Maarifa
JF-Expert Member
- Nov 23, 2006
- 4,568
- 2,911
Samahania sana kama mtakuwa tayari mmeanza kuichangia article hiyo niliyodesa kutoka IPPMEDIA. Baada ya kuisoma hadi mwisho nilibakia na maswali mengi yasiyo na majibu. Ingawa mahitimisho yangu ni kuwa sasa si ufisadi tu bali sasa nchi imeoza kwa maana all systems zimekufa.
Kashfa ya mwaka Baraza la Mitihani
2008-10-27 13:57:26
Na Waandishi Wetu
Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA), limesambaza vyeti bandia vya matokeo ya kidato cha nne mwaka jana, (result slip) katika shule mbalimbali za sekondari nchini.
Wanafunzi walioathirika na hatua hiyo, ni wale waliohitimu kidato cha nne mwaka jana, na baadhi yao wameanza kupata misukosuko, ikiwemo kufikishwa mahakamani kwa madai ya kughushi.
Akizungumza na Nipashe nyumbani kwake Magomeni, mmoja wa wazazi wa wanafunzi hao, Rehema Mlata, alisema mtoto wake, Alexander Gundula (22), hivi sasa yupo mahabusu mjini Mbeya, kwa kosa lililofanywa na NECTA, kusambaza vyeti hivyo.
Alexander alikuwa miongoni mwa askari wanafunzi katika Chuo cha Magereza Kiwira, mkoani Mbeya.
Mlata, alisema Alexander alisoma na kuhitimu katika Shule ya Sekondari Azania, mkoani Dar es Salaam kati ya mwaka 2004 hadi 2007.
Uongozi wa Azania, kupitia waraka wake wa Oktoba 3, mwaka huu kwa Mkuu wa Mafunzo, Chuo cha Magereza Kiwira, umethibitisha mwanafunzi huyo kusoma katika shule hiyo.
Mlata alisema Alexander alichukua result slip shuleni hapo Februari mwaka huu, kwa ajili ya kujiunga na Magereza, na kwamba alifanikiwa kuanza mafunzo chuoni hapo.
Alisema Septemba mwaka huu, Alexander alikamatwa mjini Mbeya na kufikishwa mahakamani, akidaiwa kughushi result slip yenye namba S0101/0032, aliyopewa na uongozi wa Azania.
Ilidaiwa kuwa hatua hiyo ilifikiwa baada ya Magereza kuthibitishiwa na NECTA, kuwa cheti hicho kilikuwa na kasoro zilizokifanya kisifanane na vingine vilivyotolewa mwaka jana, hivyo kuamua kwamba kilikuwa cha kughushi.
Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Magereza, ilimwandikia barua Alexander, yenye namba HQC.58/X1/287, ikielezea kuachishwa mafunzo kutokana na kosa la kughushi cheti hicho, na hivyo kukosa sifa ya kuajiriwa.
Kufuatia uhakiki wa ajira uliofanywa na kamati ya uhakiki kutoka Makao Makuu ya Magereza kuanzia tarehe 31 Agosti mwaka 2008 hadi Septemba mwaka huu, imedhihirika kuwa cheti cha kufuzu masomo ni cha kughushi hivyo moja kwa moja unapoteza sifa za kuajiriwa kama askari Magereza, ilieleza sehemu ya barua hiyo iliyosainiwa na Kaimu Kamishna Mkuu wa Magereza, E.M. Nkuku.
Mlata alisema alikwenda kuonana na uongozi wa Magereza jijini Dar es Salaam, na kujibiwa kwamba uthibitisho kwamba cheti hicho kilikuwa cha kughushi, ulitolewa na NECTA.
Mzazi huyo alifanikiwa kupata nyaraka kadhaa zinazothibitisha kuwa result slip hiyo, ilitolewa katika Shule ya Sekondari Azania.
