PatriotMzalendo
Member
- Jan 17, 2011
- 28
- 6
Nimesoma maoni mengi sehemu tofauti tofauti kama kwenye mitandao na kwenye magazeti machache kwamba mtu wa propaganda wa CCM,Tambwe Hiza, ni mweupe kabisa kichwani. Nilikuwa sijaamini sana lakini leo nimeamini kwamba huyu bwana ni mweupe kuliko weupe wenyewe kichwani kutokana na maoni aliyojaribu kuyatoa kuhusu nini cha kuwemo kwenye katiba mpya.Huyu bwana ni mjinga kwa sababu:-
- anapinga hoja za kupunguzwa kwa mamlaka makubwa ya rais ya kuteua watendaji mbalimbali wa umma akidhani kuwa mamlaka hayo yanayoshauriwa yapunguzwe ni ya Jakaya Kikwete wa CCM wakati wenye akili wanapendekeza hivyo kwa kuzingatia yeyote anaweza kupenya penya hadi kupata urais hata mpumbavu fulani au katili fulani kama vipengele vingine vya katiba vitatoa mwanya wa kuwezesha hilo, endapo hatutakuwa makini kuandika katiba nzuri.Ikitokea hivyo, rais huyo atafanya uteuzi wa ukichaa kichaa kwa hasara ya taifa.
- anapinga hoja hiyo bila kujali uteuzi wa rais unarudisha nyuma maendeleo ya watu wa vyama vyote vya siasa kwani wateuliwa hao huwajibika kwa mteuzi na si kwa watu wakiwemo wana CCM.
- anapinga hoja hiyo bila kufahamu kwamba CCM haitakuwa madarakani milele na hivyo kuna siku rais atatoka upinzani.
- hana uwezo hata mdogo wa kusoma alama za nyakati kujua kuwa watanzania wa sasa wanataka mabadiliko na hawawezi kumvumilia mjinga yeyote anayejaribu kuturudisha nyuma.Angekuwa na uwezo huo asingetoa hoja ya kijinga na alipoanza kupewa kwa vitendo taarifa na watanzania wenzake kwamba alikuwa anaboa, angenyamaza mara moja badala ya kukomaa kijinga na kuadhirika vibaya.
- hajui kwamba maoni yaliyokuwa yanatolewa yalikuwa ya wananchi binafsi licha ya baadhi kuwa viongozi wa vyama vya siasa.Kwa ujinga wake yeye eti alikuwa akitoa maoni hayo kama mwakilishi wa CCM! CCM kama entity haipaswi kuwa na maoni mamoja kuhusu nini cha kuwemo kwenye katiba bali watu binafsi ndiyo wenye maoni binafsi hata kama baadhi ya maoni hayo yatavipendelea vyama wanavyoongoza,wanavyokuwa ndani yake au wanavyoshabikia.
- hajui kwa nini alizomewa! Angekuwa na akili kidogo tu asingeshanga kuzomewa sana na kutakiwa atoke kwa upupu aliokuwa akiongea