Kwanini walio nje huwawia ngumu kurudi nyumbani? Tuwasaidiaje?

Niliondoka nyumbani na student visa malengo yangu yalikuwa shule kwanza ila sikuwa na tuition fees hata senti tano nilichuma matunda Sweden kwa mwaka mmoja ili nipate fees haikutosha rafiki yangu akaniambia kuna kazi Poland inalipa vizuri tukaelekea huko tukafanya kazi mwaka mmoja kazi zikaanza kupungua bado fees haijatosha tukaona wapolo wameanza kuelekea UK wanakolipa vizuri tukajiunga ndani ya nyumba ya malkia kazi ikakubali recession ikaharibu mahesabu visa ikawa inaelekea ku expire, nikatafuta chuo nikapata visa ikaleta matatizo kwa vile nilikuwa nimelipa kiasi chuo kikanisaidia ku extend nikapiga kitabu kwa mwaka mmoja nikavalishwa joho. Baada ya kumaliza chuo nikaanza kutafuta kazi ya profession yangu huko UK hadi sole ya safety boots ikaenda upande nilichokuwa napata ni zile zile kazi nilizokuwa nafanya kabla ya shule yaani kubeba mabox. Baada ya miezi kama sita hivi nikajiuliza hii shule yangu itanisaidia nini huku uamuzi niliochukua ni kubeba mikoba yangu na kutafuta next flight nyumbaniiiiii kwa baba na mama. Bahati iliyoje nilipofika tu kwa kutumia ujuzi wangu nikapata kazi ya kujiajiri au ya kuajiriwa hiyo ni siri yangu.
Mkuu Luteni,
Wakati wewe ulikuwa unatafuta kazi ya kuajiriwa, kuna wenzako wengi tu wana create hizo kazi (wanajiajiri).
Nafikiri tukubali tu hapa kwamba kila binadamu ni tofauti na hakuna solution moja kwa matatizo yote ya binadamu.
Wakati wewe unasema ulirudi TZ na kupata kazi, kuna Watanzania wengine wengi tu wanarudi na wanabaki kusota bila kazi.

Ndio maana wengine tunasema, suala la nani anaishi wapi na anafanya nini, ni la mtu binafsi na hakuna haja kuingilia uhuru wa mtu binafsi.

Nyie kama mnaweza basi tengenezeni opportunities nyingi TZ na vijana wa dunia watapima na wakiona kuna mengi ya kuwafaa TZ basi watakuja tu. Hawahitaji kushikiwa mjeredi kurudi kwao; wanachohitaji ni kuona opportunities na mazingira ambayo yanaridhisha nyoyo zao.
 
Niliondoka nyumbani na student visa malengo yangu yalikuwa shule kwanza ila sikuwa na tuition fees hata senti tano nilichuma matunda Sweden kwa mwaka mmoja ili nipate fees haikutosha rafiki yangu akaniambia kuna kazi Poland inalipa vizuri tukaelekea huko tukafanya kazi mwaka mmoja kazi zikaanza kupungua bado fees haijatosha tukaona wapolo wameanza kuelekea UK wanakolipa vizuri tukajiunga ndani ya nyumba ya malkia kazi ikakubali recession ikaharibu mahesabu visa ikawa inaelekea ku expire, nikatafuta chuo nikapata visa ikaleta matatizo kwa vile nilikuwa nimelipa kiasi chuo kikanisaidia ku extend nikapiga kitabu kwa mwaka mmoja nikavalishwa joho. Baada ya kumaliza chuo nikaanza kutafuta kazi ya profession yangu huko UK hadi sole ya safety boots ikaenda upande nilichokuwa napata ni zile zile kazi nilizokuwa nafanya kabla ya shule yaani kubeba mabox. Baada ya miezi kama sita hivi nikajiuliza hii shule yangu itanisaidia nini huku uamuzi niliochukua ni kubeba mikoba yangu na kutafuta next flight nyumbaniiiiii kwa baba na mama. Bahati iliyoje nilipofika tu kwa kutumia ujuzi wangu nikapata kazi ya kujiajiri au ya kuajiriwa hiyo ni siri yangu.

Now I understand! Gd luck bro.
 
