Ladies, are we the cause of our husbands cheating?

Kila siku wanaume kwa wanawake wanatoka nje ya mahusiano yao bila kujua au hata kujali sana kitakachotokea ikiwa watafumaniwa/gunduliwa na wenzi wao. Kama baadhi yetu tunavyoimba kila siku kwamba "Cheating is BAD" ndivyo nao wanavyoimba kwamba "Cheating is NECESSARY/INEVITABLE". Wanatoka nje ya mahusiano yao bila kufikiria wala kujali matokeo yake kwao binafsi, watoto kama wanao na wenzi wao kwa visingizio vya "nature haikubali niwe na mwanamke mmoja, mume/mke wangu haniridhishi/ mwenzangu hanijali/umbali ndio chanzo n.k"

Matokeo mabaya ya kucheat ni pamoja na kumuumiza mwenzi, kupeleka magonjwa (ya moyo/kiakili na kimwili kwa ujumla) kwa aliyetulia nyumbani, kuzaa mtoto ambae anaweza asikubaliwe na mwenzi hata kuishia kunyanyaswa, kuwakosesha watoto malezi wanayostahili, mahusiano/ndoa kuvunjika na kubwa zaidi ambalo sidhani kama watu hua wanalifikiria sana. . . nalo ni kuuwawa au hata kuumizwa sana pale atakapokamatwa.

Hizi kesi ambazo mtuhumiwa anakua amefanya kosa (laweza kuwa ni la kuua, kubaka au kumpiga hata kumuumiza mwenzake) kutokana na hisia kali sana za mapenzi au hasira baada ya kufumania huitwa Crimes of passion. Je na wewe uko tayari kuwa victim wa hili baada ya kumfanya mwenzio victim wa kudanganywa?

Mwaka jana tu tulisikia hapa kwetu mwanaume alichomwa kisu na mwanamke wake wa nje baada ya kugundua kwamba hakua mwenyewe, kuna mama wa kiMarekani (Clara Harris ukipenda kumgoogle) yeye alimgonga mume wake kwa gari mara kadhaa baada ya kumkuta hotelini na mwanamke mwingine, Zimbabwe kuna mwanaume alimchoma mke kisu. . akachinja mtoto mwenye umri wa siku mbili ambae alikua wa mwanaume mwingine kabla nae hajajitundika.

Haya ni madhara makubwa zaidi tofauti ya yale tuliyozea/wahusika wanayotegemea kwasababu yanahusu kuondoa maisha ya mtu au hata watu. Je wewe unadhani hicho unachopata huko nje ya ndoa/mahusiano yako kina thamani sawa na maisha yako wewe au ya mtu mwingine yeyote yule? Kama kina thamani kiasi hicho kwanini usiachane na maisha uliyonayo ukaenda kuanza upya huko unakopata hicho/hayo yaliyo muhimu zaidi?

Binafsi napinga sana kitendo cha mtu kutoka nje ya mahusiano yake kwa sababu yoyote ile. . tena baada ya kushuhudia mtu ambae alijitahidi kuwa mke mtulivu akiletewa UKIMWI nyumbani kwake, ugonjwa ambao unaweza ukafupisha maisha yake nashindwa kabisa kuelewa ni vipi mtu anaweza akawa mbinafsi hata kupitiliza. Jioneeni huruma, waoneeni wake/waume/wapenzi/watoto na ndugu zenu huruma. Ukiona mambo yamekufika shingoni, nyumbani hakukaliki jiweke huru. Maana kwa kutaka kuendelea kuwepo huko na bado uwepo kule kunaweza kukakufanya wewe usiwe tofauti na mtu muuaji.

Cheating is a very selfish act. . . JALI, CHUKUA HATUA!
Lizzy

Umeongea vizuri
 
Thanks Lizzy, post imetulia...

Kila Kosa huwa lina sababu.. Pia amini dalili za ku- cheat sometime zinaonekana kabla hata mahusiano hayajafika kwenye Ndoa. Ingawa wanaume ni wadhaifu sana lakini naamini wanawake wanachangia asilimia kubwa ya mwanaume ku-cheat. Tufungue midomo na tuongee suala hili katika mahusiano yetu. Kunyoosheana vidole hakutasaidia kitu...
 
