LordJustice1
JF-Expert Member
- Jan 19, 2011
- 2,263
- 530
Wazanzibari wanaogopwa sana na Viongozi wetu wa Serikali ya Muungano! Laiti kama wangeuchana tena Muswada wa kuunda Tume ya kukusanya maoni kuhusu Katiba mpya JK asingethubutu kusaini Muswada husika! Hali inavyoelekea JK atausaini Muswada huo bila kujali kelele za aina yoyote toka Bara! Hata hivyo JK ana-create matatizo makubwa sana kwa Tanzania ijayo! Kelele kuhusu "Katiba mpya nyingine" hazitaisha na umoja na mshikamano wetu utaendelea kumomonyoka siku hadi siku! Serikali kwa kutokuwashirikisha wananchi katika mchakato huu wa Katiba mpya inafanya kosa lile lile lililofanywa tangu Uhuru zilipoundwa Katiba nyinginezo!