MAGAMBA MATATU
JF-Expert Member
- Jul 2, 2011
- 646
- 1,174
MWENYEKITI Mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, ni mmoja wa wana ukoo wa Nyerere Burito.
Mkapa alipewa heshima hiyo mwanzoni mwa miaka ya 2000, baada ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Sherehe za kumtambua rasmi kama mwana ukoo zilifanyika nyumbani kwa marehemu Chifu Edward Wanzagi Nyerere, kijijini Butiama.
Juzi, Mkapa amesikika akimshambulia Mbunge wa Musoma Mjini, Vincent Nyerere (Chadema), wakati akizindua kampeni za CCM za Uchaguzi Mdogo Jimbo la Arumeru Mashariki. Mkapa akasema amefanya kazi na Mwalimu, amemzika, hajawahi kusikia Mwalimu Nyerere ana mtoto wake mwenye jina kama hilo. Akasema inawezekana huyo analitumia ajinufaishe kisiasa.
Baada ya kumsikia Mkapa kwa makini, nimeamua kuzungumza na Vincent Nyerere. Naye akaonyesha mshangao wake. Akajiuliza inakuwaje mwana ukoo mwenzake (Mkapa) amshambulie kwa sababu tu ya jina. Tena nikajiuliza, ilikuwaje siku ile alipokaribishwa rasmi kwenye ukoo, hakuhoji, mbona huyu Chifu anajitangaza kuwa mtoto wa Baba wa Taifa? Najua hakuhoji kwa sababu anajua kuwa Chifu Edward Wanzagi, baba yake ndiye huyo huyo baba yake Kambarage, yaani Nyerere.
Baada ya kutafakari, nimeona nijaribu kuweka sawa haya mambo. Kwanza nianze na ukoo huu wa Nyerere. Lakini haitakuwa vema kuuanza ukoo huu bila kumhusisha Mwalimu kwanza.
Kwa ufupi ni kwamba jina la Baba wa Taifa ni Julius Kambarage Nyerere. Jina Julius ni la ubatizo. Jina Kambarage ni la asili lenye maana ya mzimu wa mvua. Jina Mwalimu lilitokana na kazi yake ya ualimu. Kama walivyo walimu wengi, alipenda kuitwa Mwalimu badala ya Mheshimiwa au Dokta. Tena kwa wasiojua, jina la kwanza kabisa la Mwalimu Kambarage lilikuwa Mgendi, lenye maana ya mtembezi kwa lugha ya Kizanaki. Kwa nini wazazi wake waliliondoa jina hilo na kumpa jina la Kambarage, huo ni mjadala mwingine ambao nikiombwa nitauzungumzia.
Hivyo basi, mtiririko wa jina lake ni Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Burito Mazembe Wisigana Tandari. Hii ina maana kwamba Kambarage alizaliwa na Nyerere. Nyerere (Baba yake Mwalimu) alizaliwa na Burito. Burito alizaliwa na Mazembe. Mazembe alizaliwa na Tandari. Orodha ni ndefu.
Hadi hapo, utaona kuwa Nyerere si jina la Mwalimu. Bali jina lake ni Kambarage Nyerere, ikiwa na maana kwamba Nyerere ni ndiye baba yake mzazi. Ni kama leo kuna kina Mkapa wengi, hiyo haina maana kwamba wanaotumia jina hilo wanataka kujitanabahisha kuwa ni watoto wa Mkapa yule ambaye ni Rais Mstaafu. Unaweza kuuliza, iweje watoto wa Mwalimu waitwe majina kama Burito (Andrew) Nyerere, Anna (Watiku) Nyerere, Emil (Magige) Nyerere, Makongoro (Charles) Nyerere, John (Guido) Nyerere, Pauleta Nyerere, Madaraka (Godfrey) Nyerere au Rosemary Nyerere?
Matumizi ya jina Nyerere yamekuwa makubwa kwa sababu ni jina la ukoo. Ni jina kama yalivyo majina makubwa ya kina Mkwawa, Makongoro, na kadhalika. Hao watoto wa Mwalimu hawakutumia jina Nyerere kama jina la baba yao, bali ni la babu yao, yaani Nyerere Burito. Unaweza kusema Nyerere alikuwa maarufu, lakini aliyelipa umaarufu zaidi ni Mwalimu Kambarage.
