Kweli mambo ni magumu! Serikali hoi! watu wake hoi!

Kasimba G

JF-Expert Member
Jan 19, 2011
3,428
2,609
Majibu nimeya pata kuwa kwa nini watu katika kipindi hichi cha Jakaya watu hela imepotea mifukoni lakini sasa majibu yako dhahili, pesa ziko mfukoni kwa mawaziri wetu na watendaji wengine mafisadi ndani ya serikali wakishirikiana na baadhi ya wafanya biashara mafisadi, na sijui wanazificha kwenye mifuko kama alivyo fanya Mh. Bingu wa Muthalika!

Mapato serikalini yameongezeka lakini ukata uko serikalini na kisingizio kikubwa ni inflation wakati mapato yameongezeka mala 3.75, mapato ya wakati wa mkapa ya average ya 160bli yaliweza kutosheleza matumizi serikalini na chenji kibao za matanuzi zilikuwepo na chenji kibao zilikuwa zinabaki, lakini sasa mapato ya maximum ya 600bil tunaambiwa ukata serikalini! watu hawaoni!

Kumbe majibu imeisha yapata, kuna genge kubwa la wezi ndio wanachukua hela na hawana huruma na nchi hii, na majibu mengine ni kwamba hata chaguzi zinakuwa na vioja kwa sababu hiyo hiyo, yaani genge la majambazi linafadhili chaguzi ili watu Fulani washinde ili Kundi lilindwe!

Nilikuwa najiuliza hivi hela za chama kuhonga chaguzini zinatoka wapi nimepata majibu, kumbe ni hela za miradi ya maendeleo hizohizo ndizo kanga, furana, kofia zinanunuliwa! Majambazi! Majamabzi kumbe ni haohao tunaowaona wengine ni viongozi! Mmmmh! Sasa Nundu kusema anapewa maelekezo! Mmmmh! Kumbe majibu sasa mwenye hekima kidogo ameishajua, Kumbe hata wakuu kabisa nao ni majambazi! MMMH!

Nawasilisha.
 
Back
Top Bottom