Kaizer
Platinum Member
- Sep 16, 2008
- 25,320
- 17,822
Wakuu,,
Tukiendelea na hili libeneke la mahusiano ma mapenzi, kuna kitu kimenijia akilini, nacho ni:
Linapokuja suala la mavazi na muonekano wa mpenzi/mume wako, ungependa avaeje/aonekaneje mtokapo au hata muwapo nyumbani?
Tukiacha suala la mazingira na hali ya hewa pembeni, kuna wengine kwa mfano wangependa mtu anayepigilia viwalo vya kisasa, wengine wangependa mitindo ya zamani kama nywele za afro, visuruali vya 'chinjio' au wengine 'mabagi',
ukija kwen viatu, labda wengine wanapenda vya kileo, vilivyopo kwenye fasheni na vyenye majina (mf. kama raba za puma, nike, adidas -original sio hizi za 'kwa mtogole)
Kuna wengine wanapenda wapenzi wao wawe na vidani..kama cheni, kidani cha mkononi, au hata hereni kabisa,,
Sasa sijui kwa ujumla mnapenda mmwenzi wako aonekaneje..ukitilia maanani jamii na pia your own satisfaction.
hata sijui kama nimeeleweka lakini hivyo hivyo.
Tukiendelea na hili libeneke la mahusiano ma mapenzi, kuna kitu kimenijia akilini, nacho ni:
Linapokuja suala la mavazi na muonekano wa mpenzi/mume wako, ungependa avaeje/aonekaneje mtokapo au hata muwapo nyumbani?
Tukiacha suala la mazingira na hali ya hewa pembeni, kuna wengine kwa mfano wangependa mtu anayepigilia viwalo vya kisasa, wengine wangependa mitindo ya zamani kama nywele za afro, visuruali vya 'chinjio' au wengine 'mabagi',
ukija kwen viatu, labda wengine wanapenda vya kileo, vilivyopo kwenye fasheni na vyenye majina (mf. kama raba za puma, nike, adidas -original sio hizi za 'kwa mtogole)
Kuna wengine wanapenda wapenzi wao wawe na vidani..kama cheni, kidani cha mkononi, au hata hereni kabisa,,
Sasa sijui kwa ujumla mnapenda mmwenzi wako aonekaneje..ukitilia maanani jamii na pia your own satisfaction.
hata sijui kama nimeeleweka lakini hivyo hivyo.