Da Pretty
JF-Expert Member
- Dec 9, 2010
- 3,059
- 1,148
Habari wapendwa.
Miaka 12 iliyopita nilikua A'level shule moja DSM.
Kuna binti nilikaa nae hostel. Hatukua tunapatana kabisa na kiukweli nilimpa wakati mgumu sana siku zile kwa sababu nilikua na nguvu kubwa ya kushawishi kuliko yeye, ikamlazimu kuhama pale akatafuta hostel ingine lakini darasani tulikua tunakutana. Tukamaliza shule hatuongei kabisa!
Baadae kila mtu akawa na mambo yake, tukasoma vyuo tofauti katika mikoa tofauti.
Mwenzangu wakati yupo Chuo akapata kazi kwenye NGO moja na baadaye akaajiriwa hapo.
Ninavyoandika hapa, ni kwamba nimemkuta yeye ni Senior na ni Line Manager wangu!!
Ni mwezi wa nne sasa nipo kazini lakini mazingira ni magumu.
Hatusalimiani,nimejaribu kujishusha wala hana mpango.
Mbaya zaidi kila siku nakumbushwa kuwa nipo kwenye probation na anamwambia mwenzangu kama sitaki kazi niseme.
Sielewi ni utumwa na manyanyaso tu,hapa natafuta kazi nyingine.
Miaka 12 iliyopita nilikua A'level shule moja DSM.
Kuna binti nilikaa nae hostel. Hatukua tunapatana kabisa na kiukweli nilimpa wakati mgumu sana siku zile kwa sababu nilikua na nguvu kubwa ya kushawishi kuliko yeye, ikamlazimu kuhama pale akatafuta hostel ingine lakini darasani tulikua tunakutana. Tukamaliza shule hatuongei kabisa!
Baadae kila mtu akawa na mambo yake, tukasoma vyuo tofauti katika mikoa tofauti.
Mwenzangu wakati yupo Chuo akapata kazi kwenye NGO moja na baadaye akaajiriwa hapo.
Ninavyoandika hapa, ni kwamba nimemkuta yeye ni Senior na ni Line Manager wangu!!
Ni mwezi wa nne sasa nipo kazini lakini mazingira ni magumu.
Hatusalimiani,nimejaribu kujishusha wala hana mpango.
Mbaya zaidi kila siku nakumbushwa kuwa nipo kwenye probation na anamwambia mwenzangu kama sitaki kazi niseme.
Sielewi ni utumwa na manyanyaso tu,hapa natafuta kazi nyingine.