propaganda iweze kuenea na kuonekana kuwa ni kweli katika vichwa vya wananchi ni vema kuisema kila mara . Basi watu waliowengi wataamini kuwa ni kweli.
Kwa hiyo hoja ya kudai hili na lile na lawama tele kwa Bunge letu ni propaganda tu ambazo si vema kuziendeleza tuwaache wabunge wetu wachape kazi kwani maneno matupo hayafunni mfupa Mwanakijiji.
Nikianzia na hoja ya M.M Mwanakijiji ya sita ambayo kwa hakika mimi binafsi ninaamini ndiyo iliyomsukuma kuandika makala yake ya tukio la Dokta Wilbroad Slaa na Daktari mwenzake Taarabu Ally juu ya kukutwa kwa vinasa sauti ndani ya vyumba vyao.
Mimi binafsi ninaamini ni matukio ambayo ni miongoni mwa matukio kazaa ambayo yanatokea na si suala la kuanza kulaumu polisi au serikali kwani kwa hakika adui hauwezi kujau anakuja lini kukufanyia tukio hilo baya.
Ni vigumu kusema kuwa Bunge kuwawekea utaratibu wa walinzi wabunge wote katika vyumba vyao wanavyoishi kwani kila mbunge anajua ni wapi atakapoishi wakati wa kikao vya bunge vinapoanza. Inakuwa ni vigumu kwa Jeshi la Polisi kuweza kufanya kazi ya kulinda wabunge hao katika kila makazi wanayoishi labda basi Jeshi hilo kuacha kabisa kazi zingine na kujiingiza kwenye majukumu ya kumlinda kila mbunge.
Kitendo hicho ni kigumu kufanyika kwani nchi yetu ni kubwa na ninaamini ni ubinafsi ambao si kitu chema kwa taifa letu. Suala la kulaumu Jeshi la Polisi kuwa ni wanaboronga si la kiungwana kwani mangapi mema vijana wa jeshi hili wanawafanyia Watanzania hadi kudai kuwa Jeshi ili linaboronga.Kwa Hakika Mwanakijiji hapo utakuwa umekwenda kombo mno kwa kutoa hoja ambayo kwa hakika haikufanyiwa uchunguzi wa kutosha juu jambo hili na hakika hapo sichelei kusema umekwenda kombo mno.
Ni jambo baya na la kushangaza kutoa lawama pale ambapo unachokifikilia kuwa sahihi pale unapokiona hakiwi kama unavyotaka kwani hiyo ni tabia
mbaya ambayo si ya kizalendo kwa mtu yeyote anayetakia mema taifa letu la Tanzania.Hivi tulitaka hao polisi wawe kama watwana wetu kwa kitu
Labda mazuri yote ynayofanywa na Bunge, serikali na vyombo vingine ya umma si kitu kwetu au tungekuwa sisi ni miongoni mwa watekelezaji tungefanya zaidi ya hayo?
Binafsi ninaamini kuwa Jeshi la Polisi la Mkoani Dodoma chini ya Kamanda Omari Mganga wanafanya vema kazi zao ili kuhakikisha raia wa taifa hili bila kujali itikadi wanaishi kwa amani na utulivi bila uonevu.
Labda wenzetu mmekuwa hamkumbuki enzi zile za kamata kamata ya polisi mitaani na kuwapa watu kesi ya kubambikia, hivi sasa imekuwa ni hadithi ya kale kwani polisi wanajitahidi kufanya kazi kwa kujali utu na utaratibu wa haki ni vema tukawapongeza sana.
Uchapakazi huo ndio maana unahakikisha wabunge wetu kwa sehemu kubwa wamekuwa wakihudhuria vikao vya bunge bila shaka yoyote na kurudi kwenye majimbo yao kwa amani kubwa na utulivu.