Kiranga umeshinda wewe mimi huwa siwezi ligi nilichotaka ni mawazo yako nione kama yatanisaidia lakini nafikiri mawazo yako yamenitosha waachie na wengine wanipe mawazo yao asante sana.
Kiranga hajashinda wala nini, the truth ni kuwa hawa jmaa sio kwamba hawataki kurudi home ila wanaona noma , kwa sababu wenzao waliobaki home wapo far away wana kazi nzuri za maofisini ila wao wanapiga blah blha na kubeba box nz ku-make dola mia mia per day.the thruth is that everybody want to go back. nothing new abroad than taking pics and upload them in facebook.i know kiranga will criticise but thats the truth.
 
aaaah wanafanya kazi bwana TACO BELL,WINCO, MCDONALD'S,GOOD WILL ,VALUE VILLAGE, NK
na wote hawa wana elimu nzuri tu, ndio maana nchi inaajiri wahindi. our guys with their r education are selling bic macs and works in those aged people houses , though the payiment is high but the truth is that they dont get any respect, no one respect them and they dont want to agree here with the truth
 
Ni bora wakae huko huko nje ambako hata ukibeba box unapewa hela. Bongo ni noma, hakuna tena maneno ya 'tuijenge nchi yetu' nchi ipo mikononi mwa wachache sana.
 
"When I saw the coastline I knew that I had reached a new future, a new life," says Chalid, declining to give his second name. He is 30 years old and has been out of work for the past three years. A diploma in computer science is not worth much in poverty-stricken southern Tunisia. Like many unemployed specialists, he does not expect much from his country, a fact that remains unchanged even after the fall of President Ben Ali.


Utamsaidaje kijana huyu ameona nnchi yake imemtupa kabisa, wako wengi wa aina hii. Hii ndio ile ya msomi wa SUA kuajiriwa benki badala ya kukuza kilimo.
 
Kuna waliokuja huku kusoma, wakapata ajira/wakajiairi, wakalea watoto mpaka University. Watoto hao sasa wanafanya kazi na wanaendelea vizuri. Mhamiaji huyu ameshastaafu huku na ameshajenga nyumba kadhaaTanzania, na katika kustaafu kwake mara nyingi yupo Tanzania anaendeleza miradi yake na kupumzika. Karibu kila mwaka anakwenda Tanzania na kukaa miezi kadhaa. Utamuweka kwenye fungu lipi? Wapo wengi ambao mnawaita 'wabeba mabox' ambao ni hawa na wanaona huu mpangilio wa maisha ni mzuri sana kwao-familia wote wako nje, anapata matibabu, pension, n.k.
 
Hoja yako ni ya mawazo yanayotofautiana. Kwa muono wako huko sahihi kwa hoja yako. Kwa muono wangu ni hoja isiyokuwa na msingi. unazungumza vitu ambavyo vimepitwa na wakati. Dunia sasa inataka kuwa kitu kimoja. Kwani walioweka mipaka na kutugawa wamekiri kwamba ni udhalilishaji wa ubinaadamu. wameliona hilo na ndio maana ulaya mipaka iko wazi na kuwa nchi moja. Mimi naona kabla kuangalia watanzania wanoishi nje kwanza jianzie wewe mwenyewe kwa nini ujarudi kijijini kwenu tokea uje Dar es salaam miaka ishirini iliyopita. halafu waulize wahindi kwa nini awarudi kwao tokea waje kupandikizwa Tanganyika na mwingereza. sasa wewe utawasaidia vipi hao warudi kwao. Kwa undani hoja yako Ubaguzi. wewe usiende nchi ya mwenzako na mwenzako asije kwako. Alikuwako waziri Tanzania Mwingereza Bryson mbona ukumsaidia arudi uingereza. na wakati akiutubia mikutano unampigia makofi. Na mradi wa nyumba alizojenga mwenge wewe ni mmojawa unayeishi humo.
Jiulize Rais wa kwanza wa Zanzibar ni kabila gani na ni mtu wa kutoka wapi na alikuwa anafanya kazi gani kabla ajaingia katika siasa.
Jiulize jk yeye ni mkwele kwa nini kaoa mmakonde. au jk nyerere yeye ni mzanaki kwa nini alioa mjaruo. kuhusu kazi ueshimu aina yeyeto ya kazi au mfanya kazi. kila eneo la kazi ndio maendeleo ya taifa. Tanzania tuna utamaduni mbovu wa kuwadharau wabeba zege, wazoa taka au wafagiaji maofisini ndio maana tanzania atuendelei. hao viongozi wala rushwa wote wa serikali ya ccm. wote watoka mashamba awakukulia mijini. wamepiga hatua moja kwenye elimu ndio wameingia mjini. Kama mchonga meno na wenzake wote wanaofuata. Ndio maana nchi inakuwa na mwelekeo mbovu.
 
