Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,461
- 39,928
Kila kabila lina utamaduni na utaratibu wake kuhusiana na mahusiano ya wakwe. Kwa mfano, makabila mengine wakwe hawawezi kutamazana au hata kuwepo mahali pamoja. Makabila mengine kule kwenda kujitambulisha kwa wakwe tu ni kimbembe kwani kuna mchakato wa aina yake. Hata siku ya harusi au hata ndoa kuna mambo ambayo yanawahusu wakwe tu. Je, tunaweza kushirikishana mila na desturi za jamii zetu linapokuja suala la wakwe na ni kwanini kuna desturi hizi hasa?