Kwa upande wake, uongozi wa Azania uliandika barua tofauti, ikiwemo namba AZ/BMT/19, kwenda NECTA, ikieleza kuwa Alexander ni mwanafunzi halali wa shule hiyo na result slip husika ilikuwa halali na ilitolewa shuleni hapo.
Lakini Magereza waliendelea na msimamo wao kwamba wamethibitishiwa na Baraza la Mitihani kuwa result slip hiyo ni feki, alisema.
Mlata alionyesha barua ya Baraza kwenda Magereza inayotaka Alexander achukuliwe hatua za kisheria, ili iwe fundisho kwa wengine wenye kawaida ya kughushi.
Hata hivyo, Mwalimu Mkuu Msaidizi wa Azania, Benard Ngoze, alilithibitishia gazeti hili kuwa Alexander alikuwa mwanafunzi halali wa shule hiyo, na kwamba result slip iliyotolewa shuleni hapo ilitoka NECTA na si ya kughushi.
Alisema vyeti hivyo vilipelekwa shuleni hapo na NECTA mwaka jana, na kwamba vijana wengi wanaokutwa navyo hivi sasa wanakamatwa na kufikishwa mahakamani.
``Zile result slip walileta wenywe Baraza kwa dispatch na tukazipokea, wanafunzi walikuwa wakija kila mtu kwa wakati wake, wanalipia Sh. 5,000 na kuchukua, sasa wanaziruka wakati zimetoka kwao?`` alihoji.
Alisema alishaandika barua mara kadhaa kwa uongozi wa Baraza la Mitihani na Magereza kuthibitisha kuwa result slip ya Alexander ilipatikana kihalali shuleni hapo, lakini inashangaza kuona bado wahusika wanaendelea kumtia msukosuko kijana huyo.
Baada ya kugundua kuwa ni kweli hizo result slip zimetoka kwao, Baraza walichukua nyingine 17 zilizobaki hapa shuleni na walisema wanaenda kuwashughulikia watu wa idara ya uchapaji, kwamba walihusika na udanganyifu huo, alisema.
Alisema inawezekana watu wa idara hiyo katika Baraza, waliuza result slips halisi na kisha kuchapisha za kughushi na kusambaza katika shule mbalimbali nchini.
Walipokuja hapa tuliwaambia watu wa Baraza kuwa wanastahili kushtakiwa kwa kutengeneza vyeti bandia hata sisi tumeanza kuogopa, kama taasisi nyeti kama hii inafanya vitu vya ajabu kama hivi nani tutakayewaamini, alihoji Mwalimu Ngoze.
Baraza hilo limekiri kutokea kosa hilo katika barua yake ya Oktoba 13, mwaka huu, ikiwa na kumbukumbu namba MTS.2/14/Vol.L.IV/65, ya kumwomba radhi Alexander kwa kosa lililofanyika.
Uchunguzi katika kumbukumbu za Baraza la Mitihani Tanzania umeonyesha kuwa result slip ya Alexander Gundula ni sahihi.
Tayari tumemwandikia Kamishna Mkuu wa Magereza kumjulisha kuhusu uhalali wa result slip hiyo ambayo pia imerudishwa kwake tunaomba radhi kwa usumbufu wowote uliojitokeza, ilisema barua hiyo iliyosainiwa na Kaputa kwa niaba ya Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Dk Joyce Ndalichako.
Ingawa Baraza hilo halikukiri moja kwa moja katika barua yake kuwa result slip hizo zilitolewa na Baraza hilo, maofisa wake waliokwenda shule ya Azania, walikiri kuwa zilitolewa na taasisi hiyo yenye jukumu la kuandaa mitihani nchini.
Msemaji wa Magereza, Omari Mtiga, alisema uhakiki wa vyeti vya askari wanafunzi, ni mchakato wa kawaida unaofanywa na jeshi hilo.
Mtiga aliyeahidi kulifutilia suala hilo kwa undani, alisema utaalamu wa kubaini ikiwa vyeti vilivyowasilishwa na wanafunzi ni sahihi ama vimeghushiwa, unafanywa na NECTA.