Mkuu Luteni,

Labda unisaidie swali langu, na huyo aliyeko Dar akitokea Sumbawanga, kwanini humshauri arudi kwao Sumbawanga? na kule nako kwanini hawamshauri arudi kijijini kwao? Hii ndio Nyerere aliwahi kusema ukionja nyama ya mtu huwezi kuacha kuitafuna; leo huyu Mzanzibar, yule Mzanzibara; ikiisha hapo huyu Mpemba, na yule Muunguja. Nyie ndio viongozi mkipata nafasi mtaleta sera za kuwaondoa vijana mjini eti wazururaji.

Dunia ni kijiji na hakuna tofauti kati ya mtu aliyeko NewYork akifanya mambo yake na aliyeko Dar. Wote lengo lao ni moja tu la kujisaidia wao wenyewe and in a process wengine wanasaidia na ndugu pamoja na nchi.

Kama ambavyo kuna watu wanaona umuhimu wa kurudi vijijini kwao kutoka mijini, hata nje kuna watu wanaona umuhimu wa kurudi TZ wakati wengine wanaona umuhimu wa kwenda nje. Factor kubwa ni opportunities zilizopo. Jamii zinazojitosheleza huwa haziwi na wahamaji. Bahati mbaya/nzuri sasa mwanadamu ameshagundua kuna opportunities nyingi tu na muhimu na kuchungulia huku na kule. Ndio maana watu wataendelea kuhama makwao na kwenda sehemu zingine. Kuna wengi watafanikiwa na pia kuna wengi watashindwa sawa tu na wale wanaobaki pale walipozaliwa ambao nao kuna wengi wanafanikiwa na wengi wanafeli.

Sababu za mwanadamu kufanya anayofanya ni combination ya factors nyingi sana. Tusiwe simple minded kiasi hicho kufikiri tunaweza kuelewa tabia ya mwanadamu kwa kupitia stereotyping. Hata kwenye familia watu hawafanani na ni muhimu kila mtu kumpa nafasi ya kufanya mambo yake kama an independent entity.

Tanzania kuna mamilioni ya vijana hawana kazi za kufanya, unataka na hawa wengine nao warudi kuongeza kundi la wasio na kazi mitaani? Hata wale ambao hawana makaratasi kwenye nchi za watu, at least wana hope, wana kitu cha kuombea kwamba kuna siku watapata. Sio sawa na wale ambao wamekata tamaa kabisa ya maisha.

Haya mawazo ya kwako ya kwamba one solution fits all, naona yanashindwa kwenye approach ya kisomi na yanashindwa pia hata kwenye approach ya kikawaida ya maisha. jaribu kufikiria nje ya box na utapata majibu zaidi ya 1000 kwanini watu wanahama makwao na kwenda kutafuta opportunities sehemu zingine.

Kama lengo lilikuwa ni kuamsha majadiliano basi sawa lakini kama kweli unafikiria hivyo, nafikiri umejichimbia kwenye box, jaribu kutoka nje ya box na utagundua mengi tu.
Mtanzania

Mimi naangalia kwenye wigo mpana zaidi si wa kuoana mzigua na mmasai au mdengereko kupatakazi Musoma ni pamoja na kuijenga nchi kwa nyanja zingine pia ikiwa ni kuchangia pato la taifa kupitia kodi, nasikia Zitto ameliongelea hili kuwa kuwe na fomu maalum ya kujaza umelipa kodi kiasi gani kwa mwaka ndiyo mipango ya maendeleo hiyo, nchi haiendelei kwa kuhamasisha walipa kodi waondoke waende popote ndiyo maana tunajenga jumuiya ya EAC kuongeza watoa kodi, tunajua mtu hata akiwa Kenya au Rwanda kodi yake itaingia kwenye kapu moja, kwa hiyo huyo mtu mtanzania awe Sumbawanga au Dar akiwa na salon yake kodi inaingia kwenye fuko moja tofati na yule anayebeba box Reading UK kwa masaa 16 kwa siku.

