Kwenu Waandishi wa Habari na Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania...

Wasallam!Kama mwanajukwaa nitumie nafasi hii kutoa maoni yangu kwa kutumia elimu ya sayansi ya jamiii niliyoipata pale Mlimani pamoja na exprience yangu ya maisha juu ya kifo cha mpendwa na mwanaharakati mwenzetu Daud Mwangosi. Kwanza nianze kwa kutoa salamu zangu za rambirambi kwa familia yake na wapenda haki na wanaharakati wa mageuzi hapa nchini.Pili nitumie fursa hii kutoa maoni yangu.Ndugu wanajamii,serikali ya CCM kama ilivyo kwa mfumo wowote wa kisiasa umekwisha zeeka na hivyo ni kuukuu.Mfumo huu umeshindwa kuwateka wananchi kifikra kwa kuwaletea maendeleo na hivyo badala yake njia pekee iliyobakia kwao ni matumizi ya rushwa,vitisho na mauaji.Nchi kwa sasa haijiwezi imefilisika,makarani wa sensa wanalipwa ujira wao kwa mafungu katika nchi ijaayo maziwa na asali.Mfumo huu mpaka utakapokuwa unafika mwaka wa ukombozi 2015 utakuwa umegharikisha raia wasikuwa na hatia wengi sana lakini hilo halitawasaidia wala kuwafaa maana mwisho wao utafika kama ilivyo ada. Kwa upande wa kifo cha Mwangosi ni kweli inasikitisha kwa familia ya marehemu na kwa umma wa Watanzania wapenda haki lakini kifo chake ni sadaka ya ukombozi kwa wanyonge na walalahoi wa nchi hii.Tukumbuke waandishi wa habari ni askari wa kwenye uwanja wa mbele wa mapigano licha ya kutokuvaa sare(yaani SOLDIERS WITHOUT COMBAT UNIFORMS).Waandishi wa habari na mafanani ni wapiganaji wanaotumia KALAMU NA KARATASI kama BUNDUKI NA RISASI.Tukumbuke A PEN IS MIGHTIER THAN A SWORD.Na hao waliofanya mauaji pamoja na mwajiri wao wakumbuke ya kwamba HAKI YA MTU HAINYIMWI KABISA BALI INAWEZA KUCHELEWESHWA TU.Damu ya Mwangosi pamoja na wanaharakati wengine haijamwagika bure!Surely, they havent died in vain!
 
hili ni fundisho kwa wandishi wa habari kuacha unafiki na ubinafsi na kutete haki ya mtanzania,kwani kumetokea mauwaji mengi yanayo sababisha na polisi kama arusha,morogoro,mateso kama aliyopata ulimboka lkn wandishi wengi wahabari waliaza unafiki na kusambasa chuki dhidi ya dr na wananchi, kwasababu ya kujipendekeza kwa serikali.Kinachonichukiza ni kwa wandishi wa habari kuchukua hatu pale mwandishi mwenzao anapouliwa na wapendwa wao na wanafiki wenzao.simanishi wote bali wale wanafiki wa gazeti la uhuru na tbs tv na wengineo.
 
kutokana na tukio la mauaji mimi kama mtanzania nashauri waandishi wa habari kugomea kuandika habari za chama cha mapinduzi ambacho ndio kipo madarakani na kutoa tamko la adhabu kali kuchukuliwa kwa waandishi wowote watakaokiuka hili agizo...mwana JF embu na wewe washauri waandishi wa habari
 
hovyo kabisa baadhi ya waandishi na viongoz wao. wakisha Chukua Chao Mapema utasikia wakitoa BONGE la tamko kwamba tususie kuandika habari za wizara ya mambo ya ndani kwa mda wa wiki 1.
 
Uandishi wa habari una dhamana kubwa sana. Ndio maana ukapewa nguvu na kuitwa mhimili unaojitegemea.