Wakituambia kwamba cheti fulani kimeghushiwa, sisi tunaamini hivyo na hatua inayofuata ni kumfikisha mhusika katika vyombo vya sheria, alisema.
Hata hivyo, Mtiga alionyesha kushangazwa na tukio hilo alilolifananisha na mchezo wa kuigiza, na kusema taarifa zaidi itatolewa leo.
``Njoo Jumatatu, mimi nitakuwa nimesafiri, lakini taarifa zaidi utazipata kwa huyu Kaziulaya, ni mmoja wa wasaidizi wangu,`` alisema.
Kwa upande wake, Dk. Ndalichako hakuwa tayari kulizungumzia suala hilo, kwa madai kuwa halijui.
``Kuna maamuzi yanayofikiwa na wasaidizi wangu, naomba tuwasiliane kesho, nitakuwa nimelifuatilia na kukupa jibu, nipigie simu kabla hujaja ofisini kwangu,`` alisema.
Hata hivyo, Nipashe ilipowasiliana naye kwa mujibu wa ahadi yake, Dk. Ndalichako alidai yupo kwenye mkutano, na baadaye alipopigiwa mara kadhaa, simu yake ya mkononi ilikuwa inaita bila kupokewa.
Taarifa nyingine zilizopatikana hivi punde, zilidai kuwa, Magereza imeagiza Alexander kuripoti chuoni hapo na kuendelea na mafunzo, baada ya barua ya NECTA kuthibitisha kuwa result slip aliyonayo imetolewa na Baraza hilo.
Imeandaliwa na Mashaka Mgeta na Joseph Mwendapole
SOURCE: Nipashe
Je mpaka leo hii Huyu Dr Ndalichako bado anapata pay slip?
Je mpaka leo hii hakuna aliyefikishwa mahamani?
Huyu maskini kijana anaombwa radhi na kuambiwa arudi mafunzoni je hiyo tu inatosha? to what extent damage waliofanya katika maisha ya huyu kijana. NO ACCOUNTABILITY NOR RESPONSIBILITY JE TUTAFIKA JAMANI?
Kashfa ya mwaka Baraza la Mitihani
2008-10-27 13:57:26
Na Waandishi Wetu
Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA), limesambaza vyeti bandia vya matokeo ya kidato cha nne mwaka jana, (result slip) katika shule mbalimbali za sekondari nchini.
Wanafunzi walioathirika na hatua hiyo, ni wale waliohitimu kidato cha nne mwaka jana, na baadhi yao wameanza kupata misukosuko, ikiwemo kufikishwa mahakamani kwa madai ya kughushi.
Akizungumza na Nipashe nyumbani kwake Magomeni, mmoja wa wazazi wa wanafunzi hao, Rehema Mlata, alisema mtoto wake, Alexander Gundula (22), hivi sasa yupo mahabusu mjini Mbeya, kwa kosa lililofanywa na NECTA, kusambaza vyeti hivyo.
Alexander alikuwa miongoni mwa askari wanafunzi katika Chuo cha Magereza Kiwira, mkoani Mbeya.
Mlata, alisema Alexander alisoma na kuhitimu katika Shule ya Sekondari Azania, mkoani Dar es Salaam kati ya mwaka 2004 hadi 2007.
Uongozi wa Azania, kupitia waraka wake wa Oktoba 3, mwaka huu kwa Mkuu wa Mafunzo, Chuo cha Magereza Kiwira, umethibitisha mwanafunzi huyo kusoma katika shule hiyo.
Mlata alisema Alexander alichukua result slip shuleni hapo Februari mwaka huu, kwa ajili ya kujiunga na Magereza, na kwamba alifanikiwa kuanza mafunzo chuoni hapo.
