Lady Jay Dee ajibu hoja ya Wakurya!

Napenda nirekebishe baadhi ya kauli ambazo zimezungumzwa na baadhi ya wachangia maoni wa website moja hivi, (jina si muhimu kutaja).
Ila najua watasoma kwani kila mara wamekuwa wakiingia na ku copy paste ishu za humu kuziweka kwenye ubao wao na kuanza kuzijadili.

Kwenye site hiyo ambayo wengi wao hujiita wasomi na kusema sana wengine, kuna waliosema kuwa mkoa wa Mara kuna makabila matatu tu, Wakurya, Wajita na Wajaluo na zilizobaki zingine zote ni koo tu.
/

wakiingia na ku copy paste ishu za humu =tafsri yake ni nini, kwamba za humo (kwenye blog yake) ni hoja za busara zaidi au hazipaswi kujadiliwa popote?. Nini dhana ya kuja kusomea humu na kwenda kujibia kwenye blog yake ambapo kinadharia hoja imetokea humu ambao yeye anahisi hao wanao waeleza hawaingii humu?

kuziweka kwenye ubao wao = wao kina nani? sio hao ambao pia wapo humu JF?

Kwenye site hiyo ambayo wengi wao hujiita wasomi na kusema sana wengine = hujiita wasomi wapi? na kama hivyo sivyo, ya nini kusema "wanajiita" ?


Napata mashaka sana na upeo wa kufikiri wa huyu BINTI MACHOZI na majibu haya yananifanya nimwone ni mwanamke anayependa visasi, majungu na kutokubali kushindwa hata kwenye hoja za kawaida tu ambazo zinahitaji majibu ya moja kwa moja pasipo kuchambuana.

Labda kama ipo hivi hata huko nyumbani, basi ni balaa kwa "Mzee wa Majahazi":
 
wakiingia na ku copy paste ishu za humu =tafsri yake ni nini, kwamba za humo ni za busara sana au hazipaswi kujadiliwa popote?. Nini dhana ya kuja kusomea humu na kwenda kujibia kwenye blog yake ambapo kinadharia hoja imetokea humu ambao yeye anahisi hao wanao waeleza hawaingii humu?


kuziweka kwenye ubao wao = wao kina nani? sio hao ambao pia wapo humu JF?

Kwenye site hiyo ambayo wengi wao hujiita wasomi na kusema sana wengine = hujiita wasomi wapi? na kama hivyo sivyo, ya nini kusema "wanajiita" ?

Sasa inashangaza wengine wanamtetea huyu mpuuzi.
 
Sikuelewi. Unapinga nini hapa? Kwamba JD sio mpuuzi? au?

Wapi nilipopinga zaidi ya wewe kushindwa kujibu swali nililouliza?!

Hoja muhimu hapa ni kujaribu kuheshimu maoni ya mtu hata kama hukubaliani nayo na wala sio kutumwita mpuuzi. Kama waona alichoandika ni pumba basi tuandikie mchele ili tuweze kupembua mchele kutoka kwenye pumba.
 
Wapi nilipopinga zaidi ya wewe kushindwa kujibu swali nililouliza?!

Ulitegemea nijibu swali, kwani uliniajiri? unaweza kumjadili mtu mpuuzi ktk yale yasiyo ya kipuuzi, hivo ukawa sio mpuuzi. haya umeridhika?
Hoja muhimu hapa ni kujaribu kuheshimu maoni ya mtu hata kama hukubaliani nayo na wala sio kutumwita mpuuzi. Kama waona alichoandika ni pumba basi tuandikie mchele ili tuweze kupembua mchele kutoka kwenye pumba.

Na hoja yangu hapa, nikuwa wambura ni mpuuzi kutokana na maneno yake mwenyewe ambayo kayaweka kwenye ka-blog kake ka topic za saluni..hivo na wewe heshimu maoni yangu. nukta.
 
Kumbe Jay Dee ni mshashi, nilikuwa sijui; nadhani hilo ndilo kabila la mzee Wassira pia. Pamoja na udaku huo, ni kweli Jay Dee kaongea point nzito kabisa kuhusu tabia yetu mbaya ya stereotyping.
 
Kumbe Jay Dee ni mshashi, nilikuwa sijui; nadhani hilo ndilo kabila la mzee Wassira pia. Pamoja na udaku huo, ni kweli Jay Dee kaongea point nzito kabisa kuhusu tabia yetu mbaya ya stereotyping.
Kichuguu,
JD yuko related kwa Wassira.
 
