Wamtaa huu
Senior Member
- Jan 21, 2011
- 168
- 55
Kinachomharibia Zitto ni kimoja tu!Anatangulia yeye ndipo inafuatia chadema..!
Mara kadhaa kwenye thread mbalimbali kumekuwa na kundi kubwa la mashabiki na wapenzi wa chadema kuonyesha waziwazi kutokuwa na imani na Zitto Kabwe mtu ambae walimuamini na kumpenda sana kabla hawaja anza kupoteza imani na mapenzi nae.
Sasa hivi usishangae kuona wanachama na wapenzi wa chadema kutokumpa kabisa nafasi ya kumzunguza kwa mema mbunge huyo machachari na matokeo mazungumzo mema yameelekezwa sana kwa John Mnyika, Tundu Lissu, Mdee na wakati mwingine kwa Godbless Lema.
Kautafiti kangu kadogo kamenisukuma kujiuliza na kuamua kuungana nanyi magreat thinker.
Hivi ni kwa nini wapenzi na mashabiki wa chadema hawana tena imani na Zitto Kabwe?
Tafadhari weka sababu huenda zikamsaidia kujirekebisha.
Nawasilisha.
Nashindwa kuwaelewa nyie mnaomtetea Zito! hivi nyie mnampenda zito au mnataka kumzamisha kabisa? Msijidanganye kuwa kila anaemkosoa Zito ni yule anayemhitaji Mbowe au ni mchaga. Hiyo propaganda ya uchaga haina nguvu kama mnavyoipigia kelele na kimsingi baadhi ya wale tunaomshangaa Zito ni wale tuliokuwa tunamtegemea sana Zito na kosa lake sio kutaka kugombea uenyekiti maana hilo alishauriwa akajitoa. Tatizo la zito ni kuwa amebadilika sana ndugu zangu; tofauti na zamani zito sasa ana mawasiliano makubwa na JK na ambayo ni hatari kwa upinzani, mchezo wake na Kafulila unawaumiza sana wanachadema. Mipango yake ya kugombea urais sio mibaya lakini haraka alizonazo zimemfanya asiaminike tena, CHADEMA haindeshwi kihuni hata mgombea urais anapatikana kwa utafiti wa jinsi anavyokubalika kitaifa ndo maana hata mbowe pamoja na kazi nzuri anayoifanya lakini alishauriwa asigombee urais. Sasa mnaomlinda Zito mbona hamsemi imekuwaje atume polisi kwenye vikao vya NCCR? mbona hamsemi yeye alienda South Sudan na kikwete kama nani? mbona hamjiulizi ni kwanini aliamua kumuunga mkono Kafulila akamwacha mgombea wa CHADEMA? Kinachomwokoa ni busara za uongozi wa CHADEMA angekuwa NCCR nae angetimuliwa.Ni Mbowe amekutuma? Mbona unahangaika sana kuhamasisha chuki juu ya Zitto? Umeshatoa mada si utulie upate maoni au uchangie unapoona panakugusa? Umeona haitoshi unang'ang'ania wasio na imani ni wengi. Uchambuzi wako unafikiria JF iliyojaa maadui wa Zitto ndio itabadili ukweli wa mazuri yake?
Well, umetaka sababu za watu wengi kupoteza imani juu ya zitto.
1. Sio kweli kwamba watu wengi wamepoteza imani, ila kuna kundi la watu tena ndani ya chama chake kwa kumhofia wanapandikiza mbegu za chuki juu yake na kujitahidi kufanya watu wapunguze imani kwake, ila anayoyafanya yako wazi mbele ya Wote wenye macho na maskio.
2. Zitto yuko huru juu na anachoamini kuwa sahihi, hafanyi siasa za kizee na haoni tabu kumsifia mtu anapofanya jambo jema hata kama si wa chama chake. Mfano rahisi ni ishu ya posho, wameshakubaliana kama chama kwamba posho ya vikao si stahili yao, lakini watu wana tamaa wanaendelea kupokea tu huku wanasema wanapinga, sasa ujinga kama huu ndio Zitto asioweza kuuvumilia, yeye akaamua kutokupokea. Unategemea hapo watampenda?
Usiwe mwongo! ishu ya posho ipo kwenye ilani ya CDM kama vipi kasome ilani kwa hiyo zito alikuwa anatekeleza ilani na ndomaana hata mbowe alikataa VX la kiongozi wa upinzani bungeni. Na kuhusu posho kuweka kwenye akaunti za wabunge hata zito mpaka sasa anawekewe maana kimeo makinda alisema watakuwa wanawekewa tu watake wasitake.zitto kama binadamu ana mapungufu yake sawa lakini kuna kundi la watu "maalum" waliowekwa kumuharibia! kuna hot issues ambazo zitto amezisimamia hao mnaowaamini wameshindwa.mfano hai ni issue ya posho,amesimamia alichoamini. kuna wengine wanasingiza ohh pesa zinawekwa moja kwa moja kwenye akaunti za wabunge, wanataka kutuaminisha kuwa zitto hana hiyo akaunti?zitto ameibua mijadala mingi pale bungeni na kwingineko ambayo imeleta tija kwa taifa hili.so mpeni heshima yake!
Nashaukuru kwa ushauri wako nitaufanyia kazi.Mkuu ujue we una point sana, na always una hit to the tagert, ila tu hiyo Avatar yako ndo inanichefua kila nikkiangalia Mkuu, Badilisha Mkuu, haindeni kabisa na points zako,some times nikkiangalia AVATAR Yako, najikuta na scrol down nikihisi utakuwa umeandika Upupu kama hiyo AVATAR yako, kumbe sio Mkuu, itoe Mkuu
Hata observation nayo ni moja ya instruments za utafiti na inakubalika kitaalamu.Sijui umefanya wapi utafiti....
Sijui umefanya wapi utafiti....
Ben maandishi yako kiasi yanadharau kwa waliokosa opportunity ya kwenda shule kwa sababu ya system mbovu tuliyonayo, kama wewe ulibahatika kupata madarasa shukuru Mungu afterall madarasa ni kitu gani kama hayajakuelimisha.Kweli ndiyo maana Turnover ya makampuni yanayochapisha magazeti pendwa ni kubwa sana kulinganisha na magazeti mengine.....! Kwa aina hii ya waso,i , basi tusiwaonee wale ambao hawakuingia madarasani.It's a pity watu wanakuja na udaku juu ya mtu halafu watu wanaunga tela tu.Kuna baadhi ya watu hapa ambao kwa rekodi yao hapa JF wamekuwa analytical lakini walivyochangia wamenichekesha na kunisikitisha....wengine huwa sishangai
Guys let us be serious on issues...tuachane na trivial issues!