Alisema Septemba mwaka huu, Alexander alikamatwa mjini Mbeya na kufikishwa mahakamani, akidaiwa kughushi result slip yenye namba S0101/0032, aliyopewa na uongozi wa Azania.
Ilidaiwa kuwa hatua hiyo ilifikiwa baada ya Magereza kuthibitishiwa na NECTA, kuwa cheti hicho kilikuwa na kasoro zilizokifanya kisifanane na vingine vilivyotolewa mwaka jana, hivyo kuamua kwamba kilikuwa cha kughushi.
Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Magereza, ilimwandikia barua Alexander, yenye namba HQC.58/X1/287, ikielezea kuachishwa mafunzo kutokana na kosa la kughushi cheti hicho, na hivyo kukosa sifa ya kuajiriwa.
Kufuatia uhakiki wa ajira uliofanywa na kamati ya uhakiki kutoka Makao Makuu ya Magereza kuanzia tarehe 31 Agosti mwaka 2008 hadi Septemba mwaka huu, imedhihirika kuwa cheti cha kufuzu masomo ni cha kughushi hivyo moja kwa moja unapoteza sifa za kuajiriwa kama askari Magereza, ilieleza sehemu ya barua hiyo iliyosainiwa na Kaimu Kamishna Mkuu wa Magereza, E.M. Nkuku.
Mlata alisema alikwenda kuonana na uongozi wa Magereza jijini Dar es Salaam, na kujibiwa kwamba uthibitisho kwamba cheti hicho kilikuwa cha kughushi, ulitolewa na NECTA.
Mzazi huyo alifanikiwa kupata nyaraka kadhaa zinazothibitisha kuwa result slip hiyo, ilitolewa katika Shule ya Sekondari Azania.
Kwa upande wake, uongozi wa Azania uliandika barua tofauti, ikiwemo namba AZ/BMT/19, kwenda NECTA, ikieleza kuwa Alexander ni mwanafunzi halali wa shule hiyo na result slip husika ilikuwa halali na ilitolewa shuleni hapo.
Lakini Magereza waliendelea na msimamo wao kwamba wamethibitishiwa na Baraza la Mitihani kuwa result slip hiyo ni feki, alisema.
Mlata alionyesha barua ya Baraza kwenda Magereza inayotaka Alexander achukuliwe hatua za kisheria, ili iwe fundisho kwa wengine wenye kawaida ya kughushi.
Hata hivyo, Mwalimu Mkuu Msaidizi wa Azania, Benard Ngoze, alilithibitishia gazeti hili kuwa Alexander alikuwa mwanafunzi halali wa shule hiyo, na kwamba result slip iliyotolewa shuleni hapo ilitoka NECTA na si ya kughushi.
Alisema vyeti hivyo vilipelekwa shuleni hapo na NECTA mwaka jana, na kwamba vijana wengi wanaokutwa navyo hivi sasa wanakamatwa na kufikishwa mahakamani.
``Zile result slip walileta wenywe Baraza kwa dispatch na tukazipokea, wanafunzi walikuwa wakija kila mtu kwa wakati wake, wanalipia Sh. 5,000 na kuchukua, sasa wanaziruka wakati zimetoka kwao?`` alihoji.
Alisema alishaandika barua mara kadhaa kwa uongozi wa Baraza la Mitihani na Magereza kuthibitisha kuwa result slip ya Alexander ilipatikana kihalali shuleni hapo, lakini inashangaza kuona bado wahusika wanaendelea kumtia msukosuko kijana huyo.
Baada ya kugundua kuwa ni kweli hizo result slip zimetoka kwao, Baraza walichukua nyingine 17 zilizobaki hapa shuleni na walisema wanaenda kuwashughulikia watu wa idara ya uchapaji, kwamba walihusika na udanganyifu huo, alisema.
Alisema inawezekana watu wa idara hiyo katika Baraza, waliuza result slips halisi na kisha kuchapisha za kughushi na kusambaza katika shule mbalimbali nchini.