Ni sahihi Makongoro akaitwa Makongoro Kambarage, Burito Kambarage, Madaraka Kambarage, Rosemary Kambarage, Magige Kambarage, Nyerere Kambarage, na kadhalika. Nadhani hadi hapo tupo pamoja.
Je, huyu Kambarage Nyerere hakuwa na ndugu wa tumbo moja? Alikuwa nao. Baadhi yao ni Nyangete Nyerere, Nyakahu Nyerere, Nyakigi Nyerere, Kizurira (Joseph) Nyerere na kitindamimba katika tumbo la Bibi Mgaya (Christina) Nyangombe (mama wa wote hawa) ni Kiboko (Josephat Nyerere). Kitindamimba huyu alifariki dunia miaka ya karibuni kabisa. Mkapa alihudhuria mazishi yake kijijini Butiama.
Huyu huyu, Josephat Kiboko Nyerere (kitindamimba katika tumbo la Bibi Mgaya), naye kapata watoto wengi. Hapa siwezi kuwaorodhesha wote. Lakini miongoni mwao ni VINCENT NYERERE KIBOKO NYERERE.
Wazanaki ni watu wanaoheshimu mila. Kurithishana majina ni moja ya mambo muhimu sana kwa Wazanaki. Ndiyo maana alipozaliwa huyu (mbunge), baba yake (yaani Kiboko Nyerere) aliamua kumpa jina la Nyerere akiwa amempa heshima hiyo baba yake mzazi, yaani Mtemi Nyerere Burito aliyefariki dunia mwaka 1942. Alikuwa Mtemi wa Butiama. Kama mbunge huyu angeamua kutumia majina ya Kizanaki, angeitwa Nyerere Kiboko Nyerere. Alipoamua kutumia majina ya ubatizo, akaweka jina Vincent na akaongeza la kwake la kuzaliwa la Nyerere; hivyo jina lake likawa Vincent Nyerere. Angeweza kuweka kando jina la ubatizo akatumia jina la Nyerere J.K. Nyerere (Nyerere Josephat Kiboko Nyerere). Alichoamua kufanya ni kutumia jina la ubatizo na jina la kuzaliwa linalobeba jina lake na la ukoo, yaani la babu yake.
Ni kwa sababu hiyo, mgeni yeyote anayefika Butiama anaweza kupigwa bumbuwazi kwa kusikia jina Nyerere likitamkwa kama salamu. Hiyo ni kwa sababu jina Nyerere ni la ukoo, na si la Mwalimu Kambarage. Mwalimu ni sehemu ya ukoo huo.
Lakini jina la Nyerere leo limefika mbali zaidi. Kuna waigizaji wanaitwa kina Steven Nyerere, kuna Nyerere wengi sana kila kona ya Tanzania. Afrika ina kina Nyerere wengi. Marekani ndo usiseme kabisa! Hii haina maana kwamba wanaoitwa Nyerere wanataka kujitafutia umaarufu kwa kutumia jina la Mwalimu au wanataka wajulikane kuwa wamezaliwa na Mwalimu Kambarage. Hapana.
Kwa ufafanuzi huu nadhani mwana ukoo Mkapa atakuwa ametambua kuwa huyu mbunge kuitwa Vincent Nyerere si kwa sababu ya kutaka kujikweza, bali hilo ndilo jina lake halisi. Endapo atajiita Vincent Kambarage Nyerere, hapo ndipo tunaweza kusema anataka kujitambulisha kama mtoto wa Mwalimu. Na ni kweli kwamba Mwalimu Kambarage ni baba yake mkubwa Vincent Nyerere. Hilo halina mjadala.
Tunamkaribisha mwana ukoo Mkapa akutane na sisi wazee ndani ya ukoo ili tupate kumpa somo. Akumbuke kuwa Mwalimu akiwa hai alimweleza kuwa ukoo wa Burito ni mkubwa. Huo unajumuisha familia za Chifu Wanzagi, Kambarage, Jackton, Wisigana, Muhunda, Nyamboga, Daniel, Kizurira, Nyakigi, Nyabisenye na nyingine nyingi. Kwetu sisi, Vincent Nyerere ni mwana ukoo na mjukuu halisi wa Nyerere Burito Mazembe Wisigana Tandari. Hajawahi, na hatawahi kujinasibu kama mtoto wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ingawa ukweli ni kwamba kiongozi huyo ni baba yake mkubwa. Wazazi wao wametoka kwa baba mmoja na tumbo moja la mama. Kama kuna kitu nimekisahau, basi mwana ukoo mwingine asaidie kukiweka wazi.
