KYELA KUNANI PALE?? MBONA KILA SIKU Kyela tuu!!!

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Feb 4, 2009
74,833
155,780
Jamani nimekuwa nikisoma magazeti na makala mbalimbali hapa Jamii Forums,
lakini cha kushangaza ni hili jimbo la uchaguzi la Kyela, sijui kwa nini limekuwa likiongelewa sana kuliko majimbo mengine yoyote hapa nchini Tanzania.
Najiuliza, mbona kwenye vita ya ufisadi sio Mwakyembe tu ambaye yuko mstari wa mbele, wapo wabunge wengi sana, lakini majimbo yao hayajawa gumzo.
Kama ni hela za Mwakalinga, mbona wenye hela wapo wengi sana wanawania ubunge lakini majimbo yao hayajawa gumzo?
sasa kwanini kila siku Kyela ndio inazungumziwa zaidi?/
kunanipale , naomba mnijulishe na mimi ili nipate kujua siri ya Kyela kuwa midomoni mwa watu usiku na mchana.
 
Bujibuji wewe ni wa wapi? kama siyo wa kyela waachie wa kyela wajadili mustakabali wa jimbo lao. Lakini usisahau kwamba mafisadi wanachofanya ni kuhakikisha wanaowasema hawarudi tena bungeni na wamejipanga vizuri kutimiza lengo lao.
 
bendera kufuata upepo si unajua mtu akiwa maarufu? watz bado hawajaamini kuwa kunaweza kutokea mashujaa kama akina mwakyembe wakauchachafya uongozi wa juu kabisa wa nchi bila kujali kama wako chama kimoja.....ujasili wa namna hii ni zaidi ya pesa walizomwaga akina lowasa na rostamu ili kumwangusha mwakyembe..........''NABII HAKOSI HESHIMA,ISIPOKUWA NYUMBANI KWAO NA KWA NDUGU ZAKE''watu wanajaribu kudadavua huku na kule ili kujua ukweli kuhusu misimamo ya mwakyembe.
Jamani nimekuwa nikisoma magazeti na makala mbalimbali hapa Jamii Forums,
lakini cha kushangaza ni hili jimbo la uchaguzi la Kyela, sijui kwa nini limekuwa likiongelewa sana kuliko majimbo mengine yoyote hapa nchini Tanzania.
Najiuliza, mbona kwenye vita ya ufisadi sio Mwakyembe tu ambaye yuko mstari wa mbele, wapo wabunge wengi sana, lakini majimbo yao hayajawa gumzo.
Kama ni hela za Mwakalinga, mbona wenye hela wapo wengi sana wanawania ubunge lakini majimbo yao hayajawa gumzo?
sasa kwanini kila siku Kyela ndio inazungumziwa zaidi?/
kunanipale , naomba mnijulishe na mimi ili nipate kujua siri ya Kyela kuwa midomoni mwa watu usiku na mchana.
 
Back
Top Bottom