Kweli Pinda mtoto wa mkulima

Kapwani

JF-Expert Member
Nov 17, 2009
672
110
1542341.jpg


Pichani ni wazazi wa waziri mkuu Mizengo Pinda walipotembelewa na rais nyumbani kwao mpanda. Mimi nimeipenda nyie mnasemaje wakuu

Mix with yours
 
Umependa nini sasa? Nyumba ya wazazi wa Waziri Mkuu ilivyochoka?

Halafu katika nchi yenye watu 90% wakulima kuwa mtoto wa mkulima ni distinction gani? Ni kama vile unasema "Pinda ni mtoto wa Watanzania" what kind of distinction is that among Tanzanians? Kama anataka kutuambia yeye ni mtu wa kawaida na hana distinction then hawezi kuongoza, ataongozaje na yeye mtu wa kawaida tu asiye na distinction wala merit, distinction yake eti "mtoto wa wakulima" of all things.
 
Umependa nini sasa? Nyumba ya wazazi wa Waziri Mkuu ilivyochoka?

Halafu katika nchi yenye watu 90% wakulima kuwa mtoto wa mkulima ni distinction gani? Ni kama vile unasema "Pinda ni mtoto wa Watanzania" what kind of distinction is that among Tanzanians? Kama anataka kutuambia yeye ni mtu wa kawaida na hana distinction then hawezi kuongoza, ataongozaje na yeye mtu wa kawaida tu asiye na distinction wala merit, distinction yake eti "mtoto wa wakulima" of all things.

Asante mkuu kwa mchango wako! nadhani sikufafanua vema unisamehe sana...mie nimependa kuwa waziri mkuu ni mkweli alisema yeye ni mtoto wa mkulima na picha inaonyesha kweli mama yake ameshika kuku...kuku wa kienyeji ni zao la kawaida kwa mkulima wa tz
Kwamba nyumba imechoka sikuwaza hilo kwani nyumba hiyo ni nzuri sana niki ikompea na yetu ....ata ivyo sina maadili ya kubeza mali za watu...sijatoa chochote kuwasaidia kwa iyo wao kuwa na bangalow au nyumba gani nadhani hainihusu
Nilikuwa nimeoananisha maneno ya pinda na zawadi aliyoshika mama yake kumpa rais na si vinginevyo ...
Mix with yours
 
...alisema yeye ni mtoto wa mkulima na picha inaonyesha kweli mama yake ameshika kuku...kuku wa kienyeji ni zao la kawaida kwa mkulima wa tz

Kwa hiyo?

Na mimi nasema ukweli kwamba mimi ni mtoto wa mfanyakazi, nimesema ukweli, kwa hiyo? Nipewe kitumbua? Wakati Pinda anazaliwa nchi ilikuwa kwenye minyonyoro ya wakoloni, kuwa mtoto wa mkulima sio ajabu. Unaelewa? Kizazi cha Pinda hakukuwa na watoto wa matajiri!

Ulichokiona hapo kinaitwa fursa ya picha.

Kwenye siasa, fursa ya picha ni tabia ya kiongozi kujitegesha, kukaa mkao wa picha itakayomjengea taswira ya kupendeza. Mara nyingi hutumika kujionyesha unajali kitu ama watu fulani. Hapo juu Rais anasafisha taswira, ya Pinda wake, na serikali yake kwa ujumla, kujifanya watu wa watu. Anauza sura.

Sasa, Rais anatembea na wapiga picha wakati wote, na kila analofanya linaweza kupigwa picha laiti ni nje ya msalani. Unaweza kusema yeye hawezi kuepuka fursa za picha. Lakini wananchi wa jamii zilizopevuka kisiasa, picha yeyote ya Rais ya kuuza sura inachukiliwa kwa punje ya chumvi, kwa tahadhari, kwa sababu tunajua anaweza kuwa anatafuta ujiko, awe amejitegesha au hajajitegesha. Haziheshimiki.

Na kibaya zaidi Kikwete mwenyewe anazikosea hizo fursa za picha. Anaenda kwenye misiba ya wake wa matajiri na mabalozi wastaafu. Anapiga picha akimpa mtoto peremende lakini yuko ndani ya Shangingi la Rais, hashuki. Muafrika humrushii chakula kwa mbali. Anapiga picha akipokea kuku nyumbani kwao Waziri Mkuu.

Wazazi wa Waziri mkuu sio wakulima wa kawaida tena! Tanzania ndugu za viongozi wanahudumiwa kiholela holela, hata hawa usikute ni mimi ndio nawatunza na kodi yangu. Wake watatu wa Rais, sheria zinasema nini kuhusu huduma kwa wake wengi, hata haijulikani. Si ajabu hiyo nyumba ya kwao na Pinda inapata ma Land Cruiser ya kuku na mchele kila siku, ma Fuso ya ma Simtank ya maji kila siku, na ma Defender ya FFU.

Ni rahisi sana kuwa kiongozi Tanzania, Afrika. Eti bado fursa za picha zinachota watu.
 