Hii kitu ni kweli kabisa watu wanacheat bila kujali ni madhara gani yatatokea. Mimi binafsi nilishampiga mwanamke nusura kumuua coz alinicheat katika mazingira ya ajabu. Nilimpa kila kitu yaani mapenzi nilimjali 100% lakini akaishia kunicheat eti shetani alimpitia.
 
utakaaje usuburi kupewa raha na mtu mwingine? mtu anawezaje kukuongezea watoto?

Au tuseme hivi, kama unaona unaletewa magonjwa na ukaendelea kuyapokea, nani alaumiwe?

Kama unaona unakoseshwa raha, kwa nini usiende unapodhani utapewa raha?

Kama unaona unaongezewa watoto, kwa nini unaendelea kukubali?

Let us be responsible for our own mistakes.




you seem not ready for any discussion.

Aisee. . .
Sasa watu wakienda kucheat hua wanaaga hata uulize hayo maswali uliyouliza?

Anaeweza kukwepa hayo ni yule anaejua kwamba mwenzake anatoka nje ya mahusiano na sio kila anaekua cheated.
 
Aisee. . .
Sasa watu wakienda kucheat hua wanaaga hata uulize hayo maswali uliyouliza?

Anaeweza kukwepa hayo ni yule anaejua kwamba mwenzake anatoka nje ya mahusiano na sio kila anaekua cheated.

Wengi wanaocheat huwa wanawadanganya wenza wao. Sasa anayechitiwa anadhani anapendwa na huyo mwenza wake kumbe ni uongo mtupu.

Unakuta jitu linaapia kwa miungu yote kuwa linakupenda kumbe wapi! Hakuna lolote.

Sasa inapotokea unajua kuwa mwenza wako anakucheat na wewe unaendelea kubaki naye hapo wa kulaumiwa utakuwa ni wewe. But until then, the blame lies squarely on the cheater.
 
Thanks Lizzy, post imetulia...

Kila Kosa huwa lina sababu.. Pia amini dalili za ku- cheat sometime zinaonekana kabla hata mahusiano hayajafika kwenye Ndoa. Ingawa wanaume ni wadhaifu sana lakini naamini wanawake wanachangia asilimia kubwa ya mwanaume ku-cheat. Tufungue midomo na tuongee suala hili katika mahusiano yetu. Kunyoosheana vidole hakutasaidia kitu...


Tulizo kama ulivyosema dalili zinaonekana 'sometimes' na sio 'all the time'. Ndio maana hao wanaocheat wana mpaka mbinu za kukwepa kuonyesha mabadiliko nyumbani ili washtukiwe. . .kwahiyo iwe mmoja ndie kisababishi au la, anaetoka ndio mwenye maamuzi ya mwisho. Anaweza akajitahidi kumrekwbisha mwenzake na ikishindikana kabisa aende kwenye unafuu badala ya kuongeza matatizo juu ya matatizo. Sio haki kabisa kwa wale ambao wanahusika (watoto, wenzi au hata ndugu).
 
Aisee. . .
Sasa watu wakienda kucheat hua wanaaga hata uulize hayo maswali uliyouliza?

Anaeweza kukwepa hayo ni yule anaejua kwamba mwenzake anatoka nje ya mahusiano na sio kila anaekua cheated.

Unajua unaweza kuwa selfish zaidi ya huyo mwenza wako anayecheat unayemwita selfish (mtu mwenye selfish act), kwa vile unataka ku own binadamu mwenzio akufanyie (kukufurahisha, kutokuletea magonjwa na kutokuongezea watoto).
 
Hii kitu ni kweli kabisa watu wanacheat bila kujali ni madhara gani yatatokea. Mimi binafsi nilishampiga mwanamke nusura kumuua coz alinicheat katika mazingira ya ajabu. Nilimpa kila kitu yaani mapenzi nilimjali 100% lakini akaishia kunicheat eti shetani alimpitia.

Mbaya sana aisee. .
Unaweza ukajikuta unafanya kitu ambacho hukuwahi kutarajia au hata kujua unaweza. Kuna mshkaji ye alimvunja binti mbavu.
 
Wengi wanaocheat huwa wanawadanganya wenza wao. Sasa anayechitiwa anadhani anapendwa na huyo mwenza wake kumbe ni uongo mtupu.

Unakuta jitu linaapia kwa miungu yote kuwa linakupenda kumbe wapi! Hakuna lolote.