Mkapa alipewa heshima hiyo mwanzoni mwa miaka ya 2000, baada ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Sherehe za kumtambua rasmi kama mwana ukoo zilifanyika nyumbani kwa marehemu Chifu Edward Wanzagi Nyerere, kijijini Butiama.
Juzi, Mkapa amesikika akimshambulia Mbunge wa Musoma Mjini, Vincent Nyerere (Chadema), wakati akizindua kampeni za CCM za Uchaguzi Mdogo Jimbo la Arumeru Mashariki. Mkapa akasema amefanya kazi na Mwalimu, amemzika, hajawahi kusikia Mwalimu Nyerere ana mtoto wake mwenye jina kama hilo. Akasema inawezekana huyo analitumia ajinufaishe kisiasa.
Baada ya kumsikia Mkapa kwa makini, nimeamua kuzungumza na Vincent Nyerere. Naye akaonyesha mshangao wake. Akajiuliza inakuwaje mwana ukoo mwenzake (Mkapa) amshambulie kwa sababu tu ya jina. Tena nikajiuliza, ilikuwaje siku ile alipokaribishwa rasmi kwenye ukoo, hakuhoji, mbona huyu Chifu anajitangaza kuwa mtoto wa Baba wa Taifa? Najua hakuhoji kwa sababu anajua kuwa Chifu Edward Wanzagi, baba yake ndiye huyo huyo baba yake Kambarage, yaani Nyerere.
Baada ya kutafakari, nimeona nijaribu kuweka sawa haya mambo. Kwanza nianze na ukoo huu wa Nyerere. Lakini haitakuwa vema kuuanza ukoo huu bila kumhusisha Mwalimu kwanza.
Kwa ufupi ni kwamba jina la Baba wa Taifa ni Julius Kambarage Nyerere. Jina Julius ni la ubatizo. Jina Kambarage ni la asili lenye maana ya mzimu wa mvua. Jina Mwalimu lilitokana na kazi yake ya ualimu. Kama walivyo walimu wengi, alipenda kuitwa Mwalimu badala ya Mheshimiwa au Dokta. Tena kwa wasiojua, jina la kwanza kabisa la Mwalimu Kambarage lilikuwa Mgendi, lenye maana ya mtembezi kwa lugha ya Kizanaki. Kwa nini wazazi wake waliliondoa jina hilo na kumpa jina la Kambarage, huo ni mjadala mwingine ambao nikiombwa nitauzungumzia.
Hivyo basi, mtiririko wa jina lake ni Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Burito Mazembe Wisigana Tandari. Hii ina maana kwamba Kambarage alizaliwa na Nyerere. Nyerere (Baba yake Mwalimu) alizaliwa na Burito. Burito alizaliwa na Mazembe. Mazembe alizaliwa na Tandari. Orodha ni ndefu.
Hadi hapo, utaona kuwa Nyerere si jina la Mwalimu. Bali jina lake ni Kambarage Nyerere, ikiwa na maana kwamba Nyerere ni ndiye baba yake mzazi. Ni kama leo kuna kina Mkapa wengi, hiyo haina maana kwamba wanaotumia jina hilo wanataka kujitanabahisha kuwa ni watoto wa Mkapa yule ambaye ni Rais Mstaafu. Unaweza kuuliza, iweje watoto wa Mwalimu waitwe majina kama Burito (Andrew) Nyerere, Anna (Watiku) Nyerere, Emil (Magige) Nyerere, Makongoro (Charles) Nyerere, John (Guido) Nyerere, Pauleta Nyerere, Madaraka (Godfrey) Nyerere au Rosemary Nyerere?
Matumizi ya jina Nyerere yamekuwa makubwa kwa sababu ni jina la ukoo. Ni jina kama yalivyo majina makubwa ya kina Mkwawa, Makongoro, na kadhalika. Hao watoto wa Mwalimu hawakutumia jina Nyerere kama jina la baba yao, bali ni la babu yao, yaani Nyerere Burito. Unaweza kusema Nyerere alikuwa maarufu, lakini aliyelipa umaarufu zaidi ni Mwalimu Kambarage.
Ni sahihi Makongoro akaitwa Makongoro Kambarage, Burito Kambarage, Madaraka Kambarage, Rosemary Kambarage, Magige Kambarage, Nyerere Kambarage, na kadhalika. Nadhani hadi hapo tupo pamoja.