Walipokuja hapa tuliwaambia watu wa Baraza kuwa wanastahili kushtakiwa kwa kutengeneza vyeti bandia hata sisi tumeanza kuogopa, kama taasisi nyeti kama hii inafanya vitu vya ajabu kama hivi nani tutakayewaamini, alihoji Mwalimu Ngoze.
Baraza hilo limekiri kutokea kosa hilo katika barua yake ya Oktoba 13, mwaka huu, ikiwa na kumbukumbu namba MTS.2/14/Vol.L.IV/65, ya kumwomba radhi Alexander kwa kosa lililofanyika.
Uchunguzi katika kumbukumbu za Baraza la Mitihani Tanzania umeonyesha kuwa result slip ya Alexander Gundula ni sahihi.
Tayari tumemwandikia Kamishna Mkuu wa Magereza kumjulisha kuhusu uhalali wa result slip hiyo ambayo pia imerudishwa kwake tunaomba radhi kwa usumbufu wowote uliojitokeza, ilisema barua hiyo iliyosainiwa na Kaputa kwa niaba ya Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Dk Joyce Ndalichako.
Ingawa Baraza hilo halikukiri moja kwa moja katika barua yake kuwa result slip hizo zilitolewa na Baraza hilo, maofisa wake waliokwenda shule ya Azania, walikiri kuwa zilitolewa na taasisi hiyo yenye jukumu la kuandaa mitihani nchini.
Msemaji wa Magereza, Omari Mtiga, alisema uhakiki wa vyeti vya askari wanafunzi, ni mchakato wa kawaida unaofanywa na jeshi hilo.
Mtiga aliyeahidi kulifutilia suala hilo kwa undani, alisema utaalamu wa kubaini ikiwa vyeti vilivyowasilishwa na wanafunzi ni sahihi ama vimeghushiwa, unafanywa na NECTA.
Wakituambia kwamba cheti fulani kimeghushiwa, sisi tunaamini hivyo na hatua inayofuata ni kumfikisha mhusika katika vyombo vya sheria, alisema.
Hata hivyo, Mtiga alionyesha kushangazwa na tukio hilo alilolifananisha na mchezo wa kuigiza, na kusema taarifa zaidi itatolewa leo.
``Njoo Jumatatu, mimi nitakuwa nimesafiri, lakini taarifa zaidi utazipata kwa huyu Kaziulaya, ni mmoja wa wasaidizi wangu,`` alisema.
Kwa upande wake, Dk. Ndalichako hakuwa tayari kulizungumzia suala hilo, kwa madai kuwa halijui.
``Kuna maamuzi yanayofikiwa na wasaidizi wangu, naomba tuwasiliane kesho, nitakuwa nimelifuatilia na kukupa jibu, nipigie simu kabla hujaja ofisini kwangu,`` alisema.
Hata hivyo, Nipashe ilipowasiliana naye kwa mujibu wa ahadi yake, Dk. Ndalichako alidai yupo kwenye mkutano, na baadaye alipopigiwa mara kadhaa, simu yake ya mkononi ilikuwa inaita bila kupokewa.
Taarifa nyingine zilizopatikana hivi punde, zilidai kuwa, Magereza imeagiza Alexander kuripoti chuoni hapo na kuendelea na mafunzo, baada ya barua ya NECTA kuthibitisha kuwa result slip aliyonayo imetolewa na Baraza hilo.
Imeandaliwa na Mashaka Mgeta na Joseph Mwendapole
SOURCE: Nipashe
Je mpaka leo hii Huyu Dr Ndalichako bado anapata pay slip?
Je mpaka leo hii hakuna aliyefikishwa mahamani?
Huyu maskini kijana anaombwa radhi na kuambiwa arudi mafunzoni je hiyo tu inatosha? to what extent damage waliofanya katika maisha ya huyu kijana. NO ACCOUNTABILITY NOR RESPONSIBILITY JE TUTAFIKA JAMANI?