Umependa nini sasa? Nyumba ya wazazi wa Waziri Mkuu ilivyochoka?

Halafu katika nchi yenye watu 90% wakulima kuwa mtoto wa mkulima ni distinction gani? Ni kama vile unasema "Pinda ni mtoto wa Watanzania" what kind of distinction is that among Tanzanians? Kama anataka kutuambia yeye ni mtu wa kawaida na hana distinction then hawezi kuongoza, ataongozaje na yeye mtu wa kawaida tu asiye na distinction wala merit, distinction yake eti "mtoto wa wakulima" of all things.

Thanks kamanda

ni yaleyale ya kumsifia simply kwasababu hajaiba sana hivyo nyumba yake ni chovu!!! kuwa mtoto wa kulima inakua abused these days wakati asilimia mia ya watanzania wana link ya moja-kwa-moja na wakulima

ni ufisadi tu ndio unasumbua

tuliulize sasa huko kuku kweli aliliwa na JK au ndio yale ya kuse pa mitego?
 
1542341.jpg


Pichani ni wazazi wa waziri mkuu Mizengo Pinda walipotembelewa na rais nyumbani kwao mpanda. Mimi nimeipenda nyie mnasemaje wakuu

Mix with yours

Wakati Mkuu wetu wa kaya anapokea zawadi ya kuku wa kienyeji, akina Al Gore wako bize maofisini kwa tija ya nchi yao...Halafu kesho tunakwenda kuomba misaada!

510227143_2196dccc00.jpg
 
Wakati Mkuu wetu wa kaya anapokea zawadi ya kuku wa kienyeji, akina Al Gore wako bize maofisini kwa tija ya nchi yao...Halafu kesho tunakwenda kuomba misaada!

510227143_2196dccc00.jpg
Ni kweli kabisa Mkuu nakuunga mguu tutakuwa omba omba mpaka lini?ikiwa Mkuu wetu anatembela Wazazi wa Waziri mkuu je kweli huko offisini kwake nani atafanya kazi? Au ndio kumefungwa mpaka arudi mkuu wetu toka Ziara ya Mikowa?kazi kweli na bongo yetu WAFRIKA BWANA NDIVYO WALIVYO EHHH
 
Nadhani inafaa tuwe na viongozi wa aina ya Pinda kwa maana ya watu waliokulia maisha ya kawaida (wanaozitambua kwa undani changamoto anazopambana nazo mtanzania wa kawaida) lakini waadilifu wanaotaka kuitoa nchi hii kutoka kwenye umasikini kwa kutumia rasilimali zetu vizuri, siyo kwenda tunajipendekeza na kujidhalilisha kwa wazungu kuomba misaada.
Mpaka pale tutakapoacha kulaumu vita vya ukombozi wa Afrika kwa umasikini wetu, ukosefu wa pesa za kuwasaidia watu wetu, na visingizio vingine tunavyo-manufacture ili mradi ku-justify umasikini wetu ndipo tutaondokana na umasikini.
Binafsi sioni umhimu wa rais wetu kuwa kila sehemu kila siku akihudhulia uzinduzi wa maabara (tuliyojengewa kwa msaada), akipokea zawadi ya kuku (sijui ya kufuga?) akihudhulia matamasha ya mziki na akina Boys II Men, akirandaranda huku na kule kututafutia misaada. Halafu kesho yake anatudanganya kuwa ahadi zote alizotoa wakati akiomba kura 2005 zitatekelezwa na kuwa ndani ya miaka miwili kila mwalimu wa Tanzania atakuwa na laptop, wakati hata mshahara wake tumeshindwa kuuongeza ili awe motivated zaidi.... no priority, no direction, no brains, no nothing, just smiles and empty words. Hatutaki!
 
nadhani message yako hujaiweka vizuri hivyo ujumbe wako haujatufikia vizuri, lakini kuna maana sana kubwa sana kwa viongozi wa sasa wa Tanzania na familia zao zinavyohishi, ukilinganisha na hiyo picha
 
nadhani message yako hujaiweka vizuri hivyo ujumbe wako haujatufikia vizuri, lakini kuna maana sana kubwa sana kwa viongozi wa sasa wa Tanzania na familia zao zinavyohishi, ukilinganisha na hiyo picha

Asante mkuu kama umenielewa kidogo hebu nisaidie kufanunua vema kwa wana jf ...will be helpful
Mix with yours
 
Hata mi nimekubali Waziri Mkuu wetu kweli ni Mkulima namuunga mkono kwani tuko wengi hata mi najivunia hilo kwa wazazi wangu ni wakulima wakubwa tangu kitambo sana
 
Ni kweli kabisa Mkuu nakuunga mguu tutakuwa omba omba mpaka lini?ikiwa Mkuu wetu anatembela Wazazi wa Waziri mkuu je kweli huko offisini kwake nani atafanya kazi? Au ndio kumefungwa mpaka arudi mkuu wetu toka Ziara ya Mikowa?kazi kweli na bongo yetu WAFRIKA BWANA NDIVYO WALIVYO EHHH

Rais wetu anakazi nyingi sana ofisini kwake lakini kila leo yeye ni kiguu na njia; mifano mchache tu inatosha kudhihilisha haya niandikayo, hivi sasa kuna mashirika na taasisi nyingi ambazo hazina bodi wala wenyeviti na yeye ndiye mwenye mamlaka ya kuteua wenyeviti na mawaziri ngwe yao ni kuteua wajumbe lakini mpaka hivi sasa mashirika kama TCAA na Air Tanzania hayana bodi; kwahiyo yanaendeshwa kiholele!! Anangojea mpaka baada ya uchaguzi awape zawadi wapambe wake, kweli nchi hii kazi tunayo.
 
Umependa nini sasa? Nyumba ya wazazi wa Waziri Mkuu ilivyochoka?

Halafu katika nchi yenye watu 90% wakulima kuwa mtoto wa mkulima ni distinction gani? Ni kama vile unasema "Pinda ni mtoto wa Watanzania" what kind of distinction is that among Tanzanians? Kama anataka kutuambia yeye ni mtu wa kawaida na hana distinction then hawezi kuongoza, ataongozaje na yeye mtu wa kawaida tu asiye na distinction wala merit, distinction yake eti "mtoto wa wakulima" of all things.
Yeye ni mtoto wa mkulima, mimi ni mkulima mwenyewe
 

Kwa hiyo?

Na mimi nasema ukweli kwamba mimi ni Mtanzania, kwa hiyo? Nipewe kitumbua? Wakati kina wanazaliwa nchi ilikuwa kwenye minyonyoro ya wakoloni, kuwa mtoto wa mkulima sio ajabu. Unaelewa? Kizazi cha Pinda hakukuwa na watoto wa matajiri!

Ulichokiona hapo kinaitwa fursa ya picha.

Kwenye siasa fursa ya picha ni tabia ya kiongozi kujitegesha, kukaa mkao wa picha itakayomjengea taswira ya kupendeza. Mara nyingi hutumika kujionyesha unajali kitu ama watu fulani. Hapo juu Rais anasafisha taswira, ya Pinda wake, na serikali yake kwa ujumla, kujifanya watu wa watu. Anauza sura.

Sasa, Rais anatembea na wapiga picha wakati wote, na kila analofanya linaweza kupigwa picha laiti ni nje ya msalani. Unaweza kusema yeye hawezi kuepuka fursa za picha. Lakini wananchi wa jamii zilizopevuka kisiasa, picha yeyote ya Rais ya kuuza sura inachukiliwa kwa punje ya chumvi, kwa tahadhari, kwa sababu tunajua anaweza kuwa anatafuta ujiko, awe amejitegesha au hajajitegesha. Haziheshimiki.

Na kibaya zaidi Kikwete mwenyewe anazikosea hizo fursa za picha. Anaenda kwenye misiba ya wake wa matajiri na mabalozi wastaafu. Anapiga picha akimpa mtoto peremende lakini yuko ndani ya Shangingi la Rais, hashuki. Muafrika humrushii chakula kwa mbali. Anapiga picha akipokea kuku nyumbani kwao Waziri Mkuu.

Wazazi wa Waziri mkuu sio wakulima wa kawaida tena! Tanzania ndugu za viongozi wanahudumiwa kiholela holela, hata hawa usikute ni mimi ndio nawatunza na kodi yangu. Wake watatu wa Rais, sheria zinasema nini kuhusu huduma kwa wake wengi, hata haijulikani. Si ajabu hiyo nyumba ya kwao na Pinda inapata ma Land Cruiser ya kuku na mchele kila siku, ma Fuso ya ma Simtank ya maji kila siku, na ma Defender ya FFU.

Ni rahisi sana kuwa kiongozi Tanzania, Afrika. Eti bado fursa za picha zinachota watu.
Mkuu nimecheka sana. Kama ulishaishi karibu na nyumba za hawa waheshimiwa utakubaliana na maneno red, Nakumbuka jirani yangu alikuwa wa kwanza kuletewa misamaki ile mikubwa na mboga mboga toka kwa wakulima wafungwa kwenye magereza.

Hiyo nyumba huenda ni banda la nguruwe na kuku tu, Nyumba ya Pinda na wazazi wake ipo mfukoni mwa Pinda, Any time atakayo feel kuitoa mfukoni ndio mtaitambua vizuri. Hizi picha ni za kusafishana safishana machoni mwa watanzania. Hatukatai utendaji wake lakini pia hatukubali kumwagiwa changa la macho.
 
Thanks kamanda

ni yaleyale ya kumsifia simply kwasababu hajaiba sana hivyo nyumba yake ni chovu!!! kuwa mtoto wa kulima inakua abused these days wakati asilimia mia ya watanzania wana link ya moja-kwa-moja na wakulima

ni ufisadi tu ndio unasumbua

tuliulize sasa huko kuku kweli aliliwa na JK au ndio yale ya kuse pa mitego?

Hawezi kumla huyo kuku kabla wataalam hawajampigia kisomo !!
 
Back
Top Bottom