Mwacheni jamani dada wa watu mbona mnamsakama sana.Ahsanteni
Wanapomjadili anyamaze na kujifunza kutoka katika majadiliano yanayomhusu yeye. Hajajua mpaka leo gharama ya umaarufu?(hata kama ni umaarufu uchwara)
 
WAKURYA NA WASIZAKI HAWAZUNGUMZI LUGHA MOJA WALA MILA HAZIFANANI....KAMA AMBAVYO SITE MOJA YA KU COPY PASTE NA WATU WAKE WALIVYOONGELEA

Napenda nirekebishe baadhi ya kauli ambazo zimezungumzwa na baadhi ya wachangia maoni wa website moja hivi, (jina si muhimu kutaja).
Ila najua watasoma kwani kila mara wamekuwa wakiingia na ku copy paste ishu za humu kuziweka kwenye ubao wao na kuanza kuzijadili.

Kwenye site hiyo ambayo wengi wao hujiita wasomi na kusema sana wengine, kuna waliosema kuwa mkoa wa Mara kuna makabila matatu tu, Wakurya, Wajita na Wajaluo na zilizobaki zingine zote ni koo tu.
Na kuwa katika Category ya wakurya ndio kuna wazanaki ambao ni pamoja na JK Nyerere na wasizaki ambao ni kina sisi na kuwa wote tunaongea lugha moja. By the way mama yangu ni mu Ikizu sijui nae watamuweka category gani maskini ya Mungu??
Lugha ambayo na hakika kuwa matamshi yao ni sawa sawa ni Ikizu na Sizaki.

SALAAM KWA BABA:
Wa Ikizu na Wasizaki wanasema Bhaa
Wa Kurya wanasema Tata

SALAAM KWA MAMA:
Wa Ikuzu na Wasizaki wanasema Iya
Wa Kurya wanasema Mayi

SALAAM KWA BIBI:
Wa Ikizu na Wasizaki wanasema Koko
Wa Kurya wanasema Ghoko

Swala la maneno kukaribiana linaweza kuwepo kwenye lugha zozote za kibantu kwa mfano
Nyoka ni kiswahili, kikwetu ni Inzoka lakini kwa lugha ya kizulu pia ni Izinyoka
Chumvi inaitwa " munyu/ Umunyu" na makabila mengi tu....

Nakupenda kwa kichaga NAKUKUNDA, kirundi na kinyarwanda NDAGUKUNDA, na hizi ni nchi tatu tofauti...
au basi labda afrika nzima hakuna makabila zote ni koo??? maana maneno mengi tu ya lugha za afrika yanafanana, sio lazima kuwa msomi sana kutambua ulimwengu unaendaje, Dunia yenyewe shule tosha.

Wambura ni jina langu na sio surname yangu kama ambavyo wengi wanadhani, kuna makabila mengine Wambura ni mwanaume kama Wakurya ila kwa sisi Wambura wengi ni wanawake.
Baba yangu anaitwa Lameck Isambwa Mbibo (RIP)

Niliandika tu kuwa mimi kabila langu ni Msizaki na sio Mkurya kama ambavyo watu wengi wanadhani.. Ila naona imechukuliwa kana kwamba nakana ukabila

Chanzo: http://www.ladyjaydee.blogspot.com/

Hapo kwenye red sidhani, hakuna mayi kwenye ukurya , mayi ni kwa wajita, mkurya humsalimia mama, bhabha.
Mi sioni kwa nini JD anaikuza sana hii ishu na kujikita muda mwingi kubishana na JF, thats wastage of time maana watu wa jf wengi wakiamua kwenda naye papendicular sidhani kama atatoboa. so sisy just chill hata kama dunia shule tosha, hata shule ya ukweli ina umuhimu. so acha vijineno vya kitaa as if huna exposure. Ni hizi hizi critisism ambazo zinakusaidia in one way or another
 
Wanapomjadili anyamaze na kujifunza kutoka katika majadiliano yanayomhusu yeye. Hajajua mpaka leo gharama ya umaarufu?(hata kama ni umaarufu uchwara)

Hehehehe kazi kweli kweli mwaka huu tutasikia mengi.
 