Mwakijiji kama hilo halitoshi pia ameshutumu sana suala la Serikali ya Chama cha Mapinduzi katika kuitisha uchaguzi pale linapotukia tukio lolote kulingana na katiba jimbo linapokuwa wazi . Hiki si kitu chema kwani si maamuzi ya serikali bali ni katiba ya nchi hii ndivyo inavyoelekeza.
Hivi kwani ata ingeingia madarakani serikali ya kikundi gani uchaguzi usifanyike labda serikali hiyo iwekuwa ya dikteta. Kwa hakika si mbunge tu bali kila raia wa nchi hii wanalindwa ndani ya nchi na katika mipaka ya taifa letu bila shaka lolote chini ya usimamizi wa Jeshi la Wananchi la Tanzania na na Jeshi la Polisi .
Kwa kifo cha Mhe Chacha Wangwe ni jambo la ajali kama ambavyo jeshi letu la polisi lilivyotoa taarifa na uchunguzi wa Daktari ulivyodokeza hivi Mwanajijiji embu tujiulize kama kungekuwa na lakini hivi ndugu wa marehemu wangeweza kukaa kimya juu ya kifo cha ndugu yao?
Si kwa Wangwe tu bali ata kwa Bi Salome Mbatia na Juma akukweti ni ajali tu ,ambazo kwa hakika ni sehemu ya maisha ya binadamu yeyote yule ambayo inaweza kumkuta katika maisha yake. Hivi tunaweza kujiuliza ni ajali ngapi zinazoweza kutokea katika taifa ili zote zina mkono wa mtu? Binafsi ninaamini imani haba ambazo kwa hakika ni vema kuwekwa kando katika maisha yetu.
Kwa hakika embu tujiulize ni Watanzania wangapi ambao wanafariki kwa magonjwa mbalimbali, Je akifariki mbunge au waziri ni lazima iwe mkono wa mtu katika taifa letu? Hilo ni swali ambalo kila mtu ni vema kujiuliza na kupata jibu kuwa wabunge, mawaziri au kiongozi yeyote wa taifa hili ni binadamu ambao wamezaliwa ,wamekua na ni wajibu wao kama binadamu yeyote yule kuonja huo umauti ambao mimi, wewe lazima utatufika tu.
Kweli watanzania mpaka leo hii bado tunaamini kuwa kila kifo cha mtu maarufu ni mkono wa mtu. Hii ni imani haba ambayo kwa hakika inanikumbusha mchezo wa kuigiza wa Edwini Semzaba ambao ulikuwa ukionyesha watu waliokuwa matatizo miaka ile 1970 ambayo imani haba ziliwafanya kutokwenda kupata ata huduma muhimu za afya, kushiriki sensa na mambo kadha muhimu kwa taifa lao.
Kwa hakika Mwanakijiji kama Mtanzania mzalendo ni vema kwa kila kiachoandikiwa ni vema kuwa na mtazamo chanya wa kuiletea maendekleo taifa letu. Ata kama ungepewa nafasi ya kufanyia majukumu ya mbalmbali ya Tanzania nawe naamini usingeweza kukamilisha kila kitu.
Kuendesha taifa si lele mama bali kila jambo linafanywa kwa wakati ni vigumu kuweza kufanikisha kila jambo kwa wakati mmoja kama Mungu alivyowalisha mana wana wa Israeli kule jangwani wakati wa kuwapeleka wana hao kwenye nchi ya ahadi.
Hivi kweli Watanzania tuna mambo mangapi yakuyashughulikia mpaka kufikia hatua ya kulaumiana kila kukicha na kuyaacha mambo ya msingi. Kwa hakika jukumu letu ni kufanyakazi hili kuleta maendeleo na si vinginevyo.
Huu uandishi wa kila kukicha wa kulaumu, kwa hakika unakuwa haujengi bali ni kitu kibaya kwa hakika unabomoa taifa letu na hata taaalumu hii ya uandishi wa habari ni vema kukawa na mtazamo wa kina kwa kila kinachoweza kuandikwa kwenye magazeti au vyombo vyetu vya habari.
MWISHO
Last edited by a moderator: