NONGWA
Senior Member
- Mar 10, 2012
- 142
- 116
Wana jf,naombeni ushauri nina miaka mitatu katika mapenzi na huyu binti lakini hapo jana kuna njemba imenipigia simu na kusema kuwa imekuta meseji kwenye simu ya mpenzi wake ambaye ndiye mpenzi wangu mimi kwamba namwandikia meseji za mapenzi huyo binti,nilivuta pumzi na kumsikiliza vizuri,nikamuuliza wameanza lini uhusiano njemba ikaniambia wameanza mwaka jana mwezi wa kwanza so wana almost mwaka mmoja.na hapo hapo mimi nina uhusiano nae wa miaka mitatu.akanieleza habali zote za kuhusu huyo mpenzi wangu hadi lini ame kuwa nae na mda ambao mara ya mwisho amekuja kwangu kwa kumwambia huyo njemba eti anaenda kusalimia kaka ake amekuja toka mkoa.kumbe yupo kwangu.sasa nikamwambia huyo njemba kwamba yeye ndo ameingilia mapenzi yangu na huyo binti yeye mwaka mmoja mi mitatu,kweli sikuamini kama kweli huyu binti anaweza akanifanyia hivyo ilibidi nianze kuhusisha na matukio ya nyuma nikaona kweli kuna utofauti ya kwamba amekuwa aki nicheat.naombeni ushauri hapa nifanye nini na binti nampenda..