Laana Aliyoacha Benjamin Mkapa Ni Kweli?

Ndallo

JF-Expert Member
Oct 1, 2010
7,619
4,292
Nakumbuka maraisi waliomtangulia Jakaya Kikwete waliacha wosia au ndio tuiite ni laana! Mwalimu alicha wosia mwingi sana kwa taifa hili hata kwenye Tape zinazouzwa mitaani ni tosha kabisa kuamini alichokua anakiongea na vinaonekana sasa hivi, sikumbuki raisi mwinyi aliacha wosia gani kama kuna mtu anakumbuka aliacha wosia gani kwa taifa hili baada ya kumaliza muda wake wa kuongoza taifa hili atatueleza. Lakini mimi kuhusiana na heading yangu hapo juu nakumbuka baada ya miongo miwili ya utawala wa muheshimiwa Mkapa aliwacha wosia kwakusema hivi "MTANIKUMBUKA" mwisho wa kumnukuu! Wanajanvi natafakari sana kwakina huu usemi kama ukijaribu kutafakari alipotuacha na hapa tulipo, Je wanajanvi usemi huu ndio tunachokiona sasa hivi ?? Jamani naomba kuwasilisha.
 
Tutamkumbuka kwa kuuza nchi, EPA, IPTL, na kutuletea timu ya RICHMOND na takataka nyingine.

Katuachia Rais Mzuri sana ambaye kweli ukiwalinganisha, pamoja na WIZI wa Mkapa, unaona kumbe ana nafuu.

Angelishinda Slaa, sasa hivi nina imani tungelikuwa tunaimba wimbo mwingine.
 
Vision ya Mkapa ya kumaliza umasikini wa Tanzania by 2025, naona Kikwete katia kapuni, halafu ile mikakati ya kupunguza umaskini aliyokuwa nayo Mkapa kama vile MKUKUTA, MKURABITA, PEDP, SEDP, naona yote hivi sasa inalegalega. Tumepata rais ambaye kila kuchwapo yupo angani, hana muda wa kukaa ikulu atatue matatizo ya watanzania. Binafsi sioni kama maneno ya Mkapa ni laana, bali laana yenyewe ni Kikwete. Maana Mkapa kwa nafasi yake alikuwa na uwezo wa kumpiga vita Kikwete asigombee urais.
 
Nakumbuka maraisi waliomtangulia Jakaya Kikwete waliacha wosia au ndio tuiite ni laana! Mwalimu alicha wosia mwingi sana kwa taifa hili hata kwenye Tape zinazouzwa mitaani ni tosha kabisa kuamini alichokua anakiongea na vinaonekana sasa hivi, sikumbuki raisi mwinyi aliacha wosia gani kama kuna mtu anakumbuka aliacha wosia gani kwa taifa hili baada ya kumaliza muda wake wa kuongoza taifa hili atatueleza. Lakini mimi kuhusiana na heading yangu hapo juu nakumbuka baada ya miongo miwili ya utawala wa muheshimiwa Mkapa aliwacha wosia kwakusema hivi "MTANIKUMBUKA" mwisho wa kumnukuu! Wanajanvi natafakari sana kwakina huu usemi kama ukijaribu kutafakari alipotuacha na hapa tulipo, Je wanajanvi usemi huu ndio tunachokiona sasa hivi ?? Jamani naomba kuwasilisha.
Ni kweli mkuu, tunamkumbuka sana,
katuachia meremeta, mwananchi tangold, Anaben bank, EPA, kiwira, soko holela, mikataba mibovu ya madini, kuuzwa kwa shirika la ndege (ATC) likiwa na ndege zaidi ya 15 na kurudishwa likiwa na ndege 1, kuuzwa NBC kwa bei ya chee, na mengine mengi.
Tunamkumbuka sana tu.
 
Tutamkumbuka kwa kuuza nchi, EPA, IPTL, na kutuletea timu ya RICHMOND na takataka nyingine.

Katuachia Rais Mzuri sana ambaye kweli ukiwalinganisha, pamoja na WIZI wa Mkapa, unaona kumbe ana nafuu.

Angelishinda Slaa, sasa hivi nina imani tungelikuwa tunaimba wimbo mwingine.

Mkuu najiuliza tu: Mkapa alipoondoka Slaa aligombea Urais?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom