Kwanini ya Tanganyika kuogopa Muungano kuvunjika ni hii.

Bangoo

JF-Expert Member
Nov 3, 2011
5,597
1,005
Sababu kubwa sana inatokana na makosa ya serikali ya awamu ya kwanza kukubali ikulu na ofisi nyingi za serikali kukaa dare es salaam. Kama makao makuu ya serikali yangekuwa dodoma sidhani kama tungenga'nga'nia muungano! Sababu ya kwanza viongozi wetu wakuu wanaishi kando kando ya bahari, uwanja wa ndege uko dar es salaam unategemea nini kiusalama?. Lakini kama makao makuu ya serikali yangekuwa dodoma kungekuwa hakuna uoga wowote kwani dar es salaam ingekuwa kama mombasa ambao ni mkoa tu wa kenya huku Nairobi ikiwa makao makuu ya serikali.

Lakini kwa ujinga wetu tumeifanya Dar es salaam kuwa makao makuu ya nchi sehemu ambayo ni hatari ki usalama. Leo ikitokea tumevamiwa na maadui viongozi wetu wako hatarini sana kama wataamua kupitia baharini kwani wataiteka Dar kwa kasi ya ajabu sana. Lakini kama makao makuu yangekuwa dodoma mpaka adui atoke Dar es salaam mpaka afike dodoma ni ngumu sana,lakini serikali yetu haitaki kuhama, pengine tungekuwa hatuna uoga kunga'nga'nia muungano!

Naiomba serikali hii isiyo sikivu ianze mkakati wa haraka wakuhamia Dodoma kwanza tuanze na ikulu! Ijengwe haraka Dodoma na Raisi aanze wa kwanza kuhamia huko, Dar uwe mji tu wa biashara.

Mwisho muungano udumu ila tuanze kuhama. Tuko kwenye hatari kubwa sana hata ikitokea kuvunjika tuwe salama . Hivi kama Kenya wangekuwa makao makao makuu yako Mombasa
wangekuwaje na hao al shaabab? Si wangekuwa hatarini sana? Tujifunze kutokana na kosa.

Wenu
mlala hoi
Rimoy.
Nawasilisha.
 
kwa hiyo we unaona bora serikali ihamie dodoma ili wakati wa uvamizi hapa dar hao wakubwa wawe salama wamefichwa huko dodoma...kwa hiyo sisi wakazi wa dar ndio tuvamiwe sio..kwani sisi hatuna thamani kama hao wakubwa watakaoishi dodoma... Muungano upo in theory that's all, practically hakuna kitu.
 
wanaogopa kwa sababu serikali yote inak
aa Dar salaam.
 
Sababu yako haina mashiko mkuu...lieleze jamvi kuwa Zanzibar inahusikaje katika usalama wa JMT
 
Sababu kubwa sana inatokana na makosa ya serikali ya awamu ya kwanza kukubali ikulu na ofisi nyingi za serikali kukaa dare es salaam. Kama makao makuu ya serikali yangekuwa dodoma sidhani kama tungenga'nga'nia muungano! Sababu ya kwanza viongozi wetu wakuu wanaishi kando kando ya bahari, uwanja wa ndege uko dar es salaam unategemea nini kiusalama?. Lakini kama makao makuu ya serikali yangekuwa dodoma kungekuwa hakuna uoga wowote kwani dar es salaam ingekuwa kama mombasa ambao ni mkoa tu wa kenya huku Nairobi ikiwa makao makuu ya serikali.

Lakini kwa ujinga wetu tumeifanya Dar es salaam kuwa makao makuu ya nchi sehemu ambayo ni hatari ki usalama. Leo ikitokea tumevamiwa na maadui viongozi wetu wako hatarini sana kama wataamua kupitia baharini kwani wataiteka Dar kwa kasi ya ajabu sana. Lakini kama makao makuu yangekuwa dodoma mpaka adui atoke Dar es salaam mpaka afike dodoma ni ngumu sana,lakini serikali yetu haitaki kuhama, pengine tungekuwa hatuna uoga kunga'nga'nia muungano!

Naiomba serikali hii isiyo sikivu ianze mkakati wa haraka wakuhamia Dodoma kwanza tuanze na ikulu! Ijengwe haraka Dodoma na Raisi aanze wa kwanza kuhamia huko, Dar uwe mji tu wa biashara.

Mwisho muungano udumu ila tuanze kuhama. Tuko kwenye hatari kubwa sana hata ikitokea kuvunjika tuwe salama . Hivi kama Kenya wangekuwa makao makao makuu yako Mombasa
wangekuwaje na hao al shaabab? Si wangekuwa hatarini sana? Tujifunze kutokana na kosa.

Wenu
mlala hoi
Rimoy.
Nawasilisha.

Hili nalo neno!
 
Huo usalma kwa wakati huu si usalama. Wenzetu ambao wameendelea wanaweza hata kusoma gazeti unalosoma ndani ya nyumba yako. Kuungana na Zanzibar hakuwezi kuwazuia kukushambulia wewe watapita na kufanya wanayotaka. Kumbuka mwaka ule Israel ilivyoenda kuokoa mateka wake kule Entebe, pamoja na rada wanajeshi waliokuwa zamu uwanjani hapo walitua wakawachukua raia wao kwa muda wa dakika 90! wakaondoka. Kwa msingi huo Zanzibar haituhakikishii usalama wowote.
 
Back
Top Bottom