Sasa inapotokea unajua kuwa mwenza wako anakucheat na wewe unaendelea kubaki naye hapo wa kulaumiwa utakuwa ni wewe. But until then, the blame lies squarely on the cheater.

Agreed!!!
 
Unajua unaweza kuwa selfish zaidi ya huyo mwenza wako anayecheat unayemwita selfish (mtu mwenye selfish act), kwa vile unataka ku own binadamu mwenzio akufanyie (kukufurahisha, kutokuletea magonjwa na kutokuongezea watoto).
Hilo linawezekana iwapo tu huyo anaeavhwa nyumbani hampi mwenzake sababu ya kumfanyia yaliyo mazuri . . other than that hamna ambae anam-Own mwenzake kwa kutaka tu asitendewe mambo ambayo ni nje/kinyume ya makubaliano yao ikiwa na yeye anatimiza majukumu yake kama mwenzi kuendana na makubaliano.
 
Kama watu mmekubaliana kuwa uhusiano wenu uwe monogamous halafu mmoja wenu anakiuka makubaliano hayo, hivyo ni vibaya.

Kama uhusiano wenu ni huria na wote mmeliridhia hilo, basi hakuna ishu.

Tatizo ni pale mmoja anapom-lead mwenzake kudhani/ kuamini kuwa hivi halafu yeye anafanya vile. Why lie?
 
Kama watu mmekubaliana kuwa uhusiano wenu ume monogamous halafu mmoja wenu anakiuka makubaliano hayo, hivyo ni vibaya.

Kama uhusiano wenu ni huria na wote mmeliridhia hilo, basi hakuna ishu.

Tatizo ni pale mmoja anapom-lead mwenzake kudhani/ kuamini kuwa hivi halafu yeye anafanya vile. Why lie?

Because that's just what they are. . . LIARS.
Watu wengine kwao kusema ukweli ni mwiko kabisa.
 
Tulizo kama ulivyosema dalili zinaonekana 'sometimes' na sio 'all the time'. Ndio maana hao wanaocheat wana mpaka mbinu za kukwepa kuonyesha mabadiliko nyumbani ili washtukiwe. . .kwahiyo iwe mmoja ndie kisababishi au la, anaetoka ndio mwenye maamuzi ya mwisho. Anaweza akajitahidi kumrekwbisha mwenzake na ikishindikana kabisa aende kwenye unafuu badala ya kuongeza matatizo juu ya matatizo. Sio haki kabisa kwa wale ambao wanahusika (watoto, wenzi au hata ndugu).

...Nakubaliana nawe kabisa.Hivyo basi Cheating ni sawa na 'foolish pride' ya mtendaji..
 
Hii kitu ni kweli kabisa watu wanacheat bila kujali ni madhara gani yatatokea. Mimi binafsi nilishampiga mwanamke nusura kumuua coz alinicheat katika mazingira ya ajabu. Nilimpa kila kitu yaani mapenzi nilimjali 100% lakini akaishia kunicheat eti shetani alimpitia.
Wewe umewahi kucheat?
Cheating men huaga wakali na hawataki kuchitiwa hata kama ni utani wa maneno tu!
wakati mwingine nawaelewa wanawake wanaochiti - wale wenye waume malaya!Ni vizuri sana wasikie inavyouma.
Simpi sapoti mwanamke mwenye mume mwema mwenye heshima na kujali.
 
Umeongea vizuri sana Lizzy na kama haya yote uliyoandika hapa ni kutoka kwako mwenyewe basi nakushauri uanzishe au kujiunga na vituo vya ushauri kwa wanandoa na nina uhakika kuwa utasaidia wengi sana na kujiongezea kipato pia.
 
Wewe umewahi kucheat?
Cheating men huaga wakali na hawataki kuchitiwa hata kama ni utani wa maneno tu!
wakati mwingine nawaelewa wanawake wanaochiti - wale wenye waume malaya!Ni vizuri sana wasikie inavyouma.
Simpi sapoti mwanamke mwenye mume mwema mwenye heshima na kujali.
Kwa hiyo you imply that ubaya wa cheating ni relative?
 
Umeongea vizuri sana Lizzy na kama haya yote uliyoandika hapa ni kutoka kwako mwenyewe basi nakushauri uanzishe au kujiunga na vituo vya ushauri kwa wanandoa na nina uhakika kuwa utasaidia wengi sana na kujiongezea kipato pia.
Asante St. .
Nafurahi kukuona tena jukwaani.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom