Kwanini watu wanafunga NDOA!??

Iza

JF-Expert Member
Jan 8, 2009
2,026
611
Niko kwenye ndoa kama mwaka na nusu sasa na mwanamke ambaye tulikuwa kwenye uhusiano kwa muda wa zaidi ya miaka sita.Juzijuzi alipata ka-scholarship huko Ughaibuni ka muda wa muda mfupi.,tumepelekana airport kwa bashasha tele.
Mwanzoni mawasiliano yalikuwa mazuri japo siyo kwa nilivyotegemea..sikujali sana labda mazingira au masomo yalimbana..lakini kadri muda ulivyokwenda ndipo yalipozidi kupungua kwa kasi ya ajabu. Nilijitahidi kadri niwezavyo kuwa nawasiliana kwa njia zote naye lakini akawa kama vile namlazimisha kuwasiliana nami,nikajaribu kuongea naye majibu yake yakanifanya kwa mara ya kwanza tangu nifahamiane naye kutilia shaka mwenendo wake....Nikajipa moyo She can't do that...I was completely wrong..!

Akarudi toka masomoni,nikajihimu kwenda kumpokea japo mashaka fulani kuhusu mwenendo wake yalishaanza kutawala kichwa na moyo wangu kwahiyo sikuwa sana na furaha naye lakini pia sikuwa na ushahidi wa moja kwa moja kwamba hakuwa muaminifu kwa kipindi kile alichokuwa masomoni.Nikajikaza hivyohivyo tukasalimiana na bla bla bla kibao.

Next day akawa anataka kuwajulisha ndugu na jamaa kuwa kasharudi,akaniomba nimbadilishie line ya simu aliyokuwa akitumia huko ughaibuni na pia nimpunguzie salio, nikafanya kama alivyoniomba..Bahati mbaya au sijui nzuri sms ya kumuingizia salio ilivyoingia nikawa nimeingia inbox ili ni-edelete.Simu yake ni zile ambazo sms zote zinakuwa wazi kwa kiasi fulani hivyo u can see what has been written...I wish ningemtuma mtu amaletee credit..Those sms prove beyond reasonable doubt what I was feeling...She had an affair and to my surprise she told me that The relationship happened 'cause she wanted to...I felt like vomit up for the woman u give your life to confidently telling u that...,but that was part of the story..

Another day nikiwa natafuta notebook niandike vitu flani,nikawanimechukua Notebook yake maana ndio ilikuwa karibu sasa napekua nipate sehemu nzuri ya kuandika that's where the theme of this story lies..She was completely,madly begging for the LOVE of that man with her inbox full of his sms...I thought I was dreamin,I pinch myself to see If am awake or not BUT it was TRUE..SHE WAS CRYING & CONFESSING HER LOVE TO THAT MAN my foot..!

I feel dead inside kwakuwa sikutegemea haya mambo yatokee mapema kiasi hiki japo nilijua LABDA YANAWEZA kutokea lakini sio mapema kiasi hiki..But marriage people Expect Unexpected u neva know when it'll be knocking on ur door..!
Lakini nikajipa moyo tupo pamoja lakini najua sitakaa nimpende wala kumuamini tena jinsi nilivyokuwa nadhani akichoka anaweza kwenda..!

Now am back to that BIG question why do people get married?
 
Kwanza pole sana!
Ila upendo ndiyo unatupelekea kufanya haya kwakudhani ukifunga ndoa nikuonyesha upendo wako kwake maana tumekuwa tukisoma vitabu vya dini zetu natukiambiwa ili uonekane ujaenda nje ya matakwa ya mwenyezi mungu yakupasa kutimiza aliyotuelekeza tufanye ikiwa nipamoja kuoa kwa kwakufunga ndoa!!Na mwanamke hufurahi anapoona umefunga ndoa naye nderemo na chereko ametangazwa kwenye jumia ya watu wengi usikia raha ya hajabu ndiyo maana hilotendo ufanyika mara moja!lakini wanawake usahau kuwa ile tunu yakufunga naye ndoa nituzo kubwa kwani mwanamume anakuwa ameweka komitimenti na mwanamke hivyo walitakiwa kuzingatia hayo!!Naona sahau onyesha upendo kwake na mwambie makosa yake!!.........Ila nikirudi kwenye swali hamna maana yoyote ni kwasababu ya usikivu wa vitabu vya mungu!!
 
kwanza polee sana

pili jipe muda wa kuamua na kutafakari
usi rush kwenye maamuzi
 
Aisee pole sana Iza, je anaonesha kujutia alichokifanya? Kama hajutii; mimi sioni sababu ya kuendelea kuishi na mtu asiyekupenda. Badala ya kuendelea kupoteza muda ni bora muachane ili uje uanze upya!
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: Iza
Mapenzi kizungumkuti..
Ndoa ndoana..
Amua vile ambavyo ni sahihi kwako...
 
  • Thanks
Reactions: Iza
pole!ila mapenzi ni mchezo wa makosa,asipofanya yeye utafanya wewe mueleze ulishokiona na kama kweli shetani alimpitia ataomba msamaha na kuanza upya.hakuna aliyemkalifu kwenye huu mchezo ila TUNAVUMILIANA.
 
I have 1 billion reasons why i should NEVER get married. its better this way! hawa viumbe sio kabisa unampa moyo wako anakufanyia madudu kama haya, we bwana una moyo mgumu eti akichoka ataenda, yani mi nikishaconfirm amecheat hata mara moja yani hapo hakuna msamaha hata mababu wafufuke kumuombea msamaha.... ni kumtimua tu
 
Iza Bazazi ana hoja mbili tatu, hebu endelea:
  1. Bazazi ni Mkristo na Biblia inamuambia kuwa hakuna haki ya kuachana ila kwa sababu ya Uasherati.
  2. Kwavile Biblia anayoiamini imempa ruhusa hiyo angekuwa yeye angepiga chini fasta, lakini kwa kuwa Bazazi sio Iza basi usikilize moyo wako uamue haraka kabla hayajaharibika zaidi. Kama hakuna mtoto kwa uhakika piga chini fasta na ukirudi nyuma uwe kama mke wa Lutu.
  3. Watu wanaoa kwasababu nyingi lakini za muhimu ni UVIVU wa kutongoza na kupenda vya DEZO. Kwa sababu hizo Bazazi anakushauri njia nzuri ya mahusiano ni "HIT & RUN" ndio lugha wanayoielewa hawa viumbe wanaokojoa kwa kuchuchumaa na hivyo kushindwa kukojoa ktk vyoo vya kukokolea vya Nyamaume.
  4. Fikiri sana na nje ya mtazamo wako na amua kiume. Lakini kumbuka hapo nje kuna kitu kinakusubiri kinaitwa UKIMWI.


Naam Bazazi ni Bazazi!
 
Last edited by a moderator:
Inaonekana mkeo ana revenge!

Haiingii akilini akwambie black and white kuwa ni yeye amejigonga kwa huyo alo cheat nae. Tena atakuwa amefanya makusudi kuacha hizo meseji ili kuhakikisha unaziona.

Wewe hujawahi kumtenda kweli???
 
Ila watu mna uvumilivu aisee. Hivi mnaendelea ku do kama kawaida after all these???? Hata ningeombwa msamaha vipi na kujiridhisha kuwa was bahati mbaya...itachukua muda kweli kuwa turned on na mtu kama huyo. Labda anibake aisee.
 
Nilishajiambia moyoni mwangu,siku naoa nitafanya hivyo kwa sababu mimi nimeamua na sio kwa sababu nyingine yoyote ile!
 
  • Thanks
Reactions: Iza
Hakuna kitu kibaya kama mwenza wako kukuchukulia advantage... Hasa akijua uko powerless na kwamba wampenda sana sometimes to the extent kuwa huwezi fanya kitu hata pale tatizo linapotokea. Huyo ni wazi hakuthamini, na ni wazi yupo na wewe sababu kuna baadhi ya vitu ambavo anakidhi akiwa kwako.. Inaweza kuwa kitu kidogo but still anachukulia advantage.

Hakuheshimu [sababu angekuheshimu angejali kwa kufuta ushahidi wa upuuzi wote alikuwa anafanya]. Hebu jaribu kufikiria kweli hivi inawezekana una message za kimapenzi kwenye simu ukampa mtu wako kwa uhuru kabisa ashike hioi simu na hazijafutwa? Hainiingii akilini... Pia hakupendi, mie ninavoelewa once you go begging for another man or woman to love you back ni wazi kuwa huyo mwanaume/mke hana mtu ama alie nae kamtoka kama matapishi.

Inawezekana una nia naye bado sababu wampenda, ila Iza tambua kuwa it will never be the same. Hapo kafungua mlango hata asipokuwa na huyo mwanaume ambae sms zilenda kwake, in the future uwezekano wa kupata mwingine ni kubwa sana. Kama umeridhia kuwa nae bado basi ni kheri ukae nae kuongea kuhus alilofanya na kwamba huwezi vumilia tena hayo in the future [but only if you mean it]. Pole saana kaka...
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: Iza
Pole mkuu,
I know wt ua going through......
Una moyo kama wa kirikou, hongera kwa hlo
tulia, think na fanya maamuz vle moyo wako unakutuma

just remember
Every test in our life
makes us bitter or better,

Every problem comes
to make us or break us,

Choice is our whether
we become victim or victorious..!!
 
  • Thanks
Reactions: Iza
kwanza polee sana

pili jipe muda wa kuamua na kutafakari
usi rush kwenye maamuzi

Yaah ni kweli, manake akili na mwili havina uhusiano kabisa..wacha nijipe muda labda nitaelewa ni kwanini na nifanye nini..
 
kasome wakorinto wa kwanza mlango wa saba, utajua kwa nini watu wanaoa kama unamwamini Mungu lakini.

I do beleive in GOD, YES pia nimesoma hiyo mistari..sasa ikiwa ni kwa ajili ya kuzuia tamaa..,sasa unaoa/olewa ili iweje wakti bado upo macho juujuu?
 
Inaonekana mkeo ana revenge!

Haiingii akilini akwambie black and white kuwa ni yeye amejigonga kwa huyo alo cheat nae. Tena atakuwa amefanya makusudi kuacha hizo meseji ili kuhakikisha unaziona.

Wewe hujawahi kumtenda kweli???

Sijawahi na wala sikuwahi kufikiria kwamba nittatoka nje, nisichokielewa ni kwanini aliwacha mambo wazi kama yalivyo...Sijaelewa kabisa..
 
Back
Top Bottom