Je, huyu Kambarage Nyerere hakuwa na ndugu wa tumbo moja? Alikuwa nao. Baadhi yao ni Nyangete Nyerere, Nyakahu Nyerere, Nyakigi Nyerere, Kizurira (Joseph) Nyerere na kitindamimba katika tumbo la Bibi Mgaya (Christina) Nyangombe (mama wa wote hawa) ni Kiboko (Josephat Nyerere). Kitindamimba huyu alifariki dunia miaka ya karibuni kabisa. Mkapa alihudhuria mazishi yake kijijini Butiama.
Huyu huyu, Josephat Kiboko Nyerere (kitindamimba katika tumbo la Bibi Mgaya), naye kapata watoto wengi. Hapa siwezi kuwaorodhesha wote. Lakini miongoni mwao ni VINCENT NYERERE KIBOKO NYERERE.
Wazanaki ni watu wanaoheshimu mila. Kurithishana majina ni moja ya mambo muhimu sana kwa Wazanaki. Ndiyo maana alipozaliwa huyu (mbunge), baba yake (yaani Kiboko Nyerere) aliamua kumpa jina la Nyerere akiwa amempa heshima hiyo baba yake mzazi, yaani Mtemi Nyerere Burito aliyefariki dunia mwaka 1942. Alikuwa Mtemi wa Butiama. Kama mbunge huyu angeamua kutumia majina ya Kizanaki, angeitwa Nyerere Kiboko Nyerere. Alipoamua kutumia majina ya ubatizo, akaweka jina Vincent na akaongeza la kwake la kuzaliwa la Nyerere; hivyo jina lake likawa Vincent Nyerere. Angeweza kuweka kando jina la ubatizo akatumia jina la Nyerere J.K. Nyerere (Nyerere Josephat Kiboko Nyerere). Alichoamua kufanya ni kutumia jina la ubatizo na jina la kuzaliwa linalobeba jina lake na la ukoo, yaani la babu yake.
Ni kwa sababu hiyo, mgeni yeyote anayefika Butiama anaweza kupigwa bumbuwazi kwa kusikia jina Nyerere likitamkwa kama salamu. Hiyo ni kwa sababu jina Nyerere ni la ukoo, na si la Mwalimu Kambarage. Mwalimu ni sehemu ya ukoo huo.
Lakini jina la Nyerere leo limefika mbali zaidi. Kuna waigizaji wanaitwa kina Steven Nyerere, kuna Nyerere wengi sana kila kona ya Tanzania. Afrika ina kina Nyerere wengi. Marekani ndo usiseme kabisa! Hii haina maana kwamba wanaoitwa Nyerere wanataka kujitafutia umaarufu kwa kutumia jina la Mwalimu au wanataka wajulikane kuwa wamezaliwa na Mwalimu Kambarage. Hapana.
Kwa ufafanuzi huu nadhani mwana ukoo Mkapa atakuwa ametambua kuwa huyu mbunge kuitwa Vincent Nyerere si kwa sababu ya kutaka kujikweza, bali hilo ndilo jina lake halisi. Endapo atajiita Vincent Kambarage Nyerere, hapo ndipo tunaweza kusema anataka kujitambulisha kama mtoto wa Mwalimu. Na ni kweli kwamba Mwalimu Kambarage ni baba yake mkubwa Vincent Nyerere. Hilo halina mjadala.
Tunamkaribisha mwana ukoo Mkapa akutane na sisi wazee ndani ya ukoo ili tupate kumpa somo. Akumbuke kuwa Mwalimu akiwa hai alimweleza kuwa ukoo wa Burito ni mkubwa. Huo unajumuisha familia za Chifu Wanzagi, Kambarage, Jackton, Wisigana, Muhunda, Nyamboga, Daniel, Kizurira, Nyakigi, Nyabisenye na nyingine nyingi. Kwetu sisi, Vincent Nyerere ni mwana ukoo na mjukuu halisi wa Nyerere Burito Mazembe Wisigana Tandari. Hajawahi, na hatawahi kujinasibu kama mtoto wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ingawa ukweli ni kwamba kiongozi huyo ni baba yake mkubwa. Wazazi wao wametoka kwa baba mmoja na tumbo moja la mama. Kama kuna kitu nimekisahau, basi mwana ukoo mwingine asaidie kukiweka wazi.