Kwanini Zambia Wameweza Kuuangusha ‘ mbuyu’ – Ivory Coast?

maggid

JF-Expert Member
Dec 3, 2006
1,084
1,246
Ndugu zangu,

Ukitaka kuukata na kuuangusha mbuyu usianze kufikiria unene wake. Jana usiku jirani zetu Zambia wameafanya maajabu ya soka. Vijana wa Chipolopolo wamatwaa ubingwa wa Afrika kwa kuwafunga Ivory Coast.

Ndio, Zambia jana wametufanya tujisikie, kuwa; " We are all Zambians". Kwamba sote ni Wazambia.


Siri ya ushindi wa Zambia?



Ni Uzambia. Ni utaifa. Ni uzalendo. Tuliwaona vijana wa Chipolopolo wanaojituma uwanjani. Vijana waliokuwa tayari kufia uwanjani, Vijana kama akina Kampamba, Mulenga, Sunzu, Nkausu, Chansa na wengineo.

Na katika maisha, ili mwanadamu afanikiwe unahitaji kuwa na ' K' tatu; Kujitambua, Kujiamini na Kuthubutu.

Vijana wa Chipolopolo wamejitambua. Wameijua historia yao. Wamejua walikotoka. Wamejua, kuwa kuna baba zao, mwaka 1993 walikuwa njiani kwenda Senegal kucheza mechi muhimu kufuzu kutafuta tiketi ya kucheza Kombe La Dunia. Usafiri ulikuwa mgumu. Walipanda ndege ya jeshi. Ndege ilianguka pwani ya Gabon, wachezaji wote 18 walipoteza maisha. Walikufa kwa ajili ya nchi yao.


Ndio maana jana, kwa kuitambua historia hiyo. Wazambia wale waliingia uwanjani wakiwa tayari kufia uwanjani kwa ajili ya nchi yao. Tulimwona beki Joseph Mussonda akiumia vibaya. Alijikaza kuendelea. Ikaonekana haiwezekani kabisa. Akatolewa nje. Alitokwa na machozi kwa muda mwingi. Si kwa maumivu ya mguu tu, ni kwa kuona uchungu wa kukosa kuwa uwanjani kuipigania nchi yake. Huo ni moyo mkubwa wa uzalendo. Wazambia wale hawakuwa wakifikiria posho zao, bali taifa lao. Na hakuna ahadi yoyote ya fedha waliyopewa kabla ya mechi ya jana.


Ndio, Wazambia wale walionyesha kujiamini sana. Walicheza mpira wao. Walikuwa focused muda wote. Hawakujali majina makubwa kama ya akina Drogba, Kolo Toure, Yahya Toure, Koite, Gervinjo, Gosso Gosso na mengineyo. Hawakujali kama walicheza na nyota wanaovichezea vilabu vikubwa huko Ulaya. Chipolopolo walicheza mchezo wao. Mwanzo hadi mwisho. Hata pale Ivory Coast walipokuwa wakijaribu kubadilisha mbinu na hata kubadilisha nafasi za wachezaji uwanjani, bado Zambia waliendelea kucheza mpira wao.

Kuna mengi ya kujifunza kutoka kwa jirani zetu wa Zambia. Nitaendelea na uchambuzi wangu…

Maggid Mjengwa,
Iringa.
Jumatatu, Februari 13, 2012
Mjengwa Blog::Habari,Picha,Matangazo
 
Misuse of space!! Do you think this has anything to do with "Jukwaa la Siasa" at all?? I dont feel Zambian just because they are champions. Would I call myself Ivorian if they won?? No, I would not!!!

Take your post to an appropriate place!!
 
Msaada wetu kwa wazambia huu hapa!!



Impressed Tanzanian gives Zambia national soccer team cash

February 8, 2012 | Filed under: Breaking News | Posted by: editor
A Tanzanian national and businessman based in Dar es Salaam, Azim Dewji, has donated 11 000 US Dollars purse money to the Zambia national soccer team following the teams impressive run at the on going Africa Cup of Nations in Gabon and Equatorial Guinea.
Mr. Dewji has also promised to donate 300 US Dollars to each of the widows of the national team players who perished in the Gabon air crash in 1993, if the Chipolopolo beat the Black Stars of Ghana in the semi-final encounter today.
Mr. Dewji who is proprietor of Simba Logistics Ltd and also financial sponsor of the Dar es Salaam outfit, Simba Football Club, says that being the only country from the Southern African region still at the tournament, Zambia has not only made Zambians proud but the entire region as a whole.
Mr. Dewji said that people in Tanzania are rallying behind the Zambia national team and hope that they go all the way and lift the cup.
Mr. Dewji is an ardent soccer fan and veteran administrator in Tazania. He was main sponsor of SIMBA Football Club from 1990 to 2000, Tanzania national soccer team fondly known as the Taifa Stars, manager from 1994 to 1998, former vice chairman of national team support committee from 2000 to 2005 and chairman of the support committe from 2006 to 2009.
And receiving the donation, FAZ vice president Borniface Mwamelo commended Mr. Dewji for the donation saying that it was gratifying especially that it was coming from a foreigner who wanted to indentifying himself with the Chipolopolo boys.
Mr. Mwamelo said that such a gesture is motivating to the players because it shows that their efforts are being recognised and appreciated. He also appealed to the corporate world and the general public to emulate Mr. Dewji and donate purse money to the players.
 
Majjid,
Umenena vema na umetoa mtazamo mzuri, ila thread umeiweka jukwaa la Siasa badala ya sehemu yake husika.
Ndio, yapo mengi sana ya kujifunza toka Zambia. Ni vigumu sana kwa Tanzania kupata mafanikio kama ya hao majirani zetu, kwani Siasa na ubabaishaji ndio vinavyotawala na kuendesha soka.
 
Ama kweli, wazambia wathubutu, wameweza na wanasongambele, Mungu ibariki Zambia, Mungu ibariki Afrika. Tanzania bado tuko kwenye michakato, na tayari raisi wa TFF ameshaunda task force na negotiation team mara tu baada ya mchakato huu nadhani tutashiriki world cup,ila mpaka huumchakato uishe, na tufanye upembuzi yakinifu, hapo tutakuwa fiti
 
Nasi Tujiandae kisayansi. Mpira hauchezwi kwa kaulimbiu za kisiasa. Baada ya ajali iliyopoteza maisha ya timu nzima ya taifa ya zambia,nchi hiyo ilianza kuwekeza , projection yao wakijua kabisa miaka hii ndio itakuwa mavuna,na kweli tumeona! Vyama vyetu vya michezo bado vinawababaishaji.wizarani wapo.tff napo mi sisemi ila maandalizi yao ya zimamoto wote twayaona. Sasa hawa wababaishaji wanapokuwepo kwenye mfumo huu mzima ndio kwa kiasi kikubwa wanakuwa kansa inayotafuna ari , uzalendo wa wachezaji na maendeleo ya michezo yetu kwa ujumla. Viongozi wasio na vision wasipewe nafasi, Wezi na wasio wazalendo tupa pembeni na mwisho tusilazimishe uzalendo utoke tu kwa wachezaji, uzalendo uanzie kwa viongozi wa ngazi zote na tafsiri yake tuipate mwishoni kwa wachezaji. Wachezaji wanaodhulumiwa stahili zao hawawezi kuwa na uzalendo hata kdogo.
 
through the triumph of Zambia i have come to the conclusion that for one to succeed he7she needs to be respector of principles and not be the respector of names.
 
Back
Top Bottom