VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Wakati naanza shule ya msingi,niliaminishwa na kuamini kuwa wanafunzi wanaosoma Shule za Serikali ndio wenye 'akili' kuliko wale wa shule za binafsi.Nikaendelea kuamini hivyo hata nilipoanza Sekondari hadi kumaliza kwangu.Nilijivuna kwakuwa tangu chekechea hadi Chuo Kikuu nimesoma Shule na Chuo Kikuu cha Serikali.
Wakati huo matokeo ya kidato cha nne au sita yakitoka,mchuano ulikuwa ni Mzumbe,Ilboru,Tabora Boys,Kilakala,Msalato,Kibaha,na shule nyinginezo za Serikali.Sasa mambo yamebadilika. Shule za binafsi(hasa za kidini) zinazifunika za Serikali.Tunaruhusiwa kusema kuwa sasa wanafunzi wenye 'akili' wako shule za binafsi? Tujadili...
Wakati huo matokeo ya kidato cha nne au sita yakitoka,mchuano ulikuwa ni Mzumbe,Ilboru,Tabora Boys,Kilakala,Msalato,Kibaha,na shule nyinginezo za Serikali.Sasa mambo yamebadilika. Shule za binafsi(hasa za kidini) zinazifunika za Serikali.Tunaruhusiwa kusema kuwa sasa wanafunzi wenye 'akili' wako shule za binafsi? Tujadili...