Mtanzania hao unaosema hawana makaratasi wanaishi kwa hope ndio hasa target yangu hiyo hope ndiyo inawapofusha maana tunajua hata huko maisha yanazidi kupanda mfano kama anaishi UK na aliahirisha kuanza shule mwaka jana akitegemea kuanza mwaka kesho school fees imepanda mara mbili kwa home students na kwa international students.
 
na wote hawa wana elimu nzuri tu, ndio maana nchi inaajiri wahindi. our guys with their r education are selling bic macs and works in those aged people houses , though the payiment is high but the truth is that they dont get any respect, no one respect them and they dont want to agree here with the truth
Saint Ivuga

Wasiwasi wangu ni kuwa tumeendelea kupoteza resources nyingi sana nje sasa ni wakati wa kushtuka na kujirekebisha vinginevyo tutaendelea hivyo hivyo hakuna nchi inayoweza kutustua, mfano halisi mimi wakati niko ulaya nilikuwa nafanya kazi ya cleaning na mwanafunzi wa PhD ilikuwa inaniuma sana lakini nifanyeje, ukiangalia muda na resources iliyokuwa inapotea kwa watu wawili tu ni kubwa sana sasa zidisha ni watanzania wangapi walio nje wenye Masters mfano wanafanya kazi hizi at the end of the day anaishia kupata nyumba ya mortgage huko huko na kuendelea kulipa kodi kwa maisha yake yote, ukiangalia kwa juu juu unaweza kudhani ni uchaguzi wake hawezi kuingiliwa na mtu lakini uki-sum up kwa watu mia ni hasara kwa taifa. Wenzetu wana data za raia wao walio nje na wanaporudi lazima warudishe returns walichokipata huko sisi hatuna mpango huo tunajiondokea kiholela kwa hiyo ili walio nje waanze kuzalisha kwa maana ya kutambuliwa kitaifa ni lazima kuwe na mtu wa kuliona hilo kitaifa si kifamilia.
 
Hoja yako ni ya mawazo yanayotofautiana. Kwa muono wako huko sahihi kwa hoja yako. Kwa muono wangu ni hoja isiyokuwa na msingi. unazungumza vitu ambavyo vimepitwa na wakati. Dunia sasa inataka kuwa kitu kimoja. Kwani walioweka mipaka na kutugawa wamekiri kwamba ni udhalilishaji wa ubinaadamu. wameliona hilo na ndio maana ulaya mipaka iko wazi na kuwa nchi moja. Mimi naona kabla kuangalia watanzania wanoishi nje kwanza jianzie wewe mwenyewe kwa nini ujarudi kijijini kwenu tokea uje Dar es salaam miaka ishirini iliyopita. halafu waulize wahindi kwa nini awarudi kwao tokea waje kupandikizwa Tanganyika na mwingereza. sasa wewe utawasaidia vipi hao warudi kwao. Kwa undani hoja yako Ubaguzi. wewe usiende nchi ya mwenzako na mwenzako asije kwako. Alikuwako waziri Tanzania Mwingereza Bryson mbona ukumsaidia arudi uingereza. na wakati akiutubia mikutano unampigia makofi. Na mradi wa nyumba alizojenga mwenge wewe ni mmojawa unayeishi humo.
Jiulize Rais wa kwanza wa Zanzibar ni kabila gani na ni mtu wa kutoka wapi na alikuwa anafanya kazi gani kabla ajaingia katika siasa.
Jiulize jk yeye ni mkwele kwa nini kaoa mmakonde. au jk nyerere yeye ni mzanaki kwa nini alioa mjaruo. kuhusu kazi ueshimu aina yeyeto ya kazi au mfanya kazi. kila eneo la kazi ndio maendeleo ya taifa. Tanzania tuna utamaduni mbovu wa kuwadharau wabeba zege, wazoa taka au wafagiaji maofisini ndio maana tanzania atuendelei. hao viongozi wala rushwa wote wa serikali ya ccm. wote watoka mashamba awakukulia mijini. wamepiga hatua moja kwenye elimu ndio wameingia mjini. Kama mchonga meno na wenzake wote wanaofuata. Ndio maana nchi inakuwa na mwelekeo mbovu.
ismathew

Asante kwa mchango wako ila nasikitika hujanielewa ninachotaka ku deliver sio ubaguzi hata kidogo jiulize hata hao wahindi walio tanzania miaka lukuki wamesaidia nini nchi kama si kubanana kwenye msajili wa majumba upanga au ulishakuta mhindi kajenga nyumba kijijini au mhindi tajiri kajenga kiwanda mama kama vipuri zaidi ya viwanda vya kusindika juice, pipi, mikate, umeshajiuliza wakwepa kodi wengi na wenye mikataba mingi yenye utata ni akina nani, tuache hayo nitakuwa naanzisha zogo jingine ila nilikuwa nakujibu uliponiambia mbaguzi, mimi nawaomba watanzania wenzangu walio na matatizo niliyo yabainisha hapo juu wafikirie kurudi nyumbani ili tugawane umasikini.
 