Hii ndiyo sababu iliyomfanya Mwalimu Nyerere akakataza watu ku-addressiana kwa makabila yetu! Tunapoanza kubaguana ndiyo yote haya yanapoanza. Je unajua kwamba wamarekani Weusi wanahusishwa na uvunjwaji wa sheria wa aina zote? Hapa ndipo linapokuja swala la makabila! lakini kama ualivyosema tumwangalie mtu mmjoja mmoja kuliko kuujumuuisha na kuconclude. Kila mtu yuko wa kipekee na tofauti na mwingine!

Hii inaitwa stereo type!Mchaga mwizi,Mhaya malaya,Muha Mchawi,Mpare Bahili,Mzungu mwaminifu...tajiri...ana akili na busara?!?

Lakini tuangalie,baada ya media kuanza kufanya kazi na watu,ni ukatili wa aina ngapi umefunuliwa? Kwa wamawake,kwa watoto au kwa walemavu? Kila siku kuna jipya kwenye vyombo vya habari. Na karibu kila kabila linahusika!

Wanasayansi wote wanakubaliana 1+1=2 lakini ni kweli? Au inabidi tukubali kuwa lisemwalo lipo?

sayansi ya jamii je?!?
 
source: ladyjaydee.blogspot.com
Binti umenena. kwani hakuna mtu aliyechagua wazazi wa kumzaa wala kabila wote wamejikuta katika ukoo/kabila fulani. Hivyo kujumuisha ki-ujumla siyo sahihi.
Binafsi ninawafahamu wakurya wengi ambao sio tu kuwa hawana tabia ya ugomvi bali ni wastaarabu kuliko makabila mengine.
 
Carmel unashangaa JD kuendelea kubishana na JF, well ni kwa sababu sisi wadau wa JF ndio tunampa nafasi ya kubishana nasi, if we just drop this topic and think of something more productive in JF, JD hatabishana nasi!
 
Hapo kwenye red sidhani, hakuna mayi kwenye ukurya , mayi ni kwa wajita, mkurya humsalimia mama, bhabha.
Mi sioni kwa nini JD anaikuza sana hii ishu na kujikita muda mwingi kubishana na JF, thats wastage of time maana watu wa jf wengi wakiamua kwenda naye papendicular sidhani kama atatoboa. so sisy just chill hata kama dunia shule tosha, hata shule ya ukweli ina umuhimu. so acha vijineno vya kitaa as if huna exposure. Ni hizi hizi critisism ambazo zinakusaidia in one way or another

I second you and AbdulH, mbona tunampaisha huyu!!

Kwani yeye nani... huyu ni mtu asiye na upeo na mahali alipotoka. Hii si "inshu" ya kutupotezea...
 
she has all the rights to say what she feels!!!!!!


Yes, but with facts!!
Kama yeye anabisha hata mambo ya kwao inakuwaje hapo? Hii siyo sehemu ya kutafutia ummarufu, sana sana kukabiliana na challenges, which if you take them positively may reach somehwre and learn.
 
jamani kama binadamu wa kawaida nahisi alikuwa anaweka mambo sawa though siku zote alikuwa anakubali kuitwa mkurya lkn leo hataki coz mapanga yamezidi jmn! hilo kabila lipo lkn ndo vile vikabila vidogo vidogo ambavyo kumuelezea mtu hataelewa upesi so huwa wanasema ni wakurya tu ingawa sivyo na wanaingiliana sana almost kila kitu na wakurya.

zipo kabila kama wangoreme hawa pia wanaingiliana na wakurya, ni kama wazinza kutoka mwanza kabila la waziri wetu wa mambo ya nje, wanavyojiita wasukuma, wanyiha wa mbeya wanavyojiita wanyakyusa na vitu kama hivyo.

sp dada hakukosea kutuelezea tukamuelewa, tatizo anaonekana ana jazba! wamekusoma dada, usiogope! mimi MKURYA NAJIVUNIA UKURYA WANGU NA KAMWE SIJIITI MNGOREME KUWAOGOPA WATU, MAISHA NI VILE UNAVYOISHI SI WATU WANAVYOTAKA UISHI!
 
JD hakuzaliwa Mara au kama alizaliwa kule, hakukulia kule. Mengi ya kule hayajui. Angeniruhusu nimwone ningemwelimisha vya kutosha tena kwa lugha yake.
 
Back
Top Bottom