Mtakumbuka miaka michache iliyopita, mchora katuni za magazeti, anayeishi kenya, aliwachora mkilamba viatu vya kigogo mmoja aliyeko madarakani hivi sasa. Alimaanisha, mlikuwa mkitumiwa, mkipuuza taaluma yenu na kununuliwa na wanasiasa. Mlipiga kelele sana na kulalamika, lakini kwa mtazamo wangu kwa kipindi kile Gado, alikuwa yuko sahihi.

Hayo yamepita, tujifunze sasa kutumia kalamu zetu kwa haki bila ya kupendelea watawala. Tukatae rushwa zao, posho, usafiri na vitu vidogo vidogo tunavyochukua. Tusijidalilishe. Tuheshimu taaluma yetu na tufanye kazi kwa haki.

Tukumbuke, hawa watawala watatupenda iwapo tutaendelea kulamba viatu vyao, tukikataa, wananakimbilia kutumaliza, lakini mkiutendea haki umma, siku zote utasimama upande wenu!

Kifo cha Mwangosi kiturudishe katika mstari.
 
Mbona unapepesa macho na kumumunya maneno walionyeshwa kwenye ile katuni wakilamba viatu vya dakt jakaya kikwete
 
Uandishi wa habari una dhamana kubwa sana. Ndio maana ukapewa nguvu na kuitwa mhimili unaojitegemea.

Mtakumbuka miaka michache iliyopita, mchora katuni za magazeti, anayeishi kenya, aliwachora mkilamba viatu vya kigogo mmoja aliyeko madarakani hivi sasa. Alimaanisha, mlikuwa mkitumiwa, mkipuuza taaluma yenu na kununuliwa na wanasiasa. Mlipiga kelele sana na kulalamika, lakini kwa mtazamo wangu kwa kipindi kile Gado, alikuwa yuko sahihi.

Hayo yamepita, tujifunze sasa kutumia kalamu zetu kwa haki bila ya kupendelea watawala. Tukatae rushwa zao, posho, usafiri na vitu vidogo vidogo tunavyochukua. Tusijidalilishe. Tuheshimu taaluma yetu na tufanye kazi kwa haki.

Tukumbuke, hawa watawala watatupenda iwapo tutaendelea kulamba viatu vyao, tukikataa, wananakimbilia kutumaliza, lakini mkiutendea haki umma, siku zote utasimama upande wenu!

Kifo cha Mwangosi kiturudishe katika mstari.
I always hate (nawachukia) waandishi wa habari. they always biased. ndo maana siku hizi hata gazeti sinunui tena kama zamani bora hapa kwenye mtandao angalao utapata habari za pande zote.
 
Uandishi wa habari una dhamana kubwa sana. Ndio maana ukapewa nguvu na kuitwa mhimili unaojitegemea.

Mtakumbuka miaka michache iliyopita, mchora katuni za magazeti, anayeishi kenya, aliwachora mkilamba viatu vya kigogo mmoja aliyeko madarakani hivi sasa. Alimaanisha, mlikuwa mkitumiwa, mkipuuza taaluma yenu na kununuliwa na wanasiasa. Mlipiga kelele sana na kulalamika, lakini kwa mtazamo wangu kwa kipindi kile Gado, alikuwa yuko sahihi.

Hayo yamepita, tujifunze sasa kutumia kalamu zetu kwa haki bila ya kupendelea watawala. Tukatae rushwa zao, posho, usafiri na vitu vidogo vidogo tunavyochukua. Tusijidalilishe. Tuheshimu taaluma yetu na tufanye kazi kwa haki.

Tukumbuke, hawa watawala watatupenda iwapo tutaendelea kulamba viatu vyao, tukikataa, wananakimbilia kutumaliza, lakini mkiutendea haki umma, siku zote utasimama upande wenu!

Kifo cha Mwangosi kiturudishe katika mstari.

Waandishi wa habari au wandishi wa habari za siasa? mbona hatusiki habari juu ya maendeleo yanayofanywa na serikali? Mbona hatusikii habari za matokeo ya tafiti mbalimbali zenye kulenga kuendeleza taifa letu? Mbona hatusikii habari za usalama wa taifa letu , badala yake tunaishia kuyasikia VOA, BBC na vyombo vingine vya nje?
 
Back
Top Bottom