Tatizo ni kwamba wasomi wetu hawathaminiwi wala kuwa motivated,mazingira ya kazi hovyo,salary ndo kabisaa! Yaani wasome ktk mazingira na kazi hvohvo aka mwenzangu hata ningekua mimi naenda kwenye green pasture!
 
Niliondoka nyumbani na student visa malengo yangu yalikuwa shule kwanza ila sikuwa na tuition fees hata senti tano nilichuma matunda Sweden kwa mwaka mmoja ili nipate fees haikutosha rafiki yangu akaniambia kuna kazi Poland inalipa vizuri tukaelekea huko tukafanya kazi mwaka mmoja kazi zikaanza kupungua bado fees haijatosha tukaona wapolo wameanza kuelekea UK wanakolipa vizuri tukajiunga ndani ya nyumba ya malkia kazi ikakubali recession ikaharibu mahesabu visa ikawa inaelekea ku expire, nikatafuta chuo nikapata visa ikaleta matatizo kwa vile nilikuwa nimelipa kiasi chuo kikanisaidia ku extend nikapiga kitabu kwa mwaka mmoja nikavalishwa joho. Baada ya kumaliza chuo nikaanza kutafuta kazi ya profession yangu huko UK hadi sole ya safety boots ikaenda upande nilichokuwa napata ni zile zile kazi nilizokuwa nafanya kabla ya shule yaani kubeba mabox. Baada ya miezi kama sita hivi nikajiuliza hii shule yangu itanisaidia nini huku uamuzi niliochukua ni kubeba mikoba yangu na kutafuta next flight nyumbaniiiiii kwa baba na mama. Bahati iliyoje nilipofika tu kwa kutumia ujuzi wangu nikapata kazi ya kujiajiri au ya kuajiriwa hiyo ni siri yangu.

Bado sijakuelewa uliishi nchi gani. Ulisomea wapi? Umeeleza ulienda kuchuma matunda Sweden then ukaenda Poland then ukaishia UK.
Nataka kujua hiyo viza yako ilikuwa ni ya Sweden ama wapi?
Kitendo chako cha kufika huko ktk hiyo nchi ulikofikia then hukwenda shule that means ulikuwa "out of status". Ukinipa clear answer ya hiyo student viza yako ilikuwa ni ya nchi gani then nitaendelea na mjadala. Ahsante
 
Bado sijakuelewa uliishi nchi gani. Ulisomea wapi? Umeeleza ulienda kuchuma matunda Sweden then ukaenda Poland then ukaishia UK.
Nataka kujua hiyo viza yako ilikuwa ni ya Sweden ama wapi?
Kitendo chako cha kufika huko ktk hiyo nchi ulikofikia then hukwenda shule that means ulikuwa "out of status". Ukinipa clear answer ya hiyo student viza yako ilikuwa ni ya nchi gani then nitaendelea na mjadala. Ahsante
Unataka kujua visa yangu ili iweje 'am not such a person' kama hukuelewa maelezo yangu nashukuru sana kwa mchango wako.
 
Unataka kujua visa yangu ili iweje 'am not such a person' kama hukuelewa maelezo yangu nashukuru sana kwa mchango wako.

Umekuwa unasita sana kuwa open and clear kuhusu nchi gani umekaa. Umeeleza kuhusu kuchuma matunda Sweden na kupiga mzigo kule Poland na UK. Taja hiyo nchi uliyoishi.
 
Umekuwa unasita sana kuwa open and clear kuhusu nchi gani umekaa. Umeeleza kuhusu kuchuma matunda Sweden na kupiga mzigo kule Poland na UK. Taja hiyo nchi uliyoishi.
Hivi wewe kuishi unakujuaje si ameshasema amechuma matunda Sweden kwa mwaka mmoja then akaenda Poland kwa mwaka mmoja then UK mwaka mmoja sasa unataka kutuambia sehemu hizo zote alikuwa haishi, ninavyojua mimi hata ukikesha baa unalewa ndiyo kuishi huko siku imepita.
 
